Uchaguzi 2020 Kwa umati uliofurika leo Viwanja vya Matogoro Mjini Tandahimba, ni wazi hakuna wa kumzuia Tundu Lissu kuwa Rais

Uchaguzi 2020 Kwa umati uliofurika leo Viwanja vya Matogoro Mjini Tandahimba, ni wazi hakuna wa kumzuia Tundu Lissu kuwa Rais

Sasa hilo sio kweli kwasababu TL ni musomi anaejua sheria na utaratibu. Asingeweza kutangaza kwenda Tandahimba wakati anajua hana kibali cha kufanya mkutano huko. Chanzo cha taarifa sio chakuaminika.
 
Wakazi wa mji wa Tandahimba na vitongoji vyake walikusanyika kwa wingi kwenye viwanja vya shule ya msingi Matogoro ili kumpokea mgombea urais anayeiwakilisha CHADEMA Mh. Tundu Lissu.

Kwa hakika umati ulikuwa mkubwa haijapata kutokea. Hamasa ilikuwa juu sana.

Huku watu wakiendelea kumiminika, ikaletwa taarifa kwamba Tundu Lissu hatafika kwenye hadhara hiyo kwani hana kibali cha kufanya mkutano wa kampeni katika jimbo la Tandahimba.

Kwa taarifa hiyo wananchi walitakiwa kutawanyika mara moja kurejea makwao. Ila ilichukua muda wa nusu saa watu kuondoka toka viwanjani hapo kwani wengi wao walisikika wakiilaani serikali ya CCM na wengi wao waliapa kumchagua Lissu kwa kishindo kikuu ifikapo tarehe 28 Oktoba mwaka huu.

Nadiriki kusema kwa umati ulioshuhudiwa viwanjani hapo leo, hakuna wa kumzuia Lissu kuingia Ikulu ya Chamwino.

Credit: kwa rafiki yangu aliyeko Tandahimba, kwa taarifa.
Tandahimba hakuna CCM ndugu, kama wapo basi wachache sana.
Tandahimba mwaka 2015 matokeo yalitangazwa mapema sana
 
Wakazi wa mji wa Tandahimba na vitongoji vyake walikusanyika kwa wingi kwenye viwanja vya shule ya msingi Matogoro ili kumpokea mgombea urais anayeiwakilisha CHADEMA Mh. Tundu Lissu.

Kwa hakika umati ulikuwa mkubwa haijapata kutokea. Hamasa ilikuwa juu sana.

Huku watu wakiendelea kumiminika, ikaletwa taarifa kwamba Tundu Lissu hatafika kwenye hadhara hiyo kwani hana kibali cha kufanya mkutano wa kampeni katika jimbo la Tandahimba.

Kwa taarifa hiyo wananchi walitakiwa kutawanyika mara moja kurejea makwao. Ila ilichukua muda wa nusu saa watu kuondoka toka viwanjani hapo kwani wengi wao walisikika wakiilaani serikali ya CCM na wengi wao waliapa kumchagua Lissu kwa kishindo kikuu ifikapo tarehe 28 Oktoba mwaka huu.

Nadiriki kusema kwa umati ulioshuhudiwa viwanjani hapo leo, hakuna wa kumzuia Lissu kuingia Ikulu ya Chamwino.

Credit: kwa rafiki yangu aliyeko Tandahimba, kwa taarifa.
Hata sisimizi anapokutana na mende hujinasibu kuwa hakuna mdudu mkubwa kuliko mende!!!! Wewe subiri baada ya Oktoba 28 uisome namba.
 
Lindi wengi hawajajiandikisha!
Hembu tuweke utahira,usukule na ukilaza wa mbogamboga pembeni,twende na takwimu.
Idadi ya Watanzania ni Milioni 60.
Idadi ya wapiga kura walioandikishwa ni milioni 29.
Maana yake ni kuwa nusu ya Watanzania ni miaka 18 na kuendelea.
CCM mnadai Chadema iliwaambia wafuasi wake wasusie kujiandikisha.
CHADEMA ina wafuasi milioni 4.
Maana yake tulitakiwa kuwa na wapiga kura zaidi ya milioni 33,zaidi ya nusu ya Watanzania wote.
Je ni kweli Watanzania wote wenye kustahiki kupiga kura wanaweza kujiandikisha? Jibu ni si kweli.
Hesabu sahihi ni 22 milioni na 7 milioni ni ghost voters.
 
We jamaa ni mpuuzi sana. Kwa hiyo anakotembea Lisu hawajajiandikisha ila anakotembea Magu wenu ndio wamejiandikisha.

Nzishe
Mkuu,yaani unashangaa jinsi binadamu anayeweza kushika simu/pc/mac na kuandika halafu kuwa na utahira wa kiwango hiki. Ama kweli kuwa msukule lazima akili zote zitolewe.
 
Nyomi ya Arusha na Moshi ya mikutano ya JPM umeziina? Au hiyo nyomi ya Tandahimba unailinganisha na nyomi gani ya JPM!!
 
Msisahau siasa ni sayansi na sayansi ni namba. Yaani hesabu kama hizo hapo😍🇹🇿👍
Ushindi unahitaji maandalizi hakikini kadi zenu muda wa majeruhi huu😁😁😁View attachment 1609466
CCM itatawala milele
Wapinzani wanapoteza muda na Mali nyingi kwenye kampeni wakiwa na akili timamu?
Nani anaweza kupeleka kesi ya nyani kwa ngedere??
Hivi wapinzani wameshindwa kujifunza tangu 1995 CCM Haijawahi kushinda Zanzibar na Ndio inatawala!!
Mtu mwenye akili timamu hawezi kupeleka timu yake mashindanoni ilihali anajua mpinzani Ndio muamuzi!!!
Labda lissu anaweza
Nawapa pole wapinzani Tanzania na Zanzibar
Bila tiba mbadala Bure,,,
From Mombasa Republic Of Kenya 🇰🇪
 
Wakati Tundu Lissu akiendelea kulakiwa na Umati mkubwa wa Watanzania wa Kusini

John Pombe Magufuli anaendelea kuwahutubia Ghost Voters wake wa Kanda ya Kaskazini
 
CHADEMA IMEBAKIA HUKO HUKO, SISI HUKU KILIMANJARO NA ARUSHA, TUMEAMUA KUITOKOMEZA. ARUSHA LEO YULE NABII TITO MTABIRI SASA ZAMU YAKE AKAFUNGUE KANISA LAKE. HAPA NI GAMBO TUUU.
nafikiri watu wa Moshi na Arusha huwajui vzr! ngoja mtaona matokeo ndio utajua kuwa 'kucheka sio kufurahi'
 
CHADEMA IMEBAKIA HUKO HUKO, SISI HUKU KILIMANJARO NA ARUSHA, TUMEAMUA KUITOKOMEZA. ARUSHA LEO YULE NABII TITO MTABIRI SASA ZAMU YAKE AKAFUNGUE KANISA LAKE. HAPA NI GAMBO TUUU.
Magufuli anahutubia GHOST VOTERS huko, anapoteza muda wake tu.
 
Back
Top Bottom