Kwa ukatili nilioufanya kwa huyu paka, naomba tu Mungu unisamehe

Kwa ukatili nilioufanya kwa huyu paka, naomba tu Mungu unisamehe

Joined
Jan 14, 2020
Posts
19
Reaction score
42
Nikiwa zangu nimetulia na familia yangu chini ya mti hapa nyumbani akaja paka na mwanae wakakaa pembeni yetu kama kawaida kwa paka wanaoishi vizuri na binadamu hawaogopi hata wanaweza kukuchezea kama kuku tupia mguu hivi

Basi bhana yule paka mdogo sijui ni shetani gani alimuingia ghafla akakirukia kifaranga cha kuku kilichokuwa kimejikunyata kwa ugonjwa, akakibugia kichwa mdomoni, kifaranga kikaanza kufurukuta,

Nikampigia kelele nikimaanisha amwachie yeye kakimbia nae shambani, nikamfuata huko huko, sikutaka kumuonesha uso wa kukasirika nikambembeleza akamwachia ila amemla kichwa

Nikamwita taratibu mpaka akaingia ndani, nikafunga mlango na dirisha, nikaenda kuchukua kipisi cha nondo, nilichomfanyia Mungu tu anisamehe maana hayupo tena duniani,

Kama umewahi fanya ukatili kwa myama yoyote na wewe tubu hii dhambi kwani ni dhambi kama dhambi zingine.
 
😀😀😀
mambo ya utotoni hayo tumeua sana paka wezi na mbwa wezi
japo tulikuwa tunafanya kama masihara ila kwako umelifanya kwa moyo wote ndio maana kama linakutesa.
😀😀😀

pole sana ila kuupoza moyo fanya hivi,

tafuta sehemu nzuri huyo paka mzike hapo yaani fanya kama unamuhifadhi kwa heshima,
chimba shimo usawa wa magoti,
muweke hapo fukia pasawazishe moyo utatulia,

kama tayari ulikuwa umemfukia tafuta ua au lolote zuri panda juu yake au ukikosa ua panda zile mbegu za maboga moyo utatulia tu ndugu yangu

pole sana huwa inatokea sana moyo kufadhaika hasa ukifanya jambo kwa moyo wote kama hivi
 
Hiyo zambi itakutesa sana mkuu, Sisi tuliua lakini tulikuwa hatujitambui bado wewe umeuabukiwa unajitambua, Damu inadai😁
 
😀😀😀
mambo ya utotoni hayo tumeua sana paka wezi na mbwa wezi
japo tulikuwa tunafanya kama masihara ila kwako umelifanya kwa moyo wote ndio maana kama linakutesa.
😀😀😀

pole sana ila kuupoza moyo fanya hivi,

tafuta sehemu nzuri huyo paka mzike hapo yaani fanya kama unamuhifadhi kwa heshima,
chimba shimo usawa wa magoti,
muweke hapo fukia pasawazishe moyo utatulia,

kama tayari ulikuwa umemfukia tafuta ua au lolote zuri panda juu yake au ukikosa ua panda zile mbegu za maboga moyo utatulia tu ndugu yangu

pole sana huwa inatokea sana moyo kufadhaika hasa ukifanya jambo kwa moyo wote kama hivi

[emoji23][emoji23][emoji23]kama nakuona na kikundi chako vile mkiwa na silaha zenu
 
Hii kitu wengi huwa tunafanya na ni tatizo la kisaikolojia ambalo limetuathiri kulingana na mazingira tunayoishi na familia tuliyokulia. Kupiga mnyama ni jambo la kawaida sana na wengi huwa ni furaha kwetu.

Mnyama ukimpenda naye anakupenda hana unafiki analipa fadhila kwa Upendo. Ukimtendea haki utahisi furaha ndani ya moyo wako ila ukimuumiza hiyo kitu itakutesa katika maisha. Tukumbuke wana familia na wanahangaika kutunza familia zao - usiwe mmoja wapo wa kuwapa maumivu na mateso.

Take note:
Ukimfundisha mtoto wako kuwapenda wanyama Ambao hawawezi kuzungumza hii itamsaidia kuwa na moyo wa huruma na imani kuwaeleka binadamu wenzake.
View attachment 2291783
FB_IMG_1604584873763.jpg
View attachment 2291784
 
Paka alikuonesha kuwa ana njaa, wewe hukuielewa lugha yake.

Vinginevyo huyo paka aliishaanza kutumiwa na wachawi,

All in all umemkosea paka,
 
Kuna mdada kachukua vitoto vya paka na mama yao katika ndani ya kiroba wazima kachimba shimo kafukia
 
😀😀😀
mambo ya utotoni hayo tumeua sana paka wezi na mbwa wezi
japo tulikuwa tunafanya kama masihara ila kwako umelifanya kwa moyo wote ndio maana kama linakutesa.
😀😀😀

pole sana ila kuupoza moyo fanya hivi,

tafuta sehemu nzuri huyo paka mzike hapo yaani fanya kama unamuhifadhi kwa heshima,
chimba shimo usawa wa magoti,
muweke hapo fukia pasawazishe moyo utatulia,

kama tayari ulikuwa umemfukia tafuta ua au lolote zuri panda juu yake au ukikosa ua panda zile mbegu za maboga moyo utatulia tu ndugu yangu

pole sana huwa inatokea sana moyo kufadhaika hasa ukifanya jambo kwa moyo wote kama hivi
Sawa mkuu nimekuelewa
 
Hukusoma Ile posting yangu ya "Atlantis" ya siku chache zilizopita. Kwamba ulikuwepo Ustaarabu wa Atlantis,ambapo dunia ilikuwa imeendelea kuliko sasa. Lakini watu waliokuwa wabachukiana,wakapigana vita, wakaiharibu sana dunia yao.

Lakini katika kuchukiana kwao kwote,waliokuwa hawagombani na wanyama.

Ndiyo màana ya Ile sanamu yao ya Sphinx,nusu mtu,nusu mnyama,ikiwa na maana kwamba binadamu na wanyama lazima washirikiane ama sivyo hakifanyiki kitu.

Lakini leo hii utaenda kwa Mwamposya,utawasikia watu wanajisifu,na wanasifiwa, jinsi waluvyommwagia paka" mafuta matakatifu "wakamuua.
 
Paka sio wako umwite hadi ndani na aje??alafu paka akiwa na watoto alivyo mjanja eri eje kihasarahasara namna hiyo? Na nijuavyo paka mwizi hasogelei mtu karibu.na paka akishajua kaharibu anavyo kimbia humuoni kutwa nzima.
Broo hii chai
 
Nikupe hongera kwa ulichokifanya aisee mie ninahangaika na paka nataka nimteketeze yeye na familia yake(ana watoto) ananitesa sana na familia ya yangu kwanza anakula sana vifaranga lakini pia kila siku nafanya kazi ya kubadirisha nyavu za madirisha anachana sana hasa za jikoni na kujichukulia mboga anayoitaka nimejaribu simu ila hafi anadunda tu. Kwa kweli nakupengeza sana
 
Back
Top Bottom