Kwa Makala Hii ya Daraja la Kigamboni Mwanakijiji Kachemsha

Kwa Makala Hii ya Daraja la Kigamboni Mwanakijiji Kachemsha

Asante. Wazungu wametengeneza simulator ya hiyo Kigamboni new city kwenye DVD pack of 6 wanaiuza TZS 300,000. Ukiangalia utashindwa kuamini!. Nimetembelea nchi za watu, hazifikii!.

Hizo nchi za watu zisizofikia ni zipi?
 
Kwa mahesabu ya haraka haraka, DVD moja ya kawaida ina jumla 4.37 GB. Kama hiyo stimulation imekuwa recorded in HD video tutakuwa tunaongelea masaa mawili ya video stimulation per DVD x 6 DVDs = 12 hours of video simulation for the design project. Kama recording ni long-play mode (low resolution) video tutakuwa tunaongelea about 20 hours of video stimulation per a DVD x 6 DVDs = 120 hours of video stimulation.

Hata hizo simulation videos for Olympics hazifiki asilimia 5 tu ya masaa hayo, itakuwa Kigamboni!
 
"Katika kitu cha kushangaza kabisa ni kuwa Jina la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere halikutukuzwa katika hafla hiyo. Ni katika kile ambacho nimekiita kuanzia mwaka jana kuwa ni “juhudi dhaifu za kulifuta jina la Nyerere” katika mchango wa maendeleo. Katikati ya miaka 1970 ni uongozi wa Mwalimu Nyerere uliofanya upembuzi yakinifu wa kina wa ujenzi wa daraja la Kigamboni" - Mwanakijiji.


[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading, width: 100%"]Dk Magufuli atangaza neema Kigamboni [/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]Monday, 09 January 2012 21:17 [/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk Ramadhan Dau alisema tathmini ya awali ya ujenzi wa daraja hilo ilianza mwaka 1977... “Ilipofika mwaka 1991, Serikali iliendelea na upembuzi yakinifu chini ya Kampuni ya Gauff ya Ujerumani ambayo ilionyesha gharama za ujenzi huo kuwa ni zaidi ya Dola 47 milioni.”

sasa mimi sioni mnachobishana na umuhimu wake kwetu sisi watanzania..... what is the big deal? Mbona inajulikana ni mwaka gani daraja hilo lilianza kutathminiwa?
Mimi naona Serikali ya awamu ya nne inastahili pongezi kwa kupata sponsors ...... kibakuli sometimes kinasaidia!
 
"Dk. Magufuli, Waziri wa Ujenzi akizungumza katika hafla ya kutia sahihi makubaliano hayo alizungumza na kujaribu kushawishi watu waamini kuwa hatua hii imefikiwa baada ya uongozi mzuri wa Rais Jakaya Kikwete na hivyo wananchi waunge mkono na inaonekana wafanye hivyo bila kuuliza maswali!"- Mwanakijiji.

Hayo maneno aliyasema lini? Naomba tuwekee aidha video clip, au makala ya gazeti lolote.


"Mojawapo ya tafiti nyingine za Benki ya Dunia za miaka ya karibuni zaidi zilionesha kuwa daraja la Kigamboni lingegharimu karibu dola milioni 46 hivi (karibu sawa na kiasi kilichokombwa na Kagoda Agriculture katika kashfa ya EPA!) Lilichelewa kwa sababu ya umaskini au kukosekana uwezo"- Mwanakijiji.

Mkuu nadhani unazungumzia 1991,

"The project needs a fresh feasibility study and a concession document that investors can use to evaluate the project's worth"-
Dieter Schelling, World Bank Tanzania, May 2009.



Hii ishafanyiwa feasibility study na investors wameikubali.
bread_end.gif


[h=1]WB to fund new study of Kigamboni bridge[/h]"The initial plan was for a 560-metre long bridge with 14 spans of 40 metres each. The construction period was put at three-and-a-half years while its cost was $46 million"..........



46m$ mwaka 1991 ni sawa na 112m$ mwaka 2010 - Source http://www.measuringworth.com/uscompare/relativevalue.php
 
waandishi wa habari wa Bongo kwa kujipa mamlaka ya vitu wasivyo ujuvi navyo si wadogo!

Hawa si ndo waliowalisha Watanzania kasa aitwae "Kikombe cha Babu" hawa?

Labda washachukua bahasha zao? Usikute Babu nae alikuwa anagawa bahasha?
 
"Katika kitu cha kushangaza kabisa ni kuwa Jina la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere halikutukuzwa katika hafla hiyo. Ni katika kile ambacho nimekiita kuanzia mwaka jana kuwa ni “juhudi dhaifu za kulifuta jina la Nyerere” katika mchango wa maendeleo. Katikati ya miaka 1970 ni uongozi wa Mwalimu Nyerere uliofanya upembuzi yakinifu wa kina wa ujenzi wa daraja la Kigamboni" - Mwanakijiji.


[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]Dk Magufuli atangaza neema Kigamboni
[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]Monday, 09 January 2012 21:17
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk Ramadhan Dau alisema tathmini ya awali ya ujenzi wa daraja hilo ilianza mwaka 1977... “Ilipofika mwaka 1991, Serikali iliendelea na upembuzi yakinifu chini ya Kampuni ya Gauff ya Ujerumani ambayo ilionyesha gharama za ujenzi huo kuwa ni zaidi ya Dola 47 milioni.”

sasa mimi sioni mnachobishana na umuhimu wake kwetu sisi watanzania..... what is the big deal? Mbona inajulikana ni mwaka gani daraja hilo lilianza kutathminiwa?
Mimi naona Serikali ya awamu ya nne inastahili pongezi kwa kupata sponsors ...... kibakuli sometimes kinasaidia!

"Dk. Magufuli, Waziri wa Ujenzi akizungumza katika hafla ya kutia sahihi makubaliano hayo alizungumza na kujaribu kushawishi watu waamini kuwa hatua hii imefikiwa baada ya uongozi mzuri wa Rais Jakaya Kikwete na hivyo wananchi waunge mkono na inaonekana wafanye hivyo bila kuuliza maswali!"- Mwanakijiji.

Hayo maneno aliyasema lini? Naomba tuwekee aidha video clip, au makala ya gazeti lolote.


"Mojawapo ya tafiti nyingine za Benki ya Dunia za miaka ya karibuni zaidi zilionesha kuwa daraja la Kigamboni lingegharimu karibu dola milioni 46 hivi (karibu sawa na kiasi kilichokombwa na Kagoda Agriculture katika kashfa ya EPA!) Lilichelewa kwa sababu ya umaskini au kukosekana uwezo"- Mwanakijiji.

Mkuu nadhani unazungumzia 1991,

“The project needs a fresh feasibility study and a concession document that investors can use to evaluate the project’s worth”-
Dieter Schelling, World Bank Tanzania, May 2009.



Hii ishafanyiwa feasibility study na investors wameikubali.


Asante Soby kwa kuweka haya mabandiko!

Mwanakijiji anadhania CCM wote wasipotaja jina la Nyerere basi hawampendi......Nyerere is dead, buried in butiama, thats life amewaza na kumsemea mengi magufuli na hajaweka vithibitisho au sababu

mwanakijiji na 'nyerere' wake anaonekana kama michael jackson
 
Makala original ni hiyo ya Tanzania Daima ambayo imetoka karibu mwezi mmoja nyuma. Sikutuma makala nyingine Mwanahalisi.

How can they publish without your consent? please check with them.....itafute angalia hiyo artcile
 
Magufuli na daraja la Kigamboni, tushangilie?: Na M.M. Mwanakijiji

Nina uhakika katika siku za usoni Dar es Salaam watu watakuwa wanakuja kuangalia madaraja na mabarabara badala ya kuja kuangalia msongamano – Dk. John Magufuli (wakati wa kusaini mkataba wa ujenzi wa daraja la Kigamboni).

Siku ya Jumatatu kile kinachoitwa “ndoto ya daraja la Kigamboni” kilioneshwa kuwa kitaanza kutimia baada ya makubaliano ya ujenzi wa daraja hilo ambayo yatashirikisha serikali ya Tanzania, Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na Kampuni ya China kutiwa saini. Watu wengi ambao labda kutokana na kutokujua historia au kutokutaka kujua historia wameonekana kushabikia kwa furaha hatua hii ya sasa kana kwamba ni zawadi na neema ya Mungu kwa Watanzania.

Dk. Magufuli, Waziri wa Ujenzi akizungumza katika hafla ya kutia sahihi makubaliano hayo alizungumza na kujaribu kushawishi watu waamini kuwa hatua hii imefikiwa baada ya uongozi mzuri wa Rais Jakaya Kikwete na hivyo wananchi waunge mkono na inaonekana wafanye hivyo bila kuuliza maswali!

Daraja la Kigamboni si zao la fikra za Kikwete

Katika kitu cha kushangaza kabisa ni kuwa Jina la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere halikutukuzwa katika hafla hiyo. Ni katika kile ambacho nimekiita kuanzia mwaka jana kuwa ni “juhudi dhaifu za kulifuta jina la Nyerere” katika mchango wa maendeleo. Katikati ya miaka 1970 ni uongozi wa Mwalimu Nyerere uliofanya upembuzi yakinifu wa kina wa ujenzi wa daraja la Kigamboni.

Wazo la ujenzi wa daraja hili haukutokana na serikali ya awamu ya nne kama Magufuli anavyotaka watu waamini! Ni wazo ambalo lilikamilika na kufanyiwa utafiti miaka karibu arobaini iliyopita.

Ubunifu wa michoro ya daraja ilikuwa imekamilika mwaka 1977 miezi michache kabla ya nchi kwenda vitani na kabla ya ukame uliofuatia mapema miaka ya 1980. Kwa wanaokumbuka watahusisha kuwa ni utawala huo huo wa Nyerere uliofikiria na kufanyia upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Bwawa la kuzalisha umeme la Stielger’s Gorge ambalo lingeweza kuzalisha umeme wa zaidi ya MW 2000 na kuliondoa taifa katika tatizo la umeme. Gharama ya ujenzi wa Stielgers wakati ule ilikuwa kama dola bilioni 1.2 wakati ujenzi wa Kigamboni kwa fedha za wakati ule na kwa michoro iliyotolewa wakati ule ilikuwa ni kama dola milioni 28.6.

Kwa hiyo, tuweke rekodi kwa usahihi kwanza – huwezi kutenganisha mpango wa ujenzi wa Daraja la Kigamboni au baadaye Stielger’s George na mawazo ya Rais wetu wa Kwanza – Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Najua wengine watachukia, wengine watakereka lakini ukweli ni kuwa hawakuja na mawazo mapya! Hata hilo daraja la “Mkapa” si wazo la Mkapa!

Gharama ya ujenzi haijabadilika sana

Kama kweli – na sina shaka ni kweli – kwamba wazo la ujenzi wa daraja la Kigamboni ni wazo la miaka karibu arobaini iliyopita basi leo hii kusainiwa kwa mkataba huu kumekuja kukiwa kumechelewa sana. Ni wazi kuwa mazingira ya mebadilika na hivyo upembuzi yakinifu mpya ulihitajika.

Sasa hivi katika mpango wa sasa daraja litakuwa na njia sita (si mbili kama ilivyopendekezwa zamani) na urefu wake ukiongezwa kwa karibu mita mia moja zaidi na ikitumia bila ya shaka teknolojia na utaalamu ambao haukuwepo miaka arobaini iliyopita (japo kanuni za fizikia na uhandisi nyingi ni zile zile).

Leo hii tunaambiwa gharama ya ujenzi wa daraja hii inakadiriwa kuwa kati ya dola milioni 130-200. Tukichukulia fedha za mradi wa wakati wa Nyerere za dola milioni 28.6 na kuzileta kwenye fedha za leo ni sawasawa na dola milioni 107.7 Hivyo ni wazi kuwa kiasi hicho cha fedha kinachopendekezwa leo hii si kibaya sana ukizingatia ukubwa na teknolojia ambayo itatumika.

Mojawapo ya tafiti nyingine za Benki ya Dunia za miaka ya karibuni zaidi zilionesha kuwa daraja la Kigamboni lingegharimu karibu dola milioni 46 hivi (karibu sawa na kiasi kilichokombwa na Kagoda Agriculture katika kashfa ya EPA!) Lilichelewa kwa sababu ya umaskini au kukosekana uwezo?

Naomba nipendekeze kwa wasomaji wangu kuwa kuchelewa kwa ujenzi wa daraja la Kigamboni hakukutokana na ukosefu wa fedha au uwezo wa kitaalamu hasa katika miaka hii kumi na tano hivi. Wakati mradi huu umebuniwa miaka ya sabini nchi ilikuwa katika hali ngumu ya kiuchumi. Hata hivyo, baada ya mafanikio ya kampeni ya kusamehewa madeni yasiyolipika ambayo pia iliongozwa na Mwalimu Nyerere kabla ya kifo chake mwaka 1999 Tanzania ilikuwa katika nafasi ya kutumia neema hiyo kujenga miundombinu yake.

Kwa baadhi yetu tulitegemea kuwa mradi wa Kigamboni na ule wa Stielgers ingekuwa ni miradi mikubwa ya kwanza kufanyika. Wa Kigamboni ungeweza kutekelezwa mapema zaidi kwa sababu hauna gharama kubwa zaidi na ni rahisi zaidi kutekelezeka. Lakini haikuwa hivyo. Kilichotokea ni kuwa ni miaka hii kumi iliyopita tumeshuhudia ufisadi wa hali ya juu katika taasisi mbalimbali za serikali huku miradi ambayo ilikadiriwa kidogo ikila mabilioni ya fedha na watumishi wa umma wakiendelea kunufaika kwa migongo ya maskini wa taifa letu.

Ndani ya miaka hii kumi (ya 2000 hadi 2010) Tanzania imepoteza kwa njia ya ufisadi zaidi ya dola bilioni 10 (zaidi ya shilingi trilioni 11) huku Rais Kikwete akitudokeza kuwa karibu asilimia 30 ya fedha za bajeti ya taifa huishia mikononi mwa mafisadi.

Ndugu zangu, kuchelewa kwa ujenzi wa miradi hii mikubwa ambayo ingeweza kubadilisha maisha ya watu wetu ni matokeo ya moja kwa moja ya ufisadi uliokubuhu. Kiasi kilichopotezwa kwa ufisadi katika sekta mbalimbali kingeweza kujenga daraja la Kigamboni, Stielger’s na miradi mingine mikubwa bila kuwaomba NSSF au taasisi binafsi!

Leo Magufuli anataka tushangilie kuwa NSSF wamefanya kazi nzuri ya kutoa fedha za wanachama wao kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Kigamboni wakati serikali yake imekuwa dhaifu kukabiliana na ufisadi mkubwa na kuwaacha mafisadi waendelee kupeta?

NSSF na kuficha madhara ya ufisadi

Hili sitaki kuliandika sana kwa sababu watu wanaofuatilia wanaweza kuona mtindo mmoja ukijitokeza miaka ya karibuni. Pale ambapo serikali ya CCM imeshindwa kutekeleza na kusimamia fedha za umma kutekeleza miradi mbalimbali inakimbilia fedha za wanachama wa mashirika ya hifadhi ya jamii. Tumeliona hili kwenye kashfa ya Kiwira ambapo serikali iliruhusu ufisadi wa hali ya juu ya mmoja wa waliowahi kuwa viongozi wake lakini badala yake NSSF ikataka iwekeze bilioni 400 za fedha za wanachama; tumeona pia kwenye barabara ambazo Waziri Magufuli na serikali yake wamepata shida kuzisimamia na fedha za walipa kodi wakikaribisha NSSF kuingia na kuwekeza huko; tumeshuhudia hili kwenye ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma vile vile ambapo NSSF na PPF wamewekeza fedha za wanachama wao katika miradi hiyo.

Leo hii NSSF inakaribishwa tena kwenye daraja la Kigamboni na iko tayari kubeba gharama ya karibu asilimia 60 ya ujenzi na baadaye uendeshaji wa daraja hilo kurudisha fedha zake.

Sasa kinadharia hili halina tatizo hata kidogo. Pote duniani mashirika mbalimbali ya umma na hata ya hifadhi ya jamii yamewekeza kwenye miundo mbinu. Lakini kuna tofauti moja inapokuja Tanzania. Wanasiasa wanapoingiliana sana na watendaji wa taasisi hizi maamuzi ya baadhi ya taasisi hizi yanakuwa ni ya kisiasa zaidi. NSSF imekuwa ni shirika ambalo liko karibu zaidi na wanasiasa wa CCM kiasi kwamba nikiliita kuwa ni shirika la uwekezaji la CCM sitakuwa nawaita jina baya. Liko kwa ajili ya kuficha udhaifu wa uongozi, maono na usimamizi wa fedha za umma wa serikali ya CCM.

Popote pale penye mradi mkubwa ambao Serikali imeshindwa kuutekeleza kwa sababu “haina fedha” a.k.a fedha zimeliwa na mafisadi – NSSF itajitokeza kwa moyo mkunjufu kugawa fedha za wanachama kwenye miradi hiyo!

Wakati umefika kwa wanachama wa NSSF na mashirika mengine ya umma ambayo yanaingiza fedha kwenye miradi mikubwa ya serikali kuanza kudai mafao kutoka miradi hiyo. Hivi, mwana NSSF, PPF, au shirika jingine la hifadhi ya jamii anapata faida gani ya kifedha kwa shirika lake kuwekeza kwenye miradi mkubwa hii? Katika makampuni ya kawaida ya kibiashara kampuni inapowekeza kwenye miradi na kupata faida inagawa baadhi ya faida hizo moja kwa moja kwa wanahisa wake.

Je, mashirika yetu haya yanavyowekeza fedha hizi zote yanawagawia kiasi gani cha “faida” wanachama ambao fedha zao zinaingizwa huko? Mtu anayepata mafao ya shilingi elfu themanini kwa mwezi baada ya kustaafu anafaidika vipi na shirika kuwekeza mabilioni kwenye mafuta, barabara na madaraja au kuzalisha umeme? Je, wanachama wanaweza kudai kuwa asilimia kama 10 hivi kila mwaka ya faida yote ambayo NSSF inapata katika uwekezaji irudishwe kama “gawio” kwa wanachama wake? Au faida wataambiwa ni kuwa “na wao watatumia madaraja na barabara hizo”!

Nimeshawahi kusema huko nyuma kuwa mashirika ya umma kama NSSF ambayo yanawekeza mabilioni ya fedha za wanachama kwenye miradi hii mikubwa ambayo ni rahisi kuyumbushiwa na hali mbaya ya uchumi au matatizo mengine (fikiria daraja jipya likijengwa halafu likabomolewa na tsunami au tetemeko la ardhi!) yanahitaji kuwekewa utaratibu mkali sana wa uwekezaji. Hayapaswi kuachiliwa kuwekeza kana kwamba yao ni mashirika binafsi yenye lengo la faida tu!

Magufuli bila kupiga vita ufisadi anatuaminisha uongo. Mojawapo na ninaweza kusema kwangu ni tatizo kubwa la Magufuli ni kuwa haamini kabisa kuwa ufisadi ndilo tatizo kubwa kabisa linalokabili taifa sasa hivi na kuwa mambo mengi anayoyapigia kelele (kutofuatwa sheria kwa mfano) ni zao la ufisadi huo.

Magufuli anaamini kabisa kuwa serikali yake ni safi, uongozi wake ni bora zaidi na kuwa chama chake ni safi kabisa! Amefumba macho kabisa kama mbuni hasikii wala haambiwi kuhusu ufisadi.

Matokeo yake ni kuwa anajikuta anarudia vitu vile vile. Mara afute mkandarasi, mara aagize Kajima warudie barabara, mara apigie kelele watu wabomolewe nyumba.

Anafikiri – kwa makosa – watu hawajui sheria. Bila kupambana na ufisadi na mazao ya ufisadi haijalishi ni mradi gani ataupigia debe kwa kutumia takwimu zote alizonazo na hata maneno ya vijembe vya kisiasa hawezi kabisa kusimama kama kiongozi kati ya wananchi.

Watanzania wanahitaji kiongozi ambaye anafahamu na anapambana na ufisadi. Bahati mbaya sana yeye mwenyewe ni mmoja watu wambao walihusishwa na ufisadi mkubwa wa uuzaji wa nyumba za serikali miaka kadhaa iliyopita. Hadi leo hajaomba radhi taifa kwa kuruhusu jambo hilo ambalo lilisababisha gharama kubwa kwa serikali kwani pale ambapo ilikuwa rahisi kwa kiongozi kuhamia kwenye mji na kukuta nyumba ya serikali palipogeuka kuwa serikali ianze kuhudumia watumishi wake kwenye mahoteli!

Ninaogopa uongozi huu wa aina ya Magufuli. Sihoji dhamira yake hata kidogo ya kupenda au kutaka mabadiliko au kuona jiji la Dar “watu wanaishi kwa starehe”. Ninahoji kama anachosema kinawezekana bila kuwa shujaa wa kupambana na ufisadi.

Hadi leo hatujamsikia yuko upande gani kwenye kashfa za EPA, Meremeta, Kagoda, Mwananchi Gold, Richmond na Dowans! Sijui yuko upande gani kwenye kashfa ya ununuzi wa ndege ya Airbus 320 ambao wengine tuliipigia kelele miaka minne iliyopita. Magufuli yuko salama kwenye kiti chake cha enzi akiwa waziri lakini anapenda usalama tu wa ofisi yake. Hapendi kuudhi watu kwa kuchukua msimamo wa uthubutu. Binafsi sijali sana kama anasimamia barabara, daraja au jengo fulani kwani hayo yote yanaweza kufanywa hata na mafisadi na ukweli kuwa baadhi ya mafisadi waliokubuhu nchi hii ndio wasimamizi wenyewe wa miradi!

Binafsi nasubiri kwa hamu kumuona akichukua upande wa kupinga ufisadi katika serikali yake na siyo tu katika wizara yake. Nasubiri kumsikia akizungumzia ufisadi kama tishio la wazi la maisha na hali za wananchi wetu. Jiji la Dar-es-Salaam liko kama lilivyo si kwa sababu watu hawataki kufanya kazi bali kwa sababu hizo ajira zenyewe nyingi zimefungamana na ufisadi. Mtu asiyepiga magoti na kutoa sadaka kwenye madhabahu ya ufisadi habarikiwi!

Mtu akitaka kufanikiwa ni lazima aende kufanya hija kwa fisadi kiongozi au kuwadi wa ufisadi ili mambo yake yaende vizuri! Magufuli hatambui hilo anataka tuamini kuwa tatizo ni wananchi!

Nilikua ninaamini kuwa anaweza kuwa kiongozi mzuri lakini nimegundua kuwa bila ya madaraka Magufuli ni sifuli. Hana la kufanya, hana la kushawishi, na hawezi kusimamia kitu bila kuwa na madaraka. Ila anataka kuogopwa si kwa sababu anaweza kushawishi bali kwa sababu ana uwezo wa madaraka kufanya anayofanya. Binafsi nampa changamoto kuwa atoke kwenye kiti chake cha starehe na kusimama kupambana na ufisadi ambao Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliita ni “adui mkubwa wa nchi wakati wa amani kuliko vita!”

Kiongozi asiyetembua ukweli huo na asiyesimama kusimama na adui huyo mkubwa wa uhuru na utu wa Mtanzania haijalishi anatembea kwa miondoko gani au anafanya nini cha kusifiwa ni wa kuangaliwa kwa kuogopa. Mara zote uongozi ni uwezo wa kushawishi na siyo uwezo wa kutishia watu. Ni madikteta tu ambao wanaweza kuleta “maendeleo” kwa kulazimisha siyo kwa kushawishi. Matokeo yake ni kuwa “maendeleo” hayo ni ya picha!

Tanzania kuwa kama Nigeria

Tukikubali hili la kutukuza vitu na siyo utu na kuweka mkazo katika kupendezesha majengo badala ya utu wa mtu tunakubali kufuata njia ya Nigeria au nchi nyingine ambazo zina ‘vitu vizuri’ lakini hazina utu. Jamani Nigeria ina mabarabara na madaraja ya kila aina. Daraja refu zaidi katika Bara la Afrika ni lile la Third Mainland Bridge ambalo lina urefu wa kilomita 11.8. Nigeria inayo mabarabara ya juu kwa juu (flyovers) na kwa hakika ina barabara nyingi tu za kisasa kulinganisha na Tanzania.

Lakini, Nigeria imejua amani na utulivu? Je Nigeria wana umoja zaidi?Je, Nigeria ufisadi umedhibitiwa? Je, Nigeria ingeweza kutulia na kushinda ufisadi leo hii ingekuwa wapi?

Ninachokiona ndicho ambacho Tanzania inakitaka na ndio maana maneno yaliyoniudhi ya Bw. Magufuli ni hayo ya kuonekana kutaka kujenga majengo ya kisasa ili watu waje kuyaona! Hatuhitaji daraja la kisasa ili watu waje kulishuhudia! Vinginevyo, tutajenga madaraja, tutajenga mabarabara na mabarabara ya juu kwa juu lakini watu wetu wataendelea kuwa maskini, utu wao ukidhalilika na wao wakiwa watumwa wa matajiri wachache ambao watapita kwenye mabarabara hayo huko mamilioni ya Watanzania wakijivunia picha za kwenye post cards - si mnakumbuka watu hupiga picha kwenye lile daraja la wenda kwa miguu la Manzese?

Ndugu zangu, tusikubali kuwa kama Nigeria. Tusikubali kujenga vitu kwa ajili ya sisi nasi kusema “tunavyo”. Kabla hatujajenga hayo mabaraba ya kwenda mbinguni (nina uhakika wapo watakaoenda mbinguni kupitia barabara hizo) tuboreshe kwanza na kwa kiwango cha juu hivi vidogo vilivyotushinda hadi sasa.

Jamani, kama NSSF wanazo fedha hizo bwelele kwanini wasijenge mitaro ya maji machafu na maji ya mvua ili watu wa Dar waishi kwa heshima na siyo kutegemea huruma ya wingi wa mvua? Kama serikali ina mipango ya kuboresha jiji la Dar kweli kwanini tumeshindwa kujenga barabara nzuri za kawaida kwenye maeneo ya watu, kuwahakikishia umeme na maji safi huku viwanja na bustani za mapumziko zikiwepo karibu kila kwenye halmashauri!?

Ndugu zangu, tunaweza kushangilia hotuba, tunaweza kushangilia picha (nina uhakika kuna watu walikuwa wanasisimka wakiangalia picha za hilo ‘daraja’). Lakini ukweli tunapaswa kufunguliwa na kutaka kushangilia tunapoona maisha yetu yanaboreshwa zaidi na utu wetu unainuliwa zaidi.

Kama watu hawana mahali bora pa kuishi, kula au mavazi barabara za mbinguni zitawasaidia nini? Daraja la Kigamboni haliwahusu maskini wanaoishi Kigamboni linahusu matajiri wanaoishi Kigamboni! Kwa sababu maskini bado watalipa fedha kutumia daladala kuvuka; matajiri wataweza tu sasa kwenda kwa raha zao kwenye viwanja vyao na nyumba zao huko!

Siamini mpaka nione

Binafsi naomba mniruhusu niwe Tomaso! Siamini mpaka nione. Siamini kama gharama itakuwa ni hiyo bilioni kama 200 hivi hasa nikikumbuka mradi mwingine wa hii serikali waujenzi wa maghorofa pacha ya Benki Kuu.

Binafsi siamini kuwa hata daraja likijengwa litadumu kwani kama mfano wa ujenzi wa miundo mbinu mingi ukiangaliwa tunajua ni nini kinatokea mara wakishamaliza kukata utepe na kutoa hotuba za kupongezana.

Uharibifu huanza. Jamani, si tumeona kwenye daraja la Mkapa? Hili daraja likikamilika na baada ya kula fedha nyingi tusije kuja kuambiwa kuwa “daraja linafungwa kwa matengenezo makubwa”. Si tumeona kwenye barabara hizi hizi za Magufuli! Nitatoa pongezi zangu za kwanza inshallah ujenzi wadaraja utakapoanza! Hatushangilii picha, hatupongezi maneno au kutukuza takwimu! Tunapongeza ubora ndugu zangu, tunapongeza ubora! Magufuli hajanishawishi hadi hivi sasa ni sifuli.

Chanzo: Mtanzania Daima: Magufuli na daraja la Kigamboni, tushangilie?

mwanakijiji fuatilia hii article kwenye mwanahalisi, japo hazija differ sana kuna tofauti.

lakini hata hii mkuu, kuweka vitu vya baba wa taifa na kusema kuna 'hujuma ya kulifuta jina lake' sijui inatokea wapi
na mengine yanabaki vile vile tu mkuu...is just a challenge
 
Waberoya, kabla ya kwenda mbali, hiyo makala ya Mwanakijiji uliyosoma kwenye gazeti la Mwanahalisi inafanana na hiyo niliyoweka hapo juu kutoka tovuti ya freemedia.co.tz? Vichwa vya hizo makala vinatofautiana?

kuna tofauti ya mtiririkona content zingine za kwenye daimahazimo mwanahalisi!!!!

ila vipengele vinavyoni boa vimo sana tu kama

Magufuli bila kupiga vita ufisadi anatuaminisha uongo. Mojawapo na ninaweza kusema kwangu ni tatizo kubwa la Magufuli ni kuwa haamini kabisa kuwa ufisadi ndilo tatizo kubwa kabisa linalokabili taifa sasa hivi na kuwa mambo mengi anayoyapigia kelele (kutofuatwa sheria kwa mfano) ni zao la ufisadi huo.

Magufuli anaamini kabisa kuwa serikali yake ni safi, uongozi wake ni bora zaidi na kuwa chama chake ni safi kabisa! Amefumba macho kabisa kama mbuni hasikii wala haambiwi kuhusu ufisadi--mwanakijiji

Hakuna kitu kibaya kama kumwazia mtu, ukamsemea , halafu akaka kimya asikujibu , mwanakiji anaa mini kila anayepiga kelele ufisadi ndiye 'fighter'!!!
 
A million dollar question!
Kwa nini tuko desperate kuwaondolea wakaazi wa kigamboni (wenye magari)adha ya foleni ya pantoni? Foleni ya morogoro road inajulikana haswaa shida yake, why are we not doing the fly_whatevers? Watanzania, daraja linaweza lisiwahusu! Magufuli anajijua anafanya nini na kwa nini!
..mpaka sasa hivi sijui faida za ujenzi wa hili daraja ni zipi.

..je, ktk madaraja yote yanayotakiwa kujengwa, hili la kigamboni lina umuhimu kuzidi hayo mengine?
 
Nimeisoma vyema hiyo makala ya MMM ,nakiri kuwa ina mapungufu kutokana na mtiririko wa habari zima.

Napata wasiwasi kuwa mwanzisha thread hii ana mwelekeo gani kimtazamo kuhusu MMM.Kinachojadiliwa kwenye thread hii kimekosa mwelekeo kutokana na ukweli kuwa mtoa mada ameonyesha wazi kuwa huwa hakubaliani na MMM.
Binadamu ana hulka ya kutafuta makosa kwa adui yake ili aweze kumshambulia kuuonyesha uma kuwa kwa nini yeye hakubaliani /anapingana na adui yake. Mtazamo wangu ni kwamba watanzania ni washabiki wa mambo hata kama hayafai kushabikia.

du umechemsha mpaka basi!! aibu
 
Umenikumbusha initial plan ya mlimani city! Haikuwa yale ma_godown pale yaliyojengwa na temporary structures! Yalisambazwa kama insert kwenye newspapers nikasema walau! Afadhali wangempa manji akajenga ka-quality something tukawa tunaenda kushangaa maji yanarukaruka!
Hiyo simulator part of it ipo youtube na humu jf...
Tafuta hizo 6 DVD utaona simulator itakuwa kama Doha!.
 
A million dollar question!
Kwa nini tuko desperate kuwaondolea wakaazi wa kigamboni (wenye magari)adha ya foleni ya pantoni? Foleni ya morogoro road inajulikana haswaa shida yake, why are we not doing the fly_whatevers? Watanzania, daraja linaweza lisiwahusu! Magufuli anajijua anafanya nini na kwa nini!

Kikwete anataka akiondoka madarakani akumbukwe kwa kujenga daraja la Kigamboni kama Mkapa alivyojenga la Rufiji. Except hilo daraja nini zaidi cha kumkumbuka Kikwete? Hakyanani nakwambia hilo daraja kama litakamilika halitaitwa "Kigamboni Bridge" bali "Kikiwete Bridge".

Maelezo ya Mwakyembe bungeni jana yanaonyesha bado ni "plans" za kujenga daraja. Nilidhani tutakuwa kwenye "actions" sasa ikizingatiwa magufuli amesema daraja litakamilika ndani ya miezi 36? Hizi habari zinatoka bungeni jana kweli?

[TABLE="width: 100%, align: left"]
[TR]
[TD="class: theTopicHead, align: left"]From the Parliament[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: mainStory, align: left"]Plan on Kigamboni bridge still stands[/TD]
[/TR]
[/TABLE]



Friday February 03, 2012

THE government has reiterated its commitment to implement the construction of the much awaited Kigamboni Bridge in Dar es Salaam so as to ease transport, the National Assembly was told on Friday.
Deputy Minister for Works Dr Harrison Mwakyembe said when responding to a question by Faida Bakari (Special Seat - CCM), who demanded to know when the project would be implemented. Dr Mwakyembe said: "Plans are well underway to construct the Kigamboni Bridge, but at the moment we'll continue to improve the existing ferries to ensure that there is reliable transport between Kigamboni and Dar es Salaam city centre."

In her basic question, Pindi Chana (Special Seat -- CCM) had demanded to know if the government had any plans to introduce weekly or monthly payments for people using the ferry services. Responding, Dr Mwakyembe said the government introduced a pilot project for ferry passengers to pay monthly fees for cars of various institutions including development partners, students vans, parastatals, ambassadors and private banks.

However, he said the government experienced challenges on maintaining the new procedures to use seasonal tickets, saying they were at the time thinking of alternative conducive procedures to run the project. He further said that already the government through Tanzania Electrical, Mechanical and Electronics Services Agency (TEMESA) had contracted a consultant under the World Bank support.

The consultant would be tasked to come up with a vending machine system. He said the new system would enable easy usage of weekly, monthly or even seasonal tickets because, he said, the machines would be installed in different parts of the city to prevent unnecessary queues. He said the design work would be completed by June this year, and thereafter the procedure to get a contractor for the project would be announced.

Daily News | Plan on Kigamboni bridge still stands
 
Kwa hali ilivyo, tena magufuli ndo ataiomba serikali kumruhusu kufanya huo ubatizo, sasa kama hana cha kujisifia nacho afanyeje banaa!

Ila bado niko hapo, plans hata kama zitachukua another 40 yrs (manake kama issue ilianza 1977...)Kuna zao gani tunalopigania kutoa kigamboni kuleta mjini? Morogoro road inaleta mahindi na kila kitu na kufikisha mjini imekuwa shughuli, kigamboni kuna mchicha na nazi chache hazifiki kkoo! Kuna mchango gani kiuchumi kigamboni iwe na thamani hiyo? Ungeniambia tunajenga daraja la mto kilombero ili mahindi na mchele vivuke kirahisi ningeelewa zaidi!
Kikwete anataka akiondoka madarakani akumbukwe kwa kujenga daraja la Kigamboni kama Mkapa alivyojenga la Rufiji. Except hilo daraja nini zaidi cha kumkumbuka Kikwete? Hakyanani nakwambia hilo daraja kama litakamilika halitaitwa "Kigamboni Bridge" bali "Kikiwete Bridge".


THE government has reiterated its commitment to implement the construction of the much awaited Kigamboni Bridge in Dar es Salaam so as to ease transport, the National Assembly was told on Friday.
[/FONT][/COLOR]
 
  • Thanks
Reactions: EMT
mwanakijiji fuatilia hii article kwenye mwanahalisi, japo hazija differ sana kuna tofauti.

lakini hata hii mkuu, kuweka vitu vya baba wa taifa na kusema kuna 'hujuma ya kulifuta jina lake' sijui inatokea wapi
na mengine yanabaki vile vile tu mkuu...is just a challenge


Kwa kweli nikanza kufuatilia hivyo ntakuwa sina kazi nyingine. Tumia makala hiyo ya TD kama msingi wa ukosoaji wake.
 
Asante Soby kwa kuweka haya mabandiko!

Mwanakijiji anadhania CCM wote wasipotaja jina la Nyerere basi hawampendi......Nyerere is dead, buried in butiama, thats life amewaza na kumsemea mengi magufuli na hajaweka vithi
bitisho au sababu

mwanakijiji na 'nyerere' wake anaonekana kama michael jackson

Unapokataa kuwa si vyena mimi kumdhania Magufuli na jujona sahihi wewe nwenyewe unanidhania mimi na Nyerere "wangu" na hauoni tatizo. So kwako ni vibaya kwa mwanakijiji kumdhania Magufuli lakini ni sawa wewe kunidhania mimi?
 
Magufuli bila kupiga vita ufisadi anatuaminisha uongo. Mojawapo na ninaweza kusema kwangu ni tatizo kubwa la Magufuli ni kuwa haamini kabisa kuwa ufisadi ndilo tatizo kubwa kabisa linalokabili taifa sasa hivi na kuwa mambo mengi anayoyapigia kelele (kutofuatwa sheria kwa mfano) ni zao la ufisadi huo.

Magufuli anaamini kabisa kuwa serikali yake ni safi, uongozi wake ni bora zaidi na kuwa chama chake ni safi kabisa! Amefumba macho kabisa kama mbuni hasikii wala haambiwi kuhusu ufisadi--mwanakijiji

Hakuna kitu kibaya kama kumwazia mtu, ukamsemea , halafu akaka kimya asikujibu , mwanakiji anaa mini kila anayepiga kelele ufisadi ndiye 'fighter'!!!

Well, as Desmond Tutu once said "If you are neutral in situations of injustice, you have chosen the side of the oppressor. If an elephant has its foot on the tail of a mouse and you say that you are neutral, the mouse will not appreciate your neutrality." Inawezekana the like of Magufuli, Pinda, etc hawaamini serikali ya Kikwete ni safi but in public wameamua kuwa neutral kwa kutozungunzia ufisadi. Kama hata mtoto wa primary anajua ufisadi unaofanyika nchini, ndiyo sembuse Magufuli asijue?

"Nothing is more unjust, however common, than to charge with hypocrisy him that expresses zeal for those virtues which he neglects to practice; since he may be sincerely convinced of the advantages of conquering his passions, without having yet obtained the victory, as a man may be confident of the advantages of a voyage, or a journey, without having courage or industry to undertake it, and may honestly recommend to others, those attempts which he neglects himself" per Samuel Jackson.
 
Kwa kweli nikanza kufuatilia hivyo ntakuwa sina kazi nyingine. Tumia makala hiyo ya TD kama msingi wa ukosoaji wake.

sikujua kuwa uliwahi kuitoa Tanzania daima, nimesoma mwanahalisi ambako umesema haukuituma huko.........nakueleza tofauti unasema huna muda wa kufuatilia......unamdanganya nani? content za Tanzania daima na mwanahalisi zina utofauti mkuu!! usishtuke kwa hili? mtu a-edit kazi yako halafu unasema huna muda wa kufuatilia?

mwanahalisi ni wewe ulipeleka na edit iko so obvious kutokana na muda wa article uliyoandika. TD uliandika soon baada ya lile tukio, mwanahalisi umeandika baadae sana baada ya tukio hili!

TD ngau ina vichwa vidogo vidogo vya ndani ya article,this is not a case in mwanahalisi!
 
Well, as Desmond Tutu once said "If you are neutral in situations of injustice, you have chosen the side of the oppressor. If an elephant has its foot on the tail of a mouse and you say that you are neutral, the mouse will not appreciate your neutrality." Inawezekana the like of Magufuli, Pinda, etc hawaamini serikali ya Kikwete ni safi but in public wameamua kuwa neutral kwa kutozungunzia ufisadi. Kama hata mtoto wa primary anajua ufisadi unaofanyika nchini, ndiyo sembuse Magufuli asijue?

"Nothing is more unjust, however common, than to charge with hypocrisy him that expresses zeal for those virtues which he neglects to practice; since he may be sincerely convinced of the advantages of conquering his passions, without having yet obtained the victory, as a man may be confident of the advantages of a voyage, or a journey, without having courage or industry to undertake it, and may honestly recommend to others, those attempts which he neglects himself" per Samuel Jackson.

Huyo mpiganaji ni nani ndani ya CCM, mweke hapa nimjue!!

hints: soma signature yangu!
 
Back
Top Bottom