Pre GE2025 Kwa huu utitiri wa miradi aliyomwaga Rais Samia mkoa wa Mwanza, angekuwa anatokea kanda ya Ziwa wapinzani wangesema anapendelea kwao

Pre GE2025 Kwa huu utitiri wa miradi aliyomwaga Rais Samia mkoa wa Mwanza, angekuwa anatokea kanda ya Ziwa wapinzani wangesema anapendelea kwao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mradi wa Malya Sport Complex mbona ushakamilka muda tu na training ground inatumika sana. Fanya research vizuri usikurupuke tu.
Kuna Vitu vingi umeorodhesha kama vipya wakati vilishapangiwa budget na mzee Magu kabla hajafariki na mingine ilikuwa ishaanza mfano barabara ya Hungumalwa- Ngudu.
Acha kupayuka vitu usivyovijui.

Unafahamu hapo Kuna miradi mingapi?

Pia hiyo taarifa nimekuwekea hapo ni ziara ya Waziri juzi,wewe unaona hayo majengo na hizo structures zingine zimekamilika? Huoni Nondo zikipanda hapo?

Mwisho,tufanye umekamilika ni awamu ya 5 imejenga au awamu ya 6? Hata kwenye mada yangu nimeweka miradi iliyokamilika ndani ya awamu ya 6.
 
Mkoa utoe azimio la kumpa kiwanja Samia, haiwezekani akistaafu akae mbali na Mwanza, akae hapo afaidi matunda ya kazi yake. Migiro Isamilo, Jk nyegezi, hawezi kosa watu wa kupiga naye stori
 
Acha kupayuka vitu usivyovijui.

Unafahamu hapo Kuna miradi mingapi?

Pia hiyo taarifa nimekuwekea hapo ni ziara ya Waziri juzi,wewe unaona hayo majengo na hizo structures zingine zimekamilika? Huoni Nondo zikipanda hapo?

Mwisho,tufanye umekamilika ni awamu ya 5 imejenga au awamu ya 6? Hata kwenye mada yangu nimeweka miradi iliyokamilika ndani ya awamu ya 6.
Mradi ulikuwa umekamilika toka awamu ya 5 boya wewe. Labda mama yako anataka kuuongezea tu lakini usiseme mradi mpya boya.
 
Wewe ni punguani na mpumbavu.

Soma mada ndio uje kuchangia sio kukurupuka kama kenge ameona mvua.

Nimebainisha utofauti hapo Juu ni wajibu wako kubisha Kwa facts sio unaropoka tuu.

Mikoa Mingi tuu hakuna hizo Barabara na kama zinajengwa basi ni za Samia mfano Tanga,Kilimanjaro,Songwe,Njombe na mingine Mingi tuu.
Ulipaswa tu umjibu kwa ufupi tu kwamba asome mada ndo aje ajibu, kimsingi miradi mingi inatekelezwa pia lingejengwa daraja la kisorya - ngoma lenye kama km 2 hivi lingeondoa usumbufu wa wakazi wa Ukerewe na lingesaidia sana ukuaji wa uchumi kwa watu wa maeneo hayo Na Tanzania kwa ujumla
 
Ulipaswa tu umjibu kwa ufupi tu kwamba asome mada ndo aje ajibu, kimsingi miradi mingi inatekelezwa pia lingejengwa daraja la kisorya - ngoma lenye kama km 2 hivi lingeondoa usumbufu wa wakazi wa Ukerewe na lingesaidia sana ukuaji wa uchumi kwa watu wa maeneo hayo Na Tanzania kwa ujumla
Noted, Serikali itafanyia kazi
 
Wasukuma hawamtaki aiwee wana resentments bado sana jamaa
Huu utoto bakini nao huko kwenu...

Hapo Mwanza kuna kila aina ya kabila unalolijua...

Hivyo itoshe kusema kuna watu wa Mwanza wanamkubali na wasiomkubali Samia....

Hayo mambo ya kuangalia ni kabila gani linamkubali au kumkataa mtu ni huko kwenu.
 
Kinachoshusha Credibility ya Mama kwenye hiyo miladi ni kuigeuza Miladi ya kupigia Picha kila anayekuja anapita location kidogo kupata picha, We Miladi gani isiyokamilika hiyo soko kuu toka 2019 tunaelekea 2025 sasa, Mladi wa Maji Butimba ukisikia umekamilika ni chanzo cha Maji usambazaji bado ni kimberley, Daraja la JPM nalo ni yaleyale, njoo kwenye Meli nako tabu tupu, hivyo vyuo sijui Ardhi ni eneo tu limetengwa wala hakuna kitu pale, angalau TIA, Mipango na DIT ndio vimeanza Operation, Barabara zilizopangwa kujenga hazifiki hata km 60 kwa ujumla wake yaani mechukua km 3 kwa kila Barabara ndefu ni km 11 nazo ni za tactic, kiwanja cha ndege hata haielewki ni cha Kimataifa au ndo zinatafutwa kula, Alafu miladi mingi iliyobaki ni makaratasi tu hakuna kitu kwa ground mnajaza Render tu, Fungueni Miladi sisi kula tutawapa tu hamna haja ya kutesa watu mpaka siku za uchaguzi, watu wapo mbugani kule sokoni tope jingi alafu pale soko kuu hapaishi.
 
Back
Top Bottom