Kwa kasi hii ya Rais Magufuli nashindwa kuelewa mzee Mwinyi alifeli wapi hadi viwanda na mashirika ya umma yakafa!

Kwa kasi hii ya Rais Magufuli nashindwa kuelewa mzee Mwinyi alifeli wapi hadi viwanda na mashirika ya umma yakafa!

Mfumo wa uchumi wa kimashariki (Kijamaa) kupitia Azimio la Arusha uliopora viwanda na Mali nyingi za matajiri na serikali kujimilikisha na kuviendesha.

Bahati mbaya viliendeshwa kwa kupangiwa bei na serikali bila kujali gharama za uzalishaji (Production cost) Vingi vilifeli mikononi mwa Nyerere mwenyewe! Na ilibidi vipewe ruzuku toka kwenye kodi.

Njaa ya miaka ya mwisho Sabini na Vita ya Uganda na Tz vilifirisi kabisa nchi. Nyerere akaenda kwa mabeberu kuomba mkopo
Walimpa masharti yafuatayo;

i. Kujiondoa serikali kuzalisha,kuagiza na kuingiza bidhaa. Iwe inakusanya Kodi tu.

ii.Kuwepo na soko huria. Bei za bidhaa zitokane na ushindani na mahitaji ya soko. (Serikali ijiondoe kupanga bei)

iii. Ashushe thamani ya shilingi

iv. Kuwepo uchangiaji katika huduma za kijamii baina ya serikali na wananchi ( Cost sharing) ili kuipunguzia mzigo serikali.

vi.Apunguze idadi ya watumishi wa umma na mishahara yao.

vii.Abinafsishe viwanda alivyopora na vile alivyopora.

Nyerere aliyakataa masharti huku akinukuliwa kwamba anayedhani Tz itayakubali masharti hayo ni mwendazimu akiwa ziarani Uingereza (Scotland?). Mwisho alienda Mara ya pili mezani IMF na WB wakasimama kwenye masharti yao.

Nchi ilikuwa taabani na Nyerere ikabidi ang'atuke kulinda msimamo na heshima yake.

Mwinyi akachukua nchi na kutekeleza masharti.
Huu ndio ukweli wa wazi kabisa ambao hausemwi ilhali ipo wazi nyerere anatakiwa kushtakiwa kwa kuhujumu uchumi, taifa na watu wake kwa sera za hovyo.
 
Mzee Ruksa alisema kazi iliyowashinda wastaafu watatu kwa miaka 30 huyu kaifanya kwa miaka mitatu tu!

Watu wa Pwani hata mtu alitukosea let say kakukanyaga kwenye daladala tunautoa mguu kwa staha zote halafu sie ndio tunafuta vumbi kwenye kiatu cha aliekukanyaga then tunamuomba atuwie radhi atusamehe ni kughafilika tu
 
Nafuatilia kwa makini jinsi taasisi za serikali zinavyozidi kujitokeza kutoa gawio (dividends) kwa serikali.

Nimeona hadi vyuo kama SUA, IFM nk vikitoa gawio sambamba na wakala mbalimbali za serikali na hata vitega uchumi vilivyoko jeshini na magereza mfano Suma JKT.

Natafakari tu endapo Rais Magufuli ndio angekuwa aliachiwa yale maviwanda kama Kiltex, Sunguratex, Tbl,Bora nk....nk....yaani ile Pugu road yote vilikuwa viwanda vya serikali, hakika naamini leo tungekuwa mbali sana.

Najiuliza tu mstaafu Mwinyi alikwama wapi hadi viwanda na yale mashirika makubwa makubwa akina NBC NIC, THB nk yakafilisika?

Nawatakia Dominika njema

Maendeleo hayana vyama!
Halfu kufariki kwa MAVIWANDA mhusika siyo Mwinyi!!!!! Ama hujui ama unamsingizia.Kwa taarifa TU Mwinyi alitukuta tukitembea miguu chini,hatuna nguo,tunalima lakini chakula choooote kinabebwa na ushirika,halafu sisi tunauziwa ka kilo ka unga mbayaaa wa njano almaarufu unga wa yanga! Tunafua kwa kutumia ARITA NA MKONGE ndo sabuni!
Mwinyi AKATUOKOA kutoka katika madhila hayooo akaamua kuruhusu mitumba,viatu japo vya matairi aka Mtanje kuko au katambuga!
Mkuu Kama ulikuwa hujui Mwinyi ndiye aliye ruhusu hata TV na deki baadae tv stations.
"Who the cap fit let him wear it."
 
Back
Top Bottom