Kwa nini tukikutana na mwanaume ana jina la kike unakuwa mjadala wa kitaifa?

Kwa nini tukikutana na mwanaume ana jina la kike unakuwa mjadala wa kitaifa?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Mtanisamehe kwa makala ndefu ila hili inabidi leo tuliongelee.

Mimi ni mmoja wa watu ambao kuna kipindi nilikuwa nashangaa nikikuta mwanaume ana jina la kike. Kyrie, Shannon, Courtney, Lindsay, Klay yote ni majina yalikuwa yananishangaza kukuta amepewa mwanaume. Nikaja kukutana na Joyce ndiyo nikashtuka kabisa.

Baada ya kuelewa kuwa kwanza kuna issue ya tofauti za tamaduni, hauwezi ukalazimisha mambo kwa wengine kisa kwako haujayazoea kuyaona. Pili nadhani ni trend ya uwepo wa single mothers ambao wamejipa au wamelazimika kuwapa majina watoto wao, jukumu ambalo kihistoria lilibebwa na mwanaume. Sidhani kama kuna mwanaume atamuita mtoto wake wa kiume jina ambalo kimazoea ni la kike.

Alipotambulishwa mchezaji wa Simba anayeitwa Debora Fernandez Mavambo, maneno na kejeli yamekuwa mengi sana. Juzi nilikuwa naangalia mpira banda umiza, nikasikia watu wanasema wao ni wanaume wanacheza na mademu, mwingine anasema Debora ana mimba (sijawahi kuelewa kejeli za mimba, njia ambayo wote tumetokea ila hilo tuliache kwanza). Huwa najiuliza hawa wanaotania si walikuwa na Joyce Lomalisa (siyo jina moja la kike, bali mawili) kwa misimu kadhaa, mbona wanakuwa wasahaulifu?

Kuna kipindi Mzamiru alibadili jina katika jezi yake akaweka jina la Mama yake. Bernard Morrison naye alibadili jina katika jezi yake akaweka la Bibi yake. Mbona watu waliheshimu maamuzi yao na sikumbuki kuona wanakejeliwa?

Nimalizie kwa kuuliza, hivi kuitwa jina la kike kunampunguzia nini mwanaume kuwa mwanaume kamili? Baadhi ya hawa wanaume wenye majina ya kike wana nguvu ikiwemo za kiume kukushinda wewe, sasa unajisifu nini? Wewe unaweza kupambana uwanjani na kina Pacome, Aziz Ki na Aucho kwa lisaa lizima?

Kuna jambo nilijifunza kuhusu majina. Haijalishi una jina gani, suala ni umefanikiwa katika nini katika haya maisha? Kuna mkuu mmoja ni daktari bingwa, angekuwa mtu wa kawaida angepata tabu sana na jina lake. Kina Arnord Schwarzenegger, watu hawapati shida kutamka wala kuandika majina yao kwa sababu wamefanya kitu hapa duniani. Wewe mwenye jina perfect una nini cha kujivunia? Nani anakujua?

Nahisi kuna kaushamba fulani inabidi tukaache.
 
Hapo kwenye kukejeli mimba na ndipo tulipotokea panatia simanzi sana

Mm linalonishangaza ni kukuta mwanaume anakejeli mimba na mama yake aliibeba.
Huwa inanishangaza sana. Huwa najisemea kimoyomoyo labda kuna elimu ya mtaa ambayo sikuipata hadi nashindwa kuona mimba ni kitu cha kukejeli na kumdhihaki mtu.
 
Huwa inanishangaza sana. Huwa najisemea kimoyomoyo labda kuna elimu ya mtaa ambayo sikuipata hadi nashindwa kuona mimba ni kitu cha kukejeli na kumdhihaki mtu.
Hakuna cha elimu ni mibange tu ikishavutwa ikajaa kichwani.
 
mkuki kwa nguruwe eh, joyce mlimuanzishia mpaka thread hapa, mkasema haitwi lomalisa bali anaitwa joyce lomalisa mutambala, nami nasema haitwi debora anaitwa debrah.
 
Haina tatizo na kwanzia leo nakubatiza jina unaitwa Khadija
 
Mtanisamehe kwa makala ndefu ila hili inabidi leo tuliongelee.

Mimi ni mmoja wa watu ambao kuna kipindi nilikuwa nashangaa nikikuta mwanaume ana jina la kike. Kyrie, Shannon, Courtney, Lindsay, Klay yote ni majina yalikuwa yananishangaza kukuta amepewa mwanaume. Nikaja kukutana na Joyce ndiyo nikashtuka kabisa.

Baada ya kuelewa kuwa kwanza kuna issue ya tofauti za tamaduni, hauwezi ukalazimisha mambo kwa wengine kisa kwako haujayazoea kuyaona. Pili nadhani ni trend ya uwepo wa single mothers ambao wamejipa au wamelazimika kuwapa majina watoto wao, jukumu ambalo kihistoria lilibebwa na mwanaume. Sidhani kama kuna mwanaume atamuita mtoto wake wa kiume jina ambalo kimazoea ni la kike.

Alipotambulishwa mchezaji wa Simba anayeitwa Debora Fernandez Mavambo, maneno na kejeli yamekuwa mengi sana. Juzi nilikuwa naangalia mpira banda umiza, nikasikia watu wanasema wao ni wanaume wanacheza na mademu, mwingine anasema Debora ana mimba (sijawahi kuelewa kejeli za mimba, njia ambayo wote tumetokea ila hilo tuliache kwanza). Huwa najiuliza hawa wanaotania si walikuwa na Joyce Lomalisa (siyo jina moja la kike, bali mawili) kwa misimu kadhaa, mbona wanakuwa wasahaulifu?

Kuna kipindi Mzamiru alibadili jina katika jezi yake akaweka jina la Mama yake. Bernard Morrison naye alibadili jina katika jezi yake akaweka la Bibi yake. Mbona watu waliheshimu maamuzi yao na sikumbuki kuona wanakejeliwa?

Nimalizie kwa kuuliza, hivi kuitwa jina la kike kunampunguzia nini mwanaume kuwa mwanaume kamili? Baadhi ya hawa wanaume wenye majina ya kike wana nguvu ikiwemo za kiume kukushinda wewe, sasa unajisifu nini? Wewe unaweza kupambana uwanjani na kina Pacome, Aziz Ki na Aucho kwa lisaa lizima?

Kuna jambo nilijifunza kuhusu majina. Haijalishi una jina gani, suala ni umefanikiwa katika nini katika haya maisha? Kuna mkuu mmoja ni daktari bingwa, angekuwa mtu wa kawaida angepata tabu sana na jina lake. Kina Arnord Schwarzenegger, watu hawapati shida kutamka wala kuandika majina yao kwa sababu wamefanya kitu hapa duniani. Wewe mwenye jina perfect una nini cha kujivunia? Nani anakujua?

Nahisi kuna kaushamba fulani inabidi tukaache.
Huko duniani nimefanya kazi na mwanamama anaitwa Johnson
 
Kushangaa mwanaume kupewa jina la kike sio ajabu ni kawaida hata Ulaya ipo.

Wakati mchezaji Beckam yuko Real Madrid Spain alipata mtoto wa kiume akampa jina Cruz ambalo kwa waispaniola waliona ni jina wanalopewa zaidi watoto wa kike kuliko wa kiume licha ya kuwa jina linaloweza tumika na pande zote za jinsia kama ilivyo jina Zawadi, Furaha, Gift, Tunu, Nuru na mengine mengi na walimshangaa kwa nini ampe hilo jina mtoto wake.
 
Mbn ata kule oman yule mfalme wao anaitwa Haitham na ni jina la kike kbs ila mambo yanaenda freshi t
 
Mbn ata kule oman yule mfalme wao anaitwa Haitham na ni jina la kike kbs ila mambo yanaenda freshi t
20240811_061045.jpg


Yapo majina ya kiume tu na yapo majina ya kike tu.

Yapo majina ambayo anaweza pewa mtoto wa kiume na likatumika kwa mtoto wa kike pia.

Muhimu ni maana ya jina husika.
 
Mtanisamehe kwa makala ndefu ila hili inabidi leo tuliongelee.

Mimi ni mmoja wa watu ambao kuna kipindi nilikuwa nashangaa nikikuta mwanaume ana jina la kike. Kyrie, Shannon, Courtney, Lindsay, Klay yote ni majina yalikuwa yananishangaza kukuta amepewa mwanaume. Nikaja kukutana na Joyce ndiyo nikashtuka kabisa.

Baada ya kuelewa kuwa kwanza kuna issue ya tofauti za tamaduni, hauwezi ukalazimisha mambo kwa wengine kisa kwako haujayazoea kuyaona. Pili nadhani ni trend ya uwepo wa single mothers ambao wamejipa au wamelazimika kuwapa majina watoto wao, jukumu ambalo kihistoria lilibebwa na mwanaume. Sidhani kama kuna mwanaume atamuita mtoto wake wa kiume jina ambalo kimazoea ni la kike.

Alipotambulishwa mchezaji wa Simba anayeitwa Debora Fernandez Mavambo, maneno na kejeli yamekuwa mengi sana. Juzi nilikuwa naangalia mpira banda umiza, nikasikia watu wanasema wao ni wanaume wanacheza na mademu, mwingine anasema Debora ana mimba (sijawahi kuelewa kejeli za mimba, njia ambayo wote tumetokea ila hilo tuliache kwanza). Huwa najiuliza hawa wanaotania si walikuwa na Joyce Lomalisa (siyo jina moja la kike, bali mawili) kwa misimu kadhaa, mbona wanakuwa wasahaulifu?

Kuna kipindi Mzamiru alibadili jina katika jezi yake akaweka jina la Mama yake. Bernard Morrison naye alibadili jina katika jezi yake akaweka la Bibi yake. Mbona watu waliheshimu maamuzi yao na sikumbuki kuona wanakejeliwa?

Nimalizie kwa kuuliza, hivi kuitwa jina la kike kunampunguzia nini mwanaume kuwa mwanaume kamili? Baadhi ya hawa wanaume wenye majina ya kike wana nguvu ikiwemo za kiume kukushinda wewe, sasa unajisifu nini? Wewe unaweza kupambana uwanjani na kina Pacome, Aziz Ki na Aucho kwa lisaa lizima?

Kuna jambo nilijifunza kuhusu majina. Haijalishi una jina gani, suala ni umefanikiwa katika nini katika haya maisha? Kuna mkuu mmoja ni daktari bingwa, angekuwa mtu wa kawaida angepata tabu sana na jina lake. Kina Arnord Schwarzenegger, watu hawapati shida kutamka wala kuandika majina yao kwa sababu wamefanya kitu hapa duniani. Wewe mwenye jina perfect una nini cha kujivunia? Nani anakujua?

Nahisi kuna kaushamba fulani inabidi tukaache.
huu ni ujinga kwani tunatifauti kubwa ya kiutamaduni
 
Back
Top Bottom