Kwa kumbukumbu...yanayotokea kwa Chadema mwaka huu, yalitokea kwa CCM mwaka 1994!

Kwa kumbukumbu...yanayotokea kwa Chadema mwaka huu, yalitokea kwa CCM mwaka 1994!

..Chadema inahitaji Mwenyekiti atakayewatia hamasa viongozi na wanachama kukijenga chama chao.

..Pia Mwenyekiti mjenga hoja mzuri, anayeaminika ndani na nje ya chama, atakayeshawishi Watanzania wengi zaidi kujiunga, au kuiunga mkono Chadema.
Hapo tunakubaliana ila mimi naona mtu mwenye hizo sifa ni Freeman Aikaeli Mbowe. Na amefanya hivyo kwa zaidi ya miaka 20.

Huyu ni mtu aliyekubali kukaa meza moja na mtu aliyemuweka ndani kwa zaidi ya miezi 7 kwa manufaa ya chama chake. Huo ni ukomavu, sio uoga. Ingekuwa rahisi sana kwake kugoma kukutana nae na jamii ingemuelewa lakini hakufanya hivyo.

Kwangu mimi Lissu amepoteza sifa hizo kwa matendo yake ya hivi karibuni ambayo yanaweza kujenga jeraha katika chama ambalo hana uwezo wa kulitibu.

Amandla...
 
Hapo tunakubaliana ila mimi naona mtu mwenye hizo sifa ni Freeman Aikaeli Mbowe. Na amefanya hivyo kwa zaidi ya miaka 20.

Huyu ni mtu aliyekubali kukaa meza moja na mtu aliyemuweka ndani kwa zaidi ya miezi 7 kwa manufaa ya chama chake. Huo ni ukomavu, sio uoga. Ingekuwa rahisi sana kwake kugoma kukutana nae na jamii ingemuelewa lakini hakufanya hivyo.

Kwangu mimi Lissu amepoteza sifa hizo kwa matendo yake ya hivi karibuni ambayo yanaweza kujenga jeraha katika chama ambalo hana uwezo wa kulitibu.

Amandla...

..kwa maoni yangu Lissu ndiye mwanasiasa ambaye Watanzania wanamuamini zaidi sasa hivi.
 
..kwa maoni yangu Lissu ndiye mwanasiasa ambaye Watanzania wanamuamini zaidi sasa hivi.
Sio kila mtu anayeaminiwa na wengi ndie anayefaa. Wengi tulimuamini Lyatonga kumbe ni bonus. Kwa matendo yake ya hivi karibuni namuweka Lissu katika kundi la egocentric populists kama alivyokuwa Mrema. Nilikuwa na imani kubwa kwake but no more.

Amandla...
 
Kwa yaliyopo CHADEMA ni bora mtu uwe tu CCM, hawana uafadhali wa kuzidi CCM. Maybe siku chama kikiacha Kuongozwa kama Kikoba cha Mbowe!
Alfred, haya yako ni mawazo mfu yanayoonesha hakuna unalolijua ama kuhusu vyama vyetu vya siasa au kuhusu Tanzania ilikotoka, ilipo na inakoelekea.

Huo uafadhali wa CCM sijui unaupimaje. Mimi hapa siongei kama mwana Chadema, naongea kama mwanachi ambaye haridhiki kabisa na CCM inakotupeleka.

Sijawahi kuipenda CCM toka kuasisiwa kwake na ni moja wa watu waliopiga vigelele upepo wa mageuzi ulipopiga hodi nchini na kupelekea mfumo wa vyama vingi.

Huu uchaguzi ndani ya Chadema kama utafanikiwa kama ninavyotumainia, kwa mara ya kwanza tutapata fursa ya kushuhudia demokrasia ya kweli kazini.

Natoa tu tahadhari kwa Chadema kwamba wasithubutu kutoa nafasi kwa kutanguliza maslahi binafsi badala sa maslahi ya Watanzania wote kwa ujumla wao bila ubaguzi.
 
Sio kila mtu anayeaminiwa na wengi ndie anayefaa. Wengi tulimuamini Lyatonga kumbe ni bonus. Kwa matendo yake ya hivi karibuni namuweka Lissu katika kundi la egocentric populists kama alivyokuwa Mrema. Nilikuwa na imani kubwa kwake but no more.

Amandla...

..Lissu ni binadamu na ana mapungufu yake.

..kwa maoni yangu Lissu anayo mengi mazuri ya kukiaminisha chama kwa Watanzania.

..Na zaidi Watanzania wana imani kubwa naye.

..Mazingira ya sasa hivi yanahitaji kiongozi wa upinzani anayeaminika, mwenye kuweza kushawishi.

..Mbowe anaweza boardroom politics, wakati mazingira ya kisiasa yako fair.
 
..kwa maoni yangu Lissu ndiye mwanasiasa ambaye Watanzania wanamuamini zaidi sasa hivi.
Tundu Antiphas Lissu anayo historia ambayo haitaweza kufutika kirahisi kwa ujasiri wake na uthubutu wake katika kutetea uhuru, haki na utawala wa sheria bila kusahau weledi wake.

Hizo sifa ni kudra sana kwa wanasiasa walio wengi ambao misimamo yao hubadilika kulingana na matamanio binafsi ambayo ndio mbolea ya unafiki tunaoushudia katika jamii zetu.
 
Tundu Antiphas Lissu anayo historia ambayo haitaweza kufutika kirahisi kwa ujasiri wake na uthubutu wake katika kutetea uhuru, haki na utawala wa sheria bila kusahau weledi wake.

Hizo sifa ni kudra sana kwa wanasiasa walio wengi ambao misimamo yao hubadilika kulingana na matamanio binafsi ambayo ndio mbolea ya unafiki tunaoushudia katika jamii zetu.

..Chama kimepotea mioyoni mwa Watanzania.

..sina uhakika kama Mbowe anaweza kukirudisha.

..Na muda sio rafiki.
 
Sio kila mtu anayeaminiwa na wengi ndie anayefaa. Wengi tulimuamini Lyatonga kumbe ni bonus. Kwa matendo yake ya hivi karibuni namuweka Lissu katika kundi la egocentric populists kama alivyokuwa Mrema. Nilikuwa na imani kubwa kwake but no more.

Amandla...
Ndugu yangu Fundi Mchundo, nashangaa unavyojaribu kumshusha Lissu hadi kumweka kundi la Mzee wa Kiraracha. hapana, hapo mimi na wewe tutatofautiana sana tu.

Yawezekana humjui Lissu na hujui juhudi wala harakati zake katika kutetea haki tangu akiwa kijana na mara nyingi kwa kujitolea, hapana, Lissu na Mrema ni kama maji na mafuta!
 
..Lissu ni binadamu na ana mapungufu yake.

..kwa maoni yangu Lissu anayo mengi mazuri ya kukiaminisha chama kwa Watanzania.

..Na zaidi Watanzania wana imani kubwa naye.

..Mazingira ya sasa hivi yanahitaji kiongozi wa upinzani anayeaminika, mwenye kuweza kushawishi.

..Mbowe anaweza boardroom politics, wakati mazingira ya kisiasa yako fair.
Hapana. Board room politics ndio wakati wake sasa. Na kusema kuwa anafanya hizo tu sio kumtendea haki. Mbowe ameonyesha uwezo mkubwa wa kuorganise protests n.k. Uzuri wake yuko pia willing kulipia gharama.

Tatizo letu watanzania tunapenda majibu mepesi kwenye maswali magumu. Tunawapenda wale ambao wanatuambia kuwa watapigana kwa ajili yetu kuliko wale wanaotuonyesha kuwa watapigana pamoja nasi.

Sio bure watu kama Babu wa Loliondo, Mwamposa, Gwajima na wengine wanakuwa na wafuasi wengi. Hii ni kwa sababu wana ofa miracle cures zinazotoa majibu immediately. Kwa mtindo huo hatutafika mbali.

Amandla...
 
Ndugu yangu Fundi Mchundo, nashangaa unavyojaribu kumshusha Lissu hadi kumweka kundi la Mzee wa Kiraracha. hapana, hapo mimi na wewe tutatofautiana sana tu.

Yawezekana humjui Lissu na hujui juhudi wala harakati zake katika kutetea haki tangu akiwa kijana na mara nyingi kwa kujitolea, hapana, Lissu na Mrema ni kama maji na mafuta!
Mimi simjui Lissu kama vile ambavyo simjui Mbowe. Naenda kwa matendo yao. Najua kuwa ni activist na aliwapamb
ania sana wachimbaji wa madini. Najua kuwa anajua kupanga hoja na haogopi kusema ukweli to power.

Kwangu mimi ni hizi machinations zake za hivi karibuni ndiyo zilizonifanya niangalie beneath the glitter na nimuweke kundi moja na wakina Mrema.

Kwenye hilo tutaendelea kutofautiana.

Amandla...
 
Ndivyo mlivyopanga, ndivyo mnavyopanga na ndivyo CCM inavyotaka. Mimi naamini wako wana Chadema tena wengi ambao hawapati maslahi yoyote ndani ya Chadema.

Mbowe kama angewasikiliza hao wana mageuzi wa kweli na si wale wenye maslahi na uwepo wake wawe wana Chadema, CCM au vyama maslahi, angeng'atuka abaki mshauri tu.

Mbowe amekuwa kama mfungwa na nachelea kusema sidhani kama anayo mawazo huru tena. Mbowe wa miaka ya nyuma sidhani kama ni huyu aliyetangaza kutetea kiti.
Mkuu Mag3 . Mbowe hana nguvu yoyote ndani ya CHADEMA ya kushinda uchaguzi bila kusaidiwa na CCM. Hapa ndipo lilipo tatizo. Ni hivi: Samia ni rais wa kwanza kuchukiwa na wananchi na anajua uchaguzi ujao ana kazi ya ziada. Unajua mwaka 2020 Lissu alipata kura nyingi sana na hili ndilo haswa linalomwopesha Samia. Ameamua kutumia fedha na ghilba ili kumteka Mbowe na tayari amefanikiwa. Kusema kweli mimi sioni CHADEMA ikisalimika kwa namna yoyote, Mbowe akifanikiwa kupora uchaguzi. Mbowe akishinda sioni wananchi wapenda mageuzi waki-support tena CHADEMA na itakuwa kama CUF. Lissu akihama anaweza kuvutia watu wengi lakini ataenda wapi? Wazalendo kuna mtu kama Zitto ambaye naye anaweza kufananishwa na Mbowe.
 
Hapana. Board room politics ndio wakati wake sasa. Na kusema kuwa anafanya hizo tu sio kumtendea haki. Mbowe ameonyesha uwezo mkubwa wa kuorganise protests n.k. Uzuri wake yuko pia willing kulipia gharama.

Tatizo letu watanzania tunapenda majibu mepesi kwenye maswali magumu. Tunawapenda wale ambao wanatuambia kuwa watapigana kwa ajili yetu kuliko wale wanaotuonyesha kuwa watapigana pamoja nasi.

Sio bure watu kama Babu wa Loliondo, Mwamposa, Gwajima na wengine wanakuwa na wafuasi wengi. Hii ni kwa sababu wana ofa miracle cures zinazotoa majibu immediately. Kwa mtindo huo hatutafika mbali.

Amandla...
Acha hizo wewe kibaraka wa Mbowe. Mbowe ame organise protest gani? Labda hujui maana yake? Kiongozi amekaa miaka 20 ana nini ambacho hajafanya? Huu ni mwaka wa 2025 na bado kuna watu wanashadidia uongozi wa maisha! Kwa nini asiondoka na kuachia wengine washindane.
 
Mimi simjui Lissu kama vile ambavyo simjui Mbowe. Naenda kwa matendo yao. Najua kuwa ni activist na aliwapamb
ania sana wachimbaji wa madini. Najua kuwa anajua kupanga hoja na haogopi kusema ukweli to power.

Kwangu mimi ni hizi machinations zake za hivi karibuni ndiyo zilizonifanya niangalie beneath the glitter na nimuweke kundi moja na wakina Mrema.

Kwenye hilo tutaendelea kutofautiana.

Amandla...
Unajua ni wa nini nchi zilizoendelea wanabadilisha viongozi wa vyama vya siasa kila wanaposhindwa uchaguzi? Mbowe ameongoza CHADEMA vizuri sana kwa kipindi alichokaa lakini siku za karibuni kuna blunders nyingi alizofanya kiasi cha kufanya mabadiliko ya uongozi kuwa lazima.
 
Kwa maelezo haya upo upande wa T. A. Lissu.
Duh TUJIGEMEE, kwa namna moja uko sawa lakini kamwe si kama unavyowaza, mimi siku zote niko upande wa uhuru, haki na utawala wa sheria. Mpaka hapo uko sawa niko upande wa T.A. Lissu.

Lakini hapa tena si habari ya kuwa upande wa mtu binafsi, nawapenda Lissu na Mbowe kwa pamoja lakini si kwa kila jambo. Wote wawili ni binadamu na hakuna binadamu asiye na mapungufu

Mimi ni mpenda demokrasia na nilitegemea wagombea wengi tu kujitokea kugombea hicho kiti lakini kitendo cha Mbowe kujitokeza kutetea hicho kiti alichokikalia kwa miaka zaidi ya ishirini, kilishtua!

Ukweli lazima usemwe, Mbowe anaungwa mkono zaidi na wajumbe wenye maslahi katika uenyekiti wake. Kitendo chake kimesaliti dhana ya demokrasia ndani ya Chadema tegemeo pekee la wananchi.

Binafsi nilipigwa butwaa nikakumbuka kauli ya jiwe kwenye uchaguzi mkuu wa 2020 kwa wasimamizi nanukuu si kila neno, "nikuteue, nikulipe mshahara halafu umtangaze mpinzani kuwa kashinda!"

Mpaka hapo tofauti ya Chadema na chama cha wezi CCM ni ipi?
 
Hapana. Board room politics ndio wakati wake sasa. Na kusema kuwa anafanya hizo tu sio kumtendea haki. Mbowe ameonyesha uwezo mkubwa wa kuorganise protests n.k. Uzuri wake yuko pia willing kulipia gharama.

Tatizo letu watanzania tunapenda majibu mepesi kwenye maswali magumu. Tunawapenda wale ambao wanatuambia kuwa watapigana kwa ajili yetu kuliko wale wanaotuonyesha kuwa watapigana pamoja nasi.

Sio bure watu kama Babu wa Loliondo, Mwamposa, Gwajima na wengine wanakuwa na wafuasi wengi. Hii ni kwa sababu wana ofa miracle cures zinazotoa majibu immediately. Kwa mtindo huo hatutafika mbali.

Amandla...

..Lissu hajaahidi majibu ya papo kwa papo, na miujiza.

..infact amesema mambo ni mengi, tena magumu, na muda ni mchache.

..kwa maoni yangu Chadema imedorora sana siku za hivi karibuni.

..Inahitaji kiongozi anayeonyesha sense of urgency, na anayekubalika na wananchi.

..Na Chadema peke yao hawawezi.

..Hakuna wakati Chadema inawahitaji Watanzania kama kipindi hiki.

..Wajumbe wachague Mwenyekiti anayeungwa mkono, na anayejibu matarajio ya Watanzania.

..Mwenyekiti wa Chadema anapaswa kuwa daraja kati ya wananchi wa kawaida, na chama.
 
Acha hizo wewe kibaraka wa Mbowe. Mbowe ame organise protest gani? Labda hujui maana yake? Kiongozi amekaa miaka 20 ana nini ambacho hajafanya? Huu ni mwaka wa 2025 na bado kuna watu wanashadidia uongozi wa maisha! Kwa nini asiondoka na kuachia wengine washindane.
Mwingine huyu ambae sina muda wa kujibishana nae.

Amandla...
 
..Lissu hajaahidi majibu ya papo kwa papo, na miujiza.

..infact amesema mambo ni mengi, tena magumu, na muda ni mchache.

..kwa maoni yangu Chadema imedorora sana siku za hivi karibuni.

..Inahitaji kiongozi anayeonyesha sense of urgency, na anayekubalika na wananchi.

..Na Chadema peke yao hawawezi.

..Hakuna wakati Chadema inawahitaji Watanzania kama kipindi hiki.

..Wajumbe wachague Mwenyekiti anayeungwa mkono, na anayejibu matarajio ya Watanzania.

..Mwenyekiti wa Chadema anapaswa kuwa daraja kati ya wananchi wa kawaida, na chama.
Una haki na maoni yako. Lakini mimi siwezi kumkubali mtu ambae alikaa kimya wakati watu wanamtusi matusi ya nguoni mtu ambae bado ni Mwenyekiti wake. Watu wanamuita Mbowe kibaraka wa CCM, amelambishwa asali, chawa wa CCM, muuaji, mwizi, mlevi, hajakifanyia chama chake chochote lakini yeye na wafuasi wake wanakaa kimya. Huyo sio mtu wa kuaminika hata kidogo.

Kama Lissu anakubalika kiasi hicho kwa nini hamtaki ashindane na Mbowe? Akifanyiwa figisu figisu si wafuasi wake wataamka kuhakikisha kuwa haki itatendeka? Na akiona vipi, si ataweza kuondoka na kuliacha hilo jaazi linalozama kama alivyofanya Maalim alipoondoka CUF na kuhamia ACT Wazalendo?

Hii vitriol dhidi ya Mbowe inatoka wapi? Na mnategemea mwisho wake utakuwa nini? Au mnadhania Mbowe hana wafuasi?

Amandla...
 
Kwa yaliyopo CHADEMA ni bora mtu uwe tu CCM, hawana uafadhali wa kuzidi CCM. Maybe siku chama kikiacha Kuongozwa kama Kikoba cha Mbowe!
Nimecheka kinoma, eti bora uwe ccm. Yaani uache chama unachoweza kuwa huru, ukahamie kwenye chama cha machawa na nidhamu za woga?!
 
Una haki na maoni yako. Lakini mimi siwezi kumkubali mtu ambae alikaa kimya wakati watu wanamtusi matusi ya nguoni mtu ambae bado ni Mwenyekiti wake. Watu wanamuita Mbowe kibaraka wa CCM, amelambishwa asali, chawa wa CCM, muuaji, mwizi, mlevi, hajakifanyia chama chake chochote lakini yeye na wafuasi wake wanakaa kimya. Huyo sio mtu wa kuaminika hata kidogo.

Kama Lissu anakubalika kiasi hicho kwa nini hamtaki ashindane na Mbowe? Akifanyiwa figisu figisu si wafuasi wake wataamka kuhakikisha kuwa haki itatendeka? Na akiona vipi, si ataweza kuondoka na kuliacha hilo jaazi linalozama kama alivyofanya Maalim alipoondoka CUF na kuhamia ACT Wazalendo?

Hii vitriol dhidi ya Mbowe inatoka wapi? Na mnategemea mwisho wake utakuwa nini? Au mnadhania Mbowe hana wafuasi?

Amandla...

..kasikilize Powerbreakfast ya Clouds Media ndio utasikia maoni ya Tundu Lissu kuhusu Mwenyekiti Freeman Mbowe.

..sio sahihi kumlaumu Lissu, na hata Mbowe, kwa maneno, kejeli, na matusi, ya wapambe.

..Watanzania wako pale wanasubiri kuona kama wajumbe watachagua Mwenyekiti anayejibu matarajio ya wananchi, au la.

..Taifa linahitaji Mwenyekiti wa Chadema mwenye rekodi ya uadilifu, mwenye msimamo thabiti, mjenga hoja mahiri, na msomi anayeijua nchi, na dunia.
 
Back
Top Bottom