Kwa hawa watu wanaobadili dini, Ndugu na wanafamilia wa dini tofauti wajiandae kwa lipi kwenye mazishi yao?

Kwa hawa watu wanaobadili dini, Ndugu na wanafamilia wa dini tofauti wajiandae kwa lipi kwenye mazishi yao?

R-K-O

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2023
Posts
482
Reaction score
2,178
MKASA WA BINTI MKRISTO ALIEBADILI DINI:

Nimeshawahi kushuhudia mvurugano wa hali juu kwa suala hili kutoka kwa familia za wanandoa, Bint wa kimakonde Mkristo alikubaliwa na wazazi wake abadili Dini ili aolewe na kijana Muislam, Shida ikaja pale bint alipofariki, ndugu za mume wanataka kumzika yule bint kwakufuata taratibu za kiislam kwasababu mauti yamemfika akiwa Muislam, Baba na mama wa yule bint hawakuleta shida ila ndugu zao (wanafamilia)wakakataa kabisa na walikuwa tayari kususia msiba iwapo atazikwa Kiislam.

Baba na mama wa yule bint hawakuwa tayari kutengana na ndugu zao (wanafamilia Wakristo)sasa afanyeje ili aweze kushirikiana na nduguze wakristo kumzika bint yake!?

Alichofanya yule baba ni kuwakabili ndugu wa mume wa mwanae ambao ni waislam na kuwaeleza waziwazi kwamba haitawezekana mwanangu kuzikwa kwa taratibu za kiislam kwahiyo basi yule Ustadh aliemsilimisha mwanae aende akamsilimue wamzike!

Hili kauli aliitoa kwa lafudhi yake ya Kimakonde"Alienchilimicha mwanangu aje anchilimue tunnjike" Waislam wakakataa kwasababu suala la Dini mwenye mamlaka yakuchagua ni muhusika mwenyewe ambae ameshafariki na amefariki akiwa Muislam.

Hatimae maiti haikuzikwa na kesi ikapelekwa Mahakamani.
..................................................................................

Sisemi kwamba watu wasibadili dini bali wakae na kutulia kabla ya kuchukua uamuzi huo,

Nimekuwa nikiona mara kadhaa familia / ndugu wanaingia migogoro na makanisa / misikiti ya kuwania maiti ya mtu aliebadili dini, inafikia mpaka kufikishana mahakamani ama maiti kufukuliwa kabisa kuzikwa kwengine, kuna muda hugeuka vita kabisa, Ningependa hapa tupeane elimu zaidi

  • Mkristo kabadili dini kuwa muislamu huku ndugu na wanafamilia ni waisalam (Mfano mchezaji wa Yanga Mzize)
  • Muislamu kabadili dini kuwa mkristo huku ndugu na wanafamilia ni waisalam

Siku ikitokea aliebadili dini kafariki, hii inaathiri vipi mazishi hasa kwa wanafamilia na ndugu ?

1. Kutakuwa na vurugu za kugombania maiti kati ya wanafamilia/ndugu dhidi ya kanisa / msikiti ?

2. Maiti itazikwa kwa misingi ya dini ipi

3. Urithi ?

4. Washiriki katika misiba wanawake wataruhusiwa endapo akizikwa kiislam?

5. Atazikwa kwa sanda ama jeneza

6. Shughulu nyingine je?
 
Hiyo ni mipango ya familia husika na jinsi watakavyo amua.

Huwezi ku conclude kwa namna gani mtu huyo atazikwa.

Pia anaweza zikwa na serikali pia.

Ukisha kufa umekufa wala huna ufahamu tena wa yatakayo amuliwa hata ukitupwa msituni uliwe na wanyama wala hutajua.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Uzuri wa kifo haijalishi umezikwaje, hutorudi tena kwenye uhai.

Hao ndugu hata wakipigana jinsi gani ya kukuzika umauti wako hautobadilika.

Mambo ya mazishi hayana athari yeyote kwa maiti.
 
Hiyo ni mipango ya familia husika na jinsi watakavyo amua.

Huwezi ku conclude kwa namna gani mtu huyo atazikwa.

Pia anaweza zikwa na serikali pia.

Ukisha kufa umekufa wala huna ufahamu tena wa yatakayo amuliwa hata ukitupwa msituni uliwe na wanyama wala hutajua.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
Hakuna mtu asiejua kwamba kuna maiti zinazikwa na serikali

Ndio maana nimesisitiza inapotokea kwamba ndugu / familia wanataka kukuzika je wajiandae na changamoto zipi.
 
  • Mkristo kabadili dini kuwa muislamu huku ndugu na wanafamilia ni waisalam (Mfano mchezaji wa Yanga Mzize)
  • Muislamu kabadili dini kuwa mkristo huku ndugu na wanafamilia ni waisalam

Siku ikitokea aliebadili dini kafariki, hii inaathiri vipi mazishi hasa kwa wanafamilia na ndugu ?


1. Kutakuwa na vurugu za kugombania maiti kati ya wanafamilia/ndugu dhidi ya kanisa / msikiti ?

2. Maiti itazikwa kwa misingi ya dini ipi

3. Washiriki katika misiba wanawake wataruhusiwa endapo akizikwa kiislam?

4. Atazikwa kwa sanda ama jeneza

3. Shughulu nyingine je ?
Nikipata nafasi ya kuwashauri watu nitawashauri wasibadili dini zao.. Inatesa sana na inayumbisha familia ndugu hata koo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nikipata nafasi ya kuwashauri watu nitawashauri wasibadili dini zao.. Inatesa sana na inayumbisha familia ndugu hata koo

Sent using Jamii Forums mobile app
Well said Mimi nina likaka langu lilikuja dar likaoa mzaramo likabdili dini lilipofiwa yule mke tulipata matatizo ya wapi azikwe ,ni udhaifu mkubwa kubadili dini

USSR

Sent from my TECNO B1c using JamiiForums mobile app
 
Nikipata nafasi ya kuwashauri watu nitawashauri wasibadili dini zao.. Inatesa sana na inayumbisha familia ndugu hata koo

Sent using Jamii Forums mobile app
Upele umepata mkunaji, Mkuu tafadhali sana, tunaomba hii elimu hasa ukizingatia upo muda mrefu kwenye industry hii ya mazishi, Tunaomba jamiiforums tufaidike na uzoefu wako tupate elimu mapema kabla ya kufanya maamuzi ama kuwashauri wengine juu ya madhara ya hapo mbele,

Tunakuomba Mr Mshana utuwekee uzi
 
Well said Mimi nina likaka langu lilikuja dar likaoa mzaramo likabdili dini lilipofiwa yule mke tulipata matatizo ya wapi azikwe ,ni udhaifu mkubwa kubadili dini

USSR

Sent from my TECNO B1c using JamiiForums mobile app
Mke rumezoea anazikwa kwao, ilikuwaje ?
 
Hii huwa najiuliza sana ila kuna wakati naacha tu iwe itakavyokua Wakija kumchukua au akaamua kurudi dini yake nitaangalia tu maana muda wa kuvurugana na watu Sina kabisa!
Imani za kidini ni ngumu sana wakati mwingine kuliko hata uchawi wa mababu zetu.
 
Back
Top Bottom