Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 20,561
- 24,428
Sio Africans wote.Umeelewa swali langu ? Maana hujajibu swali unaingelea habari za utumwa. Swali langu liko hapa, suala la Afrika kuwa Taifa Teule umelipata wapi ?
Kingine unaonekana unatafuta na hujui unachokitafuta utakipata wapi ? Hili ni tatizo kubwa sana. Usikute hata asili ya tamko "Afrika" hujui ni nini ? Hili ni tatizo kubwa sana.
Nasuburi jibu la swali langu.
"Kanuni ya kuishi duniani ni kuharibu au kukatisha uhai wa kiumbe kingine ndo u-survive wewe, hiyo ni asili ya ulimwengu tunaoishi sisi."
Kwahiyo Mungu alileta kanuni ya usiue huku duniani huku yeye mwenyewe akiwa amewaruhusu watu wake waue kwasababu kanuni ya ulimwengu wetu huku ni ili u survive inakupasa uue! Sasa huoni Kama hapo unaleta mkanganyiko..? Na anavunja sheria zake mwenyewe au yeye kukuruhusu kuvunja haina shida..?
Ohoo! Hii mpya Sasa! Mkuu hii historia umeitoa wapi na hao waisrael weusi wapo wapi au ndo wale black America..🤣Sasa ukirudi kwenye kumbukumbu la Torati utakutana. Na baraka na laana kwa hawa wana wa Israel kama ambayo Musa aliwaambia ikiwa wataenda kinyume na Maagizo ya MUNGU na wakaapia nadhani.
Basi wote tunajua kuwa hawa jamaa hawakufuata vile waliambiwa so kilichowapata ni Laana. Sasa kipindi Yesu yuko pale ni kabila YUDA aka NEGROES kwa asilimia 99% ndio alikuwa PALE na kumbuka wao ndio walipeleka mashatka ya uongo kwa pilato na wakasema Damu yake iwe kwao na vizazi vyao. So pale. Walijivika vizuri yale. Malaana yote ya kwneye kumbukumbu la torati. Na ukisoma zile laana vizuri utaona Mungu anawaambia kuwa "nitawarudisha Misri lakini this time mtaenda na MERIKEBU" YAANI ATAWARUDISHA UTUMWANI NA kipindi wanaoingia Misri kipindi kile si walitembea tu sababu Israel. Ilikuwa ni kaskazini. Mashariki ya Africa kabla wazungu hawachimba suez kanal. Ili. Kuhalalisha uongo wao kuwa wale. Jamaa ni wazungu. So kilichotokea ndio Hiko NEGROES WALIRUDISHWA UTUMWANI KWNEYE CARIEBANS... USA etc kwa MERIKEBU mpk 400 hundreds years ndio watakuwa huru tena. Nadhani bado Haijatimia. So Ile transatlantic slave trade ilikuwa yao Ile. Na kwa kuwa walikuwa blacks kama sisi ilikuwa ngumu kuwajua so ndio wakawa wanaingia deal na wachifu hawa babu zetu sisi watoto wa Ham wawaonyeshe wageni walishuka huku ni akina nani the machifu kwa uoga wengine kwa KUPEWA pesa waliwauza kirahisi. So wazungu ili kutuzuga na kuwazuga hawa jamaa mpk Sasa Wana msemo wao kuwa Wa Africa walikuwa wanawaza wa afrika wenzao. Kitu ambacho ni Uongo hakuna chief aliyeuza ndugu zake. Bali walikuwa wanawaza wageni weusi kama wao
Mkuu huoni Kama kunakuwa na mkanganyiko kwani Mungu alete sheria ktk mazingira ambayo kuishi ni kuua..??Ulishaambiwa duniani siyo mahali salama kwako kuishi tokea siku ya anguko lako kama mwanadamu kukubaliana na shetani (lord of war/muasi) pale edeni ulipochagua kifo na immediately kizazi cha kaini kikaanza kumwaga damu na ndiyo maana ukawepo mpango wa pili wa ukombozi (kutunukiwa maisha ya milele)
Hivyo tunaposema dunia haiendi pasipo damu shida si Mungu shida ni wewe kumsikiliza yule muasi ambaye aliamishia vita vyake vya kiroho (uroho,uasi,chuki,kujiinua,ushawishi,mauaji na uungwaji mkono) juu ya wanadamu nakusababisha dunia iwe ilivyo, inamaana unapokiri nakufuata agizo la kutokuua mwanadamu mwenziyo na viumbe wasio na hatia (unamsikiliza Mungu) hapo unakuwa kinyume na sheria za utawala na maumbile ya ndani ya dunia(shetani) na hapo kusurvive kwako kutakuwa ni kwa taabu maana dunia ni uwanja wa vita.
Awali ni wazi tuliumbwa na kile sayansi inakiita survival for de fittest (kuishi kwa kukatisha uhai wa viumbe vingine katika kubalance nature na ku-enhance maisha) ila tulipaswa kutovunja miiko ya mzunguko huo kama wafanyavyo wanyama wa mwituni, wadudu na mimea ila kinyume chake binadamu amekithiri kutenda yanayopelekea uharibifu, maangamizi, kubadili asili ya mazingira na kuchochea maovu na ndiyo maana ikabidi kudhibiti yote haya kuwepo na amri 10 zenye malengo makuu mawili kuleta amani na upendo hili kumlinda mwanadamu dhidi ya mitego ya mwovu.
Kama asingesema hivyo basi isingemaanisha kafa kweli kama wanavyokufa wanadamu wengine bali kaigiza kufa hili akisema kafufuka tumwamini. Ila kitendo hicho kinatuthibitishia utimilifu wa maandiko juu ya maisha yake ya kibinahadamu hapa duniani.Kwa hiyo wakati Yesu anakufa Nani alikua anatawala dunia?
Na kwanini wakati anakufa alisema "Mungu wangu Mungu wangu,mbona unaniacha"alafu akasema "ninakabidhi roho yangu mikononi mwako" hii roho ni ya kiMungu au kibinadamu maana Mungu alimuacha? Akashuka kuzimu hivyo Mungu hakushuka kuzimu kwa sababu alimuacha.
Kwa hiyo ndio kusema...?Kama asingesema hivyo basi isingemaanisha kafa kweli kama wanavyokufa wanadamu wengine bali kaigiza kufa hili akisema kafufuka tumwamini. Ila kitendo hicho kinatuthibitishia utimilifu wa maandiko juu ya maisha yake ya kibinahadamu hapa duniani.
Simply kwa kuwa imeandikwa kuwa roho ya ndani ya binadamu ni ile pumzi ya Mungu ambayo huwa ndani yake kama nafsi hai na pindi anapokufa ile roho umrudia Mungu mwenyewe huku mfu (mwili uharibikao) akibaki halivyo pasipo kumbukumbu yeyote mpaka atakapofufuliwa tena kwa mapenzi ya Mungu mwenyewe atoae pumzi ya uhai(roho)
Ukisoma bible kiimla au juu juu tu utaishia kuchanganyikiwa kama wale wanaokoti mistari kama "masikini mpe pombe asahau shida zake" "kunywa kidogo ila usilewe" au "hakuna alichokiumba Mungu ambacho ni najisi" kuhalalisha uovu na upumbavu kwa kula vichafu, kunywa pombe na kutenda anasa.Swali kulikuwa kuna umhimu gani wa kuweka siku ya hukumu ilihali anajua hatma ya kila mtu kabla ajazaliwa? Kulikuwa na umhimu gan wa kumtuma Yesu kuja kujitoa sadaka ili kuokoa watu ilihali anajua kabsa watu wake ata kabla hawazaliwa?
Kwa mantiki hiyo mungu ni gaidi na muonevu kuliko vile tunavyo mzania maana anahukum mtu apate mateso wakati yeye ndio alikuwa ameisha mpangia kufanya hizo dhambi
Yesu alikufa kifo kamili (cha kawaida cha kibinadamu) kama wengine na akafufuka kwa uwezo wa muumba wake siku ya tatu kudhihirisha kuwa hakuna linaloshindikana tukiishi kwa unyoofu alivyofanya yeye na hata maumivu aliyahisi pia kama sisi kiasi cha kuelekea kukata tamaa na akawa akitiwa moyo na pia amenukuliwa akilalamika kibinadamu hii yote ni uthibitisho Yesu akuwahi kuexist duniani kama Mungu bali kama messenger wa kufikisha ujumbe wa Mungu kwetu wanadamu kuwa dunia bila uovu inawezekana.Kwa hiyo ndio kusema...?
Shukrani mkuu.Yesu alikufa kifo kamili (cha kawaida cha kibinadamu) kama wengine na akafufuka kwa uwezo wa muumba wake siku ya tatu kudhihirisha kuwa hakuna linaloshindikana tukiishi kwa unyoofu alivyofanya yeye na hata maumivu aliyahisi pia kama sisi kiasi cha kuelekea kukata tamaa na akawa akitiwa moyo na pia amenukuliwa akilalamika kibinadamu hii yote ni uthibitisho Yesu akuwahi kuexist duniani kama Mungu bali kama messenger wa kufikisha ujumbe wa Mungu kwetu wanadamu kuwa dunia bila uovu inawezekana.
Kuna kitu naomba ninukuhu kwanza
Yohana 14:7-11
⁷ Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona.
⁸ Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.
⁹ Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?
¹⁰ Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.
¹¹ Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe.
Kwa mjibu wa biblia inaoneaha daima yesu hakutembea mwenyewe bali mda wote alikuwa natembea na uwepo wa Mungu ndani yake. Na aliposema "Mungu wangu mbona unaniacha" haikumanisha Mungu hamuoni tena bali Mungu alijiweka pembeni ili kuacha lengo la Yesu kuja dunian litimie. Kwann alisema roho yangu naikabidhi mikononi mwako hapo sijui sasa
Aiseeeee🤔🤔🤔🤔🤔Kumekucha! kumekucha!
Hao jamaa na hekaya zao za Mungu wamewafanya mpaka African kua Brain washed hawaambiliki
Yaani Mungu wao El/YHW/JEHOVAH/Elohim
Ni Mungu mshenzi na mgomvi, katili,uncivilized,mwongo na mwenye ahadi hewa Kwa watu wake
Imagine aliwaahidi Babu zao kina Abraham Kwamba uzao wake utakua mwingi kama mchanga wa bahari😁
Akawaambia Tena Atawapa Kaanan iwe Mali Yao Kwa kupora na ubabe,
Aliwatoa misri utumwani et
anawapeleka nchi ya ahadi yenye Asali na maziwa maajabu akawatembeza jangwani miaka 40 hata hawafiki mpaka wakafa wote
Baada ya miaka 40 ndio wanaanza panga vita ya kupora ardhi ya watu yenye maziwa na asali Kwa kuua raia wote mpaka wanawake na watoto!
Alivyo juha Huyo Mungu wao badala Ile Miaka 40 awapeleke kusini mwa jangwa la Sahara kama huku East Afrika au Zimbabwe sehemu yenye maeneo makubwa na hakuna watu wanaishi akaanza akawapeleka kuvamia mashamba ya watu Kaanan
Stupid God!
Kunani tena?Aiseeeee🤔🤔🤔🤔🤔
Aliyeumba mfumo huo wa maisha ya kiumbe kula kiumbe chenzake ndipo waishi ndiye aliyeleta muongozo wakufuatwa kwa kutambua umuhimu wa muongozo huo kuwepo hili kuvilinda viumbe vyake na mazingira yao.Mkuu huoni Kama kunakuwa na mkanganyiko kwani Mungu alete sheria ktk mazingira ambayo kuishi ni kuua..??
Umejibu vyema. Lakini mkuu mbona huyo Muumba alikuwa pia akiingilia huo uhuru mchache aliowapa watu wa kuchagua mfano ktk yale mapigo kumi ya kule misri biblia imeandika kabisa waziwazi kuwa Mungu alikuwa anampa farao moyo mgumu ili asiwaachie waisrael!,hatimae akaja kumuadhibu nawakati ugumu huo alimpa yeye mwenyewe!.. hii imeakaaje..?Aliyeumba mfumo huo wa maisha ya kiumbe kula kiumbe chenzake ndipo waishi ndiye aliyeleta muongozo wakufuatwa kwa kutambua umuhimu wa muongozo huo kuwepo hili kuvilinda viumbe vyake na mazingira yao.
Hili la sheria hii ya kuua kutokuwepo lingewezekana tu endapo binadamu angemsikiliza Mungu hapo kabla ya anguko, hivyo asingeishi kwa ukatili na uharibifu uliopitiliza katika mazingira yake.
Kwa kuwa binadamu kiumbe pekee aliyejitwaalia maarifa(ambayo akupaswa kuwa nayo) kwa kujua mema na mabaya ni mtawala aliyepotoka(aliyeingia maovuni au majaribuni na ni mzigo au janga kwa viumbe alivyopewa avitawale na kwa sababu yake dunia ilitiwa unajisi) huoni kama si busara kumwacha aishi tu kwa kujiamulia kuua pasipo mipaka.
Umejibu vyema. Lakini mkuu mbona huyo Muumba alikuwa pia akiingilia huo uhuru mchache aliowapa watu wa kuchagua mfano ktk yale mapigo kumi ya kule misri biblia imeandika kabisa waziwazi kuwa Mungu alikuwa anampa farao moyo mgumu ili asiwaachie waisrael!,hatimae akaja kumuadhibu nawakati ugumu huo alimpa yeye mwenyewe!.. hii imeakaaje..?