Kwa nini shule zinafungwa na kufunguliwa siku moja kwa nchi nzima?

Kwa nini shule zinafungwa na kufunguliwa siku moja kwa nchi nzima?

DENAMWE

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2019
Posts
862
Reaction score
871
Shule zetu zinafungwa na kufunguliwa siku moja nchi nzima. Inawezekana wazo hili lina nia njema na manufaa.

Hata hivyo, naona utaratibu huu una changamoto ambazo zina athari kubwa mno kwa wanafunzi na wazazi.

Baadhi yake ni changamoto ya usafiri, malazi na chakula safarini. Vyombo vya usafiri vinashindwa kumudu kubeba abiria wote kutokana na wingi wao unaotokana na ongezeko la abiria wanafunzi. Tatizo hili ni kwenye mabasi, pikipiki, bajaji, meli na gari la moshi (treni).

Sijui hali ikoje huko angani. Fikiria shule za Mwanza na Mara zenye wanafunzi wanaokwenda Kagera kwa kutumia Meli. Itawamudu? Fikiria wanafunzi wanaotoka Dar kwenda Bara. Mabasi na treni vinawamudu?

Wingi huo unalemea pia hoteli na migahawa wanakohitaji chakula. Pia ndivyo inavyokuwa kwenye nyumba za kulala wageni.

Natamani kufahamu manufaa makubwa yanayopatikana kwa kufunga na kufungua shule siku moja kwa nchi nzima.

Vile vile, kuna faida gani kuwa na sare moja nchi nzima?
 
Nakumbuka 2015 kurudi nyuma english medium primary walikuwa wanafunga mwezi wa 4, wa 8 na wa 12 tofauti na kayumba waliokuwa wanafunga mwezi wa 6 na wa 12

Ni kwamba kipindi hicho hakukuwa na hii kero?

Sasa mbona maghufuli aliutoa huo mfumo?
 
Nakumbuka 2015 kurudi nyuma english medium primary walikuwa wanafunga mwezi wa 4, wa 8 na wa 12 tofauti na kayumba waliokuwa wanafunga mwezi wa 6 na wa 12

Ni kwamba kipindi hicho hakukuwa na hii kero?

Sasa mbona maghufuli aliutoa huo mfumo?
Huu mfumo ni mzuri sana mkuu, angalau kunakuwa na uniformity kidogo. Mengine tunajifunza taratibu.
 
Kwani Kuna case za wanafunzi kushindwa kurudi shule kwasababu ya usafiri? Mambo mengine si ya kuumizia kichwa kabisa.
 
Shule zetu zinafungwa na kufunguliwa siku moja nchi nzima. Inawezekana wazo hili lina nia njema na manufaa.

Hata hivyo, naona utaratibu huu una changamoto ambazo zina athari kubwa mno kwa wanafunzi na wazazi.

Baadhi yake ni changamoto ya usafiri, malazi na chakula safarini. Vyombo vya usafiri vinashindwa kumudu kubeba abiria wote kutokana na wingi wao unaotokana na ongezeko la abiria wanafunzi. Tatizo hili ni kwenye mabasi, pikipiki, bajaji, meli na gari la moshi (treni).

Sijui hali ikoje huko angani. Fikiria shule za Mwanza na Mara zenye wanafunzi wanaokwenda Kagera kwa kutumia Meli. Itawamudu? Fikiria wanafunzi wanaotoka Dar kwenda Bara. Mabasi na treni vinawamudu?

Wingi huo unalemea pia hoteli na migahawa wanakohitaji chakula. Pia ndivyo inavyokuwa kwenye nyumba za kulala wageni.

Natamani kufahamu manufaa makubwa yanayopatikana kwa kufunga na kufungua shule siku moja kwa nchi nzima.

Vile vile, kuna faida gani kuwa na sare moja nchi nzima?
Amri toka serikalini
 
Tupo kwenye formal and a single state country
 
Shule ziko chini ya mamlaka husika mfano wizara ya elimu. Mpangilio wote wa kufunga na kufungua unatolewa na wizara husika
 
Back
Top Bottom