Kwa nchi zinazotegemea misaada hali inazidi kuwa ngumu, Elon Musk aanzisha mpango wa kuiua USAID

Kwa nchi zinazotegemea misaada hali inazidi kuwa ngumu, Elon Musk aanzisha mpango wa kuiua USAID

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
1000021623.jpg


Elon Musk ameanza kutekeleza mpango wa kuliua Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID). Amesema anaamini USAID ni "shirika la kihalifu" ambalo linapaswa "kufa."

Kupitia mtandao wa X Musk alisema “USAID ni shirika la uhalifu. Ni wakati wa kufa”

Hii ni baada ya taarifa iliyosema kuwa maafisa wakuu wa USAID walijaribu kuwazuia watu kutoka bodi mpya ya ushauri iliyo chini ya Elon Musk iitwayo "Idara ya Ufanisi wa Serikali," (DOGE) kupata taarifa zilizomo ndani ya mifumo ya taasisi hiyo.

NBC News iliripoti kuwa utawala wa Trump umelenga kufanya mabadiliko makubwa yatakayoiathiri USAID.

Shirika hilo hutoa misaada kwa nchi nyingi zilizoathiriwa na migogoro na kusaidia nchi zinazoendelea kwa njia mbalimbali.

Shirika hilo lina bajeti ya zaidi ya dola bilioni 50 na liliundwa mnamo 1961.

Muda mfupi baada ya kuchukua madaraka, Trump alitia saini amri ya kiutendaji ambayo ilisimamisha kwa muda ufadhili kwa USAID.

Kwa sasa tovuti za shirika hilo zimefutwa na hazipatikani mtandaoni.

Hivyo zile nchi zinazotegemea misaada zijiandae na mabadiliko haya ya kudumu.

1000021631.jpg
 
USAID kweli wahuni. Hela nyingi hurudi Marekani kihuni. Wana kampuni zao ambazo hupewa tenda kilazima. Kwa mfano ukipewa tenda na USAID ya ku-supply vifaa tiba itakulazimu hivyo vifaa ununulie Marekani kwenye makampuni waliyopendekeza. Hata tafiti zinazofadhiliwa na USAID zinakuwa na ukakasi sana. Pamoja na yote bado tunawahitaji.
 
Nadhani viongozi wa Africa wanifunze kutumia Vizuri wanachokikusanya kwenye Kodi,pia wizi, matumizi mabaya ya mali ya umma yamekithiri na ni kawaida,kuna hela nyingi zinapotelea kwenye matumbo ya watu
 
Kumbe Rais ana nguvu sana hata nchi zilizoendelea sio Tz tu. Imagine Trump kaingia anabadili vitu upside down.
Kila nchi Rais anamamlaka makubwa sana na anachokifanya Trump ni kulinda rasilimali zao zisitumike vibaya na ziwanufaishe wenyewe ni tofauti na hawa wetu huku chini jangwa la Sahara, wanajifanya wanapigania rasilimali lakini wanapigania vizazi vyao vipate mali
 
View attachment 3223211

Elon Musk ameanza kutekeleza mpango wa kuliua Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID). Amesema anaamini USAID ni "shirika la kihalifu" ambalo linapaswa "kufa."

Kupitia mtandao wa X Musk alisema “USAID ni shirika la uhalifu. Ni wakati wa kufa”

Hii ni baada ya taarifa iliyosema kuwa maafisa wakuu wa USAID walijaribu kuwazuia watu kutoka bodi mpya ya ushauri iliyo chini ya Elon Musk iitwayo "Idara ya Ufanisi wa Serikali," (DOGE) kupata taarifa zilizomo ndani ya mifumo ya taasisi hiyo.

NBC News iliripoti kuwa utawala wa Trump umelenga kufanya mabadiliko makubwa yatakayoiathiri USAID.

Shirika hilo hutoa misaada kwa nchi nyingi zilizoathiriwa na migogoro na kusaidia nchi zinazoendelea kwa njia mbalimbali.

Shirika hilo lina bajeti ya zaidi ya dola bilioni 50 na liliundwa mnamo 1961.

Muda mfupi baada ya kuchukua madaraka, Trump alitia saini amri ya kiutendaji ambayo ilisimamisha kwa muda ufadhili kwa USAID.

Kwa sasa tovuti za shirika hilo zimefutwa na hazipatikani mtandaoni.

Hivyo zile nchi zinazotegemea misaada zijiandae na mabadiliko haya ya kudumu.
Nchi nyingi za Afrika zilikuwa zinaisikiliza na kuivumilia USA kwa sababu ya misaada yake. Na ndiyo maana hata barozi wa US hapa kipindi alipomjibu rais indirect alitaja hadi kiasi ambacho Marekani ilikitoa moja kwa moja kama msaada hapa nchini kupitia shirika lake hilo.
Sasa kutakuwa hakuna sababu tena ya kuisikiliza. Yani kwa njia moja hilo shirika ilikuwa ni silaha ya kuongoza na kusambaza sera zake.
Any way hakuna wa kuilaumu Marekani ni kwamba wameamua pesa yao itumike kwa mambo yao.
Tunakoelekea mambo mengi yatabadilika. Kuna wimbi pia kubwa la Wajerumani wanaotaka kujitoa umoja wa ulaya.
Kuna mtikisiko mkubwa duniani ambapo economic and technological power inahama na kila mmoja anahaha
 
Imagine waajiriwa wa US AID barani Africa especially Tanzania ni msongo gani wa mawazo wanapitia hivi sasa.

Kuna watu walikuwa wanalipwa hadi milioni 20 Tshs per month na hilo shirika hapa hapa bongo, sasa sukari zinawapanda.

Mambo hayatabiriki kwa kweli.
 
Imagine waajiriwa wa US AID barani Africa especially Tanzania ni msongo gani wa mawazo wanapitia hivi sasa.

Kuna watu walikuwa wanalipwa hadi milioni 20 Tshs per month na hilo shirika hapa hapa bongo, sasa sukari zinawapanda.

Mambo hayatabiriki kwa kweli.
Hapa kwetu kuna baadhi ya staff walikuwa wanalipwa na US AID,tangu ijumaa wamepewa barua za kusitishiwa mkataba. Ni kilio aisee
 
Hapa kinachofuatia ni nchi za Africa na wao kuanza kuweka tuvijikwazo uchwara kwa US baada ya kunyimwa pesa 🤣 🤣

Lakini uwezo wa kutunishiana misuli na US hawana wataumia..
Uwezo hatuna ila sasa kwa sababu hawajali tena kuhusu US na yeye bila shaka hajali kuhusu Afrika tutashuhudia akina Museveni wengi maana sasa wanamwoga nani.
 
Back
Top Bottom