Kwa mparaganyiko huu wa ndoa, sitaki tena kusikia wala kupokea kadi ya mchango wa harusi tena

Kwa mparaganyiko huu wa ndoa, sitaki tena kusikia wala kupokea kadi ya mchango wa harusi tena

Wanatamani ndoa wakishazipata wanaanza Tena kupambana kuzibomoa,
Yaani ndoa inakuwa na sarakasi za kutosha ikionekana huelewi Ndugu mwanaume unapelekwa mahakamani kwa kesi ya ulawiti au ubakaji kule nako unakuta yupo Mwanaharakati anakugonga nyundo. Tayari ndoa imeisha hiyo.
 
Mmchinaga mwenzangu kakaa na mwanamke wake miaka 12 yaani ile bila kuhalalisha na watoto 3, walikuwa dini tofauti, ila baada ya kuhalalisha TU, wamekaa mwaka Mmoja ndoa Chali.
 
umenikumbusha familia moja waliishi pamoja ile 'soge tukae' miaka zaidi ya 8, wakaja kufunga ndoa haikudumu hata miezi ikavunjika..!!
Hizi ndoa Mungu atusaidie kwa kweli. Huyu dada wa huku baada ya ndoa kuvunjika kakaa kidogo akazaa na jamaa mwingine yupo tu anajilelea katoto kake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wana Jf....
Nawaomba muendelee kuiombea ndoa yetu idumu kwa furaha na amani tele tulio nayo hii...😊
 
Ndio maana mimi ikiwezekana nitampanga bibie tukamalizie mambo bomani, asubuhi tunaenda zetu bomani tukitoka tunapita KFC kupata kuku na coke kubwa then tunaenda beach kuogelea, tunarudi home kulala.
Kesho yake Tunaingia zenji siku 3. Sherehe na honeymoon inakua imeisha hivyo.
 
Yaani ndoa inadumu muda mfupi kuliko hata ule uliotumika kwenye vikao??

Kuna haja ya watanzania kubadilika ktk suala hili la sherehe za harusi. Tafakari ya kina ifanyike ili tuchukue mwelekeo mpya.

Watu wafunge ndoa kwenye nyumba za Ibada na baada ya hapo waelekee majumbani mwao na siyo kwenda kwenye kumbi kufanya maigizo ya kujifaharisha.

Mnafanya maonesho ukumbini ya fahari kubwa na kujifanya mna furaha kubwa kumbe watu wenyewe hata hampendani.

Kuna ndoa nimechangia laki 2 zangu lkn imedumu siku 21 tu.
Ukweli mchungu, mi nafikiri muishi kwanza, mpate hata mtoto mmoja, ndio tufanye sherehe,Bora ndoa za, mkataba, au utoaji taraka urahisishwe, fikiria, mke anakuta SMS ya mapenzi, kwenye cm, anakuvizia umelala, anakuminya nyeti! And kudunga kisu cha kifua! Unakurupuka, unatembeza kipigo mpaka unazidiwa, wote mnakimbizwa hospitari mahututi, mume anakufa, mama yupo hoi, na pingu mkononi! Watoto mmemuachia nani,? Hapo watoto shule ndio basi, mateso,kunyanyasika, kama mtoto wa kike, ataishia kuwa danga,wa kiume kibaka, au shoga!
 
Wana Jf....
Nawaomba muendelee kuiombea ndoa yetu idumu kwa furaha na amani tele tulio nayo hii...😊
Sisi sisi au wengine babu?

Sisi ambao tunashadadia ubaya kuliko wema? We kaa tu kwenye mswala mwenyewe na bibi iombeeni wenyewe. Huku ni mwendo wa kuambiwa piga chini, utakuja kulia, ngoja tuone, mpandishe cheo na mwisho kabisa kataa....hewalaaa
 
fikiria, mke anakuta SMS ya mapenzi, kwenye cm, anakuvizia umelala, anakuminya nyeti! And kudunga kisu cha kifua! Unakurupuka, unatembeza kipigo mpaka unazidiwa, wote mnakimbizwa hospitari mahututi, mume anakufa, mama yupo hoi, na pingu mkononi! Watoto mmemuachia nani,? Hapo watoto shule ndio basi, mateso,kunyanyasika, kama mtoto wa kike, ataishia kuwa danga,wa kiume kibaka, au shoga!
Daah! Kiukweli watoto wanaingia kwenye kisima cha mateso pasipo kutarajia.
 
Kupiga parange kutaka hela za watu wakuchangie harusi unakaribisha manuksi, mikosi na mabalaa. Wengine hela zao za mashetani alafu unachukua kuchangia tendo takatifu la ndoa?? Unamkaribisha shetani kwenye ndoa yako! Usihusishe watu wasio wa muhimu katika ndoa yako hasahasa kutaka hela zao! Lipa mahari, pata ridhaa ya wazazi, nenda kanisani au serikalini (tendo la kisheria la umiliki wa mwenza) chukua mkeo nenda nyumbani! Hao unaowahusisha na kula hela zao wengi wachawi!
Kuna mzee mmoja jirani yangu huwa anatoa nadharia hii. Anasema harusi ndiyo inakaribisha ulozi, mikosi na mabalaa mbalimbali. Anatolea mfano kwa kusema kuwa utakuta watu wameishi kinyumba kwa miaka hata 5, lkn wakifunga ndoa na kufanya harusi tu migogoro inaanza.
 
Wadau wa ndoa mmeanza kuchangamka sasa[emoji23]
 
Yaani ndoa inakuwa na sarakasi za kutosha ikionekana huelewi Ndugu mwanaume unapelekwa mahakamani kwa kesi ya ulawiti au ubakaji kule nako unakuta yupo Mwanaharakati anakugonga nyundo. Tayari ndoa imeisha hiyo.
Unakutana na hakimu mwanamke aliyevurugwa na ndoa lazima uchezee miaka
 
Mnafanya maonesho ukumbini ya fahari kubwa na kujifanya mna furaha kubwa kumbe watu wenyewe hata hampendani.
Wanaopenda hawahitaji gharama kubwa kuonesha furaha yao.

Hizi furaha za kutumia pesa ni za kuforce.

Niliwahi kuongea na Dada mmoja classic sana. Msafi, mwenye hela zake.

Anavuta bangi, Sigara, pombe kali, ukimuona huwezi kumdhania. Viwanja kila weekend.

Kwa kuwa alinishirikisha jambo lake nikamsikiliza, kumbe anafanya starehe zote hizo ktk kutafuta Furaha.

Sisi tunamuona tukidhani ndio furaha yenyewe kwa kuwa ana hela na ni mzuri kumbe hamna.

Mtu mwenye furaha hahitaji kuboost furaha yake kwa kutumia gharama.

You can stay at home with family and friends and still be happy.
 
  • Thanks
Reactions: G4N
Back
Top Bottom