Kwa kipekee kabisa naipongeza Serikali kwa kuanzisha kodi ya kizalendo kwenye miamala ya simu. Naomba Watanzania tuiunge mkono

Kwa kipekee kabisa naipongeza Serikali kwa kuanzisha kodi ya kizalendo kwenye miamala ya simu. Naomba Watanzania tuiunge mkono

Sipo miongoni mwao mimi ni mwananchi wa kawaida kabisa na wala sijatumwa na mtu yeyote isipokuwa ni maoni yangu binafsi kuunga mkono kodi ya mshikamano ili kama taifa tuweze kusonga mbele kwa sababu pesa itakayokusanywa kupitia hii kodi kama ambavyo serikali imesisitiza itaenda kusaidia kutatua kama sio kumaliza kabisa changamoto ya bara bara zetu za vijijini. Kwahiyo ndugu watanzania wenzangu tusilalamike kwa sababu kodi hii ina manufaa makubwa kwetu na matunda yake tutakuja tuyaone baadae. Solidarity forever!
Una miaka mingapi?... Upo form ngapi?... What is your dream job?... Car?... House?!... Husband?!...

Wewe tujadili haya, mengine yaache
 
Hulka yetu watanzania tuliowengi hatupendi kulipa kodi kwa hiari ila ni wa kwanza kuilamu serikali pale inaposhindwa kuleta huduma za maendeleo.

Yaani tunafikiri pengine maendeleo yanakuja tu kama mvua ishukavyo kutoka mawinguni au labda kwamba nchi inaweza kujiendesha yenyewe pasipo watu kulipa kodi, jambo ambalo si kweli.

Inashangaza kwamba leo tunalia kwa sababu serikali imetuwekea kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini tunasahau kwamba taifa letu bado ni changa na linakabiliwa na changamoto lukuki zikiwemo changamoto za ubovu wa bara bara mjini na vijijini, changamoto ya maji safi na salama, changamoto ya madawati, changamoto ya walimu, hospitali, madawa, umeme n.k

Kimsingi wa kutatua changamoto hizi ni sisi wenyewe, tusitegemee kwamba kuna mtu kutoka taifa lingine wa kuja kututatulia changamoto zetu. Kumbe sasa inatupasa kufunga mikanda na vibwebwe kisawa sawa ili tuweze kuzitatua, na njia pekee ya kuzitatua ni kupitia kodi.

Hata mataifa yaliyoendelea kama marekani, uingereza, na china hayakufika hapo yalipo hivi hivi nao walipitia ugumu kidogo kama ambavyo sisi tunaona taabu kulipa kodi ya uzalendo kwenye miamala ya simu lakini baada ya muda fulani walizoea na kuona kwamba kulipa kodi ni suala la kawaida na ndio maana wameweza kupiga hatua kubwa kiuchumi na kuwa hapo walipo hii leo. Hata sisi kwakuwa ndio tunaanza mwanzo utakuwa mgumu lakini baadaye tutazoea na hii kodi ya kizalendo tutakuja kuona ni suala la kawaida kabisa.

Nachotaka kuwambia Watanzania wenzangu, tuonyeshe uzalendo tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa letu kwa sababu bila kodi.

• Hakuna bara bara itajengwa
Hakuna hospitali itajengwa,
Hakuna shule itajengwa

• Watoto wetu wataendelea kukaa chini

• Hakutakuwa na pesa za kununua madawa

• Watumishi wa umma watashindwa kupandishwa madaraja ambayo hayajapanda kwa miaka zaidi ya mitano

• Watoto wetu watakosa vipindi kwa sababu serikali haitakuwa na uwezo wa kuajiri walimu

• Mama zetu hospitali watashindwa kujifungua salama kwa sababu serikali haitakuwa na pesa za kuboresha huduma za afya

• Vile vile hata miradi mikubwa tuliyoanzisha kama SGR, SG n.k itakwama kwa sababu ili ikamilike kunahitajika fedha ambazo zinapatikana kupitia wananchi kodi ya wananchi.

Kwahivyo watanzania wenzangu tusione kama serikali haina nia njema na sisi, La hasha! tulipe kodi na tukishalipa kodi sisi kama wananchi tuchukue jukumu la kuisimamia serikali ili kusudi kodi tuliyolipa isipotee bure au kuishia kwenye mifuko ya wachache bali itumike katika malengo yaliyokusudiwa na matunda yake yaonekane.

KODI YA UZALENDO KWA MAENDLEO YA TAIFA.

Naomba kuwasilisha.
Kwa hiyo zile Kodi nyingine tunalipaga huwa zinaenda wapi.
 
Ongezo la makato lipo kwa kiasi cha juu kuanzia miamala ya Tsh 1000 hadi laki 2 hii maana yake ni kwamba,serikali inafahamu fika kuwa wanyonge ndo wanaofanya miamala kusaidia,ndugu,marafiki na jamaa,hivyo tozo kuwa kubwa katika muktadha huo watafikia malengo yao ila sisi wanyonge ndo tunaoumia
 
Mkuu nadhani kuna jambo hauelewi.., Hizi tozo wameziweka bila busara kabisa huenda hii ikasababisha badala ya Serikali kuongeza mapato ikapunguza hayo mapato..., na mbaya zaidi ikaharibu biashara za watu (mawakala na kampuni za simu) na kuongeza kero kwa mtumiaji (in short hakuna mshindi hapa)... kama nilivyoelezea kwa ufupi hapo chini:-

 
Waangalie namna ya kubalance serikali kupunguza matumizi lakini Kama kila kinachoingia wahuni wanachota, juz bot watu wamechota na hatusikii wakiadhibiwa hela itachukuliwa na bado cha msingi hakitafanyika washenzi tu.
Usemalo ni sahihi kabisa. Kodi zikusanywe na zitumike ipasavyo, itumike kwa kuasaidia wananchi, na palengwe hassa pale panapo hitajika, Lakini kwa sisi wa Afrika, sio Tanzania pekee hatuna viongozi wa kusimamia masuala hayo, wao cha kwanza kabisa ni kjijenga wao kwanza, na asilimia kubwa ya hao viongozi si kwamba wanaridhika pale wanapojipatia makazi, usafiri na huduma nzuri kwa famalia zao bali wanataka wajichotee hassa huku wakishinda nani mwenye hela zaidi. Sasa hilo ndio tatizo kubwa sana kwa nchi yetu na nchi nyingi za kiafrika. Ni jambo lakuleta chuki, ingwa kwa Tanzania yetu chuki hiyo bado haijafikia mahala pabaya ya kuleta vita na mauaji, na Mungu atuepushie majanga kama hayo ya vita, heri ushi tu kwa umaskini wako kuliko nchi ikaingia kwenye vita, Lakni tusiache kukemea masuala ya kifisadi na ubadhilifu wa mali za umma.
Kama ulivyo sema watu wanaiba na hawafanyi chochote. Mimi binafsi ningetamani vyama vya upinzani wajikite hassa kwenye suala hili la hao mafisadi kupewa adhabu kali, wange shindikiza serikalin itunge sheria mpya ya na kali kwa wezi wa mali za umma. Enzi za Slaa ndio angalau tulikua tukisikia wakiongelea sana ufisadi lakini sikuhizi naona kimya.
 
unalipa kodi alafu kuna jizi moja linakutwa na mabilioni limeficha nyumbani kwake
 
Back
Top Bottom