Pre GE2025 Kwa hali ya siasa ilivyo nchini, binafsi sioni upinzani katika ujumla wao nchini, wakipata zaidi ya 5% ya kura zote katika uchaguzi mkuu ujao 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
hilo ni miongni mwa mambo ya wazi na uhakika sana ya kisiasa CCM, kulingana na mikakati na mipango ya muda mrefu na muda mfupi, iliyowekwa na chama kwa mkoa wa Dar es salaam...

hata hivyo,
siri kuu ya yote hayo ni moja tu.
ni mafanikio makubwa, halisi yasiyo na kifani, ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya ccm kwa ya mwaka2020-2025.
Chama kiliahidi wananchi mahitaji yao muhimu kadha wa hadha na kimetekeleza na kutimiza ahadi hizo kwa sehemu kubwa, kikamilifu kwa umahiri, uaminifu, ubora na wakati muafaka....

mathalani,
miradi uhakika ya maji, elimu, afya, mikopo, masoko, miundombinu, umeme, biashara, usafirishaji, ulinzi na usalama wa watu, mali na makazi yao, ni madhubuti, uhakika na wa kuaminika ni baadhi tu ya mambo yaliyoahidiwa na kutekelezwa kikamilifu...

Lakini pia,
kukamilika kwa miradi mikubwa ya kimkakati ya SGR na bwawa la mwalimu nyerere, kumechochea zaid, kuimarisha na kuleta ahueni kubwa na upatikanaji wa huduma za muhimu sana za usafirishaji wa bidhaa na watu, lakini pia na umeme wa kutosha na wa uhakika kwa wakazi wa mkoa wa Dar es salaam na vitongoji vyake kuutumia katika kazi na matumizi yao ya uzalishaji, usiku na mchana...

katika hali jiyo,
kuna sababu hata moja kweli kwa wapinzani kunyakua hata jimbo moja tu dar?

kwa ujumla,
Mkoa wa dar es salaam una majimbo ya uchaguzi 10 ambayo ni pamoja na Jimbo la Ilala, Kawe, Kibamba, Kigamboni, Kinondoni, Mbagala, Segerea, Temeke, Ubungo na Ukonga...
pima tu nguvu, uwezo na ushawishi wa kisiasa wa wabunge wa majimbo hayo, halafu linganisha na waupinzani utaona hakuna hata moja wa kutikiswa na Upinzani...

narudia kukuhakikishia ndugu mwanafamilia wa JF kwamba, hakuna Jimbo hata moja kati ya hayo niliyoyataja itakwenda upinzani, na uchaguzi mkuu ujao utakua ni miongni mwa chaguzi Huru, za Haki na za Wazi zaidi kuliko, chaguzi nyingine zozote zilizowahi kufanyika Duniani...

usipange kukosa kushiriki uchaguzi huo muhimu sana...

Mungu Ibariki Tanzania,
Kidumu Chama Cha Mapinduzi πŸ’
 
Ruhusu Tume huru ya Uchaguzi!
Vyombo vya Ulinzi na Usalama visiingilie uchaguzi!
 
Hayo ni matokeo yako ya mfukoni,ila sasa sijui ni yako pekee ama na kundi lako🀭
 
Vipi wakibadilika na kuanza kuyafanyia kazi haya yote ulowaeleza?

Wana muda.

Chama cha MK cha Afrika Kusini ambacho Jacob Zuma alijiunga nacho kilianzishwa mwezi Disemba 2023 na mwaka huu Juni 2024 chama hicho kikashiriki uchaguzi na kushika nafasi ya tatu na kulazimisha serikali ya mseto.

Chama cha ANC nacho kimekuwa kwa miaka mingi chama cha hovyo, chenye kukumbatia mafisadi na wezi. Kama wafuatilia mambo ya huko nyumbani kwa raisi Ramnaphosa kuliibiwa fedha mamilioni ya dola ambazo zilifichwa kwenye makochi!!

Hivyo siasa za sasa wananchi wenye uelewa waweza kufanya maamuzi yatayokushangaza.
 
ni katika kuweka record sawa tu,
isije inaonekana hatukusema wala kutoa tahadhari mapema mwisho wa siku πŸ’

Hata Mendazake pamoja na kuiba uchaguzi wote hakufanikiwa kuchukua 95 % .....!!
 
Wew kula kulala kwa shemeji huna ujualo
We unawaza uchaguzi tu. Kuna mamba mengi zaidi ya uchaguzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…