Kwa kizazi hiki na tabia za sasa kuna umuhimu gani wa kupoteza fedha nyingi kutoa mahari?

Kwa kizazi hiki na tabia za sasa kuna umuhimu gani wa kupoteza fedha nyingi kutoa mahari?

Philo, nawasikitikia wazazi wako.

Mahari ni shukrani tu kwa wazazi sababu unaenda kujenga ukoo wa watu huko, Mungu akikujalia uzao huko baadae utawaongezea watu wakwao idadi. Ni vibaya wakishukuru wazazi wako na watu wa kwenu kwa kutoa kidogo?

Tabia ya mtu haina uhusiano na mahari, kijana aliyeoza anapatana na binti wakufanana nae. Vile vile walio na tabia njema wanapatana na wenzao wenye tabia nzuri
Sijui point yako umeijenga kwa msingi ipi maana kijamii katika ancient society ambayo utaratibu wa kutoa mahari ulianza bikira ilikua kigezo muhimu sana na ikigundulika mwanamke sio bikira mchakato wa ndoa unaishia hapo hapo.

Ukija kwenye imani katika ukristo mahari ilikua inatolewa kwa mwanamke bikira tu ndio maana David alimlipia mahari Michal(ambae alikua bikira) lakini hakumlipia mahari Abigail(ambae hakua bikira).
 
Wanawake wakuoa wako wengi kuliko wanaume tatizo vijana mnataka ma slay queen ila wanawake waliotulia wapo wengi huko vijijini.
Sijui nini kifanyike kuwaamsha vijana hapa kwenye suala la kuchagua mke. Linapokuja suala la kuchagua mke vijana wa leo tunachagua kiholelaholela kama vile sio maisha yetu. It's ok the future is uncertainty, but that's not the reason for you to gamble on red flags.
 
Toa hili neno "shukrani" halihusiki hapo.

Mahari ni biashara kama wewe unavyoenda kununua mbuzi,kondoo ama punda mnandani.

Kwa sababu mnakaa pande zote mbili mnaanza makubaliano. Makubaliano hayo huechukua si chini ya masaa5 au zaidi. Hivyo Kuna kushindwana Kwa upande wa muoaji kutokufikia bei na kushindwa kuoana(kuoa)


Kama mahari ingetolewa na muoaji bila ya makubaliano yoyote kutoka pande mbili ni sahihi kuita shukrani. Tofauti na hapo ni biashara kama biashara zingine tu
Analeta masiahala huyu dada., shukrani gani inatolewa kwa ku-bargain bei
 
Nilijua tu utakuja na hoja nyepesi ambazo hazina uzito wowote wa kimantiki.

Eti familia ya KE inapotoa Binti yao aolewe ni kama wanapoteza rasilimali... Kwa dunia hii ya leo? Hii hoja yako ingeweza kuwa na mashiko kama tungekuwa Bado tuko miaka ya 1970s huko lakini sio leo hii, yes, zamani Binti akiolewa alikuwa anaenda kuwa chini ya umiliki wa mume wake kwa maisha yake yote yaliyobaki na mume wake huyo atamtumia kwenye shughuli za uzalishaji Mali kadri anavyotaka na Binti huyo akuruhusiwa kurudi nyumbani kwao haijalishi ni changamoto gani atazopitia kwenye ndoa yake.

Hebu Sasa tuangalie suala hili kwa dunia ya leo hii kama Bado mantiki yake ni ile ile... Je, Sasa hivi wanawake Bado mkiolewa mnaenda kuwa chini ya total ownership ya mumeo kana kwamba chochote unachokuwa unakifanya kinakuwa ni kwa ajili ya maslahi ya mume wako kama ilivyokuwa kwa mabibi zetu?? Jibu ni HAPANA.

Siku hizi wanawake mnaolewa mkiwa tayari mna career zenu ambazo wazazi wako wamekujengea kwa kukusomesha, licha ya wewe kuolewa ila wanakuwa wanategemea kupata misaada kutoka kwako kupitia hiyo career yako. Kwa hiyo Sasa unakuta wewe umeolewa lakini Bado una uhusiano wa karibu sana na familia yako kwa maana ya kuwapa misaada na hivyo wanakuwa hawajapoteza nguvu kazi yoyote ile.... Na kama hiyo haitoshi unakuta Kuna muda unamshirikisha mume wako kutatua shida za nyumbani kwenu na anafanya hivyo kama uwezo Yuko nao....Sasa hapa Bado unasema wewe Binti ukiolewa familia yako inapoteza nguvu kazi??

" Mwanaume anapoteza nini? au wazazi wake wanapoteza nini?"

Wewe dada hivi kabla ya kuuliza hayo maswali ya kitoto ukifanya tafakari kwa kuangalia na uhalisia wa maisha ya leo? Au umeuliza tu kulingana na ulivyokariri maandiko?

KWa hii Karne tuliopo kwenye suala la ndoa mwanaume na familia yake wanapoteza vingi sana, wakati huo mwanamke na familia yake Wana gain vingi sana...

Mwanaume akioa kama yeye alikuwa ndio nguzo huko kwenye familia yake, itabidi apunguze majukumu na kuanza kuingalia familia yake mpya ambayo ni wewe... Yaani kama alikuwa anasomesha wadogo zake itabidi aache, kama alikuwa anatunza wazazi wake itabidi aache au apunguze, yaani kwa maana nyingine familia yake Inakuwa imepoteza nguvu kazi au rasilimali muhimu kwa ajili yako.

nimewahi kuona mwanaume aliyeacha kusomesha wadogo zake na kisha kuanza kumuendeleza kielimu mke wake mara tu alivyomuoa, halafu huyo mke baada ya kumaliza masomo yake na kupata kazi nzuri akaanza kuwasomesha wadogo zake(yaani shemeji zake na mumewe)... Sasa hapo ni familia ya nani ilipoteza?

Wanaume Karne hii wanaoa wanawake ambao wanalingana nao vipato au muda mwingine wanawake wao wanawazidi vipato, lakini pesa inayotumika kwenye ujenzi wa familia kama kununua assets, kujenga n.k kwa kiasi kikubwa unakuta ni ya mume, ila siku ndoa ikivunjika wanagawana Mali hizo 50-50, halafu bado unuliza mwanaume anapoteza nini akioa?

Hilo suala la mtoto kuitwa ubini wa baba ni hoja isiyokuwa na kichwa Wala miguu... Mtoto anaweza akabeba jina langu lakini asiwe na connection yoyote na Mimi yenye faida, angalia hata bwana Nasibu amebeba jina la Abdul.

Bado hujaleta hoja ya maana ni kwanini tuendelee kuwatolea mahari???
Unafikiri hawajui basi, wanajua vizuri kwamba kutokana na sifa na mienendo yao ya kisasa kuna namna hawastahili kutolewa mahari, ndio maana vigexo vinavyowakataa wanavipinga mfano kwenye body counts watakuja na usemi wao wa "past doesn't matter" sasa jiulize kama past doesn't matter kwanini huwa wanaficha idadi ya wanaume waliotembea nao. Hata kama ana list ya maex 10+ akiulizwa atasema mmoja au wawili, kwanini asiseme ukweli kashatemebea na wanaume 10.
 
Wana JF hali gani huko katika pilika za hapa na pale.

Kwa hali ilivo sasa ukiachilia mbali wazazi kusema mmesomesha mmelea na mmekuza hii hoja ya ya kutoa mahari inaanza kukosa mashiko.

Msingi wa kutoa mahari miaka ya zamani ulikua ni up?

Na je, miaka ya Sasa msingi ni upi?

NB: Angalieni na Mienendo ya watolewa mahari

Naomba kuwasilisha
Ndoa sio kwa kila Mtu tuliza kijambio hiko!kama mnawaonea gere wanaolipiwa mahari nyie toeni Bure.
 
Unalitolea mahari li MWANAMKE lililopigwa Mikunyubenga ya kutosha na bado limechomoa mimba zaidi 5!

Mwanaume anayemtolea mahari mwanamke asiyekuwa Bikira Hana akili timamu!.
Tatizo Umri Umri dogo.
 
Mahari hupoteza utu wa mwanamke,, wakati mwingine anaonekana/anafananishwa na ng'ombe/mbuzi na huyo mumewe!! 🤔🤔
 
Mahari hupoteza utu wa mwanamke,, wakati mwingine anaonekana/anafananishwa na ng'ombe/mbuzi na huyo mumewe!! 🤔🤔
Ni kweli kabisa lakini katika mazingira ambayo italazimika mahari kutolewa basi angalao tuzingatie vigezo na masherti.

Virginity, submissive, productive, mwanamke akikosa ivyo vigezo maana yake hana uhalali wa kutolewa mahari
 
Unalitolea mahari li MWANAMKE lililopigwa Mikunyubenga ya kutosha na bado limechomoa mimba zaidi 5!

Mwanaume anayemtolea mahari mwanamke asiyekuwa Bikira Hana akili timamu!.
Ko unaoa bureee?
 
Una kichwa kizito. Familia ya 'ke inapotoa binti yao aolewe ni kama 'wanapoteza' rasilimali. Wakati upande wa pili wanavuna matunda na juhudi ya ulezi waliyofanya wazazi na ndugu wa binti

Mwanamme anapoteza nini? Au wazazi wake wanapoteza nini? Atazaliwa watoto wataoitwa kwa jina lake Na kuendeleza ukoo wa mwanamme
Umejibu vizuri
 
Ko unaoa bureee?
Mwanamke asiyekuwa na Bikira hapaswi kutolewa mahari,yaani wanaume wengine wakugeuze kopo la kukojolea halafu Mimi ndiye nikutolee mahari!

Nitatoa mahari Kwa mwanamke mwenye Bikira tu!,nikikuta umepigwa na Mimi nitapiga Kisha nasepa kama walivyosepa wengine!
 
Mwanamke asiyekuwa na Bikira hapaswi kutolewa mahari,yaani wanaume wengine wakugeuze kopo la kukojolea halafu Mimi ndiye nikutolee mahari!

Nitatoa mahari Kwa mwanamke mwenye Bikira tu!,nikikuta umepigwa na Mimi nitapiga Kisha nasepa kama walivyosepa wengine!
🤣Humu tu humu tu
 
Huo ni utamaduni wa Mwafrika linapofika kwenye suala la ndoa, ukiuondoa maana yake unafuta huo utamaduni ili sasa ubaki na utamaduni wa mzungu, utambulisho wa kiafrika unauondoa kama ilivyo kwenye mavazi, lugha, style ya maisha na mambo mengine ya kiutamaduni.

Kumbuka inapofika suala la kuoa utani wa kikabila na koo mbali mbali huwa unakuwepo ili kulisherehesha jambo lenyewe, na miaka ya nyuma ili furaha ya jambo lenyewe itimie ililazimu binti awe bikira, lakini sio kwamba waliokuwa sio bikra mahar haikutolewa la hasha, hapo ilikuwa inategemeana na muoaj kama ameridhika ngoma inaendelea sema ilikuwa fedheha kwa familia ya Binti.

Mahari ilikuwa inapima uwezo wa huyu mwanaume kama anaweza kumtunza mke na familia husika, lakini Mahari ilikuwa inatoa uthibitisho wa msemo kwamba anayeolewa au kuoa sharti anaiacha familia yake(alikozaliwa) na kwenda kuanzisha familia, na inajulikana tangu zamani kutengeneza familia sio jambo jepesi inahitaji uvumilivu, hivyo wazazi wa mwanamke wanamwambia binti yao tumepokea mahari sasa kuja huku mpaka kuwe na jambo muhimu ukapambane huko.

Mahari inampa mamlaka mwanaume ambaye ndio kichwa cha nyumba kummiliki mwanamke wake na kuwa na uhuru naye, kuzaa watoto anawataka yeye bila kuingiliwa na familia ya mwanamke, na hii ilikuwa haimaanishi kuwa eti mwanamke ameuzwa hapana, manyanyaso na mateso yakiwemo mke ana nafasi ya kusema kwa wazee.

Madhara ya kuondoa mahari.

1. utakuwa umeondoa huo utamaduni wa kiafrika kama nilivyosema hapo juu

2. Utakuwa umeondoa uhuru wa mwanaume kummiliki huyo mwanamke na hapo ili ndoa iende itahitajika utashi wa mwanamke mwenyewe, lakini mwanaume ataingiliwa katika maamuzi kutoka kwa upande wa mwanamke

3. Ile heshima ya undugu kutoka upande wa mwanamke haitakuwepo kwa sababu utakuwa umepewa bure,

4. Utii wa mwanamke kwa mwanaume utaondolewa, maana mahari inamfanya mwanamke awe submissive kwa mume. Haya malalamiko ya haniheshimu, hanisikilizi yataongezeka maradufu kuliko ilivyosasa

5. Hitaji la mwanaume kuoa litapungua, wanaume wataogopa zaidi kuoa maana ni kama unaoa bomu, maana hata mkitofautiana kusikilizwa tu na upande wa mwanamke itakuwa mtihani maana wataona kama wamekubeba sana na wewe ndio msumbufu unamsumbua ndugu yao.

6. Mwisho litakuwa anguko la mwanaume, maana mahari pamoja na kwamba inatolewa na mwanaume kwenda kwa mwanamke lakini anayefaidika nayo kwa asilimia 90 ni mwanaume huyo huyo.

Nawasilisha
 
Back
Top Bottom