Uchaguzi 2020 Kwa NEC kumfungia mikutano ya kampeniTundu Lissu, ni sawasawa na kumpiga chura mateke, kwani ndiyo unazidi kumuongezea mwendo!

Uchaguzi 2020 Kwa NEC kumfungia mikutano ya kampeniTundu Lissu, ni sawasawa na kumpiga chura mateke, kwani ndiyo unazidi kumuongezea mwendo!

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Tulisikia taarifa ya Kamati ya Maadili ya Tume ya Taifa ya uchaguzi, katika kikao chake ilichoketi Jana, ikitoka na uamuzi wa kumfungia Tundu Lissu, kutofanya mikutano ya kampeni kwa wiki moja, kuanzia tarehe 3 hadi tarehe 9 ya mwezi huu wa 10

Wasidhani hiyo Kamati ya Maadili ya Tume ya uchaguzi itakuwa "imemkomoa" Tundu Lissu, badala yake ndiyo imezidi kumpa umaarufu mkubwa, ambao haumithiliki, katika uchaguzi mkuu unaotegemewa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.

Ni dhahiri sasa wananchi tutakuwa tumedhithibitisha pasipo shaka yoyote kuwa hii Tume ya uchaguzi iko "biased" na inafanya kazi kwa maagizo toka juu na inafanya upendeleo wa dhahiri kwa CCM!

Kwa kuwa kama alivyoeleza Tundu Lissu katika kikao chake na waandishi wa habari hapo jana kuwa yeye kama mgombea Urais kwa kupitia chama chake cha CHADEMA, wameshawaandikia barua 3 za malalamiko, kupeleka kwa Tume hiyo ya uchaguzi, dhidi ya vitendo vinavyokiuka Maadili ya uchaguzi, vikiwemo vitendo vya utoaji rushwa vya waziwazi katika kampeni za huyo mgombea wa CCM, John Magufuli, hata hivyo Tume hiyo, imepata "kigugumizi" na kutotaka kabisa angalau kueleza kuwa wamezipokea, barua hizo za malalamiko!

Ukiangalia historia ya mgombea huyu wa CHADEMA, amekuwa akionewa mno na vyombo vya dola vya hapa nchini.

Jaribu ku-imagine ni Tundu Lissu huyo huyo, ambaye zaidi ya miaka 3 hivi sasa, alishambuliwa kwa kimiminiwa risasi 16 mfululizo, katika jaribio la kutaka kumuua, ambapo lilimlazimu akimbizwe nje ya nchi, ambako amekuwa akipata matibabu kwa kipindi chote hiki.

Katika kipindi chote hicho cha miaka zaidi ya 3 Jeshi letu la Polisi, halijamkamata hata mtuhumiwa mmoja ili kumhoji kwa tukio hilo la kinyama kabisa!

Cha ajabu zaidi ni kitendo kilichofanywa na Spika wa Bunge, Job Ndugai cha kutompa stahiki zake za matibabu, ambapo ni kwa mujibu wa sheria, lakini kilichowasononesha zaidi watanzania, ni cha kumvua ubunge wake, kwa madai ya kuwa yeye Spika Ndugai, kwa madai yake kuwa Tundu Lissu ni mtoro na hajui alipo!

Kuna kawaida ya ubinadamu, ku-sympathize na binadamu mwenzako ambaye unaamini kabisa kuwa kuna mlolongo wa kumwonea kupita kiasi, ndiyo maana naona kwa vitendo anavyoendelea kufanyiwa mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu, vinaendelea kumpa nguvu na kuungwa mkono na Umma wa watanzania na naviona vitendo hivyo sawasawa na kumpiga chura mateke, kwani ndiyo umavyozidi kumuongezea mwendo!
 
Ukimpiga teke chura umemwongezea mwendo. Bado siku 24 Watanzania wapige kura. Kamati ya Maadili ya NEC imempiga teke Mhe. Lissu kwa kumfungia asifanye kampeni kwa siku 7. Kimsingi, Kamati imempigia kampeni bila kujijua.

Lissu anazidi kuwa maarufu kila kukicha. Magufuli, gari bovu, limerudi garage kwa siku 8 huku Lissu mpigwa risasi 16 yupo ngangari na anazuiwa asimpiku Magufuli Ila alisubiri gari la mkaa liwekewe vipuri vipya.

Lori lenyewe lilishakwenda kwa mekanika babu wa Loliondo na halikupona! Kamati imemwongezea mwendo Lissu kwa Watanzania kuwa kipenzi chao kina afya bora ya akili na mwili licha ya kupigwa risasi 16. Yule mwingine SIYO - AFYA mgogoro. Amsubiri kwanza apone ndio wote waendelee kumaliza kampeni pamoja.
 
Habari za Lissu zinatafutwa kwa bidii Sana na Watanzania,kwa mzuka mkubwa.

Wakati Habari za jiwe zinatangazwa kila mahala kwa gharama kubwa Sana,na watu Wala hawana mzuka nazo.
 
Kitu ambacho wanachokifanya hao kina Dkt Mahera, wa Tume ya uchaguzi, kwa kujua au kutojua ni kuwa wamemuongezea maradufu umaarufu wake Tundu Antipas Lissu!

Hebu fikiria pale atakapokuwa amemamaliza "kifungo" chake hapo tarehe 9, hiyo mikutano yake ya kampeni, haitakuwa tena na mafuriko ya wahudhuriaji, bali itakuwa na kimbunga cha wananchi watalaokuwa wanahudhuria!
 
yep...... scarcity creates even more demand, spontaneously upping Lissu's "electability value".

it's a rule of thumb!
 
Nashauri TL na kamati yake watumie muda huu wa kusimamishwa kwa kampeni zao kuandaa mikakati ya kupata mawakala wasomi, wenye nguvu, waaminifu,na wahakikishe kila kituo kinakuwa na mawakala zaidi ya mmoja kwa kutumia uwakilishi wa vyama rafiki hasa ACT wazalendo.

Kumbuka kivumbi, patashika nguo kuchanika, figisu, vitimbwi, mazingaombwe, vituko na kila aina ya mihemko, kura kupotea, mabox kunyakuliwa, mawakala kushambuliwa na kunyimwa nakala za matokeo, kunyimwa fomu za malalamiko, kukataa kusaini matokeo, kubadili matokeo kwa maana ya kura za A kumpa B na za B kumpa A, yote hayo muda wake ni kuanzia saa1 jioni ya tarehe 28/10/2020.

Uzoefu wangu unanionyesha kuwa hicho ndio kitakachokuwa kipindi kigumu na cha kutisha sana huenda kuliko nyakati nyingine zote katika historia ya uchaguzi wa nchi hii.

Ndio kipindi pekee cha kuhakikisha chungwa linabaki kuwa chungwa, au kwa nguvu ya ajabu, chungwa litabadilishwa kuwa limau.

Ndio kipindi cha kuamua hatima ya amani ya nchi hii.

MUNGU IBARIKI TANZANIA YANGU
 
NEC wamefanya lamaana sana, Lissu hufanya kusudi na ana kiburi sana

Wangelimwacha wala Lisu asingelijiongeza na kurudi kwenye mstari bali angeliendelea kufanya anayofanya
 
Na sentensi kama hizo, 'kwamba akishughulikiwa ndo atazidi kupaishwa nazo zimechangia kumpa bichwa Lisu', hivyo kuzidi kuuendelea kufanya vituko akiaamini hatoguswa
 
Ondoa ujinga na upuuzi wako hapo. Nyie endeleeni kumpa kichwa azidi kukiuka taratibu.Huyo chura wenu anaweza kupigwa teke akapotelea maporini.Mama,kumbuka hii ni nchi.Jidanganyeni lakini mwisho wenu ni majuto.
 
Ukimpiga teke chura umemwongezea mwendo. Bado siku 24 Watanzania wapige kura. Kamati ya Maadili ya NEC imempiga teke Mhe. Lissu kwa kumfungia asifanye kampeni kwa siku 7. Kimsingi, Kamati imempigia kampeni bila kujijua.

Lissu anazidi kuwa maarufu kila kukicha. Magufuli, gari bovu, limerudi garage kwa siku 8 huku Lissu mpigwa risasi 16 yupo ngangari na anazuiwa asimpiku Magufuli Ila alisubiri gari la mkaa liwekewe vipuri vipya.

Lori lenyewe lilishakwenda kwa mekanika babu wa Loliondo na halikupona! Kamati imemwongezea mwendo Lissu kwa Watanzania kuwa kipenzi chao kina afya bora ya akili na mwili licha ya kupigwa risasi 16. Yule mwingine SIYO - AFYA mgogoro. Amsubiri kwanza apone ndio wote waendelee kumaliza kampeni pamoja.
transport-car-transport-vehicle-pickup-breakdown-gra050212_low.jpg
 
Nashauri TL na kamati yake watumie muda huu wa kusimamishwa kwa kampeni zao kuandaa mikakati ya kupata mawakala wasomi, wenye nguvu, waaminifu,na wahakikishe kila kituo kinakuwa na mawakala zaidi ya mmoja kwa kutumia uwakilishi wa vyama rafiki hasa ACT wazalendo...
Umenena vyema.Chadema wawe na plan nyingi kadiri inachowezekana!
 
Nashauri TL na kamati yake watumie muda huu wa kusimamishwa kwa kampeni zao kuandaa mikakati ya kupata mawakala wasomi, wenye nguvu, waaminifu,na wahakikishe kila kituo kinakuwa na mawakala zaidi ya mmoja kwa kutumia uwakilishi wa vyama rafiki hasa ACT wazalendo...
Barikiwa sana
 
Nashauri TL na kamati yake watumie muda huu wa kusimamishwa kwa kampeni zao kuandaa mikakati ya kupata mawakala wasomi, wenye nguvu, waaminifu,na wahakikishe kila kituo kinakuwa na mawakala zaidi ya mmoja kwa kutumia uwakilishi wa vyama rafiki hasa ACT wazalendo...
Papa 1
Umenena vyema sana Mkuu, naamini ushauri wako utafanyiwa kazi na uongozi wa juu wa Chama cha CHADEMA.

Mungu akubariki kwa ushauri huu murua
 

BAK
Hiyo mishale anayolengwa nayo Tundu Lissu, kutoka kila aina ya kona.....................

Hakika hiyo mishale, imeshindikana kummaliza huyu Tundu Lissu.................

Kama alivyookolewa na zile "mvua" za risasi ili asife, Mungu bado anawaonyesha hao watesi wake kuwa muujiza wake bado unaendelea kufanya kazi, kwani hata hii "combination" inayofanywa na hivyo vyombo vya dola ulivyovitaja, navyo vitashindwa na hatimaye Tundu Lissu, kama alivyotabiriwa na mtumishi wa Mungu Mwingira, atatangazwa kuwa Mshindi kwa kumtoa kwa "knockout" huyu mbabe Jiwe, ambaye kila mwananchi aliamini kuwa ameshindikana!
 
Ukimpiga teke chura umemwongezea mwendo. Bado siku 24 Watanzania wapige kura. Kamati ya Maadili ya NEC imempiga teke Mhe. Lissu kwa kumfungia asifanye kampeni kwa siku 7. Kimsingi, Kamati imempigia kampeni bila kujijua...
Hawa wajinga wa NEC wanajaribu kucheza na nguvu za MUNGU,watashangaa hizo siku 8 za magufuli kujiuguza ndiyo Hali ya Afya yake inazidi kuwa mbaya sasa sijui watafanyaje!!
MUNGU huwa njia zake hazichunguziki
 
Back
Top Bottom