Kwa nini mabeki tatu wakifika mjini wanaota mapembe!

Anataka kurudi huyo[emoji3]
 
Anataka kurudi huyo[emoji3]
Simrudishi ng'oooooo

Nilishaamua nitabadilisha wasichana hata elfu moja ila stress sitaki


Nikapata mwingine mwanga mpaka anafanya mambo ya ajabu mchana wa jua kali.......nilipomrudisha alilia akaomba asiondoke kwao watamuua maana watajua ametoa siri.... nikamwambia bibi bye bye....na sayansi yako ya kiafrika katafute pa kuifanyia....

Na kesho kuna mmoja namrudisha.....alfajiiiiri na mapema
 
Teh teh pole !
 
Hawa beki tatu wazee wafamilia ndio wanawapa vichwa kwa sababu ya kuwatafuna
 
Muonee huruma bwana
Siwezi mkuu kafanya kituko cha kufungia mwaka, juzi wife kafanya usafi nyumba nzima, chumbani kwa watoto uvunguni kitandani, kakutana na maped yaliokaukiana damu kama kumi hivi, tena chumbani kwa watoto ana maana gani mpaka namhisi vibaya mkuu.
 
Sasa mie huyu wa kwangu tangu aondoke mtaani waendesha bodaboda, wananiambia umetutoroshea mke wetu.
 
Mie mwenyewe huyo niliemrudisha mwanza, usiku anaongea peke yake, muda mwingine usiku anatembea ukumbini mida ya saa saba au saa nane za usiku....huku anaongea na kuongea vitu visivyojulikana, siku moja mlango wa ndani kwangu nilikuwa nimeurudishia akaja ndani usiku karibu na kichwani kwangu nastukia anaongea vitu vya ajabu ajabu, nikamtoa nduki, asubuhi namuiliza anasema ajui lolote mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…