Kwa nini watu wananawa mikono kabla ya kula?

Kwa nini watu wananawa mikono kabla ya kula?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Kwa wengine inawezekana ni mazoea tu. Lakini kwa upande wangu mimi, ni kwa sababu za kiusafi.

Leo, nikiwa mji fulani, niliingia kwenye mghahawa mmoja ambao kwa mji huo, ni miongoni mwa mighahawa ya hadhi, kwa ajili ya mlo wa Mchana. Mwonekano wake, huduma, bei na wateja wake inaakisi nilichosema. Ni mghahawa wa hadhi kubwa.

Nikiwa mghahawani hapo, aliingia dada mmoja kupata huduma. Aliagiza ugali na samaki, nafikiri, samaki choma.

Nilijikuta namfuatilia tokea aliponawa mpaka alipoanza kula.

Kilichonifanya nimfuatilie ni baada ya kumwona, alipomaliza kunawa mikono, aliendelea kushika vitu vingine visivyohusiana na chakula kwa kutumia mkono wake wa kulia.

Kwanza, alishika kiti chake na kukiweka vizuri kwa kutumia mikono yote miwili.

Pili, alichukua mkoba wake kwa kutumia mkono wa kulia na kufanya alichokusudia.

Tatu, aliendelea kutumia simu yake ya mkononi, nafikiri kwa kuchati, kwa kutumia mkono wa kulia.

Na ugali "wake" ulipowasili, aliendelea kula bila kunawa kwa mara nyingine.

Labda wajuvi wa masuala ya afya wanikosoe! Ni sahihi alivyofanya?

Mimi, kwa mtazamo wangu, alipaswa kutokushika tena simu, mkoba, viti, n.k. kwa kutumia mkono wa kulia kabla ya kumaliza kula kwa sababu huenda vitu hivyo vikawa na "vibakteria" hivyo kuwa hatarini kuambukizwa.

Nipo sahihi?

Nini lengo la watu kunawa kabla ya kula? Ni mazoea tu au sababu za kiafya?
 
Kwa wengine inawezekana ni mazoea tu. Lakini kwa upande wangu mimi, ni kwa sababu za kiusafi.

Leo, nikiwa mji fulani, niliingia kwenye mghahawa mmoja ambao kwa mji huo, ni miongoni mwa mighahawa ya hadhi, kwa ajili ya mlo wa Mchana. Mwonekano wake, huduma, bei na wateja wake inaakisi nilichosema. Ni mghahawa wa hadhi kubwa.

Nikiwa mghahawani hapo, aliingia dada mmoja kupata huduma. Aliagiza ugali na samaki, nafikiri, samaki choma.

Nilijikuta namfuatilia tokea aliponawa mpaka alipoanza kula.

Kilichonifanya nimfuatilie ni baada ya kumwona, alipomaliza kunawa mikono, akiendelea kushika vitu vingine visivyohusiana na chakula kwa kutumia mkono wake wa kulia.

Kwanza, alishika kiti chake na kukiweka vizuri kwa kutumia mikono yote miwili.

Pili, alichukua mkoba wake kwa kutumia mkono wa kulia na kufanya alichokusudia.

Tatu, aliendelea kutumia simu yake ya mkononi, nafikiri kwa kuchati, kwa kutumia mkono wa kulia.

Na ugali "wake" ulipowasili, aliendelea kula bila kunawa kwa mara nyingine.

Labda wajuvi wa masuala ya afya wanikosoe! Ni sahihi alivyofanya?

Mimi, kwa mtazamo wangu, alipaswa kutokushika tena simu, mkoba, viti, n.k. kwa kutumia mkono wa kulia kabla ya kumaliza kula kwa sababu huenda vitu hivyo vikawa na "vibakteria" hivyo kuwa hatarini kuambukizwa.

Nipo sahihi?

Nini lengo la watu kunawa kabla ya kula? Ni mazoea tu au sababu za kiafya?
sio uhenda hapo alinawa tena akajichafua, Simu za baadhi ya watu ni chafu kuliko sinki la choo, ukiswab ukapima iyo load ni kwere
 
Kwa wengine inawezekana ni mazoea tu. Lakini kwa upande wangu mimi, ni kwa sababu za kiusafi.

Leo, nikiwa mji fulani, niliingia kwenye mghahawa mmoja ambao kwa mji huo, ni miongoni mwa mighahawa ya hadhi, kwa ajili ya mlo wa Mchana. Mwonekano wake, huduma, bei na wateja wake inaakisi nilichosema. Ni mghahawa wa hadhi kubwa.

Nikiwa mghahawani hapo, aliingia dada mmoja kupata huduma. Aliagiza ugali na samaki, nafikiri, samaki choma.

Nilijikuta namfuatilia tokea aliponawa mpaka alipoanza kula.

Kilichonifanya nimfuatilie ni baada ya kumwona, alipomaliza kunawa mikono, aliendelea kushika vitu vingine visivyohusiana na chakula kwa kutumia mkono wake wa kulia.

Kwanza, alishika kiti chake na kukiweka vizuri kwa kutumia mikono yote miwili.

Pili, alichukua mkoba wake kwa kutumia mkono wa kulia na kufanya alichokusudia.

Tatu, aliendelea kutumia simu yake ya mkononi, nafikiri kwa kuchati, kwa kutumia mkono wa kulia.

Na ugali "wake" ulipowasili, aliendelea kula bila kunawa kwa mara nyingine.

Labda wajuvi wa masuala ya afya wanikosoe! Ni sahihi alivyofanya?

Mimi, kwa mtazamo wangu, alipaswa kutokushika tena simu, mkoba, viti, n.k. kwa kutumia mkono wa kulia kabla ya kumaliza kula kwa sababu huenda vitu hivyo vikawa na "vibakteria" hivyo kuwa hatarini kuambukizwa.

Nipo sahihi?

Nini lengo la watu kunawa kabla ya kula? Ni mazoea tu au sababu za kiafya?
Lengo la kunawa ni kupunguza tu wadudu kwenye mikono. Hawaishagi hata kama utanawa na sabuni. Waliosoma microbiology wanajua hii
 
Kuna vingi wengi huwa tunakosea mfano,kuongeza chumvi kwa kushika vile vimkebe mezani,sukari kwa kutumia vijiko vya kwenye mkebe,kukamua limao kwa mkono unaokula nao hujui zimeoshwa au hazijaoshwa au waliokutangulia kama walizingatia mazingira ya usafi.

Mimi niwapo kwenye migahawa ya mtaani vitu vyote vya zaida mezani huwa navishika kwa mkono wa kushoto hata kama chakula ninachokula kinashirikisha mkono na kijiko kula,nafasi ya kijiko nitakitumia na mkono wa kushoto nafasi ya mkono nitaitumia na mkono wa kulia.
 
Kwa wengine inawezekana ni mazoea tu. Lakini kwa upande wangu mimi, ni kwa sababu za kiusafi.

Leo, nikiwa mji fulani, niliingia kwenye mghahawa mmoja ambao kwa mji huo, ni miongoni mwa mighahawa ya hadhi, kwa ajili ya mlo wa Mchana. Mwonekano wake, huduma, bei na wateja wake inaakisi nilichosema. Ni mghahawa wa hadhi kubwa.

Nikiwa mghahawani hapo, aliingia dada mmoja kupata huduma. Aliagiza ugali na samaki, nafikiri, samaki choma.

Nilijikuta namfuatilia tokea aliponawa mpaka alipoanza kula.

Kilichonifanya nimfuatilie ni baada ya kumwona, alipomaliza kunawa mikono, aliendelea kushika vitu vingine visivyohusiana na chakula kwa kutumia mkono wake wa kulia.

Kwanza, alishika kiti chake na kukiweka vizuri kwa kutumia mikono yote miwili.

Pili, alichukua mkoba wake kwa kutumia mkono wa kulia na kufanya alichokusudia.

Tatu, aliendelea kutumia simu yake ya mkononi, nafikiri kwa kuchati, kwa kutumia mkono wa kulia.

Na ugali "wake" ulipowasili, aliendelea kula bila kunawa kwa mara nyingine.

Labda wajuvi wa masuala ya afya wanikosoe! Ni sahihi alivyofanya?

Mimi, kwa mtazamo wangu, alipaswa kutokushika tena simu, mkoba, viti, n.k. kwa kutumia mkono wa kulia kabla ya kumaliza kula kwa sababu huenda vitu hivyo vikawa na "vibakteria" hivyo kuwa hatarini kuambukizwa.

Nipo sahihi?

Nini lengo la watu kunawa kabla ya kula? Ni mazoea tu au sababu za kiafya?
dada hakua muungwana kwa afya yake mwenyewe baada ya kuwachota bacteria, vijidudu na uchafu kwenye vitu alivyoshika baada ya kunawa na kuanza kufakamia msosi. Kwa alichokifanya kinaweza kumsababishia matatizo mbalimbali mathalani kichefuchefu, maumivu ya tumbo, kuhara na kuharisha kutokana na mchafuko wa tumbo, kipindundupindu n k
 
Lengo la kunawa ni kupunguza tu wadudu kwenye mikono. Hawaishagi hata kama utanawa na sabuni. Waliosoma microbiology wanajua hii
Tuachane na hiyo kupunguza wadudu,unaonaje umenawa mikono then unaenda kushika kiti usichojua mimi nilietangulia kukishika nimetoka mazingira gani tena kwa mkono ule ule unaoenda kula nao?

Wapo wengine wakitoka chooni hawanawi na sabuni sababu wanajua mlo wao watakula na kijiko.
 
Bila shaka huyo mdada ni msukuma,,,,muha ....au mgogo
Mghahawa upo Kanda ya Ziwa, ila sijui kabila la huyo dada.

Kwa mwonekano wake, asingetarajiwa kufanya vile. Anaonekana kama ni msomi hivi au mtu mwenye exposure kubwa, na ukizingatia na mghahawa wenyewe ilivyo! Wanaingia mpaka wageni (Wazungu, n.k.).

Kama ingefanywa na "mwnanzengo" wa kawaida, nisingeshangaa. Najua ni kawaida "yetu" Watanzania wengi wa kawaida. Lakini kwa mtu mwenye "exposure" kubwa ama kwa kutembea au kusoma, hilo si la kawaida.
 
Lengo la kunawa ni kupunguza tu wadudu kwenye mikono. Hawaishagi hata kama utanawa na sabuni. Waliosoma microbiology wanajua hii
Sidhani kama ndivyo mkuu! Kumbuka jinsi watu walivyokuwa wakisisitizwa kunawia kwa maji tiririka kipindi cha Corona. Inaonekana kunawia kwa maji safi na sabuni kunaondoa vijidudu hatarishi.

Kama kuna vinavyobaki, kwa mujibu wa hoja yako, vitakuwa havina uwezo wa kuleta madhara.
 
Sidhani kama ndivyo mkuu! Kumbuka jinsi watu walivyokuwa wakisisitizwa kunawia kwa maji tiririka kipindi cha Corona. Inaonekana kunawia kwa maji safi na sabuni kunaondoa vijidudu hatarishi.

Kama kuna vinavyobaki, kwa mujibu wa hoja yako, vitakuwa havina uwezo wa kuleta madhara.
Ndiyo hivyo
 
Labda kajisahau, usipende kuhukumu watu pengine mambo mengi yanachangia watu kusahau sahau matukio madogo madogo kama hayo...
Mkuu, hakuna mahali nilikohukumu. Nilitaka kujifunza, isije ikawa mimi ndiyo sijui kanuni ya usafi. Nilitaka kujifunza kutoka kwa wengine.

Pili, sidhani kama alisahau. Atasahauje jambo muhimu kiasi hicho?

Hakuishia kushika kiti, bali na mkoba, pamoja na kuperuzi kwa simu.

Inaonekana ni "tabia" yake. Vinginevyo, angekumbuka mara tu alipotaka kula.
 
Bora huyo alishika simu yake mwenyewe kisha akala
Vip kuhusu kushika noti za pesa zinapitia mikono mingapi,, na watu wananunua kitu analipa au kupokea chenji na kuendelea kula..
 
Bora huyo alishika simu yake mwenyewe kisha akala
Vip kuhusu kushika noti za pesa zinapitia mikono mingapi,, na watu wananunua kitu analipa au kupokea chenji na kuendelea kula..
Vyote si sahihi. Ni hatari kwa afya.
 
Kwanza umeuliza kwanini watu wananawa kabla ya kula. Kwa Waislam ni mafundisho ya mtume wao kuwa wanawe kabla ya kula, japo unawaji wao hasa ule wa watu wote kunawa kwenye chombo kimoja chenye maji yasiyotiririka sivyo inavyopaswa kuwa. Kiujumla ni jambo la usafi kwa watu wa dini zote na wasio na dini.

Pili umeuliza je, alichofanya bidada ni sahihi? Jibu si sahihi.
Siku nyingine mind your business unless wewe ni detective au undercover.
 
Back
Top Bottom