Kwa Experience yangu ya muda mfupi kwenye "Betting" nimegundua mambo machache

Kwa Experience yangu ya muda mfupi kwenye "Betting" nimegundua mambo machache

Hiki ndio cha muhimu kabisa.
Watu wengi wanakuwa sana sana sana maana wanataka kutajirika kwa pesa ndogo sana yan MTU anaweka 10000/ ods 300 hapo probability ya kushinda ni ndogo sana sana.

Niwakumnushe kwa mfano match ya Yanga na Dodoma Jiji.
Yanga alipewa odd 1.41 lakini probability ya kushinda ilikuwa over 99% so ukiweka 1m unapata laki nne ndani ya DAKIKA 90 tu.

Au ukitaka probability ya 100% ungeipa Yanga apate walau goli mbili ambayo odd ilikuwa 1.3.
Ukiweka 10m unapata milioni 3 ndani ya dakika 90.

Watu tunaishi tunafamilia tunasomesha na kujenga kwa betting tu.
Bet responsibly.

Kubet ni kazi ya watu wenye akili kama huna akili nenda kijijini ukalime viazi mbatata huko.
Daaah
 
Betting ni kimbilio kwa vijana wasiokuwa na ajira, inahitaji mtaji mdogo, elimu ndogo ya kujua kusoma na kuandika ni mfumo usio rasmi wa kujiingizia kipato
Nikiwangaalia maafisa wengi wenye nafasi katika ofisi za umma na binafsi wanaobeti kwa siri, nadhani kwa sasa betting ni kimbilio la watu wengi.
 
Betting, kubashiri au wengine wanaita mchezo wa kubahatisha ni aina mojawapo ya KAMARI. Kama hujashiriki kwenye betting au aina yoyote ya kamari usiingie na KIMBIA NA KAA NAYO MBALI SANA, na kama unashiriki ukiwa na matumaini kwamba siku moja utatoboa kwa betting, TOKA HARAKA SANA NA KAA MBALI NAYO SANA, betting (Kamari) ni mbaya, haifai ni uraibu ambao ukikupata umekwisha, athari za kamari sio tu katika kupoteza pesa, bali pia inalemaza akili. Najua tunaaminishwa kwamba kuna wachache walipata 'fedha nyingi' kwenye betting (Inategemea tafsiri ya 'fedha nyingi' ina maana gani kwako), lakini hebu jiulize ni asilimia ngapi hao waliopata? je ni kweli wametoboa? Lazima ufahamu kwamba kuna tofauti kati ya kushinda betting na kutoboa kimaisha. Betting inaathiri ubunifu wako wa asili na inalemaza akili na inaathiri hata watu wako wa karibu, hasa kama una familia na marafiki. Mojawapo ya athari kwa wanao bet ni kufikiri kwamba betting au kamari ni njia ya mkato katika kufanikiwa maishani. Hakuna short cut maishani, hakuna, hakuna, hakuna.

Betting inaweza kukusababishia kukata tamaa, kuwa na mawazo mengi, kuamini na kutegemea bahati nasibu kuwa ndiyo njia pekee ya mafanikio kwenye maisha. Betting inawafanya wachezaji kuondoa matumaini kwenye juhudi na maarifa katika kufanya kazi halali. Huwachochea watu wapende fedha nyingi kwa njia ya mkato

KUFANYA KAZI, KUFANYA BIASHARA KUFANYA UJASIRIAMALI (KWA BIDII, KWA NIDHAMU NA UBUNIFU) UKIWA NA MALENGO YA MUDA MREFU NDIO NJIA PEKEE YA WEWE KUPIGA HATUA NA KUPATA MAENDELEO TARATIBU NA HATIMAYE KUFANIKIWA MAISHANI MWAKO - SI KWA NJIA YA BETTING AU KAMARI.
Jema. Lakin kwa Mfano wale Wawili walioshinda Milioni 80 na kugawana kila moja Milioni 400, watakuwa Hawajoboa??
 
Nikiwangaalia maafisa wengi wenye nafasi katika ofisi za umma na binafsi wanaobeti kwa siri, nadhani kwa sasa betting ni kimbilio la watu wengi.
Duh mimi nilijua ni kwasisi ambao hatuna ajira, kumbe hadi maafisa🤣🤸🐒
 
Back
Top Bottom