Kwa tunaowajua haiwezekani Upinzani kususia bunge, huu ni utani tu!

Kwa tunaowajua haiwezekani Upinzani kususia bunge, huu ni utani tu!

William Mshumbusi

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2012
Posts
1,761
Reaction score
2,391
Tunaomjua Zitto vizuri na Mbowe hawatuchanganyi kabisa.

Mwaka 2010 baada ya UCHAGUZI mkuu wabunge wa upinzani walikusudia kususia bunge kwa sababu kama hizi hizi. Wakati huo Tundu Lissu, Heche na Mdee walikuwa moto kweli. Walilia dhulma dhidi ya wagombea wao wengi sana wa ubunge na kutangazwa kwa shida kama Wenje na yule wa Shinyanga.

Bunge lilipoanza wakasusia hotuba ya Rais Kikwete. Wakakataa kumtambua kama Rais.

Wakati huo Zitto akawa kinara wa usaliti kwa lugha yao. Walitoka wote wakati wa hotuba Ila Zitto akabaki. Wabunge wa CCM wakamshangilia sana Ila waupinzani wakamuona msaliti. Asubuhi yake Zitto akaamkia TBC kuwaponda wenzake. Wabunge wa upinzani wakaazimia Zitto afukuzwe uanachama. Mbowe akamkingia kifua. Baada ya Muda JK akatangaza mchakato katiba mpya Mbowe akamtambua JK kuwa Rais, movie ikaishia hapo.

Kinachousumbua upinzani na uslmi wao wote ni njaa. Wakiwa wabunge wanaishi maisha ya kibepari huku wakifanya harakati uchwara.

Je, Mbowe na Halima Mdee wanaweza kufanya harakati nje ya mishahara na marupurupu ya bunge?

Je, wakati wameamua kurudi bungeni mwaka 2010-2011, hali ya kisiasa ya kisiasa ilibadilika au waliangalia posho zao?

Mpaka sasa kwanini Mbowe na Mdee wapo kimya kutoa mitazamo yao?

Je, wakipitisha majina ya viti maalumu nne ya Mdee na Bulaya je Mdee atawaunga mkono waliopitishwa?

Je, Chadema, ACT na CUF wanauwezo wa kulisusia bunge mazima na kuliacha kuwa la chama kimoja complete.

Je, Chadema inaweza kumfuta uanachama mbunge wao pekee?

Kifupi lazima kila hatua wanayochukua ije na majibu ya namna ya kutibu njaa zao binafsi tofauti na hapo chama kitapasuka.
 
Bado hatuna upinzani imara, bado sana.

Inakuaje unamkataa Rais au kumtambua mteuliwa na kususia bunge lakini uchaguzi ukiitishwa unashiriki bila mambo uliyotaka yabadilishwe hayajafanyiwa chochote?

Zanzibar sheria ya kupiga kura siku mbili imepitishwa tokea 2018, hawa wapinzani kwanini walikaa kimya au kuwaelewesha wafuasi wao badala ya kuwapotosha wengine wamepoteza maisha na wengine kuambulua ulemavu?

Mbaya zaidi walisusa uchaguzi wa marudio kwa madai tume ilikataa kuwatangaza uchaguzi ukafutwa na hawakushiriki, kipi kimewasukuma kushiriki huu wa 2020 ikiwa tume na muundo wake ni ule ule?

Hapa cha msingi washirikiane na serikali na kuona namna ya kushawishi mapendekezo yao. Kuonyesha jeuri nusu nusu itawaasamvaratisha na kuwapoteza kabisa kwenye medani za siasa.

Masikini hana kiapo.
 
Bila kupuuza angalizo lako, hiyo mifano uliyotoa huko nyuma ni kweli, lakini siku za nyuma viongozi walikuwa wanaamua watakavyo na sisi wafuasi tulikuwa kimya. Ila kwa sasa viongozi wanapaswa kuamua kwa kufuata matakwa yetu sisi wafuasi wao.

Na iwapo watakwenda kushiriki hilo bunge kibogoyo, lililopatikana kwa umwagaji damu na wizi wa kura, ndio wasahau support yetu.

Wanaweza kuamua watakavyo lakini sisi wafuasi wao Misimamo yetu iko wazi. Ingekuwa bunge lenyewe lina meno hapo afadhali, sio hilo bunge kibogoyo.
 
Zitto anaipenda pesa zadi ya yuda yupo tayari kuuza hata nguo zake abaki uchi
Zitto Kabwe arudi Kigoma wafanyabiashara waliomkopesha Fedha Wanamtafuta awalipe fedha zao waendelee na Biashara zao.
Na kuna Mrembo anaitwa Rucy ulimkopa K ulimtoroka hukumlipa elfu 20.
 
Zitto Kabwe arudi Kigoma wafanyabiashara waliomkopesha Fedha Wanamtafuta awalipe fedha zao waendelee na Biashara zao.
Na kuna Mrembo anaitwa Rucy ulimkopa K ulimtoroka hukumlipa elfu 20.
Kuna mtu amesema amechoka kuapisha, sasa sijui mnahangaikia nini?
 
Zitto Kabwe arudi Kigoma wafanyabiashara waliomkopesha Fedha Wanamtafuta awalipe fedha zao waendelee na Biashara zao.
Na kuna Mrembo anaitwa Rucy ulimkopa K ulimtoroka hukumlipa elfu 20.
Sawa "Rucy", Mwami amekusikia. Pole kwa kuwa mkopesha "K".
 
Maelezo marefu hayana maana yoyote, kelele za mabadiliko ya hii mifumo ya uchaguzi ni toka 1992, ni kilio gani hakijasikika mpaka ionekane kitasikika sasa? Kama unaona hakuna upinzani imara, hebu anzisha wakwako tuuone uimara wako.

Mie sio mwanaharakati wala mwanasiasa, hapa natoa maoni yangu binafsi na sio lazima yafanane na yako au mtu mwingine yeyote yule, hiyo haki nnayo.

Twende taratibu, ikuwa walizira kumtambua rais wa awamu ya nne, kitu gani kiliwafanya wamtambue baadae?

Ikiwa mara zote wanasema tume ya uchaguzi si huru na katiba ina tatizo, kwanini wanashiriki chaguzi badala ya kushughulikia utatuzi wa hayo mambo?

Kama wanatumia mbinu zile zile kudai katiba mpya wataendelea kupata matokeo yale yale.
Kwa ufupi inabidi wabadili mikakati yao.
 
We mwanamke unawashwa nn?? Nakushauri umtafute bwana ili akujerui maana kiherehere kimekuzidi.
Zitto Kabwe arudi Kigoma wafanyabiashara waliomkopesha Fedha Wanamtafuta awalipe fedha zao waendelee na Biashara zao.
Na kuna Mrembo anaitwa Rucy ulimkopa K ulimtoroka hukumlipa elfu 20.
 
Kwani walikutangazia kuwa walimtambua au lah?? Ili kutomtambua ulitaka wafanyeje??
Unajua matokeo ya kususia uchaguzi au wasema tu?? Uliwai kumuona mkulima aliyemsusia ngederee shamba au unabwabwaja tu??
 
Una suluhisho la kupatikana kwa hayo mambo au unachangia kwa kuwa unajua kusoma na kuandika? Waliendelea kushiriki ili wapate uhalali wa kuyadai, labda ww ungesema ni njia gani watumie ili wapate watakacho.
 
Kwani walikutangazia kuwa walimtambua au lah?? Ili kutomtambua ulitaka wafanyeje??
Unajua matokeo ya kususia uchaguzi au wasema tu?? Uliwai kumuona mkulima aliyemsusia ngederee shamba au unabwabwaja tu??

You are right Sir?
 
Una suluhisho la kupatikana kwa hayo mambo au unachangia kwa kuwa unajua kusoma na kuandika? Waliendelea kushiriki ili wapate uhalali wa kuyadai, labda ww ungesema ni njia gani watumie ili wapate watakacho.

Bora umejaribu kubaki kwenye hoja. Ikiwa walifanya hivyo awali, kwanini wanagoma na kukataa kupeleka majina ya wabunge wa viti maalum na kuzuia hata yule mmoja asihudhurie bunge? Hauoni tayari inawapa pa kuanzia kwenye kudai hayo tunayoyataka mkuu?
 
Bora umejaribu kubaki kwenye hoja. Ikiwa walifanya hivyo awali, kwanini wanagoma na kukataa kupeleka majina ya wabunge wa viti maalum na kuzuia hata yule mmoja asihudhurie bunge? Hauoni tayari inawapa pa kuanzia kwenye kudai hayo tunayoyataka mkuu?

Hakuna aliyemzuia huyo mmoja acha upotoshaji usio na maana. Msimamo wa chama ni kuwa uchaguzi ulikuwa wa umwagaji damu na wizi wa kura, hivyo kupeleka viti maalum ni kuhalalisha huo ukora. Na huo wizi na umwagaji wa damu tumeshuhudia kwa macho yetu. Sasa sijui unalazimisha nini viti maalum wapelekwe huko.
 
Hakuna aliyemzuia huyo mmoja acha upotoshaji usio na maana. Msimamo wa chama ni kuwa uchaguzi ulikuwa wa umwagaji damu na wizi wa kura, hivyo kupeleka viti maalum ni kuhalalisha huo ukora. Na huo wizi na umwagaji wa damu tumeshuhudia kwa macho yetu. Sasa sijui unalazimisha nini viti maalum wapelekwe huko.

Hadi sasa sijajua unakataa nini na unakubali kipi, ikiwa uchaguzi ulikua batili ina maana hata huyo mgombea mmoja ni batili. Inaenda hivyo hivyo hadi kwa viti maalum ambao msingi wake ni kura batili alizopata mgombea wa upinzani.

Mie sina cha kulazimisha.
 
Back
Top Bottom