Kwa tukio la kuuliwa Ali Kibao nawatetea polisi.Ni kundi lenye nia mbaya na nchi

Kwa tukio la kuuliwa Ali Kibao nawatetea polisi.Ni kundi lenye nia mbaya na nchi

Sijafuatilia utekwaji na mauwaji ya huko nyuma.Lakini kwa hili na mauwaji ya Ali Mohamedi Kibao nina uhakika vyombo vya usalama havijahusika.
Waliohusika ni kundi lenye nia ya kuleta fujo nchini na ni wapinzani wa chama tawala.Waweza kuwa ni wakereketwa wa chama chochote kile cha upinzani na hata Chadema chenyewe.
Kwa maana hiyo hilo kundi halikutumwa na vyombo vya usalama na wala viongozi wa vyama vya upinzani isipokuwa wameona wakiongeza kasi ya matukio ya namna hiyo katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi basi kutatokea sintofahamu na kuitikisa nchi kwa maslahi yao.
Sababu kuu ya kuamini hivyo kwanza ni aina ya mtu waliyemlenga ambaye ana nafasi kubwa kwenye chama cha Chadema na namna walivyoamua kumuua.
Ingekuwa ni ugomvi na visasi vya kawaida basi wangemfuata nyumbani kwake na usiku au akiwa kwenye gari yake au ya ndugu zake ili isiwe rahisi kuleta hisia kwa wananchi.Badala yake wamekwenda kumkamata ndani ya basi na mchana kweupe.Kule walikomtupa ni maeneo yale yale maarufu wanakopatikana watu waliouliwa kiujambazi.
Kwanini wasimzike kwenye kaburi ambalo ingechukua muda kugundulika.Madhumuni yao ni kufanya matangazo kutokana na kifo chake ili kutokee fujo.
Kwa tukio hili sasa ndio uwezekano wa kupatikana waliokuwa wakitenda mauwaji watajulikana na kitendawili kuteguliwa pindi serikali itakapotia kulihitimisha.
INAUNGANA NA WEWE LIPO KUNDI LINALOJARIBU KUTUMIA KILA AKILI KUPANDA CHUKI KWA WATANZANIA KWA MBINU YOYOTE ILE, ALIMRADI TANZANIA IVURUGIKE, NATHUBUTU KUSEMA WANAPANDA NGAZI YA KUJARIBU KUMGUSA KIONGOZI MWENYE HAIBA NA MVUTO KWA UMMA, LET BE KEEN!
 
Kiufupi wewe ni kichaa
Wewe huenda ni miongoni mwa hao wachawi wa nchi mnaofanya mauwaji ili kuwachafua watu msiowapenda.
Wenye akili huwa hatuburuzwi namna hiyo.
 
INAUNGANA NA WEWE LIPO KUNDI LINALOJARIBU KUTUMIA KILA AKILI KUPANDA CHUKI KWA WATANZANIA KWA MBINU YOYOTE ILE, ALIMRADI TANZANIA IVURUGIKE, NATHUBUTU KUSEMA WANAPANDA NGAZI YA KUJARIBU KUMGUSA KIONGOZI MWENYE HAIBA NA MVUTO KWA UMMA, LET BE KEEN!
mpaka sasa haya mambo hayajaanza kwa huyu mzee... kiongozi ana nguvu na vyombo vyote vya usalama lakini hivyo vyombo vimekuwa vikideny kuwa hakuna jambo kama hilo. Sasa unasemaje kuwa kuna kundi linajaribu kupanda chuki wakati anavyo vyombo vya kuchunguza na havifanyi hivyo?
Hakuana genge lenye uwezo wa kuja na cruiser, na mitutu vikamteka mtu hadharani halafu polisi wasiigeuze hii nchi juu chini kuwatafuta watu wao unless wanawajua ni akina nani?
Mwanza tu alipouawa kamanda baro waligeuza jiji juu chini na ndani ya siku 2 walikuwa wamewakamata wahusika na story nzima ya kilichotokea, polisi ukiona hawafanyi kazi jua wanajua kinachoendelea.
Hakuna cha genge wala nini hawa reaction yao wanajua nani anayafanya haya ndio maana hawachunguzi
 
Kundi ambao linamiliki SMG linasimamisha gari, linamchukua abilia kwa pingu na kusepa naye kwenye Landcluiser kweupe pee na watu wanashuhudia simema.
.
Ukisema ni kundi basi Taifa kimevamiwa tayari ya banyamulenge Wa Sudan na Congo. JWTZ inabidi waliokoe taifa letu limevamiwa na Magaidi kutoka nje na hatujui lengo la hawa magaidi ni lipi maana linashughulika na wanasiasa & wanaharakati.
 
Mimi naona wanajua nani anafanya yanayofanyika na itakuwa ni kikundi ambacho kina nguvu kuliko wao ndio maana unaona hawachukui hatua za kueleweka na hawana majibu ya kueleweka. Refer alivyotekwa manji walikuwa wanajichanganya hadi wakawa kituko kwa sababu walikuwa wanajua nini kinaendelea.
Polisi watanzania wakiwa wana nia kweli ya kuchunguza tukio basi hufanya kazi kweli.
Hakuna genge la wahuni lenye guts za kusimamisha bus likamchomoa mtu hadharani bila wasiwasi likasepa naye mchana kweupe.
Na msijisaurishe huyu bwana Ally si wa kwanza kutekwa na polisi mara zote majibu yao ni denial fulani kama vile hakuna utekaji, huyu ni vile imewagusa watu wengi ndio maana umesikia katamko fulani.
Juzi barua yao ilikuwa imelenga kujitetea zaidi kuliko kueleza hatua walizozichukua ni kama vile hakukuwa na hatua.
Maiti ilipelekwa mochwari asubuhi na polisi, jioni polisi haohao wakatoa taarifa ya kuanza uchunguzi wa utakaji wa mtu ambaye maiti yake wameipeleka mochwari!! Does it make sense even though is not common??
 
Ndiyo mmeamka kuja kutetea, too late mtu wa ndani kishasema yote. Ile sinema yao waliyoicheza, ilikuwa hadharani. Traffic kwenye huo msafara wamemtambua, yeye ni muajiriwa wa Jeshi la polisi, hebu mtuache, tumuomboleze Mzee Ally kwa amani.
 
Sijafuatilia utekwaji na mauwaji ya huko nyuma.Lakini kwa hili na mauwaji ya Ali Mohamedi Kibao nina uhakika vyombo vya usalama havijahusika.
Waliohusika ni kundi lenye nia ya kuleta fujo nchini na ni wapinzani wa chama tawala.Waweza kuwa ni wakereketwa wa chama chochote kile cha upinzani na hata Chadema chenyewe.
Kwa maana hiyo hilo kundi halikutumwa na vyombo vya usalama na wala viongozi wa vyama vya upinzani isipokuwa wameona wakiongeza kasi ya matukio ya namna hiyo katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi basi kutatokea sintofahamu na kuitikisa nchi kwa maslahi yao.
Sababu kuu ya kuamini hivyo kwanza ni aina ya mtu waliyemlenga ambaye ana nafasi kubwa kwenye chama cha Chadema na namna walivyoamua kumuua.
Ingekuwa ni ugomvi na visasi vya kawaida basi wangemfuata nyumbani kwake na usiku au akiwa kwenye gari yake au ya ndugu zake ili isiwe rahisi kuleta hisia kwa wananchi.Badala yake wamekwenda kumkamata ndani ya basi na mchana kweupe.Kule walikomtupa ni maeneo yale yale maarufu wanakopatikana watu waliouliwa kiujambazi.
Kwanini wasimzike kwenye kaburi ambalo ingechukua muda kugundulika.Madhumuni yao ni kufanya matangazo kutokana na kifo chake ili kutokee fujo.
Kwa tukio hili sasa ndio uwezekano wa kupatikana waliokuwa wakitenda mauwaji watajulikana na kitendawili kuteguliwa pindi serikali itakapotia kulihitimisha.
Kama unadhani ni rahisi hivo nawe nenda zuia basi teka mtu muue umtupe porini kama utamaliza hata saa 24 mtaani. Hakuna kikundi chochote ambacho hakina uhusiano na dola ambacho kinaweza kuwa kinamiliki SMG, Pingu na magari aina ya Landcruiser hardtop na kikafanikiwa kufanya uhalifu wa aina ile mchana kweupe.
Kama hicho kikundi kipo na polisi na usalama wa taifa wameshindwa kukibaini na kimeendelea kufanya matukio bila kukoma basi nchi haiko salama.
Lakini je umechukuwa hata sekunde moja kujiuliza kuhusu kauli za Uvccm wanazotoa sehemu mbalimbali nchini? Kagera Tukiwapoteza polisi msiwatafute, Arusha mimi NDO nilikuwa naongoza kile kikosi cha chinja chinja, Longido JE?

Haya mambo kama hayajakukuta utaendelea kubwabwaja kuna mwenzako huko kigoma alitumia mpaka hela zake kuifurahisha dora naye akijiita SERIKALI, ilipofika kudai hela zake kapotezwa mpaka leo hajulikani aliko.
 
mpaka sasa haya mambo hayajaanza kwa huyu mzee... kiongozi ana nguvu na vyombo vyote vya usalama lakini hivyo vyombo vimekuwa vikideny kuwa hakuna jambo kama hilo. Sasa unasemaje kuwa kuna kundi linajaribu kupanda chuki wakati anavyo vyombo vya kuchunguza na havifanyi hivyo?
Hakuana genge lenye uwezo wa kuja na cruiser, na mitutu vikamteka mtu hadharani halafu polisi wasiigeuze hii nchi juu chini kuwatafuta watu wao unless wanawajua ni akina nani?
Mwanza tu alipouawa kamanda baro waligeuza jiji juu chini na ndani ya siku 2 walikuwa wamewakamata wahusika na story nzima ya kilichotokea, polisi ukiona hawafanyi kazi jua wanajua kinachoendelea.
Hakuna cha genge wala nini hawa reaction yao wanajua nani anayafanya haya ndio maana hawachunguzi
Aliyeuliwa ametajwa ni mzee japo si mzee kweli umuhimu wake ni hicho cheo chake ndani ya chama.
Waliomuua si lazima wawe wametumwa na jeshi kufanya hivyo japokuwa wanaweza kuwa ni askari wastaafu au walio ndani ya jeshi wenye uzoefu wa kutumia bunduki na hawana hofu kumkamata mtu yoyote yule.
Unajua namna tunavyoibiwa kirahisi katika mitandao kwa vile wanaofanya hivyo huwa wametokea huko huko kwenye mitandao na wanajua kila kitu.
 
Sijafuatilia utekwaji na mauwaji ya huko nyuma.Lakini kwa hili na mauwaji ya Ali Mohamedi Kibao nina uhakika vyombo vya usalama havijahusika.
Waliohusika ni kundi lenye nia ya kuleta fujo nchini na ni wapinzani wa chama tawala.Waweza kuwa ni wakereketwa wa chama chochote kile cha upinzani na hata Chadema chenyewe.
Kwa maana hiyo hilo kundi halikutumwa na vyombo vya usalama na wala viongozi wa vyama vya upinzani isipokuwa wameona wakiongeza kasi ya matukio ya namna hiyo katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi basi kutatokea sintofahamu na kuitikisa nchi kwa maslahi yao.
Sababu kuu ya kuamini hivyo kwanza ni aina ya mtu waliyemlenga ambaye ana nafasi kubwa kwenye chama cha Chadema na namna walivyoamua kumuua.
Ingekuwa ni ugomvi na visasi vya kawaida basi wangemfuata nyumbani kwake na usiku au akiwa kwenye gari yake au ya ndugu zake ili isiwe rahisi kuleta hisia kwa wananchi.Badala yake wamekwenda kumkamata ndani ya basi na mchana kweupe.Kule walikomtupa ni maeneo yale yale maarufu wanakopatikana watu waliouliwa kiujambazi.
Kwanini wasimzike kwenye kaburi ambalo ingechukua muda kugundulika.Madhumuni yao ni kufanya matangazo kutokana na kifo chake ili kutokee fujo.
Kwa tukio hili sasa ndio uwezekano wa kupatikana waliokuwa wakitenda mauwaji watajulikana na kitendawili kuteguliwa pindi serikali itakapotia nia kulihitimisha.
Kwa Serikali hii ya CCM kwa kutumia vyombo vyake kufanya uchunguzi!

🤮🤮🤮

Uchunguzi ufanywe na watahalam kutoka nje ya Tanzania kama vile timu ya uchunguzi ya Scotland Yard, nk.
 
Hizi ni akili za bata. Mtu anasema hakufuatilia halafu anatetea kwenye jambo ambalo anakiri halijui
 
Kuna wakati kukaa kimya ni jambo zuri sana kuliko kuongea, Unachojaribu kutaka kuongea sio tu kwamba ni ujinga bali ni jaribio lingine la unyama unaofanywa na kundi la wajinga kutetea ujinga amabo utakuja kuwagaharimu hata nyinyi wenyewe.
Kwanza mtu kama wewe unaamini uwepo wa vyama vingi ni dhambi, kwahiyo haya unayojaribu kutaka kuongea ni muendelezo wa imani yako ya kishetani dhidi ya dhulma inayoendelea.
Rais wako kajaribu kuongea lakin kwakuwa hata akili hamna hamjui hata kwenda na mwendo wa kiongzi wenu.
 
Acha dharau kwa jeshi la polisi ,unazidi kulidhalilisha kwamba hawana kitu ndiyo maana mtu anakuja kutekwa mchana kweupe bila wao kujua....Unawapaka matope vyombo vyote vya ulinzi na usalama...yaani wahuni wanakuja kuteka bus na kutokomea na mtu bila kukamatwa? Unataka kusema kama waliofanya hivyo sio wao wenyewe basi Mama Kizimkazi alifumue jeshi lote maana wananchi na nchi haiko salama.
 
Aliyeuliwa ametajwa ni mzee japo si mzee kweli umuhimu wake ni hicho cheo chake ndani ya chama.
Waliomuua si lazima wawe wametumwa na jeshi kufanya hivyo japokuwa wanaweza kuwa ni askari wastaafu au walio ndani ya jeshi wenye uzoefu wa kutumia bunduki na hawana hofu kumkamata mtu yoyote yule.
Unajua namna tunavyoibiwa kirahisi katika mitandao kwa vile wanaofanya hivyo huwa wametokea huko huko kwenye mitandao na wanajua kila kitu.
so, jeshi la polisi lisipokuja na majibu na kumbuka si mtu kwanza kutekwa kwa miezi hii ya karibuni na polisi bado hawajatoa majibu ya kueleweka siku zote ni kama vile wanapinga hili kuwa lipo. iwe alikuwa mgambo au mwanajeshi, tukio limetokea hadharani bila kuleta majibu itakuwa wanajua nani kafanya hiki kitendo. kitendo cha mtu kutekwa hadharani na watu wenye cruiser na mitutu inabidi iwe alarm kwao pia wachunguze kweli kweli maana inaonyesha kuwa kumbe kuna hatari ya kiusalama. kama likipita hivi hivi basi watakuwa wanajua nini kinaendelea.
 
Sijafuatilia utekwaji na mauwaji ya huko nyuma.Lakini kwa hili na mauwaji ya Ali Mohamedi Kibao nina uhakika vyombo vya usalama havijahusika.
Waliohusika ni kundi lenye nia ya kuleta fujo nchini na ni wapinzani wa chama tawala.Waweza kuwa ni wakereketwa wa chama chochote kile cha upinzani na hata Chadema chenyewe.
Kwa maana hiyo hilo kundi halikutumwa na vyombo vya usalama na wala viongozi wa vyama vya upinzani isipokuwa wameona wakiongeza kasi ya matukio ya namna hiyo katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi basi kutatokea sintofahamu na kuitikisa nchi kwa maslahi yao.
Sababu kuu ya kuamini hivyo kwanza ni aina ya mtu waliyemlenga ambaye ana nafasi kubwa kwenye chama cha Chadema na namna walivyoamua kumuua.
Ingekuwa ni ugomvi na visasi vya kawaida basi wangemfuata nyumbani kwake na usiku au akiwa kwenye gari yake au ya ndugu zake ili isiwe rahisi kuleta hisia kwa wananchi.Badala yake wamekwenda kumkamata ndani ya basi na mchana kweupe.Kule walikomtupa ni maeneo yale yale maarufu wanakopatikana watu waliouliwa kiujambazi.
Kwanini wasimzike kwenye kaburi ambalo ingechukua muda kugundulika.Madhumuni yao ni kufanya matangazo kutokana na kifo chake ili kutokee fujo.
Kwa tukio hili sasa ndio uwezekano wa kupatikana waliokuwa wakitenda mauwaji watajulikana na kitendawili kuteguliwa pindi serikali itakapotia nia kulihitimisha.
Unataka kusemaje mkuu? Umeandika maelezo marefu lakini hayana kichwa wala mguu.
 
Hizi ni akili za bata. Mtu anasema hakufuatilia halafu anatetea kwenye jambo ambalo anakiri halijui
ni akili za mtu aliyetimamu sana.Tumepita kati na kati.Kama waliotekeleza ni polisi basi ni wajumbe wa kundi ovu hakuna dalili ya kutumwa na jeshi lenyewe.Na hilo kundi ovu laweza kuwajumuisha mpaka wanachama wa vyama vya upinzani.
 
Back
Top Bottom