Kwa Kauli Hii ya Twaha Mwaipaya, Jeshi la Polisi Limechukua Hatua Stahiki

Napata shida kidogo kuona makosa ya Twaha hapo.
Hii inaibua maswali kadhaa,Ukinijibu tutaelewana.

1.Tunaenda kuweka hatma ya Taifa letu,kijana yoyote njoo uwanja wa Ruanda mbeya.Je kuweka hatima ni kosa?

2.Kuna viongozi wamekamatwa kwa kosa la kusafiri kuja Mbeya.Je mtu kuja Mbeya ni kosa?

3.Kujitambua kama Vijana wakenya,
Kuna jinai gani hapo.Kuna viashiria vipi kwamba mkutano utafanya maandamano kama ya kenya.

Vipi angesema tunaendakujitambua kama vijana wa CCM walivyo jitambua kungekua na kosa?
Haya ni madhara ya kufanya maovu serikalini kwa hiyo kila ukiona kuna dalili ya watu kuamka na kuhoji wewe unajihisi ni wewe unaepingwa.

Hao polisi itafika muda watakuwa hawana nguvu tena ya kudhibiti haya maandamano na watakuwa wakwanza kuomba maridhiano lakini wayakuwa wamechelewa.
 
Kwa akili yako finyu unaona ni hatari kwa nchi kuwa na muelekeo sahihi wa nchi, unapenda tuishi bila katiba kama tunavyoishi sasa! Tanzania ni nchi ya hovyo tunayoishi kwa matamko ya viongozi badala ya katiba. Kwa hiyo vijana wakiamua kuwa kuanzia sasa tunataka katiba mpya na si matamko ya viongozi wewe na genge lako mnaona ni kuhatarisha amani ya nchi! Hauko sawa kichwani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…