Kwa kilichotokea, leo ndiyo mara yangu ya mwisho kupanda mwendokasi🙌

Kwa kilichotokea, leo ndiyo mara yangu ya mwisho kupanda mwendokasi🙌

Binti Sayuni03

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2025
Posts
1,075
Reaction score
1,913
Habarini za jioni wana JamiiForums, husika na kichwa tajwa hapo juu.
Leo nilikuwa na safari ya kivukoni/posta, nikaona ni heri niende mbezi nikapande mwendokasi.

Nilifika mbezi mida ya saa9 hivi nikakata tiketi nikasubiri pamoja na abiria wengine kama nusu saa hivi, mpaka dakiki40.

Ikaja gari moja ya mwendokasi nikawauliza wahusika hii inaenda kivukoni, wakanijibu inaishia kimara ukifika pale utaunganishia unapoenda. Nikapanda mimi pamoja na abiria wengine.

Tulivyofika kimara tukaenda moja kwa moja upande wa kusubiria mwendokasi zinazoenda Gerezani na Kivukoni, muda si mrefu ikaja mwendokasi tupu watu tukakimbilia tukapanda halijaandikwa chochote hivyo wanaoenda Gerezani walipanda na sisi wengine wa Kivukoni tukapanda, kufika mbele kabisa ndiyo maandishi yanaanza kusomeka pale juu kuwa gari ni ya Gerezani.

Sijui kama ni sawa hii lakini kwa upande wangu nimechukizwa na hili jambo naahidi sitakaa nipande tena haya magari, yaani unalipa hela yako unahangaika tena kama unaenda bure hapana kwakweli🙌
 
Nauli ni hiyo hiyo Moja ,na gari tayari ni tatizo.kwa hiyo okoa muda wako panda yeyote
 
Usisahau kujiandikisha ili uweze kupiga kura October
 
Kosa ni lako Kwann upande gari bila kujua linapoenda kwanza

Kosa pia ni la dereva kuchelewa kuonesha destination ya gari

Kiufupi wote mna makosa
 
Mwendokasi hautakiwi kupanda ukiwa na stress, inatakiwa upande na ile akili ya liwalo na liwe.
Mimi nikiingia kwenye kituo cha mwendo kasi tu akili yangu inakuwa tayari kwa chochote kitakachotokea, abiria mwenzangu akinitukana fresh tu, mtu akinikanyaga fresh tu, ukinisukuma fresh tu, dereva awe na hasira zake fresh tu. Yani easy. Kama una ratiba iliyonyooka au ni mwepesi kukwazika usipande mwendokasi unaweza ukaharibu siku yako
 
Habarini za jioni wana JamiiForums, husika na kichwa tajwa hapo juu.
Leo nilikuwa na safari ya kivukoni/posta, nikaona ni heri niende mbezi nikapande mwendokasi.

Nilifika mbezi mida ya saa9 hivi nikakata tiketi nikasubiri pamoja na abiria wengine kama nusu saa hivi, mpaka dakiki40.

Ikaja gari moja ya mwendokasi nikawauliza wahusika hii inaenda kivukoni, wakanijibu inaishia kimara ukifika pale utaunganishia unapoenda. Nikapanda mimi pamoja na abiria wengine.

Tulivyofika kimara tukaenda moja kwa moja upande wa kusubiria mwendokasi zinazoenda Gerezani na Kivukoni, muda si mrefu ikaja mwendokasi tupu watu tukakimbilia tukapanda halijaandikwa chochote hivyo wanaoenda Gerezani walipanda na sisi wengine wa Kivukoni tukapanda, kufika mbele kabisa ndiyo maandishi yanaanza kusomeka pale juu kuwa gari ni ya Gerezani.

Sijui kama ni sawa hii lakini kwa upande wangu nimechukizwa na hili jambo naahidi sitakaa nipande tena haya magari, yaani unalipa hela yako unahangaika tena kama unaenda bure hapana kwakweli🙌
Pole mkuu ila inaonekana kama ni mgeni na hayo magari coz kwa jinsi ulivyoandika ni kama hauko na uzoefu sana kwenye hivyo vituo au hiko kituo cha kimara.
 
Njoo Dm uchukue namba yangu uwe unaenda kivukoni umekaa kushoto unamsikiliza fally ipupa anavyowasaidia wazee wa kataa ndoa na ngoma yake ya
Mal Acompagne.
 
Back
Top Bottom