Kwa Milioni 30, UTT amis na nyumba ya kupangisha kipi bora?

Kwa Milioni 30, UTT amis na nyumba ya kupangisha kipi bora?

Hivi huwa mnawezaje kuwaza kupata pesa kiasi fulani kikubwa kuliko uwezo wa akili zenu?

Kama umeipata kwa kubeti basi endelea kubeti hadi iishe au utapata nyingine.

Milioni 30 uwekeze kwenye faida ya laki 3, (yaani 1%).... huu ni udumavu wa ubongo.

Nipatie 10M tu nikuletee laki tano kila mwezi, hapo tumegawana faida.
 
Unataka stable income.

Wekeza kwenye nyumba ya kupanga

Tafuta location nzuri marketable au Ina projection nzuri siku za mbeleni.

Jenga vyumba vya kupanga self vikubwa. Uone kama. Utakosa Hela.

Nyumba itakupa pesa na pesa Yako unaiona hio hapo na unakuwa na option nyingi kama kukopea nyumba kuwekeza kwenye mradi mwingine na mkopo ukalipwa kwa nyumba husika ya kupanga.

Hizi UTT AMIS ni nzuri but Mimi binafsi nina mashaka nazo isije kuwa kama mambo ya Deci.

Uwekezaji wa

Fixed deposit account
Real estate
Treasury bonds

Ndio salama zaidi.
 
UTT ni stress free with very minimal risk. Hii ndio ningemshauri afanye. Yaani unaweka mzigo wa 30m, una uhakika wa zaidi ya 99% kuvuna kiasi kisichopungua 250k kila mwezi, immediately throughout the life! Uzuri wa UTT, thamani ya pesa yako inalindwa, unaweza kutumia kama dhamana ya kukopokea benki, na utamu zaidi wakati wowote (ndani ya wiki mbili) unaweza kuzichukua pesa zake zote ulizowekeza ikiwa utabadili mtazamo.

Kuhusu kujenga nyumba ya biashara, hiyo kitu inahitaji mambo kadhaa, kwa mfano:
1. Upate kiwanja. (Wapi? Bei?), ukikosea hapo, pesa inateketea na biashara haiwezi kufanyika.
2. Ramani bora. (Sio kila nyumba inaweza kufaa kupangisha popote)
3. Ujenzi (Gharama za ujenzi haziko constant)
4. Uimara wa nyumba (itadumu katika ubora wake kwa muda gani?)
5. Ukarabati (Haijarishi ni nyumba ya namna gani, kuna ukarabati ni muhimu/lazima ufanyike ndani ya miaka mitano mitano ambao utagharamu up to 10% ya thamani ya nyumba yenyewe.
6. Kupata wateja wa uhakika. (Kujenga nyumba ni jambo moja, kupata wateja wa uhakika kwa wakati wote hilo ni jambo lingine tofauti)
7. Usumbufu wa wapangaji (Hili ndio balaa kubwa, mwanzoni wanaweza kuonyesha uungwana, lakini muda unavyozidi kusogea utaona kila rangi).

Ushuhuda.
Kuna mtu kajenga nyumba nzuri ya kupangisha maeneo ya mbeya mjini, ina apartment tatu (kila moja ni Chumba, sebule, choo na jiko) kwa milioni 70, anapangisha kila moja kwa 80k kwa mwezi (jumla ya 240k kila mwezi), kuna wakati inaweza kukaa miezi hadi minne mpaka sita bila kujaa wapangaji, na kila akitoka mpangaji mmoja anafanya ukarabati wa wastani wa laki mbili.
 
Huu msemo huwa siuelewi. Real estate ndo biashara inayoweza kukupa kipato kizuri na inakufanya ukopesheke kiwepesi sana na taasisi za fedha as long as una mzunguko.

Nyumba za kukodisha na kupanga ni biashara salama kuliko hizo zote ulizotaja.

Ila, Kama biashara nyingine inatakiwa kufanya utafiti unanunua kiwanja wapi na nyumba utazijienga za aina gani na kwanini. Ukikosea hili unaingia hasara ila hasara si ya moja kwa moja kama ukiingia hasara katka kilimo sijui uchuuzi. Angalau nyumba inakuwepo pale unaweza kuuza au kukopea bank na kujaribu jambo lingine.
Real estate Kwa Tanzania hii hii.


Hiyo nyumba ya milion 30 labda kiwanja kiwepo.


Kuna nyumba huko chamazi na nje ya mji laki na nusu nyumba Kali.


Unatupa hiyo Hela unakuja kulipwa laki 2 Kwa mwezi sawa na milion 2.4 Kwa mwaka.
 
UTT ni stress free with very minimal risk. Hii ndio ningemshauri afanye. Yaani unaweka mzigo wa 30m, una uhakika wa zaidi ya 99% kuvuna kiasi kisichopungua 250k kila mwezi, immediately throughout the life! Uzuri wa UTT, thamani ya pesa yako inalindwa, unaweza kutumia kama dhamana ya kukopokea benki, na utamu zaidi wakati wowote (ndani ya wiki mbili) unaweza kuzichukua pesa zake zote ulizowekeza ikiwa utabadili mtazamo.

Kuhusu kujenga nyumba ya biashara, hiyo kitu inahitaji mambo kadhaa, kwa mfano:
1. Upate kiwanja. (Wapi? Bei?), ukikosea hapo, pesa inateketea na biashara haiwezi kufanyika.
2. Ramani bora. (Sio kila nyumba inaweza kufaa kupangisha popote)
3. Ujenzi (Gharama za ujenzi haziko constant)
4. Uimara wa nyumba (itadumu katika ubora wake kwa muda gani?)
5. Ukarabati (Haijarishi ni nyumba ya namna gani, kuna ukarabati ni muhimu/lazima ufanyike ndani ya miaka mitano mitano ambao utagharamu up to 10% ya thamani ya nyumba yenyewe.
6. Kupata wateja wa uhakika. (Kujenga nyumba ni jambo moja, kupata wateja wa uhakika kwa wakati wote hilo ni jambo lingine tofauti)
7. Usumbufu wa wapangaji (Hili ndio balaa kubwa, mwanzoni wanaweza kuonyesha uungwana, lakini muda unavyozidi kusogea utaona kila rangi).

Ushuhuda.
Kuna mtu kajenga nyumba nzuri ya kupangisha maeneo ya mbeya mjini, ina apartment tatu (kila moja ni Chumba, sebule, choo na jiko) kwa milioni 70, anapangisha kila moja kwa 80k kwa mwezi (jumla ya 240k kila mwezi), kuna wakati inaweza kukaa miezi hadi minne mpaka sita bila kujaa wapangaji, na kila akitoka mpangaji mmoja anafanya ukarabati wa wastani wa laki mbili.
Angeweka UTT Angekua na uhakika wa 8M per year. Sasa atapata kama 3M per year kama vyymba vitakua vimejaa all the time

Sent from my CPH1819 using JamiiForums mobile app
 
Unataka stable income.

Wekeza kwenye nyumba ya kupanga

Tafuta location nzuri marketable au Ina projection nzuri siku za mbeleni.

Jenga vyumba vya kupanga self vikubwa. Uone kama. Utakosa Hela.

Nyumba itakupa pesa na pesa Yako unaiona hio hapo na unakuwa na option nyingi kama kukopea nyumba kuwekeza kwenye mradi mwingine na mkopo ukalipwa kwa nyumba husika ya kupanga.

Hizi UTT AMIS ni nzuri but Mimi binafsi nina mashaka nazo isije kuwa kama mambo ya Deci.

Uwekezaji wa

Fixed deposit account
Real estate
Treasury bonds

Ndio salama zaidi.
Aiseh vitu kama hujui muwe mnakaa kimya

Kuna mifuko UTT AMIS wanawekeza kwenye Treasury bonds. Mfuko kama Bond fund wanafanya hivyo.


Unakuja kuongea uongo!


Mods comments za kupotosha kama huyu mpuuzi zifuteni
 
Hili suala la UTT linahitaji taarifa sahihi na toshelezi. Maana kuna mkanganyiko mkubwa wa taarifa.
Huo mradi usiingie kichwa kichwa watu watalia punde...Sina maana kwamba ni matapeli ila kuna madalali hawa ndio wataliza watu.

Ukipata ofisi zao kabisa haswa Dar ,Arusha ,Mwanza ,Dodoma watakupa taarifa zote ,achana na wahuni wa humu pia kuna madalali kuwa nao makini.
 
Huo mradi usiingie kichwa kichwa watu watalia punde...Sina maana kwamba ni matapeli ila kuna madalali hawa ndio wataliza watu.

Ukipata ofisi zao kabisa haswa Dar ,Arusha ,Mwanza ,Dodoma watakupa taarifa zote ,achana na wahuni wa humu pia kuna madalali kuwa nao makini
Nenda binafsi ofisi za UTT, NEVER USES AGENT, FIKA UTAFAIDIKA SANA, DAYS COMES DAYS GOBY, IN THIS LIFES HARD CASH MATTER, EASY CONVERT.
 
Kama Bado upo una fight(umri below 40), nakushauri wekeza utt. Lakini kama una familia na unasomesha, tafuta mradi wa maana. Nyumba ya kupanga siyo mradi wa maana zaidi ya mmiliki kukopesheka kwenye taasisi za kifedha.

Nje ya mada...
Anawezaje mtu amiliki 30m kupitia akili isiyoweza kufannya maamuzi magumu? Au ulishinda bahati nasibu?
Kenge wewe;!
 
Real estate Kwa Tanzania hii hii.


Hiyo nyumba ya milion 30 labda kiwanja kiwepo.


Kuna nyumba huko chamazi na nje ya mji laki na nusu nyumba Kali.


Unatupa hiyo Hela unakuja kulipwa laki 2 Kwa mwezi sawa na milion 2.4 Kwa mwaka.
Okey mkuu. Unajua hatuwezi fanana mitazamo ila still binafsi siingii kwenye biashara mpya nisiyojua siri zake kwa mtaji ambao sipo tayari kuupoteza. Nitajenga au nitaizika hiyo pesa kwenye kiwanja ambacho najua eneo litapanda thamani.
 
Okey mkuu. Unajua hatuwezi fanana mitazamo ila still binafsi siingii kwenye biashara mpya nisiyojua siri zake kwa mtaji ambao sipo tayari kuupoteza. Nitajenga au nitaizika hiyo pesa kwenye kiwanja ambacho najua eneo litapanda thamani.
Issue sio mtizamo issue ni uhalisia.
Uzoefu wa kuwekeza kwenye nyumba ya kupanga uko kibinafsi mnoo. Kwenye biashara ya kujenga ili kupangisha, uzoefu wa mtu fulani hauwezi kuwa mfano wa mtu mwingine kujifunza/kuiga na kupata matokeo yanayofanana. Tofauti kabisa na UTT. Leo hii sisi wote hapa JF (labda tuseme watu 500) kila mmoja akachukua 30m na kwenda kuiwekeza kwenye UTT, baada ya mwezi mmoja wote tutakuja hapa kukiri tumeanza kula faida inayofanana ya kiasi kisichopungua 250k.
 
Issue sio mtizamo issue ni uhalisia.
Uzoefu wa kuwekeza kwenye nyumba ya kupanga uko kibinafsi mnoo. Kwenye biashara ya kujenga ili kupangisha, uzoefu wa mtu fulani hauwezi kuwa mfano wa mtu mwingine kujifunza/kuiga na kupata matokeo yanayofanana. Tofauti kabisa na UTT. Leo hii sisi wote hapa JF (labda tuseme watu 500) kila mmoja akachukua 30m na kwenda kuiwekeza kwenye UTT, baada ya mwezi mmoja wote tutakuja hapa kukiri tumeanza kula faida inayofanana ya kiasi kisichopungua 250k.
Si kweli boss. Mitazamo na maamuzi ndo hutofautisha uhalisia wa kiwango cha mafanikio kutegemeana na maamuzi uliyochukua.

Mfano: Wewe umepeleka 30M utt ukaanza kupokea 250K, mm nikaizika pesa hapo kerege nje ya dar nikasubiri 5yrs kiwanja kipande thamani.

Baada ya miaka 5 kiwango cha utofauti wa mafanikio itategemeana na thamani ya kipande cha utt ukijumlisha na hizo laki mbili na nusu ulizopokea kwa muda wote iwapo zipo kulinganisha na thamani ya eneo nililonunua iwapo nitataka kuliuza.
 
Aiseh vitu kama hujui muwe mnakaa kimya

Kuna mifuko UTT AMIS wanawekeza kwenye Treasury bonds. Mfuko kama Bond fund wanafanya hivyo.


Unakuja kuongea uongo!


Mods comments za kupotosha kama huyu mpuuzi zifuteni
Ndio ufafanuzi sio kulalamika kwa mods

Unakuwa snitch

Snitches get stitches.
 
Si kweli boss. Mitazamo na maamuzi ndo hutofautisha uhalisia wa kiwango cha mafanikio kutegemeana na maamuzi uliyochukua.

Mfano: Wewe umepeleka 30M utt ukaanza kupokea 250K, mm nikaizika pesa hapo kerege nje ya dar nikasubiri 5yrs kiwanja kipande thamani.

Baada ya miaka 5 kiwango cha utofauti wa mafanikio itategemeana na thamani ya kipande cha utt ukijumlisha na hizo laki mbili na nusu ulizopokea kwa muda wote iwapo zipo kulinganisha na thamani ya eneo nililonunua iwapo nitataka kuliuza.
Hii hapa ndani ya miaka mitano nitakuwa na faida ya milion 22.
Screenshot_20240127-084822.jpg
 
Back
Top Bottom