Kwa nini watu wananawa mikono kabla ya kula?

Kwa nini watu wananawa mikono kabla ya kula?

Kwanza umeuliza kwanini watu wananawa kabla ya kula. Kwa Waislam ni mafundisho ya mtume wao kuwa wanawe kabla ya kula, japo unawaji wao hasa ule wa watu wote kunawa kwenye chombo kimoja chenye maji yasiyotiririka sivyo inavyopaswa kuwa. Kiujumla ni jambo la usafi kwa watu wa dini zote na wasio na dini.

Pili umeuliza je, alichofanya bidada ni sahihi? Jibu si sahihi.
Siku nyingine mind your business unless wewe ni detective au undercover.
Nashukuru kwa jibu lako mkuu🙏

Lakini kuhusu kumind my own business, sidhani kama hilo ni sahihi. Naona kama huo mtazamo una kasumba ya ubinafsi. Wanaojua wasipowafahamisha wasiofahamu, ujinga utaendelea kutamalaki.

Mimi nafikiri ungekuwa umefanya vizuri zaidi kama ungenikosoa kwa kutokumshauri huyo dada ili pengine asirudie siku nyingine kufanya kosa kama hilo.
 
Kuna vingi wengi huwa tunakosea mfano,kuongeza chumvi kwa kushika vile vimkebe mezani,sukari kwa kutumia vijiko vya kwenye mkebe,kukamua limao kwa mkono unaokula nao hujui zimeoshwa au hazijaoshwa au waliokutangulia kama walizingatia mazingira ya usafi.

Mimi niwapo kwenye migahawa ya mtaani vitu vyote vya zaida mezani huwa navishika kwa mkono wa kushoto hata kama chakula ninachokula kinashirikisha mkono na kijiko kula,nafasi ya kijiko nitakitumia na mkono wa kushoto nafasi ya mkono nitaitumia na mkono wa kulia.
🙏🙏🙏
 
Ukishanawa mikono, hupaswi kugusa hata koki ya bomba kwa kutumia kiganja cha mkono utakaoutumia kulia chakula. Vinginevyo, unaweza ukajizolea vibakteria ingawa umenawa.
 

Attachments

  • WHO__How_to_handwash__With_soap_and_water(480p).mp4
    3.6 MB
Namna sahihi ya kunawa mikono
 

Attachments

  • HATUA_ZA_KUNAWA_MIKONO_KWA_UFASAHA(360p).mp4
    8.7 MB
Back
Top Bottom