Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Endelea tu. Maisha ni magumu mdogo wangu. Jaribu ku save hizo pesa zikusaidie baadae. Ningekwambia kitu ila bado bado subiri ufike 21.Aisee, kama utani umejuaje....
Nimemaliza almost 900k hapa za mama samia chini ya miezi 2.... anasa zinaponza
Nina stress hapa nawaza napigaje simu home😥
Baada ya kumaliza Chuo mwaka jana life ikapiga vibaya mno, kila muda nilikuwa nawaza jinsi gani nitasaidia familia yangu (Ni mtoto wa kiume mkubwa) Ilikuwa inauma sana pale ambapo unaamka asubuhi huna cha kufanya hadi kuna muda unahisi kama kifua kinabana.
Kuna muda nakaa najitafakari naona kama ni mzigo home, but hakuna aliyewahi niambia, sister kuna muda mshahara ukitoka ananitoa laki basi maisha yanaenda.
Mwanzoni mwa mwaka huu kuna mchongo nikaupata katika harakati za kushughulikia ili utiki, nikawa naingia katika mzozo sana na mzee maana mara nyingi nilikuwa narudi usiku anamind, ananisema ila kwa upande wangu inaniuma lakini nakaza ili isionekane kama imeuma (akaanza kuona kama namdharau) sasa kuna muda huna nauli kuomba siwezi so nachukua bike kutoka home hadi kwenye michakato as usual narudi usiku.
Kwenye kuhangaika hivyo mchongo ukatiki nikatumiwa mkataba nikasign nikaenda kazini, nikaona afadhali nimetoka home, mchongo unalipa fresh tu, silipi kodi wala bills kama maji, umeme na utilities zingine, na ni apartment nzuri unyama ni mwingi.
Leo account imesoma kwa newhires wote mzigo umesoma almost M 8, nikatoa M2 nimewatumia home, bi mkubwa ameshukuru mnooo, kuna ile feeling ya kuwa Now na wewe ni wa muhimu, sijawahi jisikia vizuri kama leo, ameninenea maneno ya Baraka hadi nikahisi zinajaa physically. Leo na mimi nimehisi ni wa muhimu.
🤣🤣🤣🙌🙌Kama unachokisema ni kweli basi chukua ushauri huu utakusaidia sana:
Funga PM yako haraka sana. Utakuja kunishukuru baadaye!
Mwalimu wako aliyekufundisha marketing ni genius. Mfikishie hongera zangu aisee [emoji122][emoji122][emoji122]
Hata usiwaze kaka mambo hua yanakaaga sawa yenyewe kikubwa ww nae uwe unajitosa 🤔🤔shule ina njia zake na mtaa una njia zake, atakaekusaidia sio unayeamini atakusaidia ukimaliza shule utakutana na watu wengn kbsmaisha yanaogopesha sana kwa sisi watoto wa kiume wakubwa😬
sijui nikimaliza chuo itakuwaje
niambie tu usiogopeEndelea tu. Maisha ni magumu mdogo wangu. Jaribu ku save hizo pesa zikusaidie baadae. Ningekwambia kitu ila bado bado subiri ufike 21.
Zaka na sadaka ni WIZI.Usisahau zaka na sadaka hapo tenga kama millioni 1.. then hIyo million 5 iliyobaki nunua uwanja mkubwa sana hata wa million 3 then 2 nenda nayo taratbu kwa mambo mengine
NB; USISAHAU KUJIPONGEZA KWA KUFANYA JAMBO LINALOKUPA FURAHA SANA
Hata yuen kwa mwajiriwa mpya aliyekuwa jobless nyumbani hawezi kupata kiasi hicho! At most ni dola 2,000/= ambazo haziwezi kufika M8 kwa pesa za bongo!!Atakwambia anafanya kazi yueni
Ikitiki, jero tu inatoshaUkipewa nifanyie buku mwanang
Mkuyungu village njoo huku ukutane na new teacher anayepata M8 kwa mwezi!!!Taasisi x, nafasi ni new teacher
Sasa wewe hiyo hela umeipatajeYuen ni 1980 kama sijakosea
Amesema ni Mwl.Wengi mnajaribu kumbishia mleta mada kuwa account haiwezi kusoma M8 lakini labda yeye alichokosea ni kuweka story yake nusu nusu au kutoiweka vizuri.
Yawezekana hizo M8 ni limbikizo tokea huko mwanzo wa mwaka aliposema kuwa ndio hiyo mishe imetiki. Pia amesema anaishi bila cost yoyote so hebu mpeni nafasi amalizie story au arekebishe kabla hamjambishia.
Akikujibu nitagAmesema ni Mwl.
Fanya kaanza kazi mwezi wa Kwanza
Fanya hakatwi bodi Wala chama sijui Cha walimu.
Fanya pesa anayolipwa hata kumi hakatwi.
Na huu ni mwezi wa nane.
Jibu ni kuwa Mwl analipwa 1m kwa mwezi na toka mwezi wa Kwanza hajatumia hiyo hela hata Mia
Ndio hiyo 8m ilivokuja Au sio !