Kwa kampeni yenu hii, mtawatoa wote lakini hamtaweza kuyafuta waliyoyafanya

Kwa kampeni yenu hii, mtawatoa wote lakini hamtaweza kuyafuta waliyoyafanya

Kiturilo

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
708
Reaction score
2,859
Nimesikitishwa sana baada ya kutonywa na mtu kwamba eti wote waliokuwa kwenye top positions kwenye serikali ya awamu ya tano wanatakiwa kuondolewa!

Lakini nawahakikishia wote wenye hiyo mipango ovu kuwa watafanikiwa kuwatoa kwenye nafasi zao lakini kamwe hawatafanikiwa kuwatoa ndani ya mioyo ya watanzania na pia hawatafanikiwa kamwe kufuta kazi zao walizowafanyia watanzania.

Ni kweli Dk Kalemani siyo waziri tena lakini si Bwawa la nyerere lipo na linaendelea kujengwa kule Rufiji?

Nani hajui kuwa enzi ya Dk Kalemani majenereta yalikosa soko? Nani hajui kuwa enzi zake wananchi waliacha kuuziwa nguzo za umeme?

Ni kweli Dk Tito Mwinuka siyo MD wa Tanesco tena lakini si ndiyo ameifanya Tanesco iache kuagiza nguzo nje ya nchi na kuanzisha kiwanda cha kutengeneza nguzo zao wenyewe za zege,? pia na kuacha kutegemea ruzuku serikalini?

Ni kweli Dk Chamriho hayupo wizara ya ujenzi ,lakini si ndiyo amesaini na kutujengea flyover kila sehemu? Ina maana ukimtoa wananchi watasahau kuwa Mfugale na Kijazi flyovers zimesimamiwa na yeye?

Tunawaonya tu watoeni wote alafu tuone hizo kura za kuwafanya mshinde mtaenda kuomba wapi.
Kinachombeba mtu ni utendaji wa kuwafanyia kazi wananchi na siyo porojo zenu.
 
Wote nyinyi ni wachumia tumbo. Mnacho gombania hapa ni ulaji tu na madaraka. Kimsingi hatuna cha kuwasaidia, maana zamu yenu ya kuitafuna keki ya Taifa imeshapita! Ni wakati sasa kwa wengine nao kufaidi.

Kwa sisi wenzangu na mimi, bado tunaamini Katiba Mpya ya Wananchi, ndiyo dawa pekee ya kuondoa, au kupunguza kabisa huu ulafi wenu.
 
Wote nyinyi ni wachumia tumbo. Mnacho gombania hapa ni ulaji tu na madaraka. Kimsingi hatuna cha kuwasaidia, maana zamu yenu ya kuitafuna keki ya Taifa imeshapita! Ni wakati sasa kwa wengine nao kufaidi...
Utaweza kuifuta na miradi yao?
 
Nimesikitishwa sana baada ya kutonywa na mtu kwamba eti wote waliokuwa kwenye top positions kwenye serikali ya awamu ya tano wanatakiwa kuondolewa...
Kwa hiyo kwa akili yako umeona hao hawatakiwi kuguswa?

Kwani wengine hawawezi kufanya better than hao!

Yaani Mwendazake aliwaaminisha kuwa yy ni malaika au Mungumtu mpk hamtaki teuzi zake ziguswe.
 
Ni kweli Dk Tito Mwinuka siyo MD wa Tanesco tena lakini si ndiyo ameifanya Tanesco iache kuagiza nguzo nje ya nchi na kuanzisha kiwanda cha kutengeneza nguzo zao wenyewe za zege,? pia na kuacha kutegemea ruzuku serikalini?
Lakini pia si ni kweli kwamba TANESCO ina ukwasi (madeni) balaa ?
 
Kwani hao si waliwekwa na awamu ya tano? Basi awamu ya Sita na yenyewe ina haki ya kupanga kikosi chake.

Inaonekana kuna mahali ulikuwa inafaidika sasa unaona kama mrija unakwenda kukatwa.

Fanya kazi halali bwana kwani Tanzania itajengwa na sisi watanzania wenyewe na sio viongozi peke yao.

Ila niseme mpaka sasa MBOWE SIO GAIDI na KATIBA MPYA INAHITAJIKA
 
Hizi sifa za kijinga unazolazimisha hapa ungewapa na wakoloni basi,maana wao walijenga reli ya kati, ya kaskazini, miundombinu kadhaa nk. Ni upendo gani mlitengeneza kwa watanzania, kisha ilipofika wakati wa uchaguzi mkaingia madarakani kwa shuruti?
tishwaB sana baada ya kutonywa na mtu kwamba eti wote waliokuwa kwenye top positions kwenye serikali ya awamu ya tano wanatakiwa kuondolewa!

Lakini nawahakikishia wote wenye hiyo mipango ovu kuwa watafanikiwa kuwatoa kwenye nafasi zao lakini kamwe hawatafanikiwa kuwatoa ndani
 
Nimesikitishwa sana baada ya kutonywa na mtu kwamba eti wote waliokuwa kwenye top positions kwenye serikali ya awamu ya tano wanatakiwa kuondolewa!

Lakini nawahakikishia wote wenye hiyo mipango ovu kuwa watafanikiwa kuwatoa kwenye nafasi zao lakini kamwe hawatafanikiwa kuwatoa ndani ya mioyo ya watanzania na pia hawatafanikiwa kamwe kufuta kazi zao walizowafanyia watanzania.

Ni kweli Dk Kalemani siyo waziri tena lakini si Bwawa la nyerere lipo na linaendelea kujengwa kule Rufiji?
Nani hajui kuwa enzi ya Dk Kalemani majenereta yalikosa soko? Nani hajui kuwa enzi zake wananchi waliacha kuuziwa nguzo za umeme?

Ni kweli Dk Tito Mwinuka siyo MD wa Tanesco tena lakini si ndiyo ameifanya Tanesco iache kuagiza nguzo nje ya nchi na kuanzisha kiwanda cha kutengeneza nguzo zao wenyewe za zege,? pia na kuacha kutegemea ruzuku serikalini?

Ni kweli Dk Chamriho hayupo wizara ya ujenzi ,lakini si ndiyo amesaini na kutujengea flyover kila sehemu?
Ina maana ukimtoa wananchi watasahau kuwa Mfugale na Kijazi flyovers zimesimamiwa na yeye?

Tunawaonya tu watoeni wote alafu tuone hizo kura za kuwafanya mshinde mtaenda kuomba wapi.
Kinachombeba mtu ni utendaji wa kuwafanyia kazi wananchi na siyo porojo zenu.
Dkt JK alivyoingi madarakani alihakikisha washikaji/marafiki wananeemeka. Ingawa yeye Mzee wetu Dkt JK hakuwa fisadi na hana hulka ya wizi (angalia historia yake tangu akiwa CCM). Rafiki wa Dkt JK ndiyo waliomponza. Alivyoingia Dkt Magufuli yeye aliondoa wote wenye vinasaba vya wizi.

Uzuri uchunguzi na faili la kila mtendaji wa serikali lilikuwa na kila kitu hivyo kuifanya kazi ya Dkt Magufuli kuwa rahisi na kutamka kwa kujiamini yeye ni mtumbua majibu. Wezi wote wa mali za serikali waliogopa/wakaunda kila aina ya zengwe, wakatumia kila aina ya vyombo vya habari kumchafua Dkt Magufuli ila mwisho wa siku wote wakaona wameshindwa kabisa. Wakaenda mbali na kufanya vikao vya vikundi vya chama kumsengenya, ila mwisho wa siku wakasalimu amri. Mama Samia serikali yake iko tofauti na Dkt JK na Dkt Magufuli.

Tumsimlaumu Mama kufagia wateule wa Dkt Magufuli na kurejesha wenye kashfa. Hata Dkt Magufuli alimrejesha Mwigulu na Simbachawene wakati waliondolewa kwa kashfa. Hakuna anayepinga Dkt Mwigulu alihusika na kuhujumu mali za CCM, ila Dkt Magufuli alimteua tena kushika nafasi mara ya pili baada ile ya mambo ya ndani. Nadhani siasa na vetting zina zaidi ya uzalendo. Inategemea nani anamfanyia vetting na uhusiano/rushwa ili kusafisha faili na kupeleka recommendation kwa mamlaka za uteuzi. Njia pekee ni kuwa na mfumo unaoruhusu ushindani! Hivyo sidhani kama ni sahihi kumshitumu Mama eti anaondoa watu wa Dkt Magufuli.
 
Hizi sifa za kijinga unazolazimisha hapa ungewapa na wakoloni basi,maana wao walijenga reli ya kati, ya kaskazini, miundombinu kadhaa nk. Ni upendo gani mlitengeneza kwa watanzania, kisha ilipofika wakati wa uchaguzi mkaingia madarakani kwa shuruti?
Ulitegemea uje na Sera ya kutetea ushoga alafu watanzania wakuchague ?
Hovyo kabisa wewe
 
Back
Top Bottom