Kwa Utashi wangu binafsi, baada ya kuona Chuki zinazidi Kwake na Wahusika wamenyamaza namuombea Msamaha Hayati Rais Magufuli kwa Mapungufu yake

... ila liwe ni Fundisho kwa Viongozi (Watawala) Wengine waliobaki kuwa wasije Kuyarudia yale yale na kwa nimuonavyo Rais wa sasa Mama Samia sioni hata hiyo Chembe ya ama Kuumiza au Kuwakomoa Watu.
Samia kasema yeye na mwendazake ni kitu kimoja ataendeleza alipoishia mwendazake.
 
Marehemu dikiteta magufuli kama mtz mwenzetu tushamsamehe, lkn maovu yake hatutaacha kuyasema make tunayatumia kama case study kuelimisha jamii ili huko mbeleni asije kutokea rais mwovu kama marehemu dikiteta magufuli.
 
Huyu hata ukimsamehe, kuna vitu amefanya mwaka 2016-20 lakini madhara yake tutayaona hata baada ya 2035 Mungu akitupa uzima.

Naogopa Rais atakayekuwapo 2035 atalaumiwa kwa PERFORMANCE wakati ni uozo uliosababishwa na Mwendazake.

Hatumpumzishi huyu, spanna mpaka ahera
 
Finnaarrr !!...wa JEHANAMU ..!! hakuna msamaa bila chama chake kuleta katiba mpya.
aliandikiwa motoni mwache akateketee na maccm yote yatawaka mpaka ...
 
Daah hii ni hatari
 
Una uhuru wa mawazo kadri ya Katiba. Lakini ukipata muda pita Muhimbili kitengo cha magonjwa ya akili
 
mwananchit Kama hujui maovu ya Magufuli na uko Tanzania inawezekana unaumwa magonjwa ya akili. Wahi Muhimbili au Mirembe
 
Ni nani ambaye alipotoka madarakani alisifiwa kuanzia Nyerere, mwinyi, mkapa hadi Jiwe? Watanzania ni wanafiki wanasoma upepo, wanajua vyeo vinapatikanaje, SIFIA ALIEPO TUKANA ALIEPITA... Siri kuu ya wabongo kupata shekeli

Kuna mtu alitukanwa Kama Nyerere, kila Lori jipya walisema ni la Siti Mwinyi, kila uwekezaje wanasema Mkapa ana 10%, kila sheli mpya ni ya Rizimoko. Tumewazoea!!!!
 
Marehemu asemwi vibaya ila jiwe alipokufa watu mioyo yao ilishangilia.

Kufa wote tutakufa ila insue nani anatangulia?

Jiwe kanitesa binafsi ila nishamsamehe muda sana.

Tuseme Amina!!! wengine tuseme Inshaallah!!
Nani alishangalia we fedhuli na baladhuli? Hamkuona walilkuwa wanalia na kugaagaa mabarabarani?
 
Upo nje ya mada.
 
Magufuli alikuwa anatia huruma Tu hata alipokuwa Rais.

Alikuwa kama 'mwanaharakati' na sio president.

Wengi tulijua atashindwa na hata mazuri yake yanaweza sahauliwa, ndo kinachatokea.
kweli mkuu alitia huruma Sana.
 
Ongeza na Hitler pamoja na Iddi Amin
 
Finnaarrr !!...wa JEHANAMU ..!! hakuna msamaa bila chama chake kuleta katiba mpya.
aliandikiwa motoni mwache akateketee na maccm yote yatawaka mpaka ...
Au sio unajukita umekua Mungu sasa..unajua aliongea nn na Mungu wake
 
Damu yake iwasamehe kina nani ssa😂😂😂
 
Mwendazake safari yetu ya maisha aliifanya kuwa ni ya taabu Sana na mateso Tena KWA kipindi kifupi,alipotufikisha kimasafa palikuwa ni mbali ikatuchosha kufikiria kurudi,na tulivyovipoteza ni vingi hatuwez kuvihesabu,bora tuhesabu tulivyovibakiza
Huko ndio kuishi kama mashetani au kubatizwa kwa moto😄
 
Mjadala mpana wa kitaifa unahitajika na kama alivyosema mwenyewe mwendazake hayati John Pombe Joseph Magufuli kuwa historia ya kweli ifundishwe mashuleni.

Basi ktk kumuenzi mwendazake hayati Rais John Pombe Joseph Magufuli aliyetambulika kupitia propaganda za diaspora ya kiafrika kuwa ni shujaa wa afrika , somo hili la historia tusomeshwe pia ya yaliyofanyika chini ya utawala wa Magufuli na chama chake cha CCM Mpya siyo kwa ajili ya kulipa kisasi bali kutuwezesha kama jamii na wale waliopewa dhamana kama viongozi kutenda mema ili historia isije kutuhukumu siku za usoni.

Kule kwa dikteta Francisco Franco walifikia kwenda kulivamia kanisa wafukue kaburi la mwendazake Francisco Franco .

N.B
Habari zaidi za historia za tawala za mkono wa chuma kandamizi :
24 Apr 2018
Madrid, Spain

Mihimili ya Bunge na Mahakama za afiki kuweka historia sahihi ya dikteta Jenerali Franco wa Uhispania

Diktekta Jenerali Francisco Franco alitawala taifa hilo la Hispania kwa staili ya utawala wa 'mkono wa chuma' kwa muda wa miaka 39 hadi alipofariki dunia kwa afya dhoofu mwaka 1975.

Katika kipindi chake cha utawala wa Jenerali Franco, watu wengi walipotea ktk mazingira ya utatanishi na wengineo maelfu kufungwa jela kutokana na kuwa na itikadi tofauti za kisiasa zilizokwaza utawala wake.

Diktekta Franco alikuwa na mahusiano ya karibu viongozi wa juu wa kanisa, maana kanisa lilikuwa na ushawishi ktk maisha ya raia na pia kuunga mkono utawala wa kifalme ktk Hispania.

Jenerali Franco katika vita (1936-1939) vya wenyewe kwa wenyewe Hispania iliyoisha mwaka 1939 hakutaka kuona nchi hiyo ikiishia kumeguka ktk majimbo ya Catalonia n.k Hivyo alitumia majeshi kuhakikisha nchi inabakia bila mgawanyiko. Ushindi wa majeshi ya Franco, ulishangiliwa na kubatizwa kuwa ni ushindi dhidi ya wapiganaji wasio na imani ktk uwepo wa Mungu, Ufalme , uzalendo na umoja wa taifa.

Vita hivyo vilisababisha maelfu ya vifo na Diktekta Franco kuja na wazo la Kujenga basilica / makumbusho maalum ktk mfano wa kanisa kuwaenzi waliopoteza maisha ktk vita hivyo vya wenyewe kwa wenyewe.

Katika wosia wake Dikteta Franco, aliomba kuzikwa ktk basilica hilo na wahanga wengine wa vita ili kujibainisha na wafu wengine waliopigania au kufa kutetea taifa hilo la Hispania lisigawanyike.

Hata hivyo miaka 43 baadaye toka kifo cha diktekta huyo, wananchi, mwanaharakati wa haki za binadamu na wanasiasa wameona kuwa ukatili uliofanyika na utawala wake haustahili kusahauliwa.

Hivyo kupitia Bunge na Mahakama wameona kuweka historia sahihi kuwa ktk utawala wa Franco kuna unyama na ukatili mwingi ulitendeka ktk utawala wake uliodumu miaka 39.

Kuhitimisha hilo, hoja ya kufukuliwa mwili wake imepitishwa Bungeni na kutiliwa uzito mahakamani kisheria kuwa Diktekta huyo hastahili kulala ktk makumbusho hayo kutokana na vitendo viovu vilivyofanyika ktk utawala wake wa kiimla.



Spanish court has for the first time authorised the exhumation of bodies from the Valley of the Fallen. It is a vast mausoleum where the fascist dictator General Franco is buried with thousands of victims of Spain’s 1936 civil war.
 
Marehemu JPM Apumzike kwa Amani.. Nilioata Maisha Katika Awamu yake.
 
Magufuli alikuwa anatia huruma Tu hata alipokuwa Rais.

Alikuwa kama 'mwanaharakati' na sio president.

Wengi tulijua atashindwa na hata mazuri yake yanaweza sahauliwa, ndo kinachatokea.
kwamba mzuri yake yamesahauliwa[emoji23][emoji23]

na nani huyo au nyinyi ambao hamyajui kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…