Kwa Nini Shule Zote za Msingi za Serikali Zisibadilishwe na kuwa English Medium?

Kwa Nini Shule Zote za Msingi za Serikali Zisibadilishwe na kuwa English Medium?

Kichwa cha habari hapo juu chajieleza!

Nimefanya utafiti usio rasmi, kwa sasa asilimia kubwa ya wazazi (karibu wote) wanatamani, au wanataka watoto wao wakasome shule za English Medium.

Asilimia kubwa (karibu wote) wazazi wenye kipato wamepeleka watoto wao English Medium. Sijajua kama kuna mtoto hata mmoja wa mtunga sera za elimu anasoma shule za msingi za serikali.

Ukikutana na mzazj hohehahe anayesomesha shule za msingi za serikali anatamani mtoto wake na yeye angekuwa anasoma English Medium, akipata hela lazima atampeleka huko!

Kinachowavutia zaidi wanajamii ni pale wanapokutana na mtoto wa English Medium akiongea Kingereza.

Sasa, kwa nini shule za msingi zote za serikali zisianze kufundisha kwa mtaala wa Kingereza? Kwa sababu naona wazazi hawazielewi kabisa shule za msingi za serikali zinazofundisha kwa Kiswahili.

Sidhani hata watoto wa wafanyakazi wa BAKITA (Baraza la Kiswahili Tanzania) wanasoma shule za msingi za serikali.
Mwaka ujao January Morogoro wanaanza
IMG-20201229-WA0014.jpeg
 
Wazo lako linaweza kuwa la msingi sana lakini nasikitika kukwambia kuwa hilo lingewezekana enzi za jakaya aliyekuwa anatambua umuhimu wa elimu. Huyu wa sasa elimu sio kipaumbele chake yeye mwambie habari za mandege, mabarabara, flyover na madaraja ndivyo vipaumbele vyake. Kuhusu kuboresha elimu hiyo ni juu yako mzazi na mwanao...
Kwahiyo, Tanzania hakuna vyama vya siasa(vyama vina:sera, mpango mkakati shirikishi), Tanzania hakuna sera za kisekta, hakuna mipango mkakati ya kisekta shirikishi(hii hutoa dira ya kisekta). Bali kuna "ONE MAN ARMY"⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️

LITERARLY unataka kutuambia kuwa viongozi woooooote (isipokuwa huyo mmoja) wao wamelala na huyo mmoja ndiye hutekeleza vipaumbele vyake⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️⁉️
 
Kiingereza kitaharakishaje kuleta maendeleo. Mbona malawi wanasoma kiingereza ili ni maskini wa mwisho.
Kenya tunaongea several english languages; luo wanachao, taita wanachao, kalenjini chakwao: name them
 
Kichwa cha habari hapo juu chajieleza!

Nimefanya utafiti usio rasmi, kwa sasa asilimia kubwa ya wazazi (karibu wote) wanatamani, au wanataka watoto wao wakasome shule za English Medium.

Asilimia kubwa (karibu wote) wazazi wenye kipato wamepeleka watoto wao English Medium. Sijajua kama kuna mtoto hata mmoja wa mtunga sera za elimu anasoma shule za msingi za serikali.

Ukikutana na mzazj hohehahe anayesomesha shule za msingi za serikali anatamani mtoto wake na yeye angekuwa anasoma English Medium, akipata hela lazima atampeleka huko!

Kinachowavutia zaidi wanajamii ni pale wanapokutana na mtoto wa English Medium akiongea Kingereza.

Sasa, kwa nini shule za msingi zote za serikali zisianze kufundisha kwa mtaala wa Kingereza? Kwa sababu naona wazazi hawazielewi kabisa shule za msingi za serikali zinazofundisha kwa Kiswahili.

Sidhani hata watoto wa wafanyakazi wa BAKITA (Baraza la Kiswahili Tanzania) wanasoma shule za msingi za serikali.
Hivi unazijua shule za msingi za serikali kweli?
Ukizibadilisha, nani atafundisha hicho kiingereza?
Yaani walimu wengi huko, kiingereza hakipandi kabisa, wanakiogopa au kukichukua vibaya.
 
Wakubwa hawataki nchi itembee mwendo wa haraka katika kuleta maendeleo ya mtu wa kawaida.
Kubadili jambo hili inawezekana,yaani hii siri wanabaki nayo wenyewe.
Kama unataka kujua ,wanyonge wanaingizwa chaka,ni kiongozi gani ambaye mtoto wake hasomi shule za "english medium",jibu ni hakuna.
Na ndio maana shule za kawaida hakuna anayeleta ufumbuzi endelevu wa kutatua tatizo la upungufu wa madarasa na madawati, wanaishia kutoa matamko kila mwaka:"ole wake ambaye shule yake watoto watakaa chini","watumishi hakuna kwenda likizo mpaka tatizo la upungufu wa madawati na madarasa liishe"
"Utafikiri,tatizo la upungufu madawati na madarasa ni dharura,wakati kuna taasisi za takwimu,kuna makadirio ya ongezeko la vizazi na vifo kila mwaka!
Zambia ,Malawi,Uganda Zimbabwe hao wote wanaongea kizungu Ila kiuchumi wanachechemea kiingereza siyo sababu inauowafanya Watu waendelee Acha Utoto .Hao Wataalamu wote wa vyuo vikuu wanaotufundisha lugha ya kizungu na kuandika vitabu vya kizungu walisoma kiswahili kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba na kiingereza wakakikuta huko sekondari.Kumbuka kuwa Sasa tunalazimisha kuwapeleka watoto kwenye sekondari mpaka waliopata 20/100 % wakati wakati ule aliyepata 50/100% ndiyo tutamuhesabu amefaulu kwa maana hiyo mtoto. Anayekwenda sekondari na kwa kupata 20/100% hafundishiki kizungu maana uwezo wake Mdogo wa kuelewa isipokuwa ataweza kizungu endapo tu somo atakalofundishwa huko ni kizungu peke yake. Kujua kiingereza hakuna Mahusiano na Maendeleo kanuni ya Maendeleo Ni ileile tu kujilimbikizia Mali iwe kwa njia halali au haramu Ila tutamuhesabu kuwa ni Tajiri.
 
Kichwa cha habari hapo juu chajieleza!

Nimefanya utafiti usio rasmi, kwa sasa asilimia kubwa ya wazazi (karibu wote) wanatamani, au wanataka watoto wao wakasome shule za English Medium.

Asilimia kubwa (karibu wote) wazazi wenye kipato wamepeleka watoto wao English Medium. Sijajua kama kuna mtoto hata mmoja wa mtunga sera za elimu anasoma shule za msingi za serikali.

Ukikutana na mzazj hohehahe anayesomesha shule za msingi za serikali anatamani mtoto wake na yeye angekuwa anasoma English Medium, akipata hela lazima atampeleka huko!

Kinachowavutia zaidi wanajamii ni pale wanapokutana na mtoto wa English Medium akiongea Kingereza.

Sasa, kwa nini shule za msingi zote za serikali zisianze kufundisha kwa mtaala wa Kingereza? Kwa sababu naona wazazi hawazielewi kabisa shule za msingi za serikali zinazofundisha kwa Kiswahili.

Sidhani hata watoto wa wafanyakazi wa BAKITA (Baraza la Kiswahili Tanzania) wanasoma shule za msingi za serikali.

Unaugomvi na walimu eeeh
 
Ni wazo zuri, tatizo linakuja pale hao waalimu wenyewe wa hizo shule za serikali wengi wao kingereza ni sifuri...

Hizi English Medium, wanaajiri walimu ambao wengi wao ni Fluent in English sababu za ushindani wa ki - biashara...

Wengine huenda mbali hadi kuajiri wazungu...



Cc: mahondaw
Point ya muhimu ni hapo juu,
"tatizo linakuja pale hao waalimu wenyewe wa hizo shule za serikali wengi wao kingereza ni sifuri..."
 
Kama hivyo basi sasa hivi tungekuwa kama USA sababu hata sasa hivi wanaojua hicho kiingereza ni asilimia chache.

Maendeleo ya kitaifa huanzia kwa mtu mmojammoja.

Swali wewe unaweza kuandika,kusoma na kuongea kiingereza?

So ! what more if y'u know what y'u say? even redc'pe in where I'm kn'w it.
 
Tatizo kubwa naloliona kwenye shule za serikali wanafunzi wanalundikwa wengi kwa darasa moja hivyo ndo sababu wengi wanashindwa kuelewa walimu wanachofundishwa
 
Mie naona hapo neno medium ndilo linaleta tabu , Basi shule za serikali ziitwe SWAHILI MEDIUM
 
English Medium Zipigwe Marufuku..
Ukweli Zimeongeza Watu wenye uwezo wa kuongea kiingereza basic.. na uwezo mdogo wa uelewa..

Ukilinganisha na Watu waliosoma Mtaala wa Kiswahili na Kusoma Lugha ya Kiingereza kama somo.. wanauwezo mkubwa ku kujenga hoja na uelewa wa jumla.

Haya Ma english medium kama hauna ufuatiliaji wa karibu watoto wanakuja wamekariri maupupu meengi kwa kizungu na uelewa kisoda.. futa tuu.
 
Back
Top Bottom