Kwa mwenendo huu wa kibiashara, shirika la ATCL litakufa kibudu siku si nyingi

Kwa mwenendo huu wa kibiashara, shirika la ATCL litakufa kibudu siku si nyingi

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
1631359155553.png

Kusudio la kuanzishwa, kufunguliwa na kuhuishwa kwa shirika mama la usafiri wa anga la nchi yetu pendwa

Tanzania ilikuwa lijiendeshe kibiashara, lipate faida na liweze kujisimamia na kujihudumia lenyewe bila kuwa mzigo kwa serikali.

Shirika la ATCL limekuwa na flight cancellation za mara kwa mara zisizo na kichwa wala miguu, yote hayo ni sababu ndege ziko busy kufanya Safari zisizo za kibiashara.

Leo utasikia kuna uhaba wa ndege, ndege zote zimeenda service, lakini ukifiatilia itakuwa ziko kwenye ziara za kuwazungusha walao neema za nchi na kuku ya Taifa wao na familia zao.

Hakuwa na sababu na IGP kutumia ndege ya biashara kwa Safari zake za kikazi, angetumia helikopta ya polisi ingekuwa vyema zaidi.

ATCL ikiendelea na utaratibu huu wa kuwa chombo Cha starehe kwa watu fulanifulani, itarudi kaburini mapema mno.

Kuwa na fleet nyingi sio mafanikio, mafanikio ni kuwa na fleet zenye kuwahudumia watu wengi zaidi ndio maana ndege za PW zinajaza wakati ATCL ndege zao zinaenda mswaki.

PW hawategemei ruzuku, wapo angani kila siku, wanafanya biashara seriously, huwezi walinganisha na ATCL.

MSIPOBADILIKA, NECHA ITAWAONDOENI SOKONI
 
... ATCL wanazo ndege nyingi. Kama hiyo moja haikuwa na route kulikuwa na ubaya gani kumpeleka msimamizi wa usalama wa raia na mali zao mh. aijiipii ziarani hapo nchi jirani? Naona sawa tu mali za nchi hazikuwahi kuwa na mwenyewe; wanajitumbulia wenye nafasi zao.
 
Mzigo wa kulipa madeni mwisho wa siku unamuangukia mwananchi
 
Isaya 50 11 Biblia haijawahi kudanganya
Isaya 50:11 BHN

Lakini nyinyi mnaowasha moto, na kujifanyia silaha za mienge, tembeeni kwa mwanga wa moto huo, miali ya moto mliowasha nyinyi wenyewe. Mtakachopata kutoka kwa Mwenyezi-Mungu ni hiki: Nyinyi mtalala chini na mateso makali.
 
60% incompetence....taifa lina uhaba wa watu serious, kazi kubwa inahitajika sana kushape jamii na kupata watu serious ambao kila mahala ukiwaweka wanakimbizana na perfomance..

Tukiambiwa ni sleeping giant, watu wavivu wavivu tunaodeal na mambo ya hovyo hovyo huwa tunakuwa wakali sana lakini huu ndio ukweli...
 
... ATCL wanazo ndege nyingi. Kama hiyo moja haikuwa na route kulikuwa na ubaya gani kumpeleka msimamizi wa usalama wa raia na mali zao mh. aijiipii ziarani hapo nchi jirani? Naona sawa tu mali za nchi hazikuwahi kuwa na mwenyewe; wanajitumbulia wenye nafasi zao.
Kwa hiyo ni sawa kuunguza mamilioni kupeleka ndege ya biashara Rwanda? Kwa nini asipande ndege ya biashara mpaka Kigoma halafu from there akatumia helicopter?
 
Seriakli ya mama samia imekuwa na matumizi ya kvyo ya Ndge na Rasilimali fedha na mda..Sasahivi kuonana na Balozi eti kila kitu lazima Dar Es Salaam na siyo Dodoma..kwanini?
 
Seriakli ya mama samia imekuwa na matumizi ya kvyo ya Ndge na Rasilimali fedha na mda..Sasahivi kuonana na Balozi eti kila kitu lazima Dar Es Salaam na siyo Dodoma..kwanini?
Dar ni makao makuu ya overtime, na per diem za wanono
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
60% incompetence....taifa lina uhaba wa watu serious, kazi kubwa inahitajika sana kushape jamii na kupata watu serious ambao kila mahala ukiwaweka wanakimbizana na perfomance..

Tukiambiwa ni sleeping giant, watu wavivu wavivu tunaodeal na mambo ya hovyo hovyo huwa tunakuwa wakali sana lakini huu ndio ukweli...
Watetezi wa udhaifu huu kwa kupewa kale kabahasha ka buku saba ni johnthebaptist, USSR, jingalao, Bia yetu and the like. Nashindwa kuzielewa akili zao, huwa zinafurahishwa nini na huu upurupuru wa matumizi mabaya ya fedha za umma?
 
Atc hawafanyi biashara bali wanatoa Huduma!
Chama Cha Mazezeta katika ubora wao.
Mbona Bei zenu ni za juu Sana kuliko Fastjet?

Mngekuwa mnatoa huduma Bei zenu zingekuwa zinamudiwa na wananchi wa chini.

Mtu wa kipato Cha chini ya USD 1 kwa siku anawezaje kulipa nauli ya USD 150 kwenda Mwanza?

Au wananchi fukara hawastahili huduma zenu?

Ndio maana tunasema wakulima na wafanyakazi wameporwa chama chao
 
Chama Cha Mazezeta katika ubora wao.
Mbona Bei zenu ni za juu Sana kuliko Fastjet?

Mngekuwa mnatoa huduma Bei zenu zingekuwa zinamudiwa na wananchi wa chini.

Mtu wa kipato Cha chini ya USD 1 kwa siku anawezaje kulipa nauli ya USD 150 kwenda Mwanza?

Au wananchi fukara hawastahili huduma zenu?

Ndio maana tunasema wakulima na wafanyakazi wameporwa chama chao
Ndio maana nyie Wachovu mmeanzishiwa Huduma ya Kibubu!
 
Back
Top Bottom