Kwa hoja ipi watu wanaamini kuwa taifa la Israel ni taifa la Mungu ingalikuwa ni taifa linaloishi kwa Upanga?

Soma King James Version ambayo huwa haina ukakasi sawa na hizi Biblia nyingi za siku hizi zinazochakachuliwa na Manabii wa uwongo.

Waebrania 13:8

"Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele."

Yakobo 1:17

"Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka."

Mungu hajawahi kubadilika, huwa habadiliki na hatabadilika kamwe!

Mathayo 5:17

"Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza."

Yesu alisema hakuja kubatili torati bali kutimiliza(perfection/kuboresha) ktk utimilifu wala si (ukamilisho/compliment) wa sheria.

Mungu mwenyewe aliyekukataza usizini ndiye aliyekukataza usiibe na hakuna hata dhambi aliyoihalalisha wala kuitetea kuwa ni ndogo kuliko zingine.

Sisi Binadamu ndiyo huwa tunabadilika lakini kamwe! Mungu muumba mbingu na nchi huwa habadiliki milele zote, Amina.
 
Mkuu ndio maana tangu awali nikasema ERRORS EVERYWHERE bora mtu akae na MUNGU moyoni mwake afanye mema tu.Mungu kukaa pembeni maana yake kamuacha afe Yesu kama binadamu.Mkuu nisamehe kwa kuwa sipendi kuquote Ila katika biblia hizo aya zinapingana na nyingine (ERRORS).Wakati Yesu anapaa alisema anaenda kwa baba yake ambaye ni baba yetu hivyo filipo alimuona baba yupi(yesu anayejiita baba au baba wa mbinguni anayefuatwa na Yesu wakati anapaa?(still errors))

Cha ajabu hakuna sehemu yoyote ile ambayo Yesu alisema yeye ni Mungu.Alisema yeye ni baba in metaphor but Tayari nishaonyesha hiyo error hapo juu.Narudia neno "Mungu".Aliyesema Yesu ni Mungu ni Paulo.Sasa tumsikilize nani muhusika au mtu baki?

Msije kusema Yesu ni Mungu kwa sababu alisema baba yu ndani yake... wakati kuna aya zinapinga na kuonyesha baba ni mwingine na Yesu ni mwingine.
 
Wazungu katikati ya jamii za Waarabu,propaganda ni mbaya sana tena ikikaaa akilini ndio inakuwa zaidi ya tatizo.
 
Ebu rudia kusoma vizuri nilivyo andika. Mm sijasema yesu ni Mungu bali nimesema alikuwa anatembea na uwepo wa Mungu ndani yake
 
Mkuu kubadilika kwa namna gani physically au logically?

Mkuu mimi siamini kwamba Yesu ni Mungu kwakua aya zinahitilafiana.Nitaamini vipi King James version bible ni sahihi wakati agano la kale liliandikwa kwa Hebrew language.Je Kama wao wamepotosha kwa utafsiri usio sahihi?And of course wamepotosha katika song of solomon 5:16 kuna maneno "all together lovely" ilhali in Hebrew the words were pronounced Muhhamad'im the name Muhhamad the last prophet and 'im is the plural of respect same as Eloh'im Eloh referring to God in Hebrew. Kuna video ila Sina ujuzi wa kuiweka hapa inaonyesha Jewish priests wakitamka kama Muhhamad'im.Hivyo wakristo mtaendelea kumpinga Muhhamad ilhali mmepotoshwa.
 
Nitubu kwa kiumbe wa kufikirika YHWH/Elohim/Jehovah
Mmoja wa Miungu wa Summeria alioabudu Abraham na Israelites
Hapana huo Ujinga siwezi kuufanya kamanda wangu,

Halafu unaqote kitabu Cha ufunuo wa Yohana hivi wewe unamjua aliyeandika hicho kitabu akiwa mfungwa pale kisiwa Cha Patmo na unajua Alikua anamlenga nani?
Unajua Huyo mnyama aliyezungumziwa humo au unekariri tu bila kujua,
Sasa huo ufunuo wa Yohana unanihusu Nini Mimi na wakati Huyo mwandishi alimwandikia mfalme Nero na mama yake Agripa Kwa sababu walikua wanaua wakristo Ili kufikisha ujumbe Kwa waumini akatumia Lugha ya mafumbo kufikisha ujumbe
Na haijulikani mwandishi wa hicho kitabu ni Yohana Gani!
Prove me wrong kamanda!
 
Aisee kumbe ndio hvyo!? Sasa mbona kina fanana na kitabu cha Danieli cha agano la kale?
 

UFUNUO 1

1Huu ni ufunuo aliotoa Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa awaoneshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe mtumishi wake Yohane mambo hayo.

2 Naye Yohane ameshuhudia yote aliyoyaona kuhusu ujumbe wa Mungu na ushahidi wa Yesu Kristo.

UFUNUO 22

18 Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: Mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki.

19 Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uhai, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki.

20 Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: “Kweli naja upesi.”

Amina. Njoo Bwana Yesu!

21 Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amina.
 
Ulisema Yesu ni Mungu alafu baadae umesema Yesu sio Mungu bali alikua anatembea na Mungu.
Mm ndio nilijibu kimakosa. Nilijibu kwa kumaanisha kwel ni mwana wa Mungu,
Nahis nilisoma vibaya swali
 
e.

Ndugu Ephraem_EE, nakubaliana kama anavyonena hapo juu Mpendwa Patra31.

Kumbuka hapo Wayahudi walikengeuka Maandiko Matakatifu ya Mungu kwa kugeukia miungu yao waliyokuwa wanaiabudu awali lakini baadhi yao walishafunguliwa nuru ya injili ya Yesu Kristo kupitia mahubiri ya Nabii Petro.

Hivyo waliona warudi tena upya kuwapotosha wale waliokuwa wamepata injili ya kweli kuhusu Yesu Kristo kwa kuwadanganya kuwa ikiwa hawatatahiriwa basi watakuwa hawajaokoka ktk ukamilifu wa kumjua Mungu ipasavyo.

1Korintho 7:19.

"Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu."

Wagalatia 6:15.

"Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya."

Warumi 2:28-29.

"Kwamaana Myahudi wa kweli si yule anayeonekana kwa dalili za nje, wala tohara ya kweli si kitu cha kimwili. Myahudi wa kweli ni yule aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ya kweli ni jambo la moyoni, jambo la kiroho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa jinsi hii anapata sifa kutoka kwa Mungu, wala si kutoka kwa wanadamu."
 
We unajua kwanini Martin Luther alijitenga na hao Jamaa?

Ndugu usiwe unasoma Biblia kama gazeti tu, unapaswa kumwomba Roho Mtakatifu akufundishe na kukuongoza namna ya kukabiliana na mafumbo ili uelewe kwa kina zaidi.

Hivi unadhani Yesu aliposema "msiwape mmbwa chakula cha watakatifu" alimaanisha nini?

Au najisi unaelewaje hilo neno ktk maana ya kiroho?

Mungu akusaidie unapozidi kujifunza Maandiko Matakatifu yake ili uweze kutafakari zaidi ukuu wake na kuelewa kwa kina stahiki.
 
Daah makubwa.Huyo roho mtakatifu wa kufikirika baki naye.Mungu aliyeniumba yupo pamoja nami na yeye ananionyesha mema na mabaya na amenipa akili ya kutambua.Hamtakaa mniaminishe kuhusu roho mtakatifu ilhali mnanena makorokocho mnayoyaita 'kunena kwa lugha'.

Hivi mnayemuita Mungu baba ana mwili wa nyama?yeye sio roho?yeye sio mtakatifu? Kwa hiyo Mungu baba sio roho takatifu?

Mungu wangu ni mmoja akaaye ndani yangu na kuniongoza.Mimi ninafuata 30% ya Biblia,30% ya Quran,30% ya mahitaji ya moyo wangu na fikra zangu 10% ya sheria na taratibu za jamii husika.

Mimi sio mtumwa wa kifikra na kujazwa imani potofu!!!
 
Aisee kumbe ndio hvyo!? Sasa mbona kina fanana na kitabu cha Danieli cha agano la kale?
hata havijafanana hata Kila kitabu kina ujumbe wake Kwa wahusika wa wakati huo,unaona kama kuna ufanano Fulani,
Kitabu Cha Daniel kiliandikwa enzi za kina Nebuchadnezzar kikizungumzia mambo na falme za zama Hizo huko Babylon na Mesopotamia era!
Ufunuo wa Yohana hajulikani mwandishi wanaedai ni Yohana mwanafunzi wa Yesu ni waongo ila Huyo jamaa alikua na ifanano wa jina tu na ni enzi za mfalme Nero na mamaye Agrippa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…