Kwa hawa Madaktari huko mbeleni tutapata tabu

Kwa hawa Madaktari huko mbeleni tutapata tabu

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Sabato NJEMA!

Kuna madaktari waliotokea moja Kwa moja Kidato cha Sita kwenda kusoma MD, na wapo ambao wametokea Diploma(Clinical Officer, CO) kwenda kusomea MD.

Kiukweli nimeshtushwa mno baada ya kukutana na Baadhi ya Madaktari watarajiwa wasomao MD na wengine waliomaliza CO.

Mambo yaliyonishtua;

1. Hawajui Lugha ya kingereza.
Kuna kipindi nilifika Pale Mloganzila ambayo Kwa wasioijua ni sehemu ya Hospitali ya taifa ya Muhimbili ambayo kimsingi madaktari wake inatakiwa wawe vipanga na wenye uwezo Mkubwa.

Madaktari waliomafunzoni walinishtua Sana Kwa kingereza Chao kibovu kilichowafanya mara Kwa mara kucheka CHEKA Kwa aibu.

Sitaki kuzungumzia Ma-CO, ambao wengi wao nao kingereza kinawapiga chenga.

Kuna watu watasema, kingereza sio muhimu kwani ni lugha Kama lugha zingine.
Kumbuka materials nyingi za Taaluma ya Udaktari zipo katika Lugha ya kingereza, kutokujua kingereza kutamfanya Daktari kutokuwa mahiri.


2. Clinical officers wa Zama hizi wengi wao sio mahiri, hawako competent katika Taaluma Yao.

Nikikutana na wahitiu wa Diploma ya Clinical officer katika Stori nikiwasabahi nikawauliza mmoja mmoja aelezee concept ya Physiology, mwingine aelezee concept ya anatomy, na mwingine aelezee jinsi damu inavyozalishwa ndani ya Mwili WA mwanadamu.
Unajua hizo ni concept ndogo Sana ambazo hata mwanafunzi wa Kidato cha nne na sita wanaweza Kueleza.

Lakini wakaishia kubwabwaja.


Ukienda baadhi ya Hospitali, madaktari hawajui ku-take patient History, baadhi Yao wanakulazimishia vitu ambavyo havikuumi.

Na hapa nazungumzia madaktari Vijana. Unakuta kijana CV kubwa lakini uwezo unatia Shaka.

Hakuna kitu kinakera Kama uende Hospitalini alafu ukute Daktari anauwezo mdogo katika Fani yake, yaani ukimsikiliza unagundua kabisa hapa hamna kitu.

Ni Sawa na Mwanafunzi afundishwe na mwalimu kilaza, yaani inakera Sana.

Ushauri wangu, siku hizi ukienda Hospitalini kuwa Makini Sana, madaktari wa siku hizi sio wakuwaamini 💯 hasa hawa Vijana.

Serikali iangalie Kwa umakini hivi vyuo vya Kati ambavyo ongezeko lake limekuwa kubwa.

Kuna watu hawatanielewa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
 
Kuhusu Kiingereza, hilo ni janga la kitaifa [endapo kama unaithamini lugha hiyo].

Kiingereza hicho kibovu unachodai, kinaakisi uwezo wa Watanzania walio wengi.

Watanzania walio wengi lugha hiyo inawapiga chenga.

Hivyo hamna cha ajabu hapo. Watanzania kuongea Kiingereza kibovu ni jambo la kawaida sana.

Si ajabu hata wewe mwenyewe huongei Kiingereza kizuri kilichonyooka.

Just sayin’.
 
Kuhusu Kiingereza, hilo ni janga la kitaifa [endapo kama unaithamini lugha hiyo].

Kiingereza hicho kibovu unachodai, kinaakisi uwezo wa Watanzania walio wengi.

Watanzania walio wengi lugha hiyo inawapiga chenga.

Hivyo hamna cha ajabu hapo. Watanzania kuongea Kiingereza kibovu ni jambo la kawaida sana.

Si ajabu hata wewe mwenyewe huongei Kiingereza kizuri kilichonyooka.

Just sayin’.

Mkuu Mimi siongei kingereza kilichonyooka (Fluent)
Ila nikizungumza Kwa Watanzania wengi huona kimenyooka 😀😀kutokana na wengi wao hawajui vizuri.

Mimi nazungumza kingereza Kwa level ya kawaida

Sasa Watanzania wengi hata Basic English hawawezi.

Kuongea Kwa dakika tano tuu kazi
 
Mkuu Mimi siongei kingereza kilichonyooka (Fluent)
Ila nikizungumza Kwa Watanzania wengi huona kimenyooka 😀😀kutokana na wengi wao hawajui vizuri.

Mimi nazungumza kingereza Kwa level ya kawaida

Sasa Watanzania wengi hata Basic English hawawezi.

Kuongea Kwa dakika tano tuu kazi
Basi usishangae sana kuona kuna madaktari hawana uwezo wa kuongea Kiingereza kizuri/ kilichonyooka.

Ndo hali halisi ya Watanzania walio wengi.
 
Kama daktari anaweza kuokoa maisha kingereza kinasaidia nini?, Nenda China, urusi, Spain, uarabuni, uone Kama kuna mtu anahusudu kingereza.


Hakuna Daktari wa kichina na kiarabu asiyejua kingereza wadanganye hao hao wajinga.

Hao warusi ukiona hajui kingereza basi ujue anajua ki-spain au kireno.

Nenda Dubai, Qatar, kote huko
 
Ni muhimu lakini sio lazima Mkuu.
Ulazima wake kwenye udaktari ni upi? Wakiwa wanawatibu wagonjwa huwa wanawasiliana na hao wagonjwa kwa lugha ya Kiingereza?

Imeandikwa wapi kwamba kwenye udaktari Kiingereza ni lazima? Kuna sheria? Muongozo?

Nijuze nami nipate kujua.
 
Kama muda karibu wote unaongea Kiswahili (98%), Kiingereza 1%,halafu utegemee uongee English safi kama mganda itakuwa ndoto za mchana, au utegemee mtu anayeishi mjini ambaye muda wote anazungumza Kiswahili hawezi kuongea kilugha kilichonyooka kama mtu wa kijijini, lugha ni kuifanyia mazoezi haipimi kiwango cha elimu
 
Hakuna Daktari wa kichina na kiarabu asiyejua kingereza wadanganye hao hao wajinga.

Hao warusi ukiona hajui kingereza basi ujue anajua ki-spain au kireno.

Nenda Dubai, Qatar, kote huko
Mimi naongea kwa experience, wewe unatumia uzoefu wa ubishi, ngoja nikuache
 
Na Hilo la kuwa competent unalipi la kusema?
Suala la uwezo ni muhimu sana. Daktari asiyeimudu kazi yake hafai.

Lakini suala la uwezo na suala la kuongea Kiingereza ni vitu viwili tofauti kabisa.

Kuongea Kiingereza kizuri au kibaya, hakuna uhusiano wowote ule wa moja kwa moja na uwezo wa daktari katika kazi yake.
 
Ulazima wake kwenye udaktari ni upi? Wakiwa wanawatibu wagonjwa huwa wanawasiliana na hao wagonjwa kwa lugha ya Kiingereza?

Imeandikwa wapi kwamba kwenye udaktari Kiingereza ni lazima? Kuna sheria? Muongozo?

Nijuze nami nipate kujua.

Materials za Taaluma ya Udaktari nyingi zipo Kwa lugha ya kingereza.

Na kutokana na mabadiliko ya magonjwa na madawa Udaktari kila siku unahitaji ku-update.

Huwezi kuwa Daktari mahiri bila kujua Lugha ya kingereza
 
Back
Top Bottom