Kwa hili alilolifanya Diamond, litamgharimu sana katika safari yake ya kimuziki


Mie nipo kipenzi, just nimechoka kujibizana na viumbe wazito, napita kimya kimyaa....
 
Last edited by a moderator:

Msanii bila mashabiki wapi na wapi! sisi ndo tuliokuwa tunampigia kura,vijana wote wa mtaani na kwenye mavyuo wakiisha jua tu chalii ni msaliti mambo yake yameisha.kwenye hii miezi miwili ataonyesha true colour zake na watu wote watamjua,na mambo yake itaishia hapo..Things will never be the same again..
 
Huyu dogo naona waliompa kazi ya siasa hawakumfunda cha kuongea au wanampoteza.

Muda wake wote hivi sasa imekua imekua nikupost propoganda za kichochezi thidi ya kile anachokiita "UKASKAZINI" kwenye siasa.

Napenda nimshauri tu kuwa kuna maisha baada ya uchaguzi na bado ana safari ndefu katika maisha yake na sanaa yake ikilinganishwa na hao "wanaomtumia" hivi sasa ambao wako saa 12 jioni.

Siasa za uchochezi zitaku-cost siku moja dogo.
 
FACTS.
Kihistoria, hakuna msanii anayejihusisha na siasa akiwa kwenye kilele cha taaluma yake akafahulu. Diamond anaelewa vibaya sifa zake kuwa si za siasa bali ni usanii. Hasije akafikiri anaweza kucommand politics kama entertainment. Let him stick to music na awaachie wanasiasa siasa zao.
NB. Ajuwe politics is dirty game.
 
ndiyo maana anazoazoa malaya huyu kijana......mtoto mwenyewe wa kupakaziwa..
hana jipya aendelee na malaya wenzake siasa ina wenyewe!!
 
Unaota ndoto kwani ww si una chama unachoshabikia km huna la kuongea kaa kimya hilo ndo chaguo lk km ww ulivyo na chaguo lako

Sijui kama mnaelewa maana ya kuitwa kioo cha jamii. Umaarufu unaambatana na umuhimu wako katika jamii,kuwa kwa kauli yako waweza kugeuza imani ya watu na kufuata mwelekeo mwingine. Hivyo wakati mwingine yapo mambo uyapendayo yanabaki moyoni mwako ili usivuruge jamii.
Mfano, sasa hivi zipo sheria za ushoga huko majuu wanalazimisha zitumike huku kwetu nasi kwa maadili yetu tunazikataa. Lakini jee ni kweli hakuna wapenda ushoga?
Sasa wengi tuna pinga, Lakini ikitokea mhe Rais yeye binafsi anapenda na akasimama hadharani kutetea tutasema huo ni uhuru wake binafsi asiingiliwe? Mnadhani hilo litaleta repercussion gani kwa taifa kuhusu ushoga?
Majibu mnayo.
 
Yani na wewe unaamini hizi toilet papers magazeti ya shegongo ni toilet papers Lowassa
Hana mda mchafu wa kumake deals na vigalula
Kama domo anatafuta kick kwenye majina makubwa Lowassa mwenyewe anajaza mahali popote bila nguvu ya mtu yeyote Lowassa ni kkama Michael Jackson na domo ni kama ashangedere wapi na wapi??????

Hao waliomdanganya na kumfikirisha kama ana ushawishi wa kuwapigisha WATANZANIA kura kwa ccm wamempoteza domo hana influences zozote kwa WATANZANIA zaidi ya kukata viuno na hiyo ndio ajira yake kama ni ushawishi atawashawishi malaya zake.
 

Tatizo watu wengine ufikiri wao ni tofauti na wako hawaelewi maana ya vyama vingi kl mtu ana upande wake na maisha yanaendelea
 
Duh huyo Diamond nae ni binadamu kama wengine anautash wake jamani. Kwa hiyo unataka asapoti UKAWA kwa vile mashabiki wake wako ukawa. Hii sasa kuingilia utashi wa mtu duh

Umeongea point tatizo hao hata ueleze mpaka kukuche madhali hashsbikii Ukawa hawatakuelewa jana Uwoya alikuwa kwa Lowasa ny ni utashi wk ana haki ya kuchagua anapotaka
 

Usinichekeshe mbona wewe unajionyesha dhahiri sy CCM umeshindwa kujizuia na wao wasanii wana roho na nyongo km wewe acha ubinafsi
 

We kama nani hadi useme things will never be the same again???? Huongelei fact unaleta blah blah tu, ulikuwa ukimpigia kura pekeako? And how far are you sure kuwa wewe na wenzako mkiacha kumpigia kura wengine pia wataacha? Unajua idadi ya mashabiki damu wa diamond?
bado naziona hizi ni ramli tena ramli angushi.
 
Sitoacha kumpigia kura diamond wangu na sitoacha kumpa sapoti yeyote ile anayostahili kutoka kwangu kama shabiki wa damu.Natambua ni haki yake ya msingi kufanya hivyo na siwezi kumpangia cha kufanya.

Mashabiki wa diamond tupo na tutaendelea kuwepo

Ni kweli mashabiki wa diamond wanajua wanalofanya watabaki kuwa mashabiki wk na ikiwa kuna tofauti kwenye siasa hivyo ni vitu tofauti kabisa jamani watu wanapayuka mishipa ya shingo inawatoka kisa hayupo ukawa
 
Wolper mbona hamjamsema? Au anachofanya siyo kampeni kwa Lowassa?

Wolper na Ezekiel mpaka cake wamepeleka kuonyesha MAHABA yao kwa Lowasa hawajafanya makosa ni haki yao km ilivyo kwa Diamond tena Lowasa kawaomba wamfanyie kampeni ni sahihi tu wala haina shida ndiyo upande waliochagua wl hatutakiwi tuwakwaze
 
hahahaha mkuu angalia kama followers wake wamepungua.... hahaha wameongezeka from 944k to 945k hujapunguza kitu!!!!!!!

Wewe ndo huelewi unachokifanya siasa imeshaharibu ubongo wako sasa ulivyojitoa ndiyo imempunguzia nini tuambie followers wake sasa hivi wapo wangapi utakufa kwa presha
 

Verry true
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…