Kwa kumbukumbu...yanayotokea kwa Chadema mwaka huu, yalitokea kwa CCM mwaka 1994!

CHADEMA, kila unapofika uchaguzi wa mwenyekiti hua mizengwe at the very least mmoja uhama chama. Tuliona kwa akina Kabulu, Chacha, Zitto na sasa Lisu. Hii ya Lisu ndo kamwendelezo kalekale tena hakana nguvu sana safari hii.
 
Pamoja na kuwa inaelekea unadhani kuwa mimi ni kibaraka wa Mbowe, nitaingiza my two cents. Hamuwezi kulinganisha vyama tawala na vyama vya upinzani. Vyama vya upinzani vinahitaji mtu ambae ana uzoefu na ameonyesha uwezo wa kukiwezesha chama chake ki survive katika mapito magumu. Kitendo cha Lissu kurudi nchini na kuanza kukandia chama chake hadharani hakikuonyesha leadership qualities.

Mfano wa nchi zilizoendelea hauna tija hapa. Marekani ili introduce term limits baada ya kifo cha FDR ambae alikuwa Rais kwa miaka 12 ( 1933-1945) mpaka alipokufa. Republicans wakalazimisha term limits kwa kuhofia kuwa wanaweza kujikuta nje ya madaraka kwa muda mrefu. Nchi nyingine zinakuwa na term limits kwa marais ambao sio watendaji lakini hawana term limits kwa Mawaziri Wakuu ambao ndio wanaoongoza serikali.

Mimi naamini kuwa Mbowe alikuwa amepanga kutogombea lakini ni matusi kwake binafsi na figisu figisu za Lissu ndio zikamfanya aamue kugombea maana ingeweza kuwa spinned kuwa amemuogopa Lissu.

Aidha, kuna watu waliofanya kazi kwa karibu na Lissu ambao walikuwa na shaka juu ya uwezo wake wa kukiongoza chama chao. Hata hizi lugha za kuwa watu wanalinda matumbo yao hazina afya kwa mustakabali wa CDM.

Mpaka sasa hivi sijaona sababu yeyote ya maana ya kumfanya Mbowe asifae kuongoza CDM kwa miaka mingine. Kwa wale wanaoona kuwa hafai waache matusi, washindane nae kwenye hoja.

Amandla...
 
Ni imani yako. Sasa tusubiri maamuzi ya wapiga kura.

Amandla...
 
Kumbe uko hapa kubishana! Ndio maana unapata shida.
Siko hapa kubishana na watu wnao nitukana. Tubadilishane mawazo kwa hoja na sio matusi. Mbona wengi tu tuna tofautiana mawazo lakini hatuvunjiani heshima?

Amandla...
 
Siko hapa kubishana na watu wnao nitukana. Tubadilishane mawazo kwa hoja na sio matusi. Mbona wengi tu tuna tofautiana mawazo lakini hatuvunjiani heshima?

Amandla...
Utukanwe na nani boss. Fahamu huku ni kwenye mitandao ya kijamii na sio group la wanaparokia. Matumisi ni vibwagizo tu, lakini hoja zinaeleweka.
 

Kwenye huu Uzi bwana mkandara na Le Mutuz waliwaambia waziwazi kuwa Mbowe ni CCM miaka 20 mbele imebainika kumbe ni kweli

Pascal Mayalla
 
Utukanwe na nani boss. Fahamu huku ni kwenye mitandao ya kijamii na sio group la wanaparokia. Matumisi ni vibwagizo tu, lakini hoja zinaeleweka.
Na ni haki yangu mimi mparokia kumkatia mtu ambae sipendi lugha yake.

Amandla...
 
Kwa yaliyopo CHADEMA ni bora mtu uwe tu CCM, hawana uafadhali wa kuzidi CCM. Maybe siku chama kikiacha Kuongozwa kama Kikoba cha Mbowe!
Kuna tatizo gani kusubiri sanduku la kura liamue? Wagombea 3 wamechukua fomu sasa si tusubiri nani ataibuka kidedea? Au mlitaka Mbowe ajitoe? Hoja ni nini hasa hapa?? Uchaguzi usifanyike au kuwe na mgombea mmoja tuu TAL???
 
Kwa yaliyopo CHADEMA ni bora mtu uwe tu CCM, hawana uafadhali wa kuzidi CCM. Maybe siku chama kikiacha Kuongozwa kama Kikoba cha Mbowe!

Baki CCM ni uamuzi wako. Maana CCM mwenyekiti anachaguliwa Kwa kura ya ndio au hapana.
 
Hakuna popote ambapo Lissu alimpaka Matope Mbowe. Tatizo lenu mmetafsiri kitendo cha Lissu kutangaza nia ndiyo upakaji wa matope.
Lissu amemtetea zaidi Mbowe lakini ni Mbowe aliyemshambulia Lissu kupitia hotuba yake alipoita waandishi ili kutoa msimamo wake wa kama atagombea au laah!!
 

Punguza uongo. Usijisahaulishe Lissu aliyopitia kipindi Cha Magufuli. Kapigwa risasi na kafutwa ubunge. Ni mtu straight. Nakataa board room politics hazina maana Kwa CCM.
 
Na ni haki yangu mimi mparokia kumkatia mtu ambae sipendi lugha yake.

Amandla...
Haki yako inaheshimiwa. Ila kwenye mitandao ya kijamii sio sehemu utapata utulivu uutakao. Ni sawa na stand, kuna matusi ya wazi lakini watu hawaachi kusafiri.
 
Haki yako inaheshimiwa. Ila kwenye mitandao ya kijamii sio sehemu utapata utulivu uutakao. Ni sawa na stand, kuna matusi ya wazi lakini watu hawaachi kusafiri.
Mimi naona tatizo ni kuwa mmeigeuza kuwa kama Instergram/ X. Ndio gharama ya mafanikio.

Amandla...
 
Punguza uongo. Usijisahaulishe Lissu aliyopitia kipindi Cha Magufuli. Kapigwa risasi na kafutwa ubunge. Ni mtu straight. Nakataa board room politics hazina maana Kwa CCM.
Ngoja tuongee kuhusu ushujaa wa Lissu.Kuna ushujaa gani katika kupigwa risasi? Mashujaa kwangu mimi ni wale waliohakikisha haendi Muhimbili. Wale waliosimama kidete apate huduma zote muhimu.
Kuna ushujaa gani katika kutiwa ubunge kwa kutoonekana Bungeni. Kuonewa ndio, lakini sio ushujaa.
Ushujaa ambao nitampa credit ni kuweza kusimama na kuikosoa serikali bila uoga wowote. Lakini hakuwa peke yake. Halima Mdee, Esther Bulaya, Esther Matiko, Suzan Kiwanga na wengine nao walisimama bila uoga ku critice serikali. Na walienda mpaka jela kwa matendo. Walipigwa, walinyanyaswa kijinsia lakini waliendelea na msimamo wao.
Ushujaa ni ule alionyesha Husna Said wa Bawacha Chato ambae alipigana bila kuogopa kuwa yupo kijijini kwa JPM kuwa bendera ya CDM iendelee kupepea.
Ushujaa ni kwenda ku andaa maandamano Mwanza na kutotetereka unapovamiwa na kufunguliwa kesi ya ugaidi.
Ushujaa ni kukata kutoka jela mpaka wenzako wote uliofungwa nao watoke.
Ushujaa ni kutoka jela na kuitikia with wa Rais kwenda kuonana nae bila kujali kuwa wenzako hawatakuelewa.
Ushujaa ni kubeba mabango mpaka ubalozi wa Marekani kuomba washinikize ili kesi ya Mwenyekiti wenu iondolewe.
Ushujaa ni kuangalia biashara zako zikihujumiwa bila kutetereka.
Ushujaa ni kuona ndugu yako anauawa lakini hautetereki katika msimamo wako.
Na hao ni baadhi tu ya mashujaa wa CHADEMA. Msitake kutuaminisha kuwa Lissu peke yake ndio shujaa na wakina Mbowe ni vibaraka wa CCM.

Amandla...
 
Ukweli lazima usemwe, Mbowe anaungwa mkono zaidi na wajumbe wenye maslahi katika uenyekiti wake.
Nimekuelewa Mkuu. Hata hivyo, mkinyima Uwenyekiti Aikael na kumpa Uwenyekiti huo Antipasu hapo mtakuwa mnamlazimisha Aikael agombee uRais. Sasa kwa wasiwasi wako juu Chadema Maslahi ikatokea Aikael akaukwaa...huoni utakuwa umewaingiza Watanzania kwenye mkenge?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…