Kwa Makala Hii ya Daraja la Kigamboni Mwanakijiji Kachemsha


You guys are joking.Yaani Waberoya aanze kazi ya kuthibitisha kuwa MH hawajachakachua makala ya MMK kwa sababu tu Mwanakijiji amesema hakupeleka makala huko!

Hiyo si kazi yake asilani abadan. Yeye amesoma makala Mwanahalisi iliyoandikwa kuwa ni kutoka kwa Mwanakijiji, kazi yake imeishia hapo. Msomaji si kazi yake daima kujua kuwa hicho ndicho original au kimechakachuliwa. Kama Mwanakijiji ameona hakutendewa haki mada yake kubadilishwa na gazeti hiyo ni baina yake na gazeti, msomaji haijamuhusu

Msomaji ana haki ya kujadili kilichoandikwa kwenye gazeti, na kumpa majibu ya "sikuandika hivyo mwanzo. Kwa hiyo kalete ushahidi kuwa ndivyo nilivyoandika" ni outrageous
 

Gaijin hilo ni sawa kabisa. Mimi nazungumzia hoja iliyoiletwa hapa na mleta mada....inakosa nguvu kwa sababu mlengwa MMM ameweza kutengeza "reasonable doubts" kwa sisi tunaosoma humu kwa kusema kuwa hakuipeleka huko MH bali yeye alipeleka TD na kwa bahati mleta mada pia amekiri kuwa hizo makala mbili zipo tofauti. Hoja yake haiwezi kusimama bila ya hizi doubts (kuwa inawezekama MH wamechakachua au MMM anajaribu kukataa ukweli) kuondoka/kuondolewa. Kama mleta mada anataka hoja yake isimame ni wajibu wake (au member wengine) kuondoa doubts hizo.

Sasa suala la MMM kudeal na MH kwa kuchakachua makala yake (au kutumia jina lake!) hiyo sio lengo la aliyeleta mada hii. Ingekuwa ndio lengo lake then yes ningalisema hiyo sio kazi yake asilani.
 

SMU

Labda tunaona vitu kwa mitazamo tofauti. Kwangu hakuna hoja kukosa nguvu kwa sababu Mwanakijiji kasema hakupeleka. That's totally off point.

Hoja ni kilichoonekana kwenye gazeti tu. As long as iliandikwa kwa jina la Mwanakijiji yalobaki ni blah blah tu.

Mtu asiye access na JF hatayasikia haya ya "sikupeleka", nami ndivyo hivyo hivyo nachukulia

Pasco anataka Waberoya aombe radhi even kwa "uchakachuzi" wa MH even!
 
Labda! Lakini hoja hii ipo hapa JF (mimi sijasoma MH wala TD) na naamini aliyeileta anataka members wa JF waijadili hizo hoja/shutuma zake (kama angekuwa anataka tujadili kilichoandikwa kwenye gazeti angeweka hiyo makala hapa au hilo gazeti).

Mimi nimesoma alichoandika mleta mada na wachangiaji wengine akiwamo MMM. kwa namna fulani aliyeleta mada anajaribu kuonesha kuwa MMM kachemsha. MMM kasema hiyo makala sio yake.....sasa hapa JF tuanaendeleaje kujadiliana kama hakuna aanyetokea kutuonesha kuwa makala hiyo imeandikwa na MMM? Je kuandikwa kwenye Gazeti kuwa author ni MMM peke yake inatosha kuthibitisha kuwa ni kweli yeye ndiye author?

Labda nitoe mfano....wewe ni Hakimu umeletewa kesi kuhusiana na kosa fulani ambapo ushahidi unaoletwa kwako ni waraka ambao inaonekana mtuhumiwa ameusign. Mtuhumiwa anajitetea kwa kusema huo waraka unaoutumia kama ushahidi sio wake/sio yeye aliyeusign. Mtuhumiwa anatoa waraka mwingine kama huo na kukiri kuwa huo ndio wake na nyote mnakubaliana kuwa kweli nyaraka hizo mbile zipo tofauti. Katika hali kama hii huoni kua tayari kuna mashaka? Je mwenye wajibu wa kuondoa shaka hiyo ni mtuhumiwa au aliyeleta mashataka? Ukitumia kigezo kuwa kwenye huo waraka linaonekana jina la mtuhumiwa na hivyo kumtia hatiani mtuhumiwa utakuwa umemtendea haki? Hivyo ndivyo ninavyolitizama suala hili.....kama unalitizama tofauti na hivi then nakubali tu kutofautiana.
 
Mkuu Gaijin nakubaliana na wewe kote ila tukirudi kwenye hoja ya msingi ya Waberoya headline kutoendana na maudhui ndio iliyokuwa headline ya Waberoya ambayo mode wameichakachua ili kuchochea mjadala, kuna thread nimewahi kuuliza humu jee modes wa jf ni wachochezi?. Niliweka na mifano wa uchochezi wao, hawakujibu!. Leo wameigeuza hii thread kwa headline ya kichochezi na Wabe keshawapa haki yao kwa uchochezi wao!.

Nilichomwambia Wabe awe tayari kuomba radhi kuhusu headline kama ikithibitishwa ni kweli sio MMKJJ aliyepeleka kule MH nikimaanisha MH ndio waliochakachua then ni ustaarabu Wabe kusema sorry.

The burden of proof lies with MMKJJ to prove beyond reasonable doubt kuwa ni kweli hakupeleka MH na Kube ni memba humu ataibuka na kulitetea gazeti lake kwa udakuzi na uchakachuzi!.
 
Pasco said:
Asante. Wazungu wametengeneza simulator ya hiyo Kigamboni new city kwenye DVD pack of 6 wanaiuza TZS 300,000. Ukiangalia utashindwa kuamini!. Nimetembelea nchi za watu, hazifikii!.
Pasco
kwenye hiyo smulator wameonyesha

  • wameonyesha magari ya kuzoa taka taka na yatapita mra ngapi kwa wiki?
  • miundombinu ya maji taka na majisafi yatavyokuwa na yanatiririka kutoka wapi.
  • route ya mabasi?
  • maeneo mangapiya wazi ya watu kupumzika na bustani na viwanja vya michezo?

Tushushie nondo wewe uliyeona DVD tuanze kufaidi kwa hisia. Tena huliganhsi na capetown ya aarica bali doha lol.........
 

Wabongo wanalinganisha simulated city na real city.....SMH
 
Nitaconvert baadhi ya clips na mtajionea. sio tuu sewage system bali mpaka insonerator ya waste disposal itakayo generate na umeme!. Kwa kifupi ni ulaya!.
 
Mode, kwa vile thread ilihusu kichwa cha habari ambacho umekifuta, thread imepoteza maana!. Angalau kama Waberoya angekiandika tena kwenye intro yake lakini hakukiandika!.

Nawaombeni next time mkibadili headline, hakikisheni haibadili maana!.
 
Napata mashaka kidogo kama kweli Mkjj hakupeleka hiyo nakala Mwanahalisi
Au anaikana baada ya kuona mapungufu baada ya Waberonya kuikosoa
Kauli yake juu ya ufisadi huu wa habari (nikimaanisha kuchukua makala ya mtu na kui edit bila taarifa ya mwandishi) haionyeshi kukerwa wala kushtuka hasa pale aliposema eti hana muda wa kufanya hivyo.
Kwa waledi wake anapaswa kutuonyesha Mwanahalisi hawakutenda jema kufanya vile kunako weza kumletea shida au hata kushusha hadhi yake kwa jamii kwa watu kutumia makala zake na kuzi edit watakavyo.
Vinginenyo anaikana baada ya kuona amaechemsha
 
Waberoya
Post yako dhidi ya Makala ya Mwanakijiji ndio inamakosa makubwa sana hasa kwa Jamii ya watanzania wote ambao wamekwisha tambua kwamba ufisadi ni moja ya kitu ambacho kimechangia kwa kiwango kikubwa sana kuwatumisha katika lindi la umasikini tulilomo.

Kwa kitendo chako cha kuonesha kwamba sio issue kwa magufuri kutojulikana yuko upande gani katika vita dhidi ya ufisadi, kwangu ni ushahidi tosha kwamba umeelewa Mwanakijiji alikuwa ana adress issue gani lakini umeamua kwa makusudi kuipotosha.

Ninaamini kwamba, Hoja ya Mwanakijiji ni kwamba "Ni kwanini Magufuri afurahie na kuwalazimisha wananchi kuona ufanisi wa serikali hii katika uwekezaji katika miundo mbinu wakati sio inayofadhiri miundo mbinu hiyo huku ikiwa na uwezo mkubwa kabisa wa kufadhiri miradi ya namna hiyo bila kutegemea mifuko ya jamii na nchi wafadhiri" kwamba"Serikali yetu inatapanya mali ya nchi hii kisha inakimbilia kuficha aibu kwa ama kulazimisha mifuko ya jamii kuingilia kati ama kwenda kuomba nje ya nchi"

Waberoya umeamua kwa makusudi kabisa kung'ang'ania vitu ambavyo sio hoja ya msingi huku ukijua hathari za maamuzi hayo, na umeenda mbele kwa kuibua hoja kwamba vita dhidi ya ufisadi si lolote si chochote kwa namna ambayo inanisukuma kujiuliza kama nina jibu hoja ya mtu sahihi au nimepotea.

Waberoya, naomba nikurudishe katika hoja

Mosi: Ni kweli kwamba NSSF inauwezo mkubwa sana wa kifedha kuliko serikali yetu?

Pili: Kwa namna ambavyo NSSF imeamua kujiingiza kwenye miradi ya kisiasa? Je imejisecure kiasi cha kutosha kwa namna ambayo wanachama wake wanastahili kula, kulala na kufurahi maisha kwa uhakika kwamba pesa zao zinaingizwa kwenye miradi salama?

Tatu: Ni sahihi kuacha wanasiasa waendelee kujiingiza kusheherekea na kupiga mabao ya kisiasa katika miradi ambayo haifanikishwi na rasilimali tulizowapa wazisimamie?

Waberoya, wewe unaweza kumuacha mke wako arutubishwe na mwanamme mwingine alafu ujitokeze hadharani kushangilia kuzaliwa kwa mtoto wakati ulishindwa kufanya urutubisho kwa sababu za ulevi na kufukuzana na wanawake vicheche na wasio tayari kuzaa??

Nne: Ni kwanini hatuoni miradi mikubwa ya maendeleo ikifanikishwa kutokana na rasilimali zetu wenyewe hasa kodi, hata kwa kuuza twiga? kwa nini?

Naomba ujadili hoja hizi, ndio za msingi, ukitaka kuendelea kumzungumzia mwalimu na Magufuri poa vile vile.
 

A-prove beyond reasonable doubt kwani hizi shutuma ni za jinai? Hapa the burden of proof ni balance of probabilities tuu. Nakubaliana na SMU kwenye post namba 104 hapo juu. Anayetakiwa ku-prove on the balance on probabilities ni Weberoya na wala sio Mwanakijiji. Hata kama the burden of proof ingekuwa ni beyond reasonable doubt, still Weberoya ndiye aliyetakiwa ku-prove kwamba hiyo makala ya Mwanahalisi imeandikwa na Mwanakijiji. The one who alleges must prove.

Weberoya ndiye aliyeleta madai yake based on makala ya Mwanakijiji kwenye gazeti la Mwanahalisi. Mwanakijiji ame-raise a doubt kwa kudai kuwa hakupeleka makala Mwanahalisi. Anadai makala yake ni iliyoko kwenye gazeti la Tanzania Daima. Na kopi ya makala ya Tanzania Daima imewekwa hapo juu. Mpaka sasa hata Weberoya hajaiweka hapa hiyo makala aliyoisoma Mwanahalisi. Yeye ameweka tuu unsubstantiated allegations.

It would have made sense kama angeambatanisha allegations zake na kopi au link ya hiyo makala ya Mwanahalisi so that we can make an informed opinions. Hatuwezi kubase arguments zetu kwenye allegations zake na ku-conclude that Mwanakijiji amechemka. Otherwise, tutakuwa hatulitendei mema hili jukwaa which goes with the name "Great Thinkers".

Kwa hiyo, kinachotakiwa ni Weberoya ku-prove allegations zake. Kwanza atupe nakala ya hiyo makala ili tujue kama kweli ipo na pia tuweze kufanya comparative analysis. Title ya hiyo makala is crucially important too, kwa sababu anadai hakuona "uhusiano wa kichwa cha habari na habari yenyewe". Pili atudhibitishie kuwa hiyo makala ni ya Mwanakijiji. Now, Gaijin kasema hapo juu kuwa "As long as iliandikwa kwa jina la Mwanakijiji yalobaki ni blah blah tu." I beg to differ with that. The fact that Mwanakijiji's name appears on the said article is not in itself a conclusive evidence that it is his article.

Kwa upande wa Mwanakijiji, and for his own reputation, nafikiri Mkuu Pauliss anaweza kuwa na point.

 

Soma vizuri nimekanusha kitu gani na nimeelezea nini. Siyo jambo gumu kihivyo kuelewa.
 
Mkuu EMT, I'd like to differ,
1.Wabe kasoma gazeti la MH article inayoonyesha mwandishi ni MMKJJ na kuicriticise headline ya article vs contents!.
2. MMKJJ hajakanusha kuwa hajapeleka MH, bali kasema yeye alipeleka TD tuu na sio pengine popote, hivyo kanusho la MMKJJ kuwa amepeleka TD tuu, ni impliedly na sio expressly.
3.Hii ingekuwa ni kesi, Waberoya ni mlalamikaji na mlalamikiwa ni MMKJJ.
4. Maadam gazeti limeonyesha mwandishi ni MMKJJ, Waberoya yuko right until proven otherwise kumlalamikia MMKJJ na ushahidi wake (evidence) ni jina la kwenye gazeti la MH.
5. Kwenye kesi, kwa kawaida the burden of proof lies with the prosecution, ila baada ya mlalamikaji kupresent his evidence, now the burden of proof change hands kwa mlalamikiwa ku challenge hiyo evidence presented.
6. Mwenye jukumu la kuthibitisha MH wamechakachua ni mlalamikiwa. Kusema amepeleka article TD pekee, haijustify ile article ya MH imechakachuliwa!.
 
Hivi leo likitokea gazeti jingine lina makala yenye kusifia serikali kuhusiana na mgomo wa madaktari na mwandishi ni "mwanakijiji" na watu wakashambulia imekuwaje nimeacha kusupport madaktari si ni haki kwangu kutoa maelezo? Nikipitia hiyo inayodaiwa kuwa ni makala na kugundua ni mkusanyiko wa maandishi yangu na nyongeza za mhariri bado nadaiwa kutoa maelezo? Nikiwaelekeza watu kwenye makala pekee niliyoandika juu ya somo na kwaambia hiyo makala iliyowekwa jina langu sikuandika wala kutuma bado notadaiwa kutoa maelezo? Wanaosema nioneshe without reasonable doubt kuwa sikutuma ndiio wataamini nawapa challenge: pendekezeni njia moja tu ya mimi kuweza kuonesha sikutuma makala hiyo zaidi ya kauli yangu kuwa sikutuma.
 
Mkuu MMKJJ nimekusoma.
 
Tatizo ni kuwa gazeti gani limeandika?
Hata hiyo makala ya TD haina ukweli ndani yake.Ni makala iliyojaa opinions rather than facts.
Sioni mnachobishana.
 

Haijalishi kwani kama lengo lao ni kumchafua magufuli, hayo magazeti yao - ni asilimia 21% tu ya watanzania ambao source zao za news ni magazeti, tena on a weekly basis, not daily basis. Na hawa 21% ni pamoja na wale wanaoambiwa na ndugu, jamaa na marafiki zao kwamba gazeti fulani limeandika hiki na kile. Otherwise magazeti hayafikii zaidi ya 2% of the population on a daily basis. Habari hizo waziweke basi angalau front page, sio ndani kwani hata wewe umeikuta kwa bahati mbaya. Zikikaa mbele, basi katika pita pita ya vichwa vya habari kwenye radio zinazokamata nchi nzima majira ya asubuhi, angalau umma utasikia vijembe hivyo vinavyokusudiwa na wahusika, kwani zaidi ya 70% ya watanzania, source yao za habari ni radio (za simu na za kawaida combined, na mara nyingi huwa ni asubuhi.

Vinginevyo hata kama nani.... angekuwa ndiye Waziri wa ardhi, nyumba za serikali zingeuzwa tu. Inasemekana WorldBank ndio walioshinikiza hilo baada ya kuona serikali inapoteza fedha nyingi to maintain them, but only to build them again later baada ya malalamiko kuanza kuleta athari za kisiasa. But the bottom line is, serikali haistahili kumiliki utitiri wa nyumba namna ile, unless zingepelekwa kwa national housing ili zisaidie shirika lile kufanikisha malengo yake mbalimbali.

Magufuli na EPA, is a non - starter.

Magufuli na Kigamboni - pengine kinachowaumiza ni kwamba huo ni moja ya miradi michache inayoonekana kwamba itatekelezwa na serikali ya awamu ya nne, nje ya mradi wa richmond.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…