Kwa mshahara huu, Mo Dewji utajiri wako unatokana na unyonyaji wa wafanyakazi wako

Kwa mshahara huu, Mo Dewji utajiri wako unatokana na unyonyaji wa wafanyakazi wako

kama ni tanker la mafuta yanakuwaga na lita 30,000-35,000,jamaa akishapanga kuwa leo naliangusha iwe isiwe,,basi akishaendambali sana,pengine mafuta yanaenda songea na anajua tajiri yupo dar,,anahakikisha lzm afike njombe au makambako usiku mkubwa,na akifika tu wese linamiminwa kwenye kisima cha sheli km lita 20,000,na huo mpango unakuwaga ushachongwa mapema kati ya dereva na tajiri wa sheli,km tajiri ananunua lita1 hadi kufikisha makambako labda ni 1800-basi hapo dereva anamletea hadi kituoni kwa 1200 mara lita 20,000 dereva anakomba milioni zake 24 safi,kisha taratibu saa kumi afajir anaanza kuondoka makambako akitafuta yale makona kona mengi pale mlimani mwanaume analilaza kiheshima mahali kisha analegeza vifuniko wese lililobaki liendelee kumwagika chini taratibu kabla wachomoa betri hawajafika kulimalizia wese lote,,ila miaka ya sasa naona hayo madili yamepungua maana matajiri wengi wanafunga ma camera na GPS,wanakusoma tu ukiwa njiani na unachokifanya,,,,kuna mmoja miaka ya 2004 alikua na lori lake limekula kinywaji ya TBL full,akafika njiani akauza kama nusu ya mzigo,alikua anatoka arusha kwenda singida,,wanadai mzigo aliuzia babati na lipofika maeneo ya sigino kwenye mlima logia akajidai limemshinda,akaruka lori likatumbukia shimoni,,ile kinywaji ya TBL ilobakia kwenye gari wanakijiji wa pale sigino walilewa kijiji kizima,,hata wale wasiokunywaga siku hiyo walitest kinywaj pendwa na wakalewa chakari,,ogopa hadi watoto na wamama walilewa,maana vijana na wababa walikua wanaenda eneo la ajali wanabeba makreti na kuyakimbiza kijijini majumbani kwao kisha wanarudi kuchukua tena,,wakati huo kule home watoto wanafungua chupa na kutest wakijua ni soda
😂😂wanatest wakijua ni soda hatimae kichwa kinakua kizito.
 
Katika mfumo wa kibepari mfanyakazi ni gharama tu anaepunguza faida hivyo....the lower the cost the better...kwa maana nyingine lengo lake ni kuwa na gharama ndogo iwezekanavyo.....uhuru wa kweli ninkujiamini na kutafuta fursa inayoendana na thamani yako...
Nimeipenda hii"UHURU WA KWELI NI KUJIAMINI NA KUTAFUTA FURSA INAYOENDANA NA THAMANI YAKO"
 
Katika mfumo wa kibepari mfanyakazi ni gharama tu anaepunguza faida hivyo....the lower the cost the better...kwa maana nyingine lengo lake ni kuwa na gharama ndogo iwezekanavyo.....uhuru wa kweli ninkujiamini na kutafuta fursa inayoendana na thamani yako...
Soda zenyewe sijui juice zile zinauzwa jero, tra kilasiku wanavuka malengo unataka wakulipe she ngapi? Elimu yenyewe Ni experienced tu wa secondary education sijui umeishia form two B, kwanza huo Ni mkubwa mno.
 
Wauza maduka ya nguo kino wengi wanalipwa 150,000 leo kampuni kubwa inamlipa dereva 130,000!
Mie naona JPM aruhusu waganda wakenya na wanyarwanda wajiiriwe muone Kama hizo mtazipata mtu mwenyewe dereva pyekepyeke nyingi kafungue duka ujiajiri
 
The end justifies the means... Kinachoangaliwa ni matokeo sio mchakato....
 
Mm binafisi nimewahi fanya biashara katika kiwanda cha tiles kule mkuranga kinamilikiwa na mchina anajiita goodwill aisee mshahara n kichomi sana
 
Mkuu naomba nifafanue hapa kuhusu hicho Kidogo wanachopata. Hii nafasi ya hawa SalesPerson cum driver, wanapewa Allowance ya Tsh. 100 katika Kila Carton 1 ya Maji au Soda. Akiuza Carton 100 kwa siku Ana Tsh. 10,000/= x siku 26 ni 260,000/= kwa mwezi, wakati mwingine hata Jumapili wanaingia kazini. Hapo ni kama Ameuza Cartons 100, wapo ambao wanauza mpaka cartons 500 per day. Ukiangalia huu mfumo ndo wenzetu wa Nchi zilizoendelea wanatumia, yani mtu alipwe kulingana na alichozalisha. Utaona kwa sisi ambao tunapenda Kazi ya Sales, hatuangalii Mshahara, Tunaangalia percentage on Commission based. Ugonjwa mkubwa wa Watanzania waliyo wengi anataka aone fixed salary ili apate mtelemko kila mwisho wa mwezi. Yani ufanye kazi usifanye mwisho wa mwezi hela yako iingie. Huu Upuuzi ambao matajiri wengi walishaachana nao. Hata ningekua ni Mimi lazima nione unachozalisha katika kampuni ndo nikupe mshahara mzuri. Watanzania Tubadilike. Vijana wengo mnaotoka chuoni mkiambiwa njoo ufanye kazi ya Commission hamtaki kwasababu mnapenda mitelemko. Dunia imebadilika. Mwisho, Hiyo 130,000/= wanalipwa kama hela ya Kujikimu tu In case hajafanya mauzo mwezi mzima, lakini kinyume chake Commission wanazopata ni kubwa maradufu kuliko mshahara ambao ww umelalamikia hapa. Asante
Ukweli mtupu 🤣🤣🤣!!!

Wengi tunataka uhakika wa kulipa kodi na kuishi vyema regardless ya kampuni ipate faida au la, so gross figure ikiwa ndogo automatically inakatisha tamaa.

Raha ya kazi ikuondolee stress za maisha ulipwe vizuri umudu cost na kubakiwa na kipande u save kidogo.
 
Mm binafisi nimewahi fanya biashara katika kiwanda cha tiles kule mkuranga kinamilikiwa na mchina anajiita goodwill aisee mshahara n kichomi sana
Ila si mnampigaga sana kwenye stoo!
 
Hapo mwanzo nilikuwa nashangaa Kwanini matajiri wa kihindi wana roho mbaya na kuwalipa mishahara midogo watu weusi......hadi hapo nilipopata nafasi ya kusimamia kiwanda kimoja hivi.......ni kiwanda kidogo lakini kimenifunza mengi sana juu ya sisi Watanzania........

Kwa mtu ambaye alishawahi kuwasimamia kazi Watanzania anaweza akanielewa.....

Kiukweli kuna utofauti mkubwa sana kati ya WaTanzania na watu wa mataifa mengine.....hasa kwenye uchapakazi......

Ukifanya kazi na Watanzania na ukawaendekeza na kuwapeleka kiungwana lazima utapata hasara na kufunga biashara.........

Kwanza Mtanzania hawezi kufanya kazi mpaka asimamiwe kama wapo wa hivyo ni wachache sana.....pili ni uvivu
Mtanzania anakuwa na kimuhe muhe cha kazi akiwa hana kazi lakini akishapata kazi ndio utamjua.......

Hapo kiwandani kulikuwa na kamera....yaani upande wa ndugu zangu kule Yaani muda wote kama Hakuna mtu wao ni story na kubishana mipira na siasa.......

Lakini upande wa ndugu zetu wa nje muda wote wanapiga kazi hata kama superviser hayupo wao ni kazi tu....sasa mtu kama huyo unaachaje kumlipa mshahara mkubwa.....!!?

Kwa kweli ukiwa hujawahi kuwasimamia au kufanya kazi na waTanzania huwezi kuona madhaifu yao.........

Ni bora ufanye kazi na wahindi au Wachina kumi kuliko kufanya kazi na Watanzania mia......

Sehemu pekee unapoziona nguvu za Watanzania kazini ni muda wa kufunga kazi na muda wa kupokea mishahara yao.......

WATANZANIA TUBADILIKE
🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Mtanzania kadri unavyomlipa mshahara mkubwa ndio anazidi kuwa mvivu.......

Mshahara haumpi Mtanzania motisha ya kazi bali unampa nafasi ya kuwa mzembe na mwenye kiburi kazini....

Naongea kutokana na uzoefu
Hahahah hii sidhani kama inawagusa kada zote, daktari anaanzaje kuwa mvivu au mwalimu?
 
Watu wa sales wanalipwa kulingana na jinsi wanavyouza hapo hiyo 130000 ni Kama pesa ya kulinda mkataba, hayo magari hata akija dereva mpya tayari route zimeshatengenezwa hivyo hawezi kukosa incentive ya mwezi maana target inafika tu nje ya juhudi zake na hapo utakuta Kila mwezi analipwa mshahara tofauti Tena kuanzia 1000000, mauzo yote yanatokea sales na ili upitishe lazima utumie mtu wa route ndo maana watu wa sales wanawekewa hela kidogo kwenye mikataba lakini ndo watu wanalipwa vizuri na kuheshimiwa na makampuni.
 
Watu wa sales wanalipwa kulingana na jinsi wanavyouza hapo hiyo 130000 ni Kama pesa ya kulinda mkataba, hayo magari hata akija dereva mpya tayari route zimeshatengenezwa hivyo hawezi kukosa incentive ya mwezi maana target inafika tu nje ya juhudi zake na hapo utakuta Kila mwezi analipwa mshahara tofauti Tena kuanzia 1000000, mauzo yote yanatokea sales na ili upitishe lazima utumie mtu wa route ndo maana watu wa sales wanawekewa hela kidogo kwenye mikataba lakini ndo watu wanalipwa vizuri na kuheshimiwa na makampuni.
Asante kwa maelezo
 
Back
Top Bottom