Kwa kumbukumbu...yanayotokea kwa Chadema mwaka huu, yalitokea kwa CCM mwaka 1994!

Kwa kumbukumbu...yanayotokea kwa Chadema mwaka huu, yalitokea kwa CCM mwaka 1994!

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592
Mwaka 1994, wana CCM waliokuwa wakifaidika chini ya utawala wa Rais Mwinyi, kwa kuogopa mabadiliko, hawakutaka ang'atuke baada ya kumaliza kipindi chake.

Kampeni kubwa ilifanywa ya kutaka Katiba ifanyiwe mabadiliko Mwinyi awe mgombea pekee kwa kuogopa nguvu na moto waliyokuwa nao wapinzani na hasa NCCR.

Wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM walikuwa tayari kupitisha azimio hilo la kuomuongezea Mwinyi awamu ya tatu kwa wasi wasi wa kupoteza uchaguzi mwaka uliofuata.

Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alijitokeza na kupinga kwa nguvu azimio hilo akionya kuwa Katiba si kama shati unalochagua uvae lipi kila ukiamka.

Wazo la Mwinyi kuendelea likafa kibudu lakini CCM ikaendelea kuwa pamoja licha ya wagombea kujitokeza huku kampeni za kumpata mrithi zikiendelea bila mizengwe.

Mwaka huu Chadema nayo imejikuta iko njia panda na wajumbe wana wasiwasi kuwa mwenyekiti aking'atuka hawajui hatma yao na chama kwa ujumla itakuwaje .

Je wazee wenye hekima, busara na ushawisi kama Mwalimu hawapo tena? Woga wangu ni kuwa inawezekana wapo wajumbe ambao hawana maisha nje ya Chadema.

KIla baada ya miaka mitano Watanzania wenzetu wengi hujitokeza kugombea Urais Tanzania lakini, pamoja na mizengwe, mwisho wa siku sote tunabaki ni Watanzania.

Kwa nini kwa Chadema, chama cha kidemokrasia na maendeleo, hii isiwezekane kwa wagombea kujitokeza na wana Chadema wakabaki wamoja baada ya uchaguzi?

Najua jinsi ndani ya CCM, chama cha majizi kinachoendeshwa kimla, hili haliwezi kutokea na watafanya kila wawezalo kuhujumu uchaguzi huru na kuwasambaratisha.

Walaaniwe wale wote watakaojaribu kuuvuruga uchaguzi wa Chadema utakaofanyika tarehe 23/1/2025 kwani ni uchaguzi unaotazamiwa kuwa wa kihistoria nchini.

Tahadhari...nawaomba wana Chadema, kwa kuwa mnajua mnaandika historia, hiyo hiyo historia itawahukumu na kama kutatokea mizengewe isiyo ya lazima...hatutawasemehe!
 
Matokeo ni ama Mbowe awe Mwenyekiti au Mwenyekiti awe Mbowe. Wanachadema hawana chaguo jingine.
Ndivyo mlivyopanga, ndivyo mnavyopanga na ndivyo CCM inavyotaka. Mimi naamini wako wana Chadema tena wengi ambao hawapati maslahi yoyote ndani ya Chadema.

Mbowe kama angewasikiliza hao wana mageuzi wa kweli na si wale wenye maslahi na uwepo wake wawe wana Chadema, CCM au vyama maslahi, angeng'atuka abaki mshauri tu.

Mbowe amekuwa kama mfungwa na nachelea kusema sidhani kama anayo mawazo huru tena. Mbowe wa miaka ya nyuma sidhani kama ni huyu aliyetangaza kutetea kiti.
 
Mwaka 1994, wana CCM waliokuwa wakifaidika chini ya utawala wa Rais Mwinyi, kwa kuogopa mabadiliko, hawakutaka ang'atuke baada ya kumaliza kipindi chake.

Kampeni kubwa ilifanywa ya kutaka Katiba ifanyiwe mabadiliko Mwinyi awe mgombea pekee kwa kuogopa nguvu na moto waliyokuwa nao wapinzani na hasa NCCR.

Wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM walikuwa tayari kupitisha azimio hilo la kuomuongezea Mwinyi awamu ya tatu kwa wasi wasi wa kupoteza uchaguzi mwaka uliofuata.

Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alijitokeza na kupinga kwa nguvu azimio hilo akionya kuwa Katiba si kama shati unalochagua uvae lipi kila ukiamka.

Wazo la Mwinyi kuendelea likafa kibudu lakini CCM ikaendelea kuwa pamoja licha ya wagombea kujitokeza huku kampeni za kumpata mrithi zikiendelea bila mizengwe.

Mwaka huu Chadema nayo imejikuta iko njia panda na wajumbe wana wasiwasi kuwa mwenyekiti aking'atuka hawajui hatma yao na chama kwa ujumla itakuwaje .

Je wazee wenye hekima, busara na ushawisi kama Mwalimu hawapo tena? Woga wangu ni kuwa inawezekana wapo wajumbe ambao hawana maisha nje ya Chadema.

KIla baada ya miaka mitano Watanzania wenzetu wengi hujitokeza kugombea Urais Tanzania lakini, pamoja na mizengwe, mwisho wa siku sote tunabaki ni Watanzania.

Kwa nini kwa Chadema, chama cha kidemokrasia na maendeleo, hii isiwezekane kwa wagombea kujitokeza na wana Chadema wakabaki wamoja baada ya uchaguzi?

Najua jinsi ndani ya CCM, chama cha majizi kinachoendeshwa kimla, hili haliwezi kutokea na watafanya kila wawezalo kuhujumu uchaguzi huru na kuwasambaratisha.

Walaaniwe wale wote watakaojaribu kuuvuruga uchaguzi wa Chadema utakaofanyika tarehe 23/1/2025 kwani ni uchaguzi unaotazamiwa kuwa wa kihistoria nchini.

Tahadhari...nawaomba wana Chadema, kwa kuwa mnajua mnaandika historia, hiyo hiyo historia itawahukumu na kama kutatokea mizengewe isiyo ya lazima...hatutawasemehe!
Mimi binafsi sina tatizo na Lissu kugombea Uenyekiti. Naamini inaonyesha ukomavu wa chama chake. Ninachopinga ni namna alivyoingia kwenye hicho kinyang'anyiro. Hapakuwa na sababu za kumpaka matope Mwenyekiti aliyekuwepo. Yeye angejikita kwenye kuuelezea umma sababu za yeye kuamua kugombea. Na pale surrogates au wafuasi wake walipoanza kumsema vibaya Mbowe angewanyamazisha kama vile McCain alivyofanya pale shabiki wake alipotaka kupaka matope Obama. Yeye bado relatively ni kijana ambae bado ana nafasi ya kugombea urais na Uenyekiti hata mwaka 2030. Alikosea kuacha kampeni ya kumfanya Mbowe aonekane ndio villain namba moja wa Chadema iendelee. Hapo ndipo aliponi boa.

Amandla...
 
Ndivyo mlivyopanga, ndivyo mnavyopanga na ndivyo CCM inavyotaka. Mimi naamini wako wana Chadema tena wengi ambao hawapati maslahi yoyote ndani ya Chadema.

Mbowe kama angewasikiliza hao wana mageuzi wa kweli na si wale wenye maslahi na uwepo wake wawe wana Chadema, CCM au vyama maslahi, angeng'atuka abaki mshauri tu.

Mbowe amekuwa kama mfungwa na nachelea kusema kusema sidhani kama anayo mawazo huru tena. Mbowe wa miaka ya nyuma sidhani kama ni huyu aliyetangaza kutetea kiti.
Kwanza let me declare interest: nilijiunga na CHASO 2012, nikaachana na CHADEMA 2015 walipoamua kulamba matapishi.

Ninatamani sana Lissu ashinde, walau ana unafuu miongoni mwa wanasiasa wengi. Lakini to be realistic; CCM, Mbowe na vibaraka wake hawataruhusu.

Mbowe hajawahi kuwa mpinzani wa kweli kuanzia mwanzo, ni vile umechelewa tu kumfahamu.
 
Mimi binafsi sina tatizo na Lissu kugombea Uenyekiti. Naamini inaonyesha ukomavu wa chama chake. Ninachopinga ni namna alivyoingia kwenye hicho kinyang'anyiro. Hapakuwa na sababu za kumpaka matope Mwenyekiti aliyekuwepo. Yeye angejikita kwenye kuuelezea umma sababu za yeye kuamua kugombea. Na pale surrogates au wafuasi wake walipoanza kumsema vibaya Mbowe angewanyamazisha kama vile McCain alivyofanya pale shabiki wake alipotaka kupaka matope Obama. Yeye bado relatively ni kijana ambae bado ana nafasi ya kugombea urais na Uenyekiti hata mwaka 2030. Alikosea kuacha kampeni ya kumfanya Mbowe aonekane ndio villain namba moja wa Chadema iendelee. Hapo ndipo aliponi boa.

Amandla...

..kwa sasa hivi Chadema ni chama tegemeo kwa Watanzania.

..Watanzania walio wengi wanaamini hicho ndicho chama pekee cha upinzani kilichobaki.

..Wajumbe wa Mkutano Mkuu watapiga kura kwa niaba ya Watanzania wasio na nafasi ya kupiga kura.

..Mgombea watakayemchagua anapaswa kuwa yule atakayewashawishi Watanzania kuendelea kuiamini Chadema.
 
Mbowe amekuwa kama mfungwa na nachelea kusema kusema sidhani kama anayo mawazo huru tena. Mbowe wa miaka ya nyuma sidhani kama ni huyu aliyetangaza kutetea kiti.
Kwa maelezo haya upo upande wa T. A. Lissu.
===
Karibu sana Mwalimu wangu wa Tuisheni hapa JF
 
..kwa sasa hivi Chadema ni chama tegemeo kwa Watanzania.

..Watanzania walio wengi wanaamini hicho ndicho chama pekee cha upinzani kilichobaki.

..Wajumbe wa Mkutano Mkuu watapiga kura kwa niaba ya Watanzania wasio na nafasi ya kupiga kura.

..Mgombea watakayemchagua anapaswa kuwa yule atakayewashawishi Watanzania kuendelea kuiamini Chadema.
Katika hao watanzania kuna wanachama wa ACT Wazalendo, CCM n.k. Kwa hao Chadema sio tegemeo lao.

Watanzania wa Unguja na Pemba hawakiona kama ni chama pekee cha upinzania

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wanapiga kura kwa niaba ya wanachama wenzao na sio watanzania wote. Katika huo uchaguzi priority ni future ya Chadema, sio ya Tanzania.

Kazi kubwa ya atakaeshinda ni kuhakikisha kuwa wanachama wenzake wanaendelea na imani na viongozi wao kuwa watakiongoza chama chao kwa weledi na uaminifu. Wakifanya hivyo ndio watanzania wengi watakuwa na imani na hicho chama. Hamna mtu atakayekiamini chama ambacho hakina muelekeo na kila siku watu wanagombana.

Amandla...
 
Katika hao watanzania kuna wanachama wa ACT Wazalendo, CCM n.k. Kwa hao Chadema sio tegemeo lao.

Watanzania wa Unguja na Pemba hawakiona kama ni chama pekee cha upinzania

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wanapiga kura kwa niaba ya wanachama wenzao na sio watanzania wote. Katika huo uchaguzi priority ni future ya Chadema, sio ya Tanzania.

Kazi kubwa ya atakaeshinda ni kuhakikisha kuwa wanachama wenzake wanaendelea na imani na viongozi wao kuwa watakiongoza chama chao kwa weledi na uaminifu. Wakifanya hivyo ndio watanzania wengi watakuwa na imani na hicho chama. Hamna mtu atakayekiamini chama ambacho hakina muelekeo na kila siku watu wanagombana.

Amandla...

..wanahitaji Mwenyekiti atakayewavuta Watanzania wengi zaidi waiunge mkono Chadema. Mtu ambaye Watanzania wana imani naye.

NB:

..vyama vingine vya upinzani ambavyo ni serious vinatamani kufanya kazi na Chadema.
 
..wanahitaji Mwenyekiti atakayewavuta Watanzania wengi zaidi waiunge mkono Chadema. Mtu ambaye Watanzania wana imani naye.

NB:

..vyama vingine vya upinzani ambavyo ni serious vinatamani kufanya kazi na Chadema.
Chama sio Mwenyekiti peke yake. Naamini kuna wengi walijenga imani na Chadema kutokana na watu kama Halima Mdee, Lissu, Heche na hata watu kama Mdude Nyangali. Wote hawa hawakuwa wenyeviti. Kazi kubwa ya Mwenyekiti ni kutambua uwezo uliokuwemo ndani ya chama chake na kuutumia ipasavyo. Chama hakitakiwi kuwa cha mtu mmoja. Kumtegemea Lissu ndio kutakipeleka huko.

Amandla...
 
Chama sio Mwenyekiti peke yake. Naamini kuna wengi walijenga imani na Chadema kutokana na watu kama Halima Mdee, Lissu, Heche na hata watu kama Mdude Nyangali. Wote hawa hawakuwa wenyeviti. Kazi kubwa ya Mwenyekiti ni kutambua uwezo uliokuwemo ndani ya chama chake na kuutumia ipasavyo. Chama hakitakiwi kuwa cha mtu mmoja. Kumtegemea Lissu ndio kutakipeleka huko.

Amandla...

..Chadema inahitaji Mwenyekiti atakayewatia hamasa viongozi na wanachama kukijenga chama chao.

..Pia Mwenyekiti mjenga hoja mzuri, anayeaminika ndani na nje ya chama, atakayeshawishi Watanzania wengi zaidi kujiunga, au kuiunga mkono Chadema.
 
Back
Top Bottom