Kwa uteuzi wa Prof. Kabudi katiba na sheria tukubaliane tu Mwambukusi atanyoosha mikono kama ilivyokuwa kwa Lissu na kudhibitiwa

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Kwa wenye kutazama vitu kwa jicho la tatu watagundua toka Mwambukusi achaguliwe kama Rais wa TLS ni kama ilikuwa inageuzwa kuwa tawi la CHADEMA.

Kwa uteuzi wa jana wa Prof. Kabudi kama waziri wa katiba na Sheria, Mwambukusi hana kwa kufurukuta tena, mtaalamu mbobezi wa sheria anaenda 'kumdogodesha' na pengine atakuwa Rais wa TLS mbovu zaidi katika historia ya Chama hicho toka kianzishwe kama hatobadilika. Hongera Rais Samia kwa uteuzi huu.
 
Mwambukusi anaamini nchi hii hakuna anayeijua Sheria kuliko yeye kwa sasa, Lissu aliamini hivyo hivyo kipindi kile lakini Kabudi alimuonesha ni bwana mdogo ikafikia mahali Lissu akawa analalamika tu kwamba Kabudi anatumia uwezo mkubwa wa kiakili alionao kupotosha. Haikuwa kweli kama Lissu alivyofikiri ila alikutana na kisiki cha mpingo kwenye sheria. Hiki ndicho Mwambukusi atakutana nacho
 
Lissu aliyasema hayo lini? Na huo ubobezi wa Kabudi ulisaidia vipi kipindi kile ndege za serikali zilizokuwa zinakamatwa kila mara na serikali kushindwa kesi?
 
Lissu kahuisha lesseni yake ya uwakili…Kwa mujibu wa Mbowe jana… Sasa Serikali ijiandae kufunguliwa kesi kila kona… mawakili wa TLS wana mtu wa kumshitaki (Serikali) na kupata uzoefu wa kazi- elimu Kwa vitendo itaanzia hapo- twende kazi…
 
Kabudi huyu aliyeshiriki ushirikina wa magufuli wa kikombe cha Madagascar unaona ana akili?
 
Nadhani mngejikita kwenye kesi mnazolipa mabilion huko yasio na kichwa wala miguu hawa wakina Mwambukusi watumieni na si kupambana nao huku Nchi ikiangamia kwa kuwalipa wahuni kila kukicha...
 
Binafsi nafikiri wote wanajenga nyumba moja
mtu akikuambia kuwa nyumba yako inavuja, ni vizuri uangalie kama kweli inavuja urekebishe na sio kubisha kuwa haivuji ukajiona umeshinda, kwani mvua zikinyesha utavujiwa tu
Ninachomaanisha hapa; kila mmoja ana nafasi yake na ikichukuliwa positive; wala hakuna mashindano hapo
 
Ufafanuzi wa katiba tuko awamu ya ngapi na tunaenda awamu ya ngapi
 
trust me, kabudi hana uwezi hata wa kubishana kwa hoja tu na mwabukusi au na wakili yeyote. ila ni mwanasiasa.
 
Kama namuona Kabudi usiku akiandaa pambio lake kwa ‘bi-tozo’ ikitokea kapewa muda atoe neno.
 
Tunataka,tunataka Waziri wa Sheria mbobobezi na mfuata Sheria,tunataka Rais wa TLS mbobezi wa Sheria na atakayesimamia ufanisi wa Sheria,haingii akilini kumwona mtu mwenye akili zake akishadidia umatulinga kwenye mambo ambayo utekelezaji wake unatakiwa kufuata Sheria,Kanuni,taratibu na miongozo iliyopo
 
Hadi hapa inaonesha mnamuogopa ndiyo maana mnatafuta kila namna kumthibiti.
 
Kama una watoto nachelea kusema watoto hawana baba/mama
 
Mawazo mgando!
 
Huyo unayemsifia kaenda law school?Tupe maelezo ya unguli wake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…