Uchaguzi 2020 Kwa kupinga Uwanja wa Ndege Chato iliyo Geita na kupinga uwepo wa Mbuga, wana Geita wote msimpe Lissu na CHADEMA kura hata moja

Kaangalie mji unavyokua kwa kasi kaangalie Aina za nyumba zinazojengwa kule Chato hoteli zilizoko kule unaongea utafikiri Chato wanaishi maskini

Chato inakua kwa msukumo wa kawaida wa kiuchumi au kwa nguvu za dola na rasilimali ya umma? Wawekezaji gani wako huko?
 


Kapublish huko unaleta academics za utopian, hayo ni mawazo yako, kila mkoa una hadhi sawa, swala la kufua au kuchimba chuma sio mahususi kwa Rais Magufuli.
 
acha kupotosha mleta mada, uwanja umejengwa CHATO na sio Geita...kuna umbali mrefu baina ya hiyo miji miwili.

utumwa wa kisiasa mbaya sana unatetea hata visivyofaa, hapa Jiwe kaonesha upendeleo wa dhahiri kwao ambao marais wote waliomtangulia hawajawahi kufanya hivyo!!!.
 
Acha janjajanja yako wewe, watu tuna akili na tuna macho tunaona, kinachopingwa hapa siyo uwanja wa ndege kujengwa mkoa wa Geita, kinachopingwa ni uwanja wa ndege kujengwa sebuleni kwa mtu na mbuga kuporwa kutoka mkoa mwingine na kupelekwa nyumbani kama nyumbani kwa mtu.
 
expand...
Una familia au mtu anayekutegemea??
 
Bora waseme ukweli wanyimwe kura, kuliko kunafikiana
 
Hata wakazi wa Chato hawaoni faida yoyote ya uwanja wala hifadhi ya wanyama. Yaani viwepo au visiwepo kwao ni sawa tu. Nakushangaa unavyojipendekeza kwao!

Tena kwa taarifa yako wakazi wa vijiji zaidi ya 40 vya Chato vinavyopakana na hifadhi wanaona hasara zaidi kuliko faida kwa sababu ni maskini sana wanaotegemea kukata mkaa, mbao na uwindaji.

Wanaojiweza kidogo ambao ni wafugaji hawana sehemu ya kulishia mifugo halafu wamepakana na msitu ambao unatunza mbweha, nyoka na vicheche tu ambavyo vinaingia vijijini kuwaharibia hata vidogo walivyonavyo!

Kuna taasisi fulani ilifanya utafiti maeneo hayo kupata maoni ya jamii juu ya umuhimu wa hifadhi ya burigi-chato. Zaidi ya 80% walipendekeza iondolewe kabisa.

Ushauri: Kipaumbele cha kwanza kwa wananchi ni uchumi imara wa mifukoni (si kwenye makaratasi). Maisha ya watu yakiwa bora ndipo faida za vitu kama hifadhi wataziona kwa urahisi. Otherwise vitu hivyo ni sahihi lakini si kwa wakati sahihi.
 
Hakuna sehemu iliyojikuta tu umekuwa mjini, hata uko Dar es salaam, au sehem nyingne unapoona Ni sehemu sahihi,hapakuwa hivyo zamani, na uthubutu Kama huu ndo umepelekea paonekane hivyo, unavyopaona kwasasa.Development is a gradual process.Au chato sio Tz?
 
Lissu kaongea vizuri sana,kasema miji ya Katoro,Bukombe,Na Geita makao makuu ya Mkoa ni potential kuliko Chato.Geita mji wa tatu kwa migodi Afrika ukitoa Sauzi,na Ghana,hauna kiwanja cha ndege cha kimataifa kama kile kilichopo kijijini Chato.Hii Misumari na Sumu Lissu anaenda kuitema palepale Geita.Na watamuelewa
 
Nani kakudanganya🤣? Kimsingi kila mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake, Kama wewe hauoni umuhimu wowote wa matumizi ya ndege katika shughuli zako, acha watanzania wengine tuzitumie.Kimsingi katika swala zima la maendeleo, Ni ngumu Sana kumgusa kila mtu kwa wakati mmoja.Kwahiyo wasionufaika na ndege, watanufaika hata kwa vitu vingine..!
 
kama unaona hivo mkuu, je chadema na lissu kupinga wazi wazi maendeleo kwa geita ambayo ni sehem ya tanzania wapo sahih?

kila mkoa una haki yakupata maendeleo sawa na mikoa mingine hatupaswi kuleta kauli za kijinga namna ile as if kule si tanzania.
Naamini kabisa kutoka moyoni, watu wa geita wangeshirikishwa kuchaguwa miradi wa maendeleo mkoani mwao, wasingechagua uwanja wa ndege.
 
Cc. YEHODAYA.
 
Cc. YEHODAYA
 
Hebu niambie geita mjini ni seven gan palipo flat panafaa kujenga uwanja zaidi ya kutokea kasamwa kwenda geita ambapo nimakazi ya watu
Wewe unaongelea Geography wakati mimi naishi Geita. Mwanza na Geita wapi kuna milima mingi? Uwanja wa ndege wa mwanza uko milimani?
 
Naamini kabisa kutoka moyoni, watu wa geita wangeshirikishwa kuchaguwa miradi wa maendeleo mkoani mwao, wasingechagua uwanja wa ndege.
ni wapi wananchi hushirikishwa kuchagua miradi inayoanzishwa na serikali?
 

we dada kweli ni zero brain, hivi kuna sehemu yenye milima kama mwanza? mbn kuna uwanja wa ndege?
ukweli lazma usemwe kujenga international airport chato ni matumizi mabaya ya fedha,
 
Atajionea mwenyewe akienda, watu wanahasira naye kinoma, watamchana makavu! Anahezea wachimbaji huyu, Atawaambia ni Watanzania gani wanaostahili vitu vizuri kuliko wanaGeita na wachimbaji madini huko!

Kwanza binafsi ninamashaka na na uwezo wake wa Kufikiri kama unafanya kazi sawasawa,

Hilo halikuwa la kulibeba mpaka mtu ukatoa na mishipa Kwa kuwadharau Watanzania wa mkoa wa Geita kuita Miradi iliyopelekwa huko haiwafai

Swali ni moja tu, Alitaka iwafae Watanzania wenye asili gani?

Mimi mwenyewe nilianza kumpuuza alipoanza Kuinanga Miradi hiyo
 
Wananchi wa Geita na Chato ni wakulima na wafugaji wazuri lakini masikini wa kutupwa kwa kukosa ardhi kwa shughuli zao za kiuchumi na huduma muhimu kama ya maji ingawa ziwa lipo. Hali hiyo mbaya ya Raia wa Mkoa wa Geita imeletwa na uongozi mbaya wa CCM na Mwenyekiti wao ambaye ni Rais wetu mpendwa na wao pia kwa kuanzisha miradi isiyo na tija kwa wananchi. Mifano ya miradi hiyo ni mingi lakini tutaje michache tu ingawa ule wa taa za Traffic za kuongoza punda wavuta mikokote unatajwa tu kwa kupitia. Mh. Tundu Lissu, CHADEMA Chama chake na Watanzania wenye nia njema na maendeleo ya watu wa Geita wamekuwa wakipinga kwa sauti kununuliwa kwa madege ya Magufuli. Fedha zilizonunua madege hayo, ambayo sasa ni miaka yamepark tu kwa kukosa abiria wa kwenda au kutoka Chato, ingemwagwa kwenye miradi muhimu Mkoani Geita, wote mngeimba kidumu Chama. Kile kiwanja cha ndege Chato kimechukua maelfu ya ekari ya ardhi nzuri ya kilimo, kama kila mkulima wa Wilaya angegawiwa ekari chache za kulima chakula na pamba, wimbo ungekuwa zidumu fikra za Mwenyekiti. Badala ya kuleta swala na simba toka mbali, wafugaji wangeachiwa mbuga ya Burigi walishe mifugo yao kwa ajili ya Viwanda vya nyama kwa hiyo wafugaji wangetajirika na wimbo ungekuwa CCM mbele kwa mbele. Wananchi wa Geita wanajua mkombozi wao ni Mh. Tundu Lissu na Chama chake CHADEMA, CCM be na Mwenyekiti wake tupilia mbali maana hayo madege yataishia hukohuko, Uwanja utabaki gofu na Burigi itakuwa si ruksa kuwinda hata Swala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…