Kwa hoja ipi watu wanaamini kuwa taifa la Israel ni taifa la Mungu ingalikuwa ni taifa linaloishi kwa Upanga?

Hekima za mungu sio za utambuzi wako wewe binadamu kiumbe dhaifu,wala ufahamu wako kiduchu hauta weza kutambua hata 1 ya 1000000 za hekima zake tukufu, yeye awezaye kulikinga jambo baya kwa ubaya.
#Msikome kuomba na kumsifu. The one who is one the omniponent the Alfa and Omega.
-->>Hata ukiifikirishaje akili yako kumuhusu yeye unafanya kazi bure, maana kwake yeye wewe si chochote.
 
Hao NEGROES ndio ISRAEL WENYEWE. Sio hao wahuni ambao mtoa mada anafikiri ndio wenyewe.
 
Sio Africans wote.
Kuna Negroes hawa waliingia Africa baada ya Yesu kuondoka na Roma Negroes kuanzisha Timbwili na waroma kutaka uhuru wa kapigwa vibaya na temple kuvunjwa. Na Yesu aliwaambia mkiona Mji wa Yerusalem umezingirwa basi kimbilieni Milimani aka down south aka huku chini afrika. Remember kipindi hiko Roma. Alikuwa anatawaka huko Juu kote so hawakuweza kwenda huko so walishuka chini ndani Africa then wakakutana na watoto au wajukuu wa HAM sie na machifu wetu. But jua kwamba b4 that yake makabila mengine 10 yalishakuwa huku Africa pia na ndio walitufundisha sisi watoto wa Ham mambo mengine mengi ya Msingi hata kutahiri. Pale kipindi cha Yesu walibaki kabila la YUDA tu na kidogo LAWI na kidogoooo Benjamin.
So walishuka huku hao NEGROES walitapakaa zaidi West Africa. Kiasi kidogo waliokuja East Africa. Yale mengine 10 ndio wengi walijaa Eat Africa. But now tumezaliana Sana nao so ni ngumu kujua yupi ni yupi. Ila Yeye Mungu anawajua wtu wake.
 
Sasa ukirudi kwenye kumbukumbu la Torati utakutana. Na baraka na laana kwa hawa wana wa Israel kama ambayo Musa aliwaambia ikiwa wataenda kinyume na Maagizo ya MUNGU na wakaapia nadhani.
Basi wote tunajua kuwa hawa jamaa hawakufuata vile waliambiwa so kilichowapata ni Laana. Sasa kipindi Yesu yuko pale ni kabila YUDA aka NEGROES kwa asilimia 99% ndio alikuwa PALE na kumbuka wao ndio walipeleka mashatka ya uongo kwa pilato na wakasema Damu yake iwe kwao na vizazi vyao. So pale. Walijivika vizuri yale. Malaana yote ya kwneye kumbukumbu la torati. Na ukisoma zile laana vizuri utaona Mungu anawaambia kuwa "nitawarudisha Misri lakini this time mtaenda na MERIKEBU" YAANI ATAWARUDISHA UTUMWANI NA kipindi wanaoingia Misri kipindi kile si walitembea tu sababu Israel. Ilikuwa ni kaskazini. Mashariki ya Africa kabla wazungu hawachimba suez kanal. Ili. Kuhalalisha uongo wao kuwa wale. Jamaa ni wazungu. So kilichotokea ndio Hiko NEGROES WALIRUDISHWA UTUMWANI KWNEYE CARIEBANS... USA etc kwa MERIKEBU mpk 400 hundreds years ndio watakuwa huru tena. Nadhani bado Haijatimia. So Ile transatlantic slave trade ilikuwa yao Ile. Na kwa kuwa walikuwa blacks kama sisi ilikuwa ngumu kuwajua so ndio wakawa wanaingia deal na wachifu hawa babu zetu sisi watoto wa Ham wawaonyeshe wageni walishuka huku ni akina nani the machifu kwa uoga wengine kwa KUPEWA pesa waliwauza kirahisi. So wazungu ili kutuzuga na kuwazuga hawa jamaa mpk Sasa Wana msemo wao kuwa Wa Africa walikuwa wanawaza wa afrika wenzao. Kitu ambacho ni Uongo hakuna chief aliyeuza ndugu zake. Bali walikuwa wanawaza wageni weusi kama wao
 
Na ndio. Maana hata huko walipo bado ni full. Mateso wanapigwa na polisi risasi kila siku huko Haiti ni matetemeko mpk basi sababu still. Wapo kwenye laaana ya kukataa maagiza ya Mungu wao.
Wale. Waliokaa pale sio. Wenyewe nj wahuni tu wa kizungu wakisaidiwa na USA. Na ndio maana walitaka kuwa weka Uganda kipindi fulani.
 

Ulishaambiwa duniani siyo mahali salama kwako kuishi tokea siku ya anguko lako kama mwanadamu kukubaliana na shetani (lord of war/muasi) pale edeni ulipochagua kifo na immediately kizazi cha kaini kikaanza kumwaga damu na ndiyo maana ukawepo mpango wa pili wa ukombozi (kutunukiwa maisha ya milele)

Hivyo tunaposema dunia haiendi pasipo damu shida si Mungu shida ni wewe kumsikiliza yule muasi ambaye aliamishia vita vyake vya kiroho (uroho,uasi,chuki,kujiinua,ushawishi,mauaji na uungwaji mkono) juu ya wanadamu nakusababisha dunia iwe ilivyo, inamaana unapokiri nakufuata agizo la kutokuua mwanadamu mwenziyo na viumbe wasio na hatia (unamsikiliza Mungu) hapo unakuwa kinyume na sheria za utawala na maumbile ya ndani ya dunia(shetani) na hapo kusurvive kwako kutakuwa ni kwa taabu maana dunia ni uwanja wa vita.

Awali ni wazi tuliumbwa na kile sayansi inakiita survival for de fittest (kuishi kwa kukatisha uhai wa viumbe vingine katika kubalance nature na ku-enhance maisha) ila tulipaswa kutovunja miiko ya mzunguko huo kama wafanyavyo wanyama wa mwituni, wadudu na mimea ila kinyume chake binadamu amekithiri kutenda yanayopelekea uharibifu, maangamizi, kubadili asili ya mazingira na kuchochea maovu na ndiyo maana ikabidi kudhibiti yote haya kuwepo na amri 10 zenye malengo makuu mawili kuleta amani na upendo hili kumlinda mwanadamu dhidi ya mitego ya mwovu.
 
Ohoo! Hii mpya Sasa! Mkuu hii historia umeitoa wapi na hao waisrael weusi wapo wapi au ndo wale black America..🤣
 
Mkuu huoni Kama kunakuwa na mkanganyiko kwani Mungu alete sheria ktk mazingira ambayo kuishi ni kuua..??
 
Kama asingesema hivyo basi isingemaanisha kafa kweli kama wanavyokufa wanadamu wengine bali kaigiza kufa hili akisema kafufuka tumwamini. Ila kitendo hicho kinatuthibitishia utimilifu wa maandiko juu ya maisha yake ya kibinahadamu hapa duniani.

Simply kwa kuwa imeandikwa kuwa roho ya ndani ya binadamu ni ile pumzi ya Mungu ambayo huwa ndani yake kama nafsi hai na pindi anapokufa ile roho umrudia Mungu mwenyewe huku mfu (mwili uharibikao) akibaki halivyo pasipo kumbukumbu yeyote mpaka atakapofufuliwa tena kwa mapenzi ya Mungu mwenyewe atoae pumzi ya uhai(roho)
 
Kwa hiyo ndio kusema...?
 
Ukisoma bible kiimla au juu juu tu utaishia kuchanganyikiwa kama wale wanaokoti mistari kama "masikini mpe pombe asahau shida zake" "kunywa kidogo ila usilewe" au "hakuna alichokiumba Mungu ambacho ni najisi" kuhalalisha uovu na upumbavu kwa kula vichafu, kunywa pombe na kutenda anasa.

Kipi kinakupa mashaka juu ya uelewa wa Mungu mjua vyote aliye Alfa na Omega juu ya maisha yako yote mwanzo na mwisho wake, ni kweli tokea ujazaliwa anakufahamu na utakavyoishi mpaka mwisho alishajua,

Je unahisi kuwa kama kakuumba na destiny yako ni kwenda motoni kakosea? Na kwa kuwa ni mapenzi yake kukuumba (hata angeamua asingefanya hivyo) na kukupa destiny hiyo ni nani awezae kumuhoji au kujua kama ni sahihi au si sahihi?

Kwa maana vile vyote vionekanavyo sawa machoni petu au katika maarifa yetu, vingi ni upumbavu na upotofu mbele zake yeye mwenye utukufu mkuu na ujuzi wa kila kitu na ndiye mwanzo na mwisho wa kila kitu hivyo katika yeye kunamo kila kitu na pasipo yeye akiwezi kuwepo chochote.

Je, wajua vipi kama kakuumba hivyo kwa makusudi yake na hata huko kwenye hukumu pengine akawa na consideration kulingana na role aliyokupa uitimize ukiwa duniani iwe ni nzuri au mbaya.

Mfano; Mdogo ni nani alimpa moyo mgumu Pharaoh kuwaachia wana waisraeli waondoke misri? Nani alimtia moyo mgumu Yona kuwahurumia watu wa Ninawi? Ni nani alimpa destiny Yuda ya kumsaliti Yesu? Je, kama Yesu alimjua atakayemsaliti hata kabla ya tukio kwanini hakustopisha mapenzi ya Mungu? Je, yote haya Mwenyezi Mungu aliyaacha yatokee pasipo kuwa na sababu?

Simply ni kuwa Mungu utenda kila jambo kwa usahihi na mahesabu makubwa (katu apangiwi au kuchaguliwa afanye nini na kiumbe yeyote aliyemuumba yeye na ndiyo maana anastahili kuombwa na kutukuzwa) ambayo kwa bongo zetu wanadamu hatuzifikii hata robo hivyo nivigumu sana kumkosoa kwa matendo yake au maamuzi yake na kufikiria twajua zaidi yake.

Nafikiri ukisoma kitabu cha Yobu alipojibiwa maswali yake magumu kama haya na Mungu mwenyewe utokuwa na mashaka tena na maneno toka kifungu hiki.
 
Kwa hiyo ndio kusema...?
Yesu alikufa kifo kamili (cha kawaida cha kibinadamu) kama wengine na akafufuka kwa uwezo wa muumba wake siku ya tatu kudhihirisha kuwa hakuna linaloshindikana tukiishi kwa unyoofu alivyofanya yeye na hata maumivu aliyahisi pia kama sisi kiasi cha kuelekea kukata tamaa na akawa akitiwa moyo na pia amenukuliwa akilalamika kibinadamu hii yote ni uthibitisho Yesu akuwahi kuexist duniani kama Mungu bali kama messenger wa kufikisha ujumbe wa Mungu kwetu wanadamu kuwa dunia bila uovu inawezekana.
 
Shukrani mkuu.
 

Mojawapo ya maeneo ambayo yanamkanganyiko wa tafsiri(Siyo biblia imejikanganya hapana bali ni sisi tu na vichwa vyetu kutotaka kutumia akili zetu kung'amua kilichomaanishwa hapo)

Hii imepelekea kuzalishwa kwa imani na nadharia tofauti tofauti juu ya Mungu na Yesu ni kitabu hiki hiki cha Yohana ambacho nadhani kama ni mkristo unayefuata mafundisho ya Yesu Kristo basi unapaswa kukisoma kwa umakini nakujaribu kukielewa kwa binafsi yako kwanza pasipo kumhusisha yeyote kukuelezea au ku-apply nadharia yeyote unayohifamu kabla.

Binafsi yangu nimekielewa namna hii;

Yesu kavaa uhusika wetu hivyo ni binadamu mwenzetu na wakati akitufundisha maandiko, alikuwa akitumia nafsi ya kwanza kujielezea kama binadamu au mtoto wa Mungu (na mara kadhaa alilisisitiza hili kuwa tu wana wa Mungu au miungu inayoishi na akuonesha kujitenga nasi) lengo likiwa ni kuhubiri Neno (habari za uzima) kwa wana wa Mungu (akijijumuisha na yeye pia)

Unapojiuliza yu wapi Mungu au anafananaje Mungu? Jibu la Yesu hapo limejitosheleza;

Unapaswa kujiuliza kwanza kuwa kama Mungu ni Roho na ndani yangu alinipulizia pumzi ya uhai (Roho yake) nikaanza kuishi (yeye ndani yako na wewe ndani yake) huku sehemu ya roho yake inayoniunda mimi ikiwa ndani yangu, je huyo Mungu wahisi kwa umbo la kimwili anafananeje?

Hivyo hapa ni sawa na Yesu kama binadamu akuambie ukiniona mimi yaani binadamu mwenzio tiyari umeshamwona Mungu kwa kuwa kila aliye hai ndani yake anaishi Mungu (mwili wenu ni hekalu langu-ndiyo maana ya kuitaji kutukuzwa kupitia mwili huo) na Mungu ni Roho.

Yesu alinukuliwa pia akisema kuhusu yeyote hatourithi ufalme wa mbinguni pasipo kupitia kwake yeye au maombi yote yaelekezwe kwake naye baba atayajibu:- Kwa maana akuna atakaye enda kwa Baba ila kupitia kwangu kwa kuwa Mimi na Baba ni wamoja. Je, hapa Yesu anamaanisha nini? Je, anamaanisha kuwa yeye ni Mungu au sawa na Mungu?

Jibu ni hapana, Yesu (hapa anamwakilisha Neno au Sauti ya Mungu hivyo anapaswa kuwasilisha agizo lilivyo pasipo kubadili au kupindisha maana) hapa ni chombo kilichotumika kuwasilisha(hivyo tusidili na mwili, nafsi au mtu) au kinywa ambacho ndani yake ndipo linapotoka NENO LA UZIMA (Maagizo ya Mungu)

Hivyo anaposema hakuna atakayeurithi ufalme wa mbingu au maombi yake kujibiwa pasipo yeye, anamaanisha kuwa pasipo sisi kukiri na kupokea Neno la Mungu anavyotuambia nakulitekeleza hamna namna yoyote yakumfikia Mungu.

Hivyo Yesu akwambii umwabudu yeye bali Mungu wako na yeye anatwambia kuwa hakuna aliye mkamilifu ila Baba peke yake na kamwe hakuja kujitukuza bali kwa mapenzi ya aliyemtuma.

Nashukuruni mpaka hapo kwa waliosoma nilichoandika nina imani kwa kiasi chake wamenufaika kidogo na kile nilichookoteza kwenye kitabu hiki cha Yohana kwa ufupi. Na pia naruhusu kurekebishwa.
 
Aiseeeee🤔🤔🤔🤔🤔
 
Mkuu huoni Kama kunakuwa na mkanganyiko kwani Mungu alete sheria ktk mazingira ambayo kuishi ni kuua..??
Aliyeumba mfumo huo wa maisha ya kiumbe kula kiumbe chenzake ndipo waishi ndiye aliyeleta muongozo wakufuatwa kwa kutambua umuhimu wa muongozo huo kuwepo hili kuvilinda viumbe vyake na mazingira yao.

Hili la sheria hii ya kuua kutokuwepo lingewezekana tu endapo binadamu angemsikiliza Mungu hapo kabla ya anguko, hivyo asingeishi kwa ukatili na uharibifu uliopitiliza katika mazingira yake.

Kwa kuwa binadamu kiumbe pekee aliyejitwaalia maarifa(ambayo akupaswa kuwa nayo) kwa kujua mema na mabaya ni mtawala aliyepotoka(aliyeingia maovuni au majaribuni na ni mzigo au janga kwa viumbe alivyopewa avitawale na kwa sababu yake dunia ilitiwa unajisi) huoni kama si busara kumwacha aishi tu kwa kujiamulia kuua pasipo mipaka.
 
Umejibu vyema. Lakini mkuu mbona huyo Muumba alikuwa pia akiingilia huo uhuru mchache aliowapa watu wa kuchagua mfano ktk yale mapigo kumi ya kule misri biblia imeandika kabisa waziwazi kuwa Mungu alikuwa anampa farao moyo mgumu ili asiwaachie waisrael!,hatimae akaja kumuadhibu nawakati ugumu huo alimpa yeye mwenyewe!.. hii imeakaaje..?
 

Chukulia mfano wewe ni mwili na Mungu ni akili, kati yako wewe na akili nani mtoa maamuzi na nani ni mtendaji? (..hakika nawahakikishieni Mimi na Baba yangu ni wamoja..")

Kama Mungu ni component inayoishi ndani yako basi jua kuwa wewe pia waishi ndani ya mwili wake, ina maana wewe ni spare part mojawapo kwenye mwili wake na hili akuondoe wewe lazima ajidhuru yeye pia (jibu rahisi la tafsiri ya Yesu kufa kwa ajili ya dhambi zetu)

Ndiyo maana Yesu anasema kama mguu unakukwamisha au jicho linakukosesha ling'oe utupe kwa maana ni heri kuishi chongo kuliko kuwa mdhambi. ("..Ulitakalo lifanyike duniani iwe kama mbinguni..") Kwahyo hicho anachokuagiza ufuate ndicho anachokifanya pia.

Swali lako la sababu ya kufanya moyo wa farao kuwa mgumu nilishalijibu kwa kirefu na kwa njia ya mtego wa maswali hivyo sitolirudia, ila kwa ufafanuzi huo mfupi kuna kitu kipya naamini umepata.

NB; Mwenyezi Mungu kama owner wa binadamu na kila kitu pia ana maamuzi yake ya kumfanya binadamu afanye jambo lolote iwe linahukumiwa kibinadamu kuwa na manufaa au bila manufaa pasipo kuingiliwa wala kuojiwa na mtu yeyote. Lakini amini yeye ni mkamilifu kamwe hakosei na maamuzi yake daima yana sababu na hayatiliwi mashaka, na akiahidi yeye kahaidi kweli lazima litimie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…