Kwa Al Ahly hii ya Klabu ya World Cup, hata Mungu hawezi kuisaidia Simba SC

Mungu ana maslahi gani kwenye mpira mpaka aisaidie timu kushinda?

Mungu aache kudili na ufalme wake aje azisaidie timu za mipira? Kweli?? Atasaidia timu gani sasa? Naomba jibu
 
We ni noma umeupima hadi uwezo wa mungu ukajua ni wa kiasi gani? Hatari sana.
 
Ndugu acha kufuru! Mungu hawezi kufanya nini? Ushabiki usivuke mipaka tukamdhihaki Mungu kiasi hiki!
 
Wewe Umejuaje kama Mungu hatoweza kuisaidia Simba. je uliongea naye je ulishawahi kufanya sala kuiombea Simba halafu ukajibiwa kwamba ah kwa timu ile siwezi? acha unafiki Simba anaweza kuongoza kundi ujue Mungu hayupo upande Mmoja mkikaa vibaya mtayuokotea fainali nawaambieni tena mkikaa vibaya mtatuokotea fainali
 
Uzuri wa waarabu hawa wa mzee Pitso Mosimane, wanaweza wakapiga wote kwenye kundi atakayesalimika sana sana sare labda

Anyway bado kuna dk 90 za mpira ingawa kwa uwezo walionao jamaa hata mm naona kuna hatari ya timu kupigwa nje ndani.. Na wala sitawalaumu simba, jamaa hawa wa sasa hivi wametoka kumtoa bingwa wa amerika kusini huko
 
Kwa hiyo Ahly wao hawana mungu? Au miungu itatofautiana? Huy ataisaidia simba na huyu Ahly? Kama ni mmoja atasaidia timu gani?
 
Itategemea ni Mungu wa namna gani kama ni Mungu wa upotolo ni feki maana jana hakusikiliza maombi yao au inawezekana sio feki ila aliona maombi ya upotolo yalijaa wivu na unafiki
 
Mungu ana maslahi gani kwenye mpira mpaka aisaidie timu kushinda?

Mungu aache kudili na ufalme wake aje azisaidie timu za mipira? Kweli?? Atasaidia timu gani sasa? Naomba jibu
Wewe hujui wengine wanamwomba Mungu riziki kupitia mpira wewe vipi
 
Timu itayofungwa inakosa mshahara ama?
Hoja sio kufungwa hoja ni mpira unatoa riziki halali ambayo mtu anaweza kumwomba Mungu na akapewa au mpira ni haramu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…