hilo ni miongni mwa mambo ya wazi na uhakika sana ya kisiasa CCM, kulingana na mikakati na mipango ya muda mrefu na muda mfupi, iliyowekwa na chama kwa mkoa wa Dar es salaam...
hata hivyo,
siri kuu ya yote hayo ni moja tu.
ni mafanikio makubwa, halisi yasiyo na kifani, ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya ccm kwa ya mwaka2020-2025.
Chama kiliahidi wananchi mahitaji yao muhimu kadha wa hadha na kimetekeleza na kutimiza ahadi hizo kwa sehemu kubwa, kikamilifu kwa umahiri, uaminifu, ubora na wakati muafaka....
mathalani,
miradi uhakika ya maji, elimu, afya, mikopo, masoko, miundombinu, umeme, biashara, usafirishaji, ulinzi na usalama wa watu, mali na makazi yao, ni madhubuti, uhakika na wa kuaminika ni baadhi tu ya mambo yaliyoahidiwa na kutekelezwa kikamilifu...
Lakini pia,
kukamilika kwa miradi mikubwa ya kimkakati ya SGR na bwawa la mwalimu nyerere, kumechochea zaid, kuimarisha na kuleta ahueni kubwa na upatikanaji wa huduma za muhimu sana za usafirishaji wa bidhaa na watu, lakini pia na umeme wa kutosha na wa uhakika kwa wakazi wa mkoa wa Dar es salaam na vitongoji vyake kuutumia katika kazi na matumizi yao ya uzalishaji, usiku na mchana...
katika hali jiyo,
kuna sababu hata moja kweli kwa wapinzani kunyakua hata jimbo moja tu dar?
kwa ujumla,
Mkoa wa dar es salaam una majimbo ya uchaguzi 10 ambayo ni pamoja na Jimbo la Ilala, Kawe, Kibamba, Kigamboni, Kinondoni, Mbagala, Segerea, Temeke, Ubungo na Ukonga...
pima tu nguvu, uwezo na ushawishi wa kisiasa wa wabunge wa majimbo hayo, halafu linganisha na waupinzani utaona hakuna hata moja wa kutikiswa na Upinzani...
narudia kukuhakikishia ndugu mwanafamilia wa JF kwamba, hakuna Jimbo hata moja kati ya hayo niliyoyataja itakwenda upinzani, na uchaguzi mkuu ujao utakua ni miongni mwa chaguzi Huru, za Haki na za Wazi zaidi kuliko, chaguzi nyingine zozote zilizowahi kufanyika Duniani...
usipange kukosa kushiriki uchaguzi huo muhimu sana...
Mungu Ibariki Tanzania,
Kidumu Chama Cha Mapinduzi π