Kwa Fomula ya Mbowe, Samia Suluhu Hassan hatakiwi kugombea Urais

Kwa Fomula ya Mbowe, Samia Suluhu Hassan hatakiwi kugombea Urais

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Mbowe kwenye hotuba yake, akielezea kuwa hawezi kuwaachia watu wengine waongoze chama, baada ya yeye kuwa mwenyekiti kwa miaka 21, alisema kuwa Mtei aliachia umwenyekiti wa chama alipofikishia umri wa miaka 68. Halikadhalika, Bob Makani naye aliachia uongozi wa chama alipofikisha umri wa miaka 68.

Hivyo yeye kwa kuwa sasa ana umri wa miaka 63, hawezi kuachia uongozi kwa chama kwa watu wengine kwa sababu hajafikisha umri ambao watangulizi wake waliachia madaraka, ataachia akigikisha umri wa miaka 68. Aliyasema hayo, bila ya kujali aliowataja, wote waliongoza kwa kipindi cha miaka 5, kila mmoja.

Kama tungekuwa tunafuata falsafa hii ya Mbowe ya kufuata umri wa kiongozi wa mwanzo alioamua kuachia madaraka, ingebidi Marais wote wa Tanzania wasiwe na sifa ya kugombea Urais wakifikisha umri wa miaka 63, kwa sababu Mwalimu Nyerere, Rais wetu wa kwanza, na Baba wa Taifa, aliacha kuendelea kugombea Urais mwaka 1985, akiwa na umri wa miaka 63. Rais Samia kwa sasa ana umri wa miaka 64.

Na kwa tukifuata fikra hizi, yeye Mbowe kwa falsafa yake mwenyewe, hana sifa ya kugombea Urais maana amekwishaufikia umri ambao Mwalimu Nyerere aliondoka madarakani.

NB: Madaraka ya muda mrefu hulevya na kupofusha akili na weledi.
 
Hiyo sidhani ingekua hoja kwa mwanasiasa mkongwe kama Mbowe, anyway mbowe amesha filisika kisiasa hana hoja......
 
Logic ya Sultani Mbowe ni kwamba anaishukuru ATM kwa kutoa fedha zake mwenyewe, eti maridhiano yamesababisha kufunguliwa kwa mikutano ya Siasa wakati ni HAKI yetu ya KIKATIBA 😆😆😆😂 tate nane...

Tundu Lissu ataleta aggressive politics.
 
Akifika miaka 68 atasema alikosea tarehe ya kuzaliwa hivyo anamiaka 60, walewale tu akina kaguta museveni
 
Mbowe kwenye hotuba yake, akielezea kuwa hawezi kuwaachia watu wengine waongoze chama, baada ya yeye kuwa mwenyekiti kwa miaka 21...
Mbowe namfananisha na raisi aliefanya umafia sana madarakani kiasi ya kwamba anaogopa akitoka madarakani raisi atakaeingia atamtupa ndani.

Anaweza kuachia kiti kama kiongozi atakaefata atakuwa ni mtoto wake au swaiba wake.
 
Mbowe namfananisha na raisi aliefanya umafia sana madarakani kiasi ya kwamba anaogopa akitoka madarakani raisi atakaeingia atamtupa ndani.

Anaweza kuachia kiti kama kiongozi atakaefata atakuwa ni mtoto wake au swaiba wake.
Yanawakuta mu7 na Kagame
 
Yanawakuta mu7 na Kagame
Hao washafanya umafia sana ndomaana viti vyao wanapanga kuwaachia watoto wao.

Sijui kama na Mbowe anapanga kumuachia mwanae James Mbowe kiti hapo baadae.
 
Kwahiyo mnasema DEMOKRASIA ya kweli haipo CHADEMA?
 
Back
Top Bottom