Uchaguzi 2020 Kwa hizi sababu Lissu anaweza kukosa sifa za kupeperusha bendera ya CHADEMA kwenye kumpa changamoto Mgombea wa CCM

Hivi hofu juu ya Lissu ni ipi mpaka mnahangaika naye kiasi hiki? Mnadhani mnamchafua kumbe ndio kwanza mnamjenga na kumtangaza zaidi

Jr[emoji769]
Wenzetu hofu inawahangaisha sana. Hawajiamini pamoja na tume ya uchaguzi, kanuni za uchaguzi, na dola kuwa vyote vya kwao. Shida iko wapi? Wasubiri 99.999% ya ushindi. Wanahangaishwa na madhambi wanayofanya.
 
Wenzetu hofu inawahangaisha sana. Hawajiamini pamoja na tume ya uchaguzi, kanuni za uchaguzi, na dola kuwa vyote vya kwao. Shida iko wapi? Wasubiri 99.999% ya ushindi. Wanahangaishwa na madhambi wanayofanya.
Nyie mtulie siku mkishinda utafanya hivyo
 
Membe tunawapa awaongeze nguvu Mkuu walau mpate kura laki moja maana huu mwaka mtapigwa asubuhi
Membe c anashindana na jiwe ccm, Nyalandu au msigwa hao wengine ni watia nia ila mgombea ni mmoja Lissu na chadema inachukua majimbo yote safari hii
 
Umesshau alivyokuwa akikesha usiku na mchana kuitukana Nchi yetu kwa kuwanyima Mabeberu madini ?

Nchi hii ina kipi cha kutukanwa usiku na mchana? Hiyo mikataba ya madini mmeingia na waswahili mpaka useme wazungu walikuwa wanamngojea Lissu ndio waanze kuyapata? Tuwekee hiyo mikataba ya sasa ya hao wazungu, ili tuone saini ya Lisu ndio tujiridhishe yeye ndio kawatetea mpaka wamepata hayo madini.
 
Sijaambiwa na mtu nimesoma tathimini za awali na za sasa za ndani zilizofanyika

Ni wazi Chadema haina jimbo hata moja
Tunatunza huu uzi man. Uzuri wake huwa hazifutwi hizi
 
Kwa Tanzania ukimtukana Baba wa Taifa lazima mikosi na laana zikuandame

Tujifunze tusiwe km Lissu kuepuka laana na mikosi
Acha ujinga mkuu, huyo baba wa Taifa hakutaka kuabudiwa kama mnavyo fanya
 
Mh. TL akitaka aupate urais ni kwamba aje na sera nzuri kama zile za 2015. Zilikuwa zimekaa vizuri shida yangu nayoona ni kwamba ataanza kutwambia mara tudai katiba mpya wakati hata ile ya zamani iliyopo hatujamaliza kuisoma. Hapo nakwambia hata wanaoishi vijijini hawatamuelewa. Kule vijijini wao wambie maji, umeme, barabara n.k.
 
Kulipwa mshara hiyo ni haki yake,nazungumzia serikali kumtibu kama ilivyo mtibu J.ndugai
 
Hivi kuna Mtanzania anaweza kumpigia kura huyo ropokaji ?
 
Hatumwabudu pia Hatuwezi kumtukana na kumdhihaki km alichofanya lissu ni kujitakia laana kule
Acha ujinga mkuu, huyo baba wa Taifa hakutaka kuabudiwa kama mnavyo fanya
 
Sawa kabisa usibadili I'd Mkuu baada ya Uchaguzi
Niko hapa tangu 2007. Sijawahi kimbia hoja wala kubadili ID wala sina multiple ID man. Kwamba wapinzani wakose hata diwani mmoja? Unless muwaue kwanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…