Kwa Pesa wanazoiba, inanivunja moyo kulipa kodi

Kwa Pesa wanazoiba, inanivunja moyo kulipa kodi

Kwakweli wanazingua sana,hela zinaibiwa za kutosha tu alafu bado Raisi wetu yupo kimya na kesho yake utasikia tumepewa mkopo wenye mashart Nafuuu,hizo hela zinazoibiwa akiweza kuzisimamia vizuri si tutapunguza kiasi cha kukopa nje?.
Ila mama wacha jasho limtoke tulimwambia umeachana na Uliowakuta unaingiza waliotolewa watakutia aibu wale ni majambazi sio wezi tu,akashupaza shingo leo kaishia kusema tu Pumbavuuuu,stupid haisaidiii.
Naskia jamaa kaagiza mabasi 100 na basi moja mln 300.

[emoji1787] couldn’t feel a better reaction than a serious laugh!

Kulia hakutasaidia.
 
Inasikitisha sana...

Bajaji wanalalamika kupandishiwa kodi, ambazo hizo pesa wanaenda kupandhishiana mishahara...
 
Mi nilishagoma kulipa kodi, labda wakate juu kwa juu.
Siwezi lipa kodi afu mpumbavu akafanyie upumbavu
 
Nimeamua sasa rasmi.

Kunikamata hawatoweza milele na nasema wazi kuanzia sasa sitolipa tena kodi wala tra hawatoniona tena kwenye makadirio.

Kwa sisi mabingwa uhangaikie kodi ulipe halafu watu wamekaa ofisini wanajipigia wakati mvua na jua linatupata sisi mahustler hapana.

Nasema tena hapana, nilikua Raia mwema kwa sasa imetosha hapa nilipofika ndio mwisho na sirudi tena nyuma
Watu waibe mabilioni halafu bado wako kazini, niunguzwe na makemikali, niangukie na magogo ya timba, nilale kwenye turubai kesho nilipe kodi halafu kodi yenyewe inapigwa hivyo.

Uzalendo bora ufie hapa potelea pote, tujenge nchi kwa jasho wengine wajilie haiwezekani.

Nasema huo ndio msimamo wangu, hali labda ikibadilika mbeleni huko nitaanza kulipa tena lakini kwa sasa hapana hapana.
😅😅😅Kodi yako haifiki serikalini wenye system wanailamba kama asali
 
Back
Top Bottom