Kwa anaejua chimbo Kali la kitimoto kigamboni

Kama kuna vijidudu havifi kwa kupikwa tungeathirika wengi. Ila wengi huwa hawapiki vizuri ndio sababu hivyo vijidudu havifi. Nimesikia wana minyoo ya hatari.
Kama ni mtumiaji mzuri wa mbuzi wa Vatican basi jenga tabia ya kunywa dawa ya minyoo kila baada ya miezi mitatu. Kuna minyoo hatari ukila nyama ambayo haijapikwa vizuri wanaweza kufika mpaka kichwani kwenye medulla oblongata. Wakifika huko hakuna tiba isipokuwa tu kuimba parapanda! Na unakufa kifo kibaya cha kuehuka na mateso kibao...
 
Duh kuna jamaa alinisimulia kuwa kuna mzee wao alikuwa anaumwa sana kichwa ikafikia hatua hapa Tz wakataka kumpasua, ndugu wakakataa wakampeleka India. Wanasema alipofika kule akaambiwa ana mnyoo kichwani ila walimpa dawa tu akarudi hadi leo anadunda.. Hii stori niliona kama 'chai' ndio maana sikuiweka mpaka wewe uliposema kuwa mnyoo unaweza kufika hadi huko. Inatisha kwa kweli.
 
Na huyu watakuwa walimuwahi. Au wana uzoefu na hilo tatizo hilo.

Kuna jamaa yetu aliondoka mchezo mchezo tu hivi kama utani. Mwishoni kabisa huko kichwa kinamuuma kachanganyikiwa. Daktari mmoja ndo kashtuka kuuliza kama jamaa ni mlaji wa kitimoto. Lakini ikawa too late akafa.

Kula kitimoto mahali ambapo unajua uandaaji wake uko salama yaani inapikwa sawasawa. Vinginevyo kunywa dawa nzuri za minyoo baada ya hapo na/au fanya detox ya tumbo!
 
Asante mkuu, ingawa si mlaji sana wa hii kitu ila umenithibitishia na umenipa somo kubwa,ubarikiwe.
 
😁😁jamani mnanifokea sana..
Sijabadilisha kitimoto kuwa mchicha mjue🀣🀣
 
Asante kwa somo zuri Daddy
 
Eheee😳😳😳
 
Wale wa "kisikauke sana", kuna jambo la kujifunza hapa
 
Shukrani sana kwa masahihisho ila Si unaona hata kiwango cha hiyo myoglobin imelinganishwa kwa kuku na samaki. Hapo kuna jambo 😊😊
Karibu sana.tuache utani pork ni habari nyingine haloo😍😍

Ninatamani sana kuwa vegetarian au pescatarian lakini ndio siwezi kuacha kula nyama😌
 
Dawa ya minyoo yoyote tu mkuu. Mimi sio mlaji sana ila nataka kujua maana kuna sehemu unaweza kula labda cha kuokwa na hakikukaushwa vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…