Shida siyo mitaji, ila bei kupangwa na serikali ndio inasababisha wakulima wengi kukimbia kilimo. Hebu imagine kwa sasa bei ya diesel ilivyo juu alaf nimelima tu alizeti kangu alaf mtu aje akupangie bei ya kuuza.
Na hii ndio sababu moja wapo kubwa kwann sikipendi kilimo,na sitokaa nikipende kwasababu hiii
siwezi lima kisasa,kwa gharama,nimefanya research zangu,nmetafuta wataalamu,nmechukua udongo
nimepeleka maabara umepimwa nimepata uhakika kabisa kwa udongo huu zao flan na flan linatoka
halafu baada ya mahangaiko yote hayo,mazao yangu yamekubali kwa 95% anatokea mjinga mmoja (serikali)
ananiambia bei ya hayo maharage yako kilo 1 n sh 1000,hutakiwi uza zaidi ya 1000,Ananipangia bei yeye kama nani? gharama nilizotumia hadi navuna mazao yangu anazijua?
au anahisi nilichimba tu mashmo nikafukia mbegu zikaja zikajiotea zenyewe? ki ufupi serikali isipo ondoka
kwenye kilimo ikaacha watu walime wenyewe na wauze wenyewe Kilimo ndio kitakua dili,ila kwasasa hivi huwezi kuwa mkulima wa Heka 5 10 15 ukaona mafanikio ya kueleweka,ni kudanganyana tu.
ila naweza kaanga Kuku wangu nikawaunga nikawatia mbwembwe nikatoa mshkaki wa kuku nikauza mshkaki m1 20,000, tena nimeweka finyango 3 na karoti zimejipangaaa na vikachumbari umbea,Nauza 20k mshakika wa Kuku 1.
Kuku m1 ananipa mishkaki mpk mi 4,yani napga 80k kwa kuku nliemnunua 7000, Unafkiri ingekuwaje kama serikali ingeniambia mshkaki wa kuku siruhusiwi kuuza zaidi ya 1000,unadhani ningetoboa?
Mahali popote penye kiherehere (serikali) huwezi ona Faida otherwise uwe na capital iliyoshiba na wengi wetu tunasema tukpata capital tutalima ila leo unipe 1B uniambie nilime aw weeee silimi ng'ooo biashara kibaooo nijipeleke kilimoni,siweziiii.
So imekaa hivyo,kilimo ni uti wa mgongo wa maskini sio Tajiri...Tajiri akilima n anaongeza tu income ila tayari ana channel zake hukoooo tusizozijua.
Kilimo Tanzania ni Utumwa.Full Stop.