Kwa mara ya kwanza nimemuona Malaika

Kwa mara ya kwanza nimemuona Malaika

Nilikuwa nasikia tu na kusoma vitabu kwamba malaika wapo, na kwamba kuna watu wametokewa na malaika, lakini sikuelewa sana. Sasa na mimi kwa mara ya kwanza nimethibitisha malaika wapo.

Mwezi uliopita niliugua sana nikawa katika hali ya kufa. Nilikuwa sina hamu ya kula chakula, nilikuwa nasikia joto kali, mara baridi kali. Kichwa kilikuwa kinauma sana. Mwili wote ulikuwa umelegea, kwa sababu hiyo nilikuwa natamani kulala tu kila wakati. Nikahisi labda ni uchovu kwa sababu ya shamba nililokuwa nimelima siku kadhaa kabla ya kuanza kuugua. Hali ilivyozidi kuwa mbaya nilienda hospitali, wakanipima vipimo vyote muhimu lakini hawakuona tatizo lolote. Siku hiyohiyo kama saa saba hivi usiku niliamka kitandani nikaenda “toilet.” Taa ya umeme ilikuwa imeungua humo, ikanibidi nitumie tochi ya kwenye simu yangu inimulikie. Mara baada ya kujihudumia, nikiwa bado nimesimama pale, nilipatwa ghafla na kizunguzungu kikali sana. Nilikuja kutambua baadaye kumbe muda huohuo nilipoteza fahamu, na simu niliyokuwa nimeishika mkononi niliiachilia, bila kutambua, ikaangukia chooni(choo cha kukalia). Baada ya kupoteza fahamu kumbe nilidondoka chini; lakini kabla kichwa hakijagusa chini kwenye sakafu ya choo, kuna mtu alitokea ghafla akanidaka kichwa na kunisogeza nje ya mlango wa choo. Nikiwa bado chini fahamu zilirejea,nikamuona mtu huyo amenishika na kuniinua. Nikapata nguvu kidogo nikapanda tena kitandani kulala. Kabla sijalala nilitafuta simu yangu ili niwapashe habari ndugu na jamaa, yaliyonitokea. Simu sikuiona, kumbe ilikuwa imeangukia chooni ikajaa maji na kujizima!

To cut a long story short, nilihisi huenda udhaifu huo ni dalili ya Coronavirus(Covid-19) kwakuwa nilikuwa nimesikia kwamba dalili za wimbi la pili zinatofautiana kidogo na zile za wimbi la kwanza. Kwa sababu hiyo nikaanza kula sana matunda: malimao, vitunguu saumu, tangawizi, asali, nk. Namshukuru Mungu nimepona, na nimehakikisha kuwa ni kweli Mungu yupo na malaika wake wapo na wanawahudumia wanadamu. Huyo aliyenidaka alikuwa malaika japo mimi nilimuona katika umbo la kawaida tu la kibinadamu kama ilivyotokea kwa Ibrahimu. Asante Mungu kwakuwa sawasawa na ahadi yako katika Zab 91:11-12 uliniagizia malaika wako anilinde na mikononi mwake alinichukua, kichwa changu kisiumie sakafuni.
Mkuu wewe kweli una imani timilifu.
Endelea hivyo hivyo sio wale wanaenda kwa Kakobe na Mwamposa.
 
Mkuu wewe kweli una imani timilifu.
Endelea hivyo hivyo sio wale wanaenda kwa Kakobe na Mwamposa.
Bado, mkuu.
Natamani nimjue sana Mwana wa Mungu; niwe mtu aliyekomaa na kuufikia utimilifu wake Kristo mwenyewe. Ili nisiwe tena kama mtoto, nikitupwa na kupeperushwa huko na huko kwa kila upepo wa mafundisho wanayozua watu wadanganyifu ili wawapotoshe wengine kwa hila. Waefeso 4:13-14
 
Bado, mkuu.
Natamani nimjue sana Mwana wa Mungu; niwe mtu aliyekomaa na kuufikia utimilifu wake Kristo mwenyewe. Ili nisiwe tena kama mtoto, nikitupwa na kupeperushwa huko na huko kwa kila upepo wa mafundisho wanayozua watu wadanganyifu ili wawapotoshe wengine kwa hila. Waefeso 4:13-14
Hujijui lakini Roho Mwema yupo ndani yako.
 
Mungu akipenda kukufanyia Jambo Ni kwa upendo wake tu. Mimi hapa nyumbani kwangu hiyo Beena tumepewa na imekuwa Ni wakati nzuri kwa familia yangu maana wote tumepata neema hiyo na si Mara moja au mbili ni Kila Mara. Utukufu Ni kwa Mungu muumba wa vyote.
 
Mungu akipenda kukufanyia Jambo Ni kwa upendo wake tu. Mimi hapa nyumbani kwangu hiyo Beena tumepewa na imekuwa Ni wakati nzuri kwa familia yangu maana wote tumepata neema hiyo na si Mara moja au mbili ni Kila Mara. Utukufu Ni kwa Mungu muumba wa vyote.
Amen
 
Kwa nini makanisa ya kilokole mafundisho yao huegemea juu ya miujiza? Na ushuhuda wa miujiza?
 
Kwa nini makanisa ya kilokole mafundisho yao huegemea juu ya miujiza? Na ushuhuda wa miujiza?
Mungu anajidhihirisha kwetu kwa namna nyingi thus way kila mtu ana namna yake(miujiza) ya kumjua Mungu.
Ili umjue Mungu yakupasa kuwa na ushahidi wa jambo fulani
eg. Unaweza ukasali ombi likijibiwa ndo utaingiwa na hiyo imani.
Katika Biblia Bwana wetu Yesu Kristo alifanya miujiza mingi Ila kwa lengo Kuu Moja tu, nalo ni kuuthibisha ukuu wa Baba Muumba.
Sasa baada ya uthibitisho ni Kazi ya kila mmoja kutafuta kusudio la kuumbwa kwake. Hapo Mungu Baba anakuwa ameshakuonyesha njia yakumjua yeye na maamuzi yote yanabakia juu yako.
Tuna amini kila mmoja duniani ni lazima ataonja neema ya Bwana na ni kweli ipo hivi.
Lakini baadhi yetu wamekuwa wagumu kuamini.
 
Kwa nini makanisa ya kilokole mafundisho yao huegemea juu ya miujiza? Na ushuhuda wa miujiza?
Miujiza ipo toka Mwanzo hadi sasa ni muujiza, uwepo wako na uimbaji wako tu ni muujiza. Kimsingi, miujiza ipo kwa ajili ya kutujenga kiimani. Yesu aliponya, alilisha watu, alifufua watu n.k hiyo yote ni miujiza. Sema kosa la kanisa la sasa ni kufanya muujiza ni muhimu kuliko Neno na maisha ya kumpendeza/kujitoa kwa ajili ya Mungu. Yesu alifundisha Neno na kuhubiri sana kuliko kutenda miujiza.
 
Kwa nini makanisa ya kilokole mafundisho yao huegemea juu ya miujiza? Na ushuhuda wa miujiza?
Huegemea?!

Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Efe 2:20
 
Malaika wapo tena sana tu, sema huwa kujidhihirisha kwao ni vigumu kwa macho yetu ya kawaida kuwa identify, ni wengi pia inawatokea hvo lkn hawajui who saved them...ila kwako nahis alitaka kujidhihirisha kwa namna hyo na amefaulu kujidhihirisha, una bahati sana na huenda Mungu akawa na makusudi makubwa sana ndani ya maisha yako, ongea naye vzur, Mungu ana makusudi na kila mtu lkn kwa namna tofauti tofaut...Hongera hawez tutumia wote the same......
 
Tatizo umri mkubwa,mademu wazee na madeni kibao,jamaa wanakuja kimazingala unasema malaika.
 
Back
Top Bottom