Kwa mshahara huu, Mo Dewji utajiri wako unatokana na unyonyaji wa wafanyakazi wako

Kwa mshahara huu, Mo Dewji utajiri wako unatokana na unyonyaji wa wafanyakazi wako

General Mangi

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2013
Posts
15,303
Reaction score
23,064
Huwa najiuliza sana taasisi kama Forbes inatumia vigezo gani kumjua tajiri namba moja katika nchi husika. Wanashindwa hata kutembelea wafanyakazi wa kampuni za tajiri husika kuangalia hali zao nao zikoje?

Juzi hapa nilileta bandiko kuhusu mishahara ya wafanyakazi wanaofanya katika kampuni za matajiri hawa wawili hapa Tz, Mo Dewji na Bakhresa.
METL GROUP, BAKHRESA GROUP Kampuni kubwa Tanzania zisizojali Wafanyakazi wake

Nilieleza jinsi wanafunzi wa nchi kama Marekani, hata hapo Kenya wanavyotamani kufanya kazi katika kampuni za matajiri wa nchi zao.

Lakini kwa hapa Bongo mambo ni tofauti kabisa, wafanyakazi wa Mo na Bakhersa wanafanya kazi kwakua hakuna mbadala, ajira hakuna. Na hiki ndicho kigezo hutumia kuwanyonya wafanyakazi kwani wanajua hana pa kwenda hata kama mshahara ni mdogo.

Embu wana JF tuangalie hili tangazo la kampuni ya tajiri namba moja Tz, Dewji.
Ni la dereva atakae husika na mauzo pia.

Hivi kweli kwa hali ya hapa Dar unamlipaje mtu mshahara wa Tsh 130,000 kwa mwezi? Mtu huyo anafamilia, analipa kodi, anasomesha, umeme, maji nk Ushahidi link hii hapa chini na screenshot zake, wasije wakabadilisha au kulitoa.

Salesperson Cum Driver. in Dar Es Salaam

Yani hata kima cha chini hawaja kifikia. Mbaya zaidi Serikali inajua haya lakini wanashindana na Mange Kimambi mitandaoni.

Waziri wa kazi na ajira tekeleza majukumu yako, sioni sababu ya nyie kushikilia nafasi hizo huku wananchi wanabyonywa na hawa mabepari wanao zidisha umasikini kwa wananchi.

Screenshot_2018-03-17-23-12-59-904_com.android.chrome.jpg
Screenshot_2018-03-17-23-13-20-705_com.android.chrome.jpg
 
Katika mfumo wa kibepari mfanyakazi ni gharama tu anaepunguza faida hivyo....the lower the cost the better...kwa maana nyingine lengo lake ni kuwa na gharama ndogo iwezekanavyo.....uhuru wa kweli ninkujiamini na kutafuta fursa inayoendana na thamani yako...
 
Kuna mtu akiwanyoosha hawa mnasema anawachukia. Acheni tu wasiingiliwe maanake watafunga biashara halafu mtoe lawama mtetezi wa wanyonge anaua uchumi.

Mtu yeyote mwenye uchungu na nchi ukiingia deep na kuwajua vizuri hawa 'matajiri' ukipata nafasi lazima uwanyooshe
 
shida wafanyakazi wengi hawajitambui.. kazi ya mshahara laki na 30 unaandika barua ya kuiomba ya nini?

mfumo wetu wa elimu na maisha ni mbovu.. kuna graduates wengi sana wamefanya kazi hata 10 yrs wengine ila hana asset yeyote zaidi ya liabilities kibao... akiachishwa kazi umwambie atafute hata laki 3 kwa mwezi sawa na elfu 10 kila siku hawezi... mtu kama huyu kazi hata ya laki moja anaandika barua anaomba..

hivi dereva ulipwe laki moja.. huwezi hata kuuza chips, maji, mtaani
 
Back
Top Bottom