Kwa suala la ununuzi wa rada nne nitakupongeza daima hayati JPM kazi ya kizalendo sana

Kwa suala la ununuzi wa rada nne nitakupongeza daima hayati JPM kazi ya kizalendo sana

Rada haijui hiyo habari ya Osama au beberu. Tambua kuwa nchi yetu inatazamwa yote na mamlaka ya anga TCAA.

JPM alinunua rada nne zenye kumilika kila kona ya TZ, hakuna hata mdudu anayeweza kuruka angani akaingia nchini asionekane.
Kununua radar ni jambo nzuri. Tuwapongeze watanzania kwa kulipa kodi na kuweza kununua radar.
 
Malengo ya hizo ni mazuri ila haimaanishi hatutoibiwa! Kwa maana wanaoiba ni viongozi wakuu ambao wana mamlaka ya moja kwa moja yakutoa oda kuwa ao wanaokuja wasikaguliwe.

2013 Twiga wanapandishwa kwenye ndege na kuondoka haikufanyika hivo sababu hatuna Rada za kumulika nchi nzima, maana Rada ilikuwepo kwa upande wa KIA ikipiga kazi maeneo yote ya ARUSHA, MWANZA, KIRIMANJARO mpaka Tanga, tuseme tu wenye mamlaka walilidhia sisi tuibiwe.
Mambo ya 2013 miaka kumi iliyopita. Ubunifu tatizo letu waafrika. Rasilimali zipo nyingi lakini hatuna akili za kuzitumia.

Mgeni akija na kuanza kutajirika nazo tunaanza kulia wivu kwanini eti mgeni aje na kutumia cha kwetu, sisi wenyewe hatuna ujanja wa kukitumia tukapata pesa kutokana na hizo mali wenye akili wakija tunaanza kulialia.

Wezi kama wakiamua kuiba wataiba lakini mpaka sisi tunaibiwa huwa tunakuwa wapi siku zote?.
 
Kuna watu hapa JF wanakariri habari za miaka ya nyuma halafu wanazileta sasa bila ya kujua nini haswa wanachokiandika.

Ni hawa wanaopenda kuandika habari za nchi kuibiwa, na habari za ndege kuonekana huko maporini. Hawa kuna mahali hawaelewi labda hawafahamu kuwa TZ ya sasa imenunua rada nne zinazotumika kuilinda nchi nzima kwa ujumla wake.

Bilioni takriban 67 zilitengwa na serikali ya awamu ya tano ya hayati JPM na zikanunuliwa rada nne kutoka kampuni moja ya Ufaransa, zikafungwa na zinafanya kazi ya kuilinda nchi.

Hakuna kinachoingia ndani ya anga la TZ kisionwe na rada hizo, hakipo kwa sasa na siku zijazo. Faida nyingine ya rada hizo ni kuongeza pato la taifa. Kila ndege inayokatiza katika anga letu inatazamwa moja kwa moja na mamlaka ya anga halafu invoice inatumwa kwa mamlaka ya anga ya nchi ambayo ndege inatoka.

Anga letu ni mali yetu kwa asilimia mia moja tofauti na miaka ile ambayo Paul Kagame alidhani anatuzidi akili alipo hodhi sehemu ya magharibi ya anga wakati sisi tupo tu.

Wanaoleta nyuzi za kichonganishi kwa kusema ndege zinatua huko porini waje na taarifa sahihi na zilizokamilika waachane na hizi kasumba za kufanya siasa nyepesi za kichonganishi.

Kwa sasa hakuna ndege inayoweza kutua ndani ya JMT bila ya kuonwa na mamlaka ya anga, hakipo kitu hicho. Hizi sio nyakati za zile ndege za kwenda mgodini kuchukua dhahabu kila alhamisi, zama hizo zimebakia historia.

JPM anaweza kuonekana hakufanya la maana, lakini ametuachia msingi mzuri wa kuipeleka nchi hii katika uchumi wa kati na ule wa juu zaidi. Aendelee kupumzika kwa amani.
Tangulia chattle ukazikwe
 
Samia atawakwaza wengi na wataumia wengi na atakapoondoka ikulu madhambi mengi tutayajua, hivyo hao wa kuzikwa nae watakuwepo tu.

Ndio maana ya majukumu ya urais, huwezi kuwakera wote na kuwafurahisha wote. Wapo wenye akili watakaokukumbuka.

Tofautisha kuwakwaza watu kinyume cha katiba.

Mbona kina Kikwette au Mwinyi wanadunda mtaani?

Mbona hawapo wanaoelekezwa kwenda kuzikwa na kina Nyerere au che Nkapa?

Azory, Ben, Lijenje au wenzao walimkwaza nini Mzilankende kwa kuwapo kwao duniani?

Hivi kwa kutuona je ndugu?
 
Tofautisha kuwakwaza watu kinyume cha katiba.

Mbona kina Kikwette au Mwinyi wanadunda mtaani?

Mbona hawapo wanaoelekezwa kwenda kuzikwa na kina Nyerere au che Nkapa?

Azory, Ben, Lijenje au wenzao walimkwaza nini Mzilankende kwa kuwapo kwao duniani?

Hivi kwa kutuona he ndugu?
Chuki zako binafsi zinakufanya uende mbali kabisa na mada husika.
 
Chuki zako binafsi zinakufanya uende mbali kabisa na mada husika.
Hakuna mada hapa mjomba si kwa beberu wala mrusi haipo rada yenye kuona kila ndege.

Hadithi zingine za kimahaba mahaba hizi sukuma genge danganyaneni wenyewe huko.

Kama vipi zindueni kabisa umoja party kumuenzi shujaa wenu.
 
Hakuna mada hapa mjomba si kwa beberu wala mrusi haipo rada yenye kuona kila ndege.

Hadithi zingine za kimahaba mahaba hizi sukuma genge danganyaneni wenyewe huko.

Kama vipi zindueni kabisa umoja party kumuenzi shujaa wenu.
Rada imenunuliwa kutoka kampuni ya Ufaransa haijatoka Russia. Unaijua hiyo kampuni?, unajua wameshauza katika nchi gani hizo rada?.

Kabla hamjaweka maoni yenu hadharani jitahidini kwanza muwe na uelewa wa nini mnachotaka kuandika,
 
Rada imenunuliwa kutoka kampuni ya Ufaransa haijatoka Russia. Unaijua hiyo kampuni?, unajua wameshauza katika nchi gani hizo rada?.

Kabla hamjaweka maoni yenu hadharani jitahidini kwanza muwe na uelewa wa nini mnachotaka kuandika,
Mkuu ungejikita umoja party huko ungejitendea haki zaidi. Haya ya rada na ufundi wake ni mambo mengine nje ya uwezo wako.

Umesoma wapi nikisema umesema rada ilinunuliwa urusi?

"Kwamba ni kampuni gani, imeuza wapi au nani wameuziwa?" Yanihusu nini mimi hayo kama si kuweweseka kwako tu ndugu?

"Ni kawaida kutengenezwa vyombo dhidi ya teknolojia iliyopo."

Ninakazia: Kudhania jiwe ndiyo alileta sasa Ile foolproof hiyo danganyaneni Sukuma genge wenyewe huko.
 
Mkuu ungejikita zaidi umoja party huko ungejitendea haki zaidi. Haya ya rada na ufundi wake ni mambo mengine nje ya uwezo wako.

Umesoma wapi nikisema umesema rada ilinunuliwa urusi?

"Kwamba ni kampuni gani, imeuza wapi au nani wmeuziwa?" Yanihusu nini mimi hayo kama si kuweweseka kwako tu ndugu?

"Ni kawaida kutengenezwa vyombo dhidi ya teknolojia iliyopo."

Ninakazia: Kudhania jiwe ndiyo alileta sasa Ile foolproof hiyo danganyaneni Sukuma genge wenyewe huko.
Unaongea hata ueleweki ujumbe wako haswa ni upi. Kunywa maji upumzike kwanza akili ndio uje uchangie mawazo.
 
Kwani Sukuma genge kwani kuna mnachoelewa zaidi ya kuweka makazi ya milele chattle?
Kusifia alichokifanya JPM sio lazima uwe sukuma gang ni suala la uzalendo tu. Rada zitailinda TZ kwa miaka mingi ijayo.

Tujikite katika kutazama uwezo wa viongozi wetu bila kuangalia majina na asili zao.
 
Punguza mawazo hasi ya kuona unaibiwa wewe tu kila siku.
Tatizo la watanzania wameingiziwa hofu ya kuamini kuibiwa kila kitu na kasumba yakufundishwa wazungu watu wabaya wanatuibia mara makoloni mara wengine wanadai kuibiwa madini wakati migodini serikali imeweka maafisa wake Mwenye mgodi lazima asafirishe Mali aliyozalisha na kulipia kwakupitia njia salama hivyo kwenye migodi kuwa na Kiwanja Cha ndege ni muhimu
 
Back
Top Bottom