Kwa kumbukumbu...yanayotokea kwa Chadema mwaka huu, yalitokea kwa CCM mwaka 1994!

Kwa kumbukumbu...yanayotokea kwa Chadema mwaka huu, yalitokea kwa CCM mwaka 1994!

Mkuu Asante kwa maelezo ya kina. Hata hivyo, hivi kusema Aikael hajafikisha miaka 68 hivyo anatakiwa Agombee hiyo ni hoja kweli?
Mkuu mbona unapotosha? Mbowe amesema hatagombea tena. Ili kukazia hiyo nia ya kutogombea tena ndio alisema kuwa wakati huo atakuwa na miaka 68. Hakusema kuwa anagombea kwa sababu hajafikisha miaka 68. Kwa Katiba yao ilivyo, hata kama atashindwa safari hii ana haki ya kugombea tena 2030. Kwa hii ahadi yake ni kuwa hatagombea tena hata akishindwa.

Amandla....
 
Ni imani yako. Sasa tusubiri maamuzi ya wapiga kura.

Amandla...
Eti uchaguzi, you've got to be kidding! Bila shaka ulishuhudia uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu uliosimamiwa na TAMISENI, je ule unauita uchaguzi? TAMISENI walihakikisha wagombea wao wanashinda kwa asilimia 99%!
 
Ndivyo mlivyopanga, ndivyo mnavyopanga na ndivyo CCM inavyotaka. Mimi naamini wako wana Chadema tena wengi ambao hawapati maslahi yoyote ndani ya Chadema.

Mbowe kama angewasikiliza hao wana mageuzi wa kweli na si wale wenye maslahi na uwepo wake wawe wana Chadema, CCM au vyama maslahi, angeng'atuka abaki mshauri tu.

Mbowe amekuwa kama mfungwa na nachelea kusema sidhani kama anayo mawazo huru tena. Mbowe wa miaka ya nyuma sidhani kama ni huyu aliyetangaza kutetea kiti.
Munamfanya Lissu kama vile mtakatiiiiifu!!! na wengine mashetani tu!!!
 
Eti uchaguzi, you've got to be kidding! Bila shaka ulishuhudia uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu uliosimamiwa na TAMISENI, je ule unauita uchaguzi? TAMISENI walihakikisha wagombea wao wanashinda kwa asilimia 99%!
Uchaguzi wa Chadema utasimamiwa na TAMISEMI? Au unataka kutuambia kuwa uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema utauona wa haki tuu kama Lissu atashinda? Hiyo si itakuwa bad faith?
Mimi hapo ndipo mnaponishangaza. Najua Mbowe atakubali kushindwa na atampongeza Lissu kama ndie atakayeshinda. Na atawataka wafuasi wake wampe ushirikiano Mwenyekiti mpya. Wakati kama upande wenu utashindwa mtatumia play book ya Trump kuwa uchaguzi ulikuwa na figisu figisu. Visingizio vitakuwa vingi na mtawataka wenzenu ( pamoja na mgombe wenu) wasitoe ushirikiano wowote kwa Mbowe.

Amandla...
 
Kuna tatizo gani kusubiri sanduku la kura liamue? Wagombea 3 wamechukua fomu sasa si tusubiri nani ataibuka kidedea? Au mlitaka Mbowe ajitoe? Hoja ni nini hasa hapa?? Uchaguzi usifanyike au kuwe na mgombea mmoja tuu TAL???
Hii hoja iko sawa
 
Nimecheka kinoma, eti bora uwe ccm. Yaani uache chama unachoweza kuwa huru, ukahamie kwenye chama cha machawa na nidhamu za woga?!
Hakuna tofauti mkuu.. ya nini Maigizo?
 
Huu uchaguzi ndani ya Chadema kama utafanikiwa kama ninavyotumainia, kwa mara ya kwanza tutapata fursa ya kushuhudia demokrasia ya kweli kazini.
Umenidownplay, ila hilo naliacha kwanza!

Unatumainia nini kwenye huu uchaguzi?
 
Umenidownplay, ila hilo naliacha kwanza!
Sijakudownplay (your words sic!) ila kwa bahati wewe unayo choice...Chadema ikikuzingua, CCM inakusubiri kwa mikono miwili. Wengine hatuna hiyo choice, hakuna namna naweza nikahamia chama hicho...not over my dead body!
Unatumainia nini kwenye huu uchaguzi?
Wapambe maslahi ni wa kuogopwa kama ukimwi.

Baba wa taifa alitaka kuachia uongozi mapema sana lakini wapambe maslahi hawakuwa tayari, walimlilia wakitaka aendelee kwa kudai hakuwepo mtu wa kuvaa viatu vyake.

Mwaka 1975 wapambe maslahi walimsihi aendelee wakidai haukuwa wakati muafaka wa kuachia madaraka kati ya chochoko za Idi Amin Dada wa Uganda zilikuwa zimepamba moto.

Mwaka 1980, wapambe hao hao nuksi walimuomba aendelee tena wakidai ndiyo tumetoka vitani (vita vya Kagera) na hivyo uongozi wake bado ulihitajika kuliko wakati wowote ule!

Mwalimu alikubali lakini kwa sharti moja ingekuwa awamu yake ya mwisho na kweli mwaka 1985 aling'atuka baada ya kutembea nchi nzima akimnadi mrithi wake Hasan Mwinyi wa Zanzibar.

Sasa shuhudia lawama alizopewa Mwalimu baada ya kung'atuka madarakani alipopinga Mwinyi huyo huyo kuongezewa miaka mingine mitano baada ya kumaliza muda wake mwaka 1995!

Wapambe maslahi wa Mwinyi walimtaka Mwalimu akae kimya wakidai inakuwaje apinge wakati yeye mwenyewe aling'ang'ania madaraka kwa miaka zaidi ya ishirini bila kumpisha mtu!

Chama kile kile, wapambe wale wale...na sasa tunawashuhudia wapambe wa mwenyekiti wa chama mbadala Chadema wakiwa kazini wakifuata nyayo za wapambe wa CCM, hakuna cha ajabu!

Birds of a feather fly together...ndege wafananao huruka pamoja! Ni Lissu tu ndio mpaka sasa ameaonesha nia na ari ya kulikwamua taifa letu kutoka mikononi mwa walafi, wanafiki na wafuata nyayo!
 
Uchaguzi wa Chadema utasimamiwa na TAMISEMI?
Wapi nimesema TAMISENI ndio itasimamia uchaguzi wa Chadema? This is too low coming from you!
Au unataka kutuambia kuwa uchaguzi wa Mwenyekiti wa Chadema utauona wa haki tuu kama Lissu atashinda?
Wapambe wa mwenyekeiti ndio hao hao watakaosimamia uchaguzi labda mambo yabadilike.
Hiyo si itakuwa bad faith?
I have no idea what you are talking about sir!
 
Eti uchaguzi, you've got to be kidding! Bila shaka ulishuhudia uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu uliosimamiwa na TAMISENI, je ule unauita uchaguzi? TAMISENI walihakikisha wagombea wao wanashinda kwa asilimia 99%!
Mag3, Unaanzaje kuingiza TAMISEMI kwenye mjadala unaohusu uchaguzi wa CHADEMA unless kama kwa njia moja au nyingine una insinuate kuwa TAMISEMI watahusika na huo uchaguzi. Mimi naona katika juhudi zako za kum legitimise Mbowe unatumia mifano ambayo sio sahihi. Kwa nini haukusema Mbowe ana behave kama dictator alipo ram through appointment ya Lissu kuwa Makamu Mwenyekiti? Kuanza kusema leo ( kama alivyosema Lissu) kuwa Mbowe atahujumu ( in fact, Lissu ame hint kuwa tayari ameanza taratibu za kujaza kura za bandia, kuiba mabox ya kura kama vile TAMISEMI walivyofanya) uchaguzi ni mpango wa kuondoa uwezekano wa kushindwa kwa Lissu. Hatua inayofuata ni kusema hamna imani na sekretariat. Kwa kweli huu mchezo mnaocheza hauna tija kwa Chadema.

Amandla...
 
Wapi nimesema TAMISENI ndio itasimamia uchaguzi wa Chadema? This is too low coming from you!

Wapambe wa mwenyekeiti ndio hao hao watakaosimamia uchaguzi labda mambo yabadilike.

I have no idea what you are talking about sir!
Kasome tena ulicho andika. Sasa kama hamna imani na sekretariat ambayo siku zote imekuwa inasimamia chaguzi kwa nini mnagombea? Imani yenu ni transactional? Kuwa inaonekana haiko biased pale tu matokeo ya uchaguzi yanapo wafurahisha? Badala ya kutoa unfounded allegations kwa nini msikae mka propose namna ya ku secure uchaguzi ili uwe transparent na fair?

If you have no idea what I am talking about, hamna kilicho haribika.

Mimi ningetegemea priority ya kwanza ya mgombea uchaguzi ni kuhakikisha chama kinabaki salama baada ya uchaguzi hata kama atashindwa. Mnachofanya ni kutoboa mtumbwi uliowabeba na atakaefaidika ni vyama ambavyo havikitakii Chadema mema. Inasikitisha sana kuwa mmefika hapo.

Amandla...
 
Kuna tatizo gani kusubiri sanduku la kura liamue? Wagombea 3 wamechukua fomu sasa si tusubiri nani ataibuka kidedea? Au mlitaka Mbowe ajitoe? Hoja ni nini hasa hapa?? Uchaguzi usifanyike au kuwe na mgombea mmoja tuu TAL???
Hawa watu walitegemea wakim bully kwa false allegations hatachukua fomu. Sasa hiyo imebuma wameanza kusambaza rumors kuwa ana mpango wa kuiba maboksi ya kura na kujaza kura feki ili ashinde. Wao wanachotaka ni coronation ya mtu wao, sio uchaguzi wa ushindani. Hawa wako tayari CDM isambaratike kama mtu wao hatashinda.

Amandla...
 
Back
Top Bottom