Kwa hali hii ya Kigoma, tujiandae kuzika

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
59,045
Reaction score
94,974
Siandiki kumtisha MTU, ndio ukweli mtupu! Kigoma tayari kulikua na maambukizi makubwa sana kwa mujibu wa VP akiwa Makere-Kasulu alitamka hivyo.

Nilitegemea serikali yenye akili ingeweza hata kuwaelimisha watu wake kuhusu hii mikusanyiko, matokeo yake wamehamishia akili zao walizonazo kuudhibiti Upinzani

Kwa hali ya Kigoma, wala hakuna haja ya kusali wala kuomba, tujiandae tu kuzika au kusafirisha in coming few days.

Sibishani
 
Ujinga wa mawazo.
Sie tunao tumia daladala tuna pumuliana visogoni,tulio sokoni ,makanisani na misikitini,
Ferry kwny ma boat na mabasi ya mikoani.treni n.k
Jeshini,Shuleni,vyuoni.
Bado nch nzima ina wagonjwa chini ya 200.
Nabaki nacheka tu huyu anaezusha ugonjwa kuepo,anatuchekesha sana.
 
Waonacho hatari kwao ni makongamano yenye maelekezo ya kujikinga kikamilifu ya madai ya katiba ndio hatari kisa Katiba mpya inajadiliwa na ndio kitisho ila covid 19 wameikumbatia kwakuwa sii hatari kwao hata wanaiimarishia nakuihakikishia ulinzi.
 
Sawa huyo anazusha jipongeze kwa kutambua anayekutahadharisha anazusha.
 
Hebu soma ulichoandika kwanza Hasa hio mistari mitatu ya mwisho. Nimekuwekea picha ili upunguze ujinga, hayo ni matakwimu ya CCM





 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…